Kilangi aweza kuwa ndiye AG mbovu kuliko wote waliowahi kuhudumu nchini Tanzania tangu Wakoloni waondoke

Mbona unazungukazunguka sema tu kisa ni gaidi kusweka ndani ndio ,maana mna chuki , Prof kaokotwa? unaijua CV yake? haya sasa ni majungu.
 
Kuelekea mkutano wa Baraza la Usalama UN hapa kwetu TZ tutaona mengi..sishangai AG kuwekwa kando..
 
hahahahaaaa....imeshakula kwake
 
Sidhani kama ni wabovu. Ni ma mafia ili waendani na Mafia Mkuu Jiwe.
 
Jiwe ameharibu nchi hii. Na hizi ni matokeo
 
Mimi nilivyojua hatukuwa na AG na nashangaa kusikia katumbuliwa! Mbona sikuwahi kumsikia hata mara moja hadi leo? Watu wa aina hii alikuwa akiwapeda sana dhalimu mwendakuzimu...yaani wapo wapo tu, huwa hawana tofauti na kivuli!

Pamoja na mashtaka yote ya kipuuzi na kubambikizana kesi hakuwahi kutoa kauli yoyote! Aliokotwa wapi huyu? Good riddance ingawa aliyechukua nafasi yake huenda naye akawa hivyo hivyo, masikini Tanzania; cry my beloved country!
 
Kilangi alikuwa mzuri tu kabla ya kuingia ccm
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…