Kilimo cha Kisasa cha Mahindi: Mbegu bora, Mbolea bora na magonjwa

Kwa kawaida mbolea ya kupandia ni mfuko 1.kwa eka.
 
Mbegu ziko nyingi ila Mimi Niko kanda ya kati natumia Zamseed kwa eka 3 ni kg 6 yaani pakti 3 za kilo mbilimbili
 
Kuna mbegu ya DK 80 - 53 pia inafanya vizuri maeneo mengi nchini na pia inavumilia mabadiliko ya Tabia ya nchi yaani hata kukiwa na mvua nyingi utavuna na kukiwa na mvua chache utavuna
 
Mpaka sasa mkulima aliyefanikiwa ni yule aliyekamata Bombadia kule canada, ukulima ni tusi (we mshamba nini?)
 
Labda uweke stoo usubiri njaa ianze ndio uuze
 
Yaani ardhi ina rutuba afu unasema Hekari moja itoe gunia 7 sasa hapo rutuba iko wapi!
 
Nimepanga kulima maeneo ya kijingu mkuu pia kuna shamba jingine nimepata maeneo ya lantomoni ila bado sijafanya maamuzi yakulichukua.
nilijaribu heka kumi na hesabu zilikua kama zako nilipata 482,000 sema sijui dogo alinipiga ngoja mkuu nijipange nitakutafuta maana nataka nisimamie mwenyewe kabisa
 
Salamu Settler 900 ....vipi nikitaka kufanya Biashara mkishavuna nije nifanye Biashara gani kwenu walowezi na wapagazi wa Kiteto!
 
Duh aisee mtu anapalilia ekari mzima kwa elf 10? Jipange kukabiliana na changamoto zaidi ya hizi
1. Usimamizi hakikisha 95% unasimamia ww mwenyewe front shamba
2. Kukutana na bei za uzalishaji tofauti na hizo ulizoziandika
3. Kutowapata vibarua kwa wakati, waaminifu na wavumilivu
 
Kongolee
Ila mimi nahitaji mbegu chotara ya maharage ya njano , soya au meupe niko Pwani naipata wapi?
 
Binadamu wasikuvunje moyo maana Kama wanasema ( wanaume wa dar) na huku wanaamini ili ufanikiwe lazima uje dar inakuaje
Mpaka sasa mkulima aliyefanikiwa ni yule aliyekamata Bombadia kule canada, ukulima ni tusi (we mshamba nini?)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…