Huu ni mfano mzuri wa jinsi kesi zinavyo pindishwa“Mwanzo walisema alikuwa anafukuza mirungi na pikipiki, wakati anazuia pikipiki yenye mirungi ikaja pikipiki nyingine yenye mirungi ikamgonga akaangukia kwenye kisiki akafa, jambo ambalo lilizua taharuki kidogo kwa sababu ukweli ulikuwa unajulikana,” alidai Mwenyekiti huyo wakati akizungumza na Mwananchi
Labda walificha bangi huko kwenye kiti Cha mbele Kila mutu alitaka aimiliki ndo maana waligombania kukaa mbele Hadi kuuana.Kiti cha mbele kina nini hasa!??
Hata Kama hamna risasi hauruhusiwi kumnyoshea mtutu wa bunduki Askari mwenzio au mutu yoyote,ukishitakiwa kwa kumnyoshea Ni sawa na kutishia kuua hata Kama Haina risasi.Mara nyingi Police hupenda kutaniana. Mara zote katika operation yoyote kiongozi anajulikana na hukaa mbele. Hakuna kitu kama hicho Cha kugombea siti. Mtaniaji ali- assume kwamba hakuna risasi chemba na pengine vilevile kifunga usalama Kiko mahali pake
Wanatumia,msuba au ganja wanapenda Sana Ni Bora uwanyime chakula kuliko msuba hapo mtauana,ndo changamsha kichwa yao.Na ndiyo maana wakitukamataga na misuba haifiki yote kituoni sijui huwa wanapeleka wapi!
Laana ya kubambikiza watu Bangi na kesi za ajabu hata wasiohusika...
Hii inaniingia kiaina!Mara nyingi Police hupenda kutaniana. Mara zote katika operation yoyote kiongozi anajulikana na hukaa mbele. Hakuna kitu kama hicho Cha kugombea siti. Mtaniaji ali- assume kwamba hakuna risasi chemba na pengine vilevile kifunga usalama Kiko mahali pake
Hairuhusiwi kbs hata kubambikiza kesi.....lakin ona wanavyofanya!!Hairususiwi kabisa kumuelekezea mwenzio bunduki hata kwa bahati mbaya na ni kosa kubwa jeshini ukionekana umemuelekezea mwenzio bunduki.
Unahukumiwa kama uliyejaribu kuua.
Kwa maelezo ya mtoa mada, muuaji alifanya kama mzaha kutokana na kauli ya kujutia aliyoitoa baada ya kuua.Wanasemaga "meno ya mbwa hayaumani" sasa hapo sijui imekuwaje
Siyo la mwanaume mwingine.Hivi mtoto wa kiume unaanzaje kushobokea gari lá mwanaume mwengine?
Duuuh najaribu kuwaza yule askari aliye mnyooshea Nape bastola angejisahau kidogo tungekuwa tunaongea mengine. Cha kustikisha unaweza kuta bado anakula mshaara wa serikali wakati alifanya makosa makubwa sana.Kwa maelezo ya mtoa mada, muuaji alifanya kama mzaha kutokana na kauli ya kujutia aliyoitoa baada ya kuua.
Hukumu ya kosa hilo hataiepuka kwa sababu kafanya uzembe usiomithilika wenye kuweza kuepukika, kalibeba sasa ni lake na litamkost sana.
Kifupi, kosa hilo nami nusura linikumbe enzi zetu zilee!
Kuna siku kiutani utani tu, hapa na hapa(zero distance) nikamnyooshea jamaa yangu bastola bila kuihakiki nikijua kwamba ipo tupu!
Kilichonisaidia mpaka leo huwa nasema ni Mungu pekee na siku zangu za kuadhirika na kudhalilika zilikuwa hazijapangwa!
Ile bastola sijui ni nani aliyeitumia na kuiacha ikiwa na risasi chemba kisha kurudisha hamer mbele bila ya kutoa risasi kwanza!
Katika mzaha huo, roho ilikuwa ikinituma nirudishe hamer nyuma kisha nifyatue ili katokee kale kamlio 'ndaa' kama jokes za kikamanda!
Roho ilisita, nikatoa magazine, kuangalia haina risasi, lakini niliopoikoki, lahaulah risasi ilikuwa chemba ikadondoka!
Nilinywea na kukosa raha hadi leo siwezi kusahau, lakini nikaficha mzaha huo wa kifo niliotaka kuufanya.
Katika mafunzo ya kutumia silaha, hata bunduki isiwe na risasi hauruhusiwi kuelekeza mtu, unatakiwa kuelekeza juu ama chini.
Pole kwa wafiwa, pole kwa muuwaji ninajua hakudhamiria, lakini hapo mkosi wa kimaisha tayari ushamkumba.
..Una Hoja kubwa hapo Mkuu. Kumbuka na yule wa kule Mwanza ambaye tuliambiwa amezama baharini wakati akimfukumza mhalifu!Laana ya kubambikiza watu Bangi na kesi za ajabu hata wasiohusika...
Hawa jamaa askari waliwahi mrubuni bodaboda wangu Bangi wakamkamatisha, nikaitwa mwenye pikipiki kituo cha sekei Arusha wanataka million moja waachie pikipiki, sitasahau... Story ndefu lkn hizi ni laana..Una Hoja kubwa hapo Mkuu. Kumbuka na yule wa kule Mwanza ambaye tuliambiwa amezama baharini wakati akimfukumza mhalifu!
Mhalifu alipojitupa ziwani ili kuwakimbia Polisi Askari naye akajitosa Ziwani kumkimbiza ila akajikuta akikamwa na nyavu za kuvua samaki na akazama?
Karma??[emoji848][emoji848]
Kama Police kwa Police wanaficha ukweli. Vipi kwa mwananchi wa kawaida?Mwanzo walisema alikuwa anafukuza mirungi na pikipiki, wakati anazuia pikipiki yenye mirungi ikaja pikipiki nyingine yenye mirungi ikamgonga akaangukia kwenye kisiki akafa, jambo ambalo lilizua taharuki kidogo kwa sababu ukweli ulikuwa unajulikana,” alidai Mwenyekiti huyo wakati akizungumza na Mwananchi