Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

mmmm!sasa hili debe lako kwa lowassa mzee halivumiliki...ni wazi na wewe unatumiwa,jana ulikuja kiujanja na ukafanikiwa kuwateka baadhi yetu humu lakini leo kwa maandishi yako haya licha ya kuyaanda kitaalum mi naona niwe wa kwanza kuyatilia shaka,ila tu nikukaribishe kama wapiga debe wengine wa lowassa humu,eti tukienda kwenye vijiwe vyetu vile vya jioni tusiomuongelee vibaya jamaa!!!!vitisho vya kitoto kweli katika karne hii kuweza kuwaingia watu na wakatishika kweli!

eti walitaka dr slaa ashinde,huo ni uongo,kilichopunguza kura za ccm ikiwemo ya kwangu sio ushawishi wala maarifa ya lowassa na genge lake bali ni kitendo cha ccm kuonekana wanawakumbatia mafisadi kina lowassa,rostam na wengine na kuonekana wanapambana na wapinga ufisadi samuel sitta na genge lake,huo ndio ukweli,mengine uliyoandika ni upotoshaji,nimeona nikuvae baada ya kuona wengi wanakuogopa na kuamini kila unaloshawishi hapa!

Du Mdau wewe unaishi Tanzania ipi ambayo tayari maeneo unayoyazungumzia na vijiwe muhimu vyenye story za kitaani kuhusu siasa za Watanzania watetezi wa EL wamejaa tele tena wanajaziba kama nini.Tena like Swala la JK kukaa kimya pasipo kujibu swali la EL kwenye mkutano Dodoma uwa ndio kimbilio lao.Wakikuta huna foundation ya uelewa wa siasa za bongo watakupelemba wewe mpaka utaaanza kuwa kasuku wa ushuhuda wa RICHMOND na DOWANS kuwa ni swala la JK na sio yeye.

Hakika ndio hwajui ni kwanini JK alikaa kimya na kuishi ku guna kwa ishara ambayo kama ni mtu mwenye busara na unajua story za historia ya mchezo huo,basi kukaa kimya kwa JK ni dalili ya ukomavu kuwa anajua utu uzima dawa.

Manake picha hii ya JK kukaa kimya huko Dodoma uwa naifananisha na kama umeenda a mtoni unaoga kisha mwendawazimu anakuja na kuchukua nguo zako na kuamua kukimbia nazo,basi kwa muungwana itabidi kuchutamana [Kukaa Kimya] na kumuacha mwendewazimu kusepa na viwalo vyako,uku ukisubili wapita njia kuja kukuepusha na aibu ya mwendawazimu huyo.Vinginevyo ukiamua kumkimbiza [Payuka] basi tofauti haitabainika wazi nani ni mwendawazimu kati yenu wawili.

Michezo michafu uondolewa kwa mbinu kali zenye kuitaji ustadi mkubwa na si kukulupuka.Mfano wa mbinu hizo ni zile alizotumia Mwalimu mwaka 1995.Bahati mbaya safari hii the Court Break Became a Court Breaker.Hivyo kwa kujua kuwa mwalimu alitumia UWT kumsimamisha ndoto zake ikabidi awajenge yeye mwenyewe,ingawa kwa kazi yao yote kama ni dhahiili wanajua na kufuata maadili ya kazi na si ufahari wa kidunia si ajabu kwa baaadhi yao pia wako kazini muda tu unasubiliwa kama ule wa THERE IS A WISH AM GOING TO GRANT!!!!!!!!!!! na Mara nyingi Idala za aina hiyo uwa makosa mwiko.
 
Ni tetesi lakini hazifanani na za marehemu Balali kuoneka akishop in a mall...!ni wazi kwamba kulikua na kitisho serious thats why kuna mtu akagoma kuja kufanya kazi live arusha akasisitize atumie video na hilo likafanyka!
Balali alionekana akishop ama alikutana na mtu?

Hata kama alionekana, huoni kuna habari kwamba inajulikana alipo and its just a matter of time before they get to him?

Pia hizi tetesi zina version nyingi tu, so huwezi kudai moja ni zaidi ya nyingine bila facts.

Hilo la kuuwawa na wanyarwanda ni tetesi sawa tu kuuwawa kwake mara baada ya kukutana na Balali.

Kila mmoja anaweza kuconnect dots kwa namna za tofauti, na kwasababu kuna mgawanyiko na kambi humu, basi kila kambi itaikubali tetesi kutokana na jinsi either inavyowanufaisha wao ama hata inavyomdhoofisha adui.
 
mkuu kwa mnyonge mie ndio maana natumia jina feki hapa(hata wewe vile vile!).hao wapambe godfather wao lowasa! Mie hata dhamana itabidi aje mjomba wangu muuza mbandule kule nyarutunguru kuokoa jahazi!
nimekusoma.....!mi sitamuogopa mtu kamwe,lowassa asili ya udikteta na vitisho ndio muone mfano hii hajaingia madarakani anahangaika ku create fear kwa wapiga kura!
 
balali alionekana akishop ama alikutana na mtu?

Hata kama alionekana, huoni kuna habari kwamba inajulikana alipo and its just a matter of time before they get to him?

Pia hizi tetesi zina version nyingi tu, so huwezi kudai moja ni zaidi ya nyingine bila facts.

Hilo la kuuwawa na wanyarwanda ni tetesi sawa tu kuuwawa kwake mara baada ya kukutana na balali.

Kila mmoja anaweza kuconnect dots kwa namna za tofauti, na kwasababu kuna mgawanyiko na kambi humu, basi kila kambi itaikubali tetesi kutokana na jinsi either inavyowanufaisha wao ama hata inavyomdhoofisha adui.

mzee sitaki kujitumbukiza kwenye ubishi wa uhai wa marehemu balali,cuz anao ndugu zake anao jamaa zake n.k na wote hana mawasiliano nao au nikubaliane na baadhi ya watu kwamba wote wamenyamazishwa na wamenyamaza!
 
du mdau wewe unaishi tanzania ipi ambayo tayari maeneo unayoyazungumzia na vijiwe muhimu vyenye story za kitaani kuhusu siasa za watanzania watetezi wa el wamejaa tele tena wanajaziba kama nini.tena like swala la jk kukaa kimya pasipo kujibu swali la el kwenye mkutano dodoma uwa ndio kimbilio lao.wakikuta huna foundation ya uelewa wa siasa za bongo watakupelemba wewe mpaka utaaanza kuwa kasuku wa ushuhuda wa richmond na dowans kuwa ni swala la jk na sio yeye.

Hakika ndio hwajui ni kwanini jk alikaa kimya na kuishi ku guna kwa ishara ambayo kama ni mtu mwenye busara na unajua story za historia ya mchezo huo,basi kukaa kimya kwa jk ni dalili ya ukomavu kuwa anajua utu uzima dawa.

manake picha hii ya jk kukaa kimya huko dodoma uwa naifananisha na kama umeenda a mtoni unaoga kisha mwendawazimu anakuja na kuchukua nguo zako na kuamua kukimbia nazo,basi kwa muungwana itabidi kuchutamana [kukaa kimya] na kumuacha mwendewazimu kusepa na viwalo vyako,uku ukisubili wapita njia kuja kukuepusha na aibu ya mwendawazimu huyo.vinginevyo ukiamua kumkimbiza [payuka] basi tofauti haitabainika wazi nani ni mwendawazimu kati yenu wawili.

michezo michafu uondolewa kwa mbinu kali zenye kuitaji ustadi mkubwa na si kukulupuka.mfano wa mbinu hizo ni zile alizotumia mwalimu mwaka 1995.bahati mbaya safari hii the court break became a court breaker.hivyo kwa kujua kuwa mwalimu alitumia uwt kumsimamisha ndoto zake ikabidi awajenge yeye mwenyewe,ingawa kwa kazi yao yote kama ni dhahiili wanajua na kufuata maadili ya kazi na si ufahari wa kidunia si ajabu kwa baaadhi yao pia wako kazini muda tu unasubiliwa kama ule wa there is a wish am going to grant!!!!!!!!!!! Na mara nyingi idala za aina hiyo uwa makosa mwiko.

sijakuelewa kwa nini umenivaa mimi,ok anywayz uko huru kuandika chochote kamanda...
 
Pengine sijaeleweka. Sina maana ya kwamba watu hawa ni wa kuogopa, hivyo wazalendo wa nchi hii wafunge midomo yao. Ujumbe wangu kwa wazalendo wote wa nchi hii ni kwamba vijana hao wapo kazini, kila sehemu, hivyo ni muhimu kulijua hilo, sasa kwa wale watakaochukulia hivi ni vitisho, sawa, kwa wale watakaochukulia hii ni taarifa muhimu ya kuijua katika mapambano, nayo sawa tu. Mimi sina nia nyingine zaidi ya kutoa tu taarifa.

Hawa ni watu hatari, na kupambana nao ni muhumi lakini pale tu kila mpambanaji atakapokuwa na taarifa. Kama Jenerali Ulimwengu ni mtu wako wa karibu, muulize jinsi gani kina EL walivyomfanyia unyama miaka ya nyuma pale walipokodi watu kwenda kumwingilia kinyume na maumbile. Hawa watu ni wanyama, na ndio kiini cha tahadhari nazotoa.

miaka ya nyuma mwaka gani labda ambapo jenerali aliwahi kuwa na biff ama kutoelewana labda na lowassa na genge lake kuwa specific,then nitarudi...
 
miaka ya nyuma mwaka gani labda ambapo jenerali aliwahi kuwa na biff ama kutoelewana labda na lowassa na genge lake kuwa specific,then nitarudi...

Suala la msingi hapa ni kuchukua tahadhari. Sidhani kama ni busara kumjadili mzee wetu Ulimwengu kuhusu yaliyompata. Kafanye tu utafiti to verify then tuliache hilo na kurudi kwenye mada iliyo mbele yetu.
 
mzee sitaki kujitumbukiza kwenye ubishi wa uhai wa marehemu balali,cuz anao ndugu zake anao jamaa zake n.k na wote hana mawasiliano nao au nikubaliane na baadhi ya watu kwamba wote wamenyamazishwa na wamenyamaza!
Mkuu hata mimi kama ningekuwa ndugu wa Balali ningekwambia kuwa huwa nawasiliana naye?
 
mtoa habari..mbona RA alimlalamikia sana NAPE wakati anajiuzulu?alishindwaje kumpoteza hadi akabwaga manyanga?

Ajipendi kumbuka NAPE huyo mtoto ni uzao wa mjeda tena mjeda aliyepata kuheshimika kwenye midani ya siasa za Jeshi.ukimpoteza wajeda watakumaind wewe na ukoo wako. Kwa kuwa wao kumbe kesho na keshokutwa wanasiasa watawapoteza watoto wao kwa upumbavu wa kutetea maslahi yao ya kijinga.

Msione wajeda wamekaa kimya jamaa wana akili kibao sana na ni watu makini sema Mwalimu alivyojenga Jeshi chini ya nidhamu yake ndio imekuwa msingi wa ustahimilivu mkubwa na adabu ya subira isiyo na ukomo mpaka wakuu wao wnaposema basi enough is enough hapo ndio moto uwaka.

Na moto wa jeshi ukiwaka wewe na mimi mitaani uwa hatujui kilichojili kwao, na uchukua muda sisi kujua yanayofanya nao.

Kama umezaliwa na kukua kwenye mazingira ya kambi hasa kambi za Jeshi,Polisi, Magereza au vijiji vya kazi, watoto wa uzao wa mazingira hayo huwa ni watato tofauti sana na watoto waliozaliwa katika mazingira ya kawaida ya mijini na vijijini mwetu.Fanya utafiti utalijua hilo.
 
sijakuelewa kwa nini umenivaa mimi,ok anywayz uko huru kuandika chochote kamanda...

ila tu nikukaribishe kama wapiga debe wengine wa lowassa humu,eti tukienda kwenye vijiwe vyetu vile vya jioni tusiomuongelee vibaya jamaa!!!!vitisho vya kitoto kweli katika karne hii kuweza kuwaingia watu na wakatishika kweli!.

Haya maandishi mekundu ndio yaliopelekea mimi kukujibu.
 
THE ROMANTIC, umeshawahi kwenda tweet halafu ukatype jina la Balali?
 
Haya maandishi mekundu ndio yaliopelekea mimi kukujibu.

ok sasa nimekupata kamanda lakini pale mwanzo sikukupata cuz ulicchoquote ni kingine,yani uliquote wrong ikaonekana kama unaijibu ile..mimi kwenye kijiwe chetu anachanwa yeyote tu,lau masha alitaka kupigana siku moja,watu wakamtuliza wakamwambia kijana hii ndio club bwana,namkubali chenge huwa anapambana kwa hoja sio kwa jazba...
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Mkuu hata mimi kama ningekuwa ndugu wa Balali ningekwambia kuwa huwa nawasiliana naye?

intelijensia isingesubiri kuambiwa na wewe kama ambavyo watu wanataka tuamini haikusubiri kuambiwa na mwaikusa bali ilichukua hatua!
 
ama uzi huu si wa mchezo, embu tupeni bac huo ujio wa chama kipya, kitaitwaje? kadri uzi unavyoendelea na kama mengi yasemwayo ni kweli, si ccm, wala cuf ama chadema wanaofaa kuongoza hili taifa, moyo unauma sana nikifikiria wakina sie tunaokubari wanayotuambia na kuamini wanavyotuongoza, kumbe yote si kweli wanayapanga na kucheza na akili zetu. kuna watu wamepoteza maisha kwenye chaguzi mbalimbali kwa ajili ya mapenzi ya vyama vyao, sie twachinjana kumbe wao wanapangiana. mtoahabari yote umesema lakini hilo la vyama vya upinzani navyo mpaka kumegewa pesa na hao tunaowaita mafisida, aisee nimechoka na kuchoka, kweli usilolijuwa dah
 
Lau yupo popote pale atakapoelekezwa na ENL. Historia fupi ya Lau na familia: Mzazi Lau (Masha Senior), alikuwa ni mmoja wa wasaidizi wa Mwalimu wakati wa kutafuta uhuru, lakini baadae alikuja kuwa sehemu ya timu iliyokula njama kumhujumu Mwalimu, akabahatika kutoroka nchi kupitia Kenya, na kwenda Marekani (NY), huku wenzake wakitiwa kizuizini. Kutokana na elimu yake nzuri, alipata kazi nzuri sana Umoja wa Mataifa, NY. Na katika maisha yake mapya ukimbizini, aliapia kwamba ipo siku atarudi Tanzania na wanae watakuja kutawala Tanzania, hivyo, akawaandaa kufanikisa hilo. Lau na nduguze waliishi vizuri sana huko New Rochelle, nje kidogo ya jiji la New York, na kupelekewa shule nzuri sana nchini marekani. Baadae hali ya kisiasa ilipobadilika Tanzania, Masha Senior alirudi na wanae Tanzania ili kuja kutimiza ndoto yake. Lau akaingia kwenye uwakili kwa malengo ya kisiasa, huku mdogo wake akaingia jeshini (JWTZ). Mdogo wa Lau ni msomi mzuri wa Chuo maarufu sana cha kijeshi nchini Marekani kinachoitwa West Point College. Pia ana Masters kutoka University of Westminster Uingereza. Lakini cha ajabu, aliporudi Tanzania, akajiunga moja kwa moja na jeshi kama kuruta. Hivi sasa amepanda cheo na kuwa Kanali Masha.

IMMA advocate ilipoanzishwa, iliwavutia mtandao original na wakaanza kuitumia kwa shughuli zao mbli mbali. IMMA pia wakamwahidi JK kwamba watamsomesha Ridhiwani Degree ya Sheria Uingereza bure, na kumwajiri. Walimpeleka Ridhiwani Uingereza kama walivyoahidi, akafeli katikat chuo cha kwanza, akapelekwa cha pili, napo huko akafeli. Sifa zake za elimu hapa Tanzania, pamoja na uwakili wake wa mahakama kuu ni wa kiujanja ujanja, wakufanyiwa mipango pamoja na mitihani na IMMA advocate. Ingawa Bado Ridhiwani ana ukaribu wa kikazi na IMMA, lakini hawapo nae tena kiroho, na hawamtaki, na wameapia kumvua nguo muda utakaporuhusu. Hii inatokana na tofauti zilizojitokeza baina ya God Father wa IMMA (ENL) na Baba mzazi wa Ridhiwani, huku Ridhiwani na yeye akipiga vijembe vya chini kwa chini.

Nilipotoa tahadhari hapo awali kuhusu mazungumzo juu ya ENL huko kwenye mabaa ni kwamba, vijana wote wa mjini wenye akili zao timamu, elimu nzuri, na pesa zao, kama wale wanaojiita G8, na wengineo wengi, wote wapo upande wa ENL, na wapo vitani na wote wale watakaothubutu kuchafua hali ya hewa juu ya God Father. Iwe ni kwenye mabaa, gesti, mahoteli makubwa kwa madogo, gymkhana, maeneo ya starehe ufukweni, au popote pale, vijana hawa wapo kazini, masikio yao ni marefu na mikono yao kunyamazisha maadui, ni mirefu zaidi, kuliko ile iliyopo ndani ya Ghorofa jipya la TISS, Ostabei.

Mtoa habari, hapo kwenye bold, umenikumbusha mbali!, niliwahi kuishi mitaa hiyo kwa Mtanzania mmoja aliyeishi hapo, basi siku moja mwenyeji wangu hayupo, nikajitokea nje na kunyoosha nyoosha miguu hapo mtaani, nikitembea mtaa mmoja hadi mwingine na kurudi njia hizo hizo ili nisipotee. Kumbe mtaa unalindwa na security cameras, mara nikaona kuna gari dogo la polisi nikitembea linasimama nyuma yangu kila ninapokwenda, nikaamua kujirudia hapo kwa mwenyeji wangu nikaa barazani, gari ile ikaja, polisi mmoja akashuka na kunionyeshea kitambulisho chake na kuniuliza "who are you and what are you doing here? nikajieleza wakaomba any form of identificatin, nikawapa passport, wakatazama kwenye chart yao, wakaona kweli nyumba ile ni ya Mtanzania, wale polisi wakaniambia you have been reported by neighbourhood as strange person in their streets!. Mwenyeji wangu aliporudi nikamhadidhia mkasa ulionikuta, ndipo akanijulisha hiyo ni white neighbourhood!, sisi watu weusi tulionekana kama wezi fulani!. Kama mitaa hiyo ndiko Lau alikokulia, then ule zungu uzungu anao beheva sio pretence is for real. Thanks far such info.

Ila mtoa habari, mimi pia nimeshajitanabaisha nampigania Lowassa ateuliwe mgombea wa CCM, nakushukuru kwa kutupatia hizi za deep inside TISS, ninajifunza mengi sana kutokana na post zako, thanks!.
 
Suala la msingi hapa ni kuchukua tahadhari. Sidhani kama ni busara kumjadili mzee wetu Ulimwengu kuhusu yaliyompata. Kafanye tu utafiti to verify then tuliache hilo na kurudi kwenye mada iliyo mbele yetu.

Sisi wote tuliosoma uzi mrefu na uliojaa mambo mengi ya kuyawekea maanani kuhusu mustakabari wa nchi yetu inabidi tuchukue hatua ya ziada kumzuia huyu kiwavi mchwa, zinge wa madaraka Lowassa kuendelea kutuchezea kama sisi ni wanasesere

Hapo nyuma niliiwahi kusoma hapahapa JF uzi mwingine ambao kuna mwana JF alimweleza Lowassa alivyo na roho mbaya na roho ya umafia kuhusu madaraka na siku nyingine nikasoma katika gazeti la Raia Mwema habari iliyoandikwa na mwandishi anayejiita Msomaji wa Raia Mwema alielezea Lowassa alivyosuka mpango kwa kushirikiana na Jakaya Kumtisha na mpaka Mzee wa watu Mkapa mpaka akashindwa kusimamia haki ya kupendekeza jina la mgombea wa CCM huku akija na kauli mbiu kuwa tunataka Raisi kijana, Mkapa akaogopa kuicha nchi kwenye machufuko waliandaa genge la wana CCM kibao toka kanda ya Ziwa kufanya fujo kama jina la Kikwete lisingependekezwa

Mwandishi huyo akaendelea kuelezea kitendo alichofanya mwishoni mwa 2010 kwenye NEC ya CCM kwamba aliagiza vijana nchi nzima si chini ya 5000 kwenda Dodoma kumtisha rafiki yake Jakaya kweli alitishika uenyekiti ukamtoka agenda zikamwishia akashindwa kuwavua magamba ,magamba yakabaki yemening'inia viuononi
Mtoa habari leo hii umetufumbua macho huyu jambazi ,Mafia mkuu wa nchi hii Lowassa atakkabailiwa na Nguvu ya UMMA ndio jibu lake hafai kabisa kwa sababu anataka kuingia kwenye madaraka akiwa ameumiza watu wengi sana , na damu za watu zikitiririka .Akina Sumaye,Salimu,Mwandosya ni baadhi ya wanajua adha alivyotumia vyombo vya habari kuwadharilisha mbele ya jamii

Utajiri wake unatumika kudhulumu haki ya wapiga kura hakika tukiamua kupitia nguvu ya UMMA kamwe hatakuwa Raisi na atakufa vibaya kwa mawazo kiasi cha kwamba tutachimba kaburi lake kwa mwaka mzima ndio tumzike wa ovyo sana Lowassa

Musikate tamaa tupeni wananchi wenzenu habari hizi ni muhimu kuwajua wazandiki waroho wa madaraka watu wasioitakia mema nchi yetu kama akina Lowassa

Hakika kwa mbinu za udharimu kiasi hiki atakuwa Raisi wa kumwongoza nani
 
Back
Top Bottom