---
Hivi Ndivyo Kikwete Anavyomfahamu Rais Samia, 'Anaongoza Nchi Vizuri, Ana UtulivuWakati wa kuahirisha kikao cha demokrasia kilichofanyika jijini Arusha, Rais Kikwete ameweza kukumbushia historia ya safari uongozi wa Rais Samia baada ya swali aliloulizwa na mwandishi wa habari wa The Chanzo, Khalifa Said.
Rais Kikwete anakiri kujivunia sana na safari ya uongozi wa Rais Samia, na kumpongeza kuwa anaongoza nchi vizuri. Baadhi ya sifa muhimu alizozitaja ni pamoja na kuwa ana utulivu na hana hasira. Kikwete pia amekumbushia misukosuko katika uongozi wake.