Kilimanjaro Hotel Korogwe bei ya vyakula ipo juu sana

Kilimanjaro Hotel Korogwe bei ya vyakula ipo juu sana

Zamani tukienda Arusha kifamilia ilikua anakaushwa kuku, na chapati au mikate flani hivi ya ufuta na maji tunabeba. Sasa hivi nikisafiri safari yoyote hua sili njiani,hutokufa ukiacha kula masaa 24.

Njiani vyakula ni expensive na low quality,Bora Nile nikifika. Maji,korosho na energy drink inantosheleza. Nishawahi kununua kahawa ambayo ni maji moto,vijiko vitatu vya instant coffee africafe nikalipa 5000. Kwa mda ule nilihitaji kahawa sikuona tabu kulipa ila it was overpriced sana.
Mkuu zingatia Sana kula milo mitatu kwa siku ukiwa mtu wakupuuzia kula kwa maana ya kwamba wewe ukila milo miwili kwa siku unaona ni sawa ni mbaya Sana itapotokea siku katika maisha ya utafutaji au mahusiano ukakumbana na jambo ambalo litakupa stress kwa muda utapata vidonda vya tumbo
 
Hili suala naona mamlaka husika liangalie,juzi nimenunua nyama choma njia ya Dodoma,nyama bei mbaya sana alafu ilikuwa mbichi,hapo nagundua ni mbichi gari imeshachanja mbuga. Hii dhulma inayofanyika mamlaka husika inabidi iingilie kati.
Hizi mamlaka mnazipa kazi nyingi sana ambazo wenyewe mngeweza kuzimaliza. Be Beba msosi wako tu pia ukifunga 12hrs huwezi kufa.
 
Kwa safar ya Dar-Arusha kama utapata breakfast nyumbani kwako sidhani kama ni safari inayohitaji kula njiani. Labda kama sio mzoefu wa safari
 
Heshima sana,

Jana nilikuwa natokea Dar kwenda Arusha.Muda wa saa 2 asubuhi tukapitia hotel ya Kilimanjaro Bus pale Korogwe.
Nikaagiza mtori na sambusa tatu na mwenzangu naye akaagiza kama mimi.Baada ya kumaliza tukaletewa bill kibakuli cha Mtori tsh 5,000 sambusa moja 2,000.

Nikawauliza huu mtori wa ndizi mbili tatu na nyama mbili sh 5,000 na sambusa 2,000 nikaambiwa ndio duh nikalipa bill kwa mshangao.

Nikaondoka kuendelea na safari mbele kidogo ipo hotel nyingine parking imejaa kweli kweli tofauti na Kilimanjaro.Kwakuwa muda wa saa 2 asubuhi magari mengi yalikuwa binafsi nikagundua wadau wa usafiri njia ya Dar to Arusha wameistukia hotel ya Kilimanjaro inauza vyakula bei za kiukraine.

Nilichojifunza wasafiri wanaotumia mabus ya Kilimanjaro wanauziwa vyakula bei kubwa na hawana option labda turejee zama zile za kusafiri na vyakula.
Acha uroho,wee saa 2 asubuhi unakimbilia Kula?
 
Hivi Watanzania wa siku hizi mnakosea wapi? Enzi zetu tulibeba mpaka maji ya kunywa kwenye vidumu!
Njaa ilipouma wakatibwa safari, tulikandamiza zetu wali, ndizi na nyama za kukaanga! Halafu safari ikawa ni ya furaha kabisa.

Hebu fanyeni kurudia maisha ya zamani bhana. Gari likisimama kwenye hiyo hotel, fungua ma hot pot yako, kula mpaka ushibe. Na hakuna atakaye kuuliza! Zaidi ya wapuuzi wachache tu kukushangaa.

[emoji23][emoji30]
 
Kuna hotel sijui korogwe pale zile chips na nyama zao hazielewek kabisa afu hiyo bei sasa tuna kula tusife tu
 
Miongoni mwa upumbavu ninaouchukia ni kutoa hela nyingi na kupewa chakula kidogo siku nitakojolea chakula cha mtu kwa hasira ntakung'uta kabisa pump isibaki hata na tone la mkojo ndani ntaukamulia wote kwenye sahani
 
Acha uroho,wee saa 2 asubuhi unakimbilia Kula?
Niliondoka Dar saa 11 asubuhi sikuwa nimepata breakfast 🍳.Sidhani kama ipo Hotel kwa muda huo unaweza kupata breakfast.

Ndio maana saa 2 kasoro tayari nilishafika Korogwe na nilikuta magari mengi sana yalishafika,maana yake wengine walianza safari saa 10 au saa 9.Hapakuwa na bus hata moja nadhani mabus ya kwanza yanafika Korogwe kati ya saa 4 asubuhi mengi nilipishana nayo kati ya Same na Mwanga.
 
Mwezi huu..hapo utalipa buku saba na ukikaa vibaya utaambiwa hakuna chakula.
Hasa tarehe za leo,Kesho.

Hapo niliwahi ona jamaa amewekewa mifupa kama mifupa😀😀😀😀

Jamaa aliwasha moto hapo pakawa padogo.

Kuna wajinga wengine wako kule Njia ya Mwanza- Singida, wanaweka chakula kwenye bahasha nusu..
Yaani Kama unachukua kajipaja wasikukatie kabsa...utanishukuru later
 
Nilidhani ulipewa bill ya Elfu 50 kumbe buku 7 tu,mkuu tafuta pesa
Kama naweza kuendesha gari (Private) na si usafiri (public) unadhani nitakuwa na tatizo kubwa la fedha ?.

Kwa upande wangu hata nikiwa na fedha nyingi kiasi gani, bado siwezi kuchezea kwasababu ninazo.
 
Heshima sana,

Jana nilikuwa natokea Dar kwenda Arusha.Muda wa saa 2 asubuhi tukapitia hotel ya Kilimanjaro Bus pale Korogwe.
Nikaagiza mtori na sambusa tatu na mwenzangu naye akaagiza kama mimi.Baada ya kumaliza tukaletewa bill kibakuli cha Mtori tsh 5,000 sambusa moja 2,000.

Nikawauliza huu mtori wa ndizi mbili tatu na nyama mbili sh 5,000 na sambusa 2,000 nikaambiwa ndio duh nikalipa bill kwa mshangao.

Nikaondoka kuendelea na safari mbele kidogo ipo hotel nyingine parking imejaa kweli kweli tofauti na Kilimanjaro.Kwakuwa muda wa saa 2 asubuhi magari mengi yalikuwa binafsi nikagundua wadau wa usafiri njia ya Dar to Arusha wameistukia hotel ya Kilimanjaro inauza vyakula bei za kiukraine.

Nilichojifunza wasafiri wanaotumia mabus ya Kilimanjaro wanauziwa vyakula bei kubwa na hawana option labda turejee zama zile za kusafiri na vyakula.
Bei ni kubwa ndio ila mimi niko radhi kulipia sababu ya sifa zifustavyo.

1.Usafi: Pale ni pasafi sana kuliko hotel zingine.

2. Huduma: Unapata huduma ya uhakika, nikilipia bei juu is okay for me.

3.Muda: Mabasi ya Kilimanjaro yanatoa dk 30 kwa abiria kwa ajili ya kula, mabasi mengine wanatoa dk 10 tu halafu watu wanaingia na chakula kwenye basi, hii tabia spendi sana. Gari zima linatoka harufu ya chakula na kutia kinyaa baadhi ya watu wanavyokula chakula
 
Bei ni kubwa ndio ila mimi niko radhi kulipia sababu ya sifa zifustavyo.

1.Usafi: Pale ni pasafi sana kuliko hotel zingine.

2. Huduma: Unapata huduma ya uhakika, nikilipia bei juu is okay for me.

3.Muda: Mabasi ya Kilimanjaro yanatoa dk 30 kwa abiria kwa ajili ya kula, mabasi mengine wanatoa dk 10 tu halafu watu wanaingia na chakula kwenye basi, hii tabia spendi sana. Gari zima linatoka harufu ya chakula na kutia kinyaa baadhi ya watu wanavyokula chakula

Ni kweli Kilimanjaro wanatoa dk 30 na wanalazimisha abiria wote washuke na wanafunga mlango kabisa.

Suala la usafi ni kawaida sana sijaona tofauti ya Kilimanjaro na Rock.

Suala la dakika 30 halina mashiko kwa watu binafsi (private) wanajipangia muda wao kadri watakavyo.

Tatizo ni bei ya vyakula samosa 2,000 haina kiwango cha samosa ya Nazi Hotel ambayo bei yake ni 1,000.Mtori nyama mbili 5,000 ?. Labda hizi ndizi wanaagiza toka Jamaica!.
 
Niliondoka Dar saa 11 asubuhi sikuwa nimepata breakfast 🍳.Sidhani kama ipo Hotel kwa muda huo unaweza kupata breakfast.

Ndio maana saa 2 kasoro tayari nilishafika Korogwe na nilikuta magari mengi sana yalishafika,maana yake wengine walianza safari saa 10 au saa 9.Hapakuwa na bus hata moja nadhani mabus ya kwanza yanafika Korogwe kati ya saa 4 asubuhi mengi nilipishana nayo kati ya Same na Mwanga.
Watu wanasafiri DSM to KGM bila kula chochote,wewe kutoka Dar to Moshi saa 2 asubuhi umekumbilia mtori kwanini usipigwe?
Kama ulishindwa kuvumilia masaa 7 ya kwenda kula huko Moshi usiwapangie bei wenye hotels zao
 
Ni kweli Kilimanjaro wanatoa dk 30 na wanalazimisha abiria wote washuke na wanafunga mlango kabisa.

Suala la usafi ni kawaida sana sijaona tofauti ya Kilimanjaro na Rock.

Suala la dakika 30 halina mashiko kwa watu binafsi (private) wanajipangia muda wao kadri watakavyo.

Tatizo ni bei ya vyakula samosa 2,000 haina kiwango cha samosa ya Nazi Hotel ambayo bei yake ni 1,000.Mtori nyama mbili 5,000 ?. Labda hizi ndizi wanaagiza toka Jamaica!.
Mkuu Soda Bar inauzwa 1000 ila mtaani 500 why hujawahi lalamika? Sambusa ni 2000 leo nimekula sehemu moja inaitwa Maembe pale Moshi.
Maji madogo 1000 badala ya 500 same to Kilimanjaro.

Wanalipa kodi na risiti unapata uzuri wake
 
Back
Top Bottom