Kilimo cha Nyanya: Aina za mbegu, mbinu za kulima na masoko yake

Kilimo cha Nyanya: Aina za mbegu, mbinu za kulima na masoko yake

Wapendwa mwenye mchanguo wa Kilimo cha zao tajwa kwaajili ya biashara, ninaomba ujuzi wenu,nimepata shamba Iringa linafaa kwa kulima nyanya sina ujuzi wowote na hili zao ndiyo Mara ya kwanza kulima, naomba mawazo yenu ndugu yangu kuanzia kulima,hadi kuvuna na masoko, natanguliza shukrani, asanteni
 
Mkuu raky jaribu kuperuzi katika jukwaa la ujasiriamali kuna posts nyingi tu wadau wamefafanua juu ya kilimo cha nyanya.
Usipopata basi niite nije nikushushie nondo hizo hapa hapa kwenye uzi wako.
Mkuu GEBA2013 njoo huku umsaidie mdau.
 
Last edited by a moderator:
Wapendwa naomba mwenye ujuzi juu ya hilo zao naomba tushee ujuzi, pia mwenye mchanganuo kuanzia kulima, mbegu bora hadi kuvuna,nataka nilime nyanya kwaajili ya kuuza, asanten sana kwa michango yenu.

Nenda kwenye study tour shamba darasa pale Ununio njia ya boko ile nji ya chini Mahaba beach kule.
 
Wadau naomba mwenye uzoefu wa kilimo hiki hasa kipindi cha masika. Nataka nianze mwezi wa kumi ili nivune kama mwezi wa kwanza kipindi mvua inapokuwa kali na nyanya kuwa adimu.

Shamba lipo Mbeya ukubwa wa hekari mbili. Mtaji nataka niweke maximum wa 3mil kwa hekari zote mbili.

Naomba mnisaidie challenge nitakazokutana nazo mbegu nitatumia anna f1.


cc: malila
Na Ukitaka Mbolea nzuri na yenye kukuletea faida ya mazao yako ya nyanya bonyeza hapa.

Topic: Kwa wale wanaotaka Mbolea ya kuwauwa wadudu waharabifu na kuzalisha mazao kwa wingi
 
Hata mimi nataka nilime nyanya hapo kibaha;
Naomba ushauri kwa mtaalam kuhusu hilo.

Ila nitaanza kwa kulima eneo dogo tu kama majaribio; lets say 20x20.
 
Habari,

Kulima kipindi hicho nyanya inawezekana kabisa ila cha kuzingatia itabidi utumie mbegu hybrid kama Eden na Anna, ila zaidi ntakushauri Eden kwani inastahimili open field farming kuliko Anna ambayo inafaa zaidi kwa kilimo cha greehouse.

Cha kuzingatia shmba liwe level vizuri kuwezesha maji wasitwame sana shamban na pia uweke matuta makubwa. Me nililima Eden na Anna kipindi cha masika, japo nilivuna kwa muda mfupi ila nilipata kipato kizuri tu.

Wadau naomba mwenye uzoefu wa kilimo hiki hasa kipindi cha masika. Nataka nianze mwezi wa kumi ili nivune kama mwezi wa kwanza kipindi mvua inapokuwa kali na nyanya kuwa adimu.

Shamba lipo Mbeya ukubwa wa hekari mbili. Mtaji nataka niweke maximum wa 3mil kwa hekari zote mbili.

Naomba mnisaidie challenge nitakazokutana nazo mbegu nitatumia anna f1.


cc: malila
 

Attachments

  • IMG-20140305-00012.jpg
    IMG-20140305-00012.jpg
    923.7 KB · Views: 338
Kilele F1 ni nyanya chotara yenye umbo la yai. Yaweza wekewa miti ama kuachwa itambae ina uwezo mkubwa wa kuzaa kwa kikonyo kimoja hubeba matunda saba mpaka tisa kwa wingi na machache huwa kati ya matano ama kumi na moja kwa kikonyo inakibali maeneo ya joto na baridi. Hukomaa ndani ya siku sabini toka iwekwe shambani. Ina ukinzani wa baadhi ya magonjwa kama virusi vya nyanya na aina mojawapo ya mnyauko
 
Habari JF Senior, nimeona ujumbe wako kuhusu ushauri wa kilimo, sisi Balton Tanzania ltd tunatoa huduma zifuatazo;
mbegu bora za nyanya inaitwa shanty F1,ina ngozi ngumu ambayo inaweza kukaa kwa mda mrefu baada ya kuvuna (shelf life). Pili kilimo unachotaka kufanya anza mwezi 8 au 9 ili uvune mwezi wa 11-3 kwa mbegu ya shanty F1, lakini ukitaka kilimo chenye tija zaidi nakushauri utumie drip irrigation ili ikusaidie wakat wa kipindi cha kiangazi (off season), nazo tunatoa kwanzia 250sqm mpaka 4000sqm(1acre) na bei zetu ni nafuu, kwa mazungumzo zaidi tuwasiliane kwa 0714 919019
Mkuu Shanty F1 unaweza kulima nje (siyo kwenye green house) wakati wa masika? mavuno yake yakoje kwa mche au Kwa ekari moja?
 
Kwanza hakikisha hiyo aridhi haijatumika sana,pili uwe na mfanyakazi wa kudumu kwa ajili ya shughuli za kila siku,pili uwe karibu na maji mto au bwawa tatu nunua mbegu aina ya asila au Tanya au mwanga,then kwa udongo wa hapo kasulu tumia mbolea aina ya urea sana na DAP..madawa itategemea na ugonjwa utakaojitokeza
 
Habari wajasiriamali... natumaini mwaendelea na mapumziko ya mwisho wa mwezi salama, kwa ambao mambo hayako sawa ni mapitio ya kibinadamu..

Nimeleta uzi huu kuomba werevu wa kilimo cha nyanya hasa kwa ukanda wa mkoa wa kilimanjaro. Ikihusisha aina za mbegu ambazo zinastawi na kutoa matokeo mazuri...

Ningependa kufahamu kuna mbegu ambazo zinakubali sehemu moja na nyingine kukataa pia kuelewa mfululizo wa mbolea na aina zake katika ukuaji wa nyanya hadi kuivuna... na mengineyo muhimu katika kilimo cha nyanya...

Asanteni na muwe na jumapili njema wasalam..
 
Asante sana hizi info za Moro ndo nilikuwa nahitaji maana ni washindani wakuu. Ningependa kuanza na eka chache Pwani nitapanda kwenye September au October ili nipishane nao. Thanks and blessings

vipi ulipanda mbegu gani? Tupe mrejesho.
 
Vp kwa wale wanaopanda kuanzia mwez wa 5. bei inakadiliwa kuwaje kwa kipind hcho, ambapo mtu kama huyo anakadiliwa kuvuna miez ya 8 na 9
 
Baadhi ya vijiji wanaziita moyo,
Ni nzuri kama ulivyosema, ni tamu sana hata kwa kuzila mbichi!!!!!! na zinazaa sana,zenyewe hazihitaji miti ya kuegeshea kwenda juu kama money maker na marglobe, zinakuwa chini chini hivi. Go for garden man.

Mkuu mi nipo iringa(kilolo) kuna baridi sana eneo hili.. 1.Je nyanya zitakubali?
2. Mbegu gani nitumie?
3. Mbolea aina gani?
4. Ni dawa aina gani muhim kuwa nazo ktk shughuli hii?
Pia naomba ufafanuzi wa vitu vyote muhim maana nataka niazime kwa Mara moja niwe navyo store tu
 
Anikeni kila kitu hapa wazi sio pm mbona mnatunyima raha na utam tusiojua kuuliza na pia non member.
 
Mkuu mi nipo iringa(kilolo) kuna baridi sana eneo hili.. 1.Je nyanya zitakubali?
2. Mbegu gani nitumie?
3. Mbolea aina gani?
4. Ni dawa aina gani muhim kuwa nazo ktk shughuli hii?
Pia naomba ufafanuzi wa vitu vyote muhim maana nataka niazime kwa Mara moja niwe navyo store tu

Bahati nzuri Kilolo naifahamu kwa sehemu, Kilolo ambayo hutapata shida kama utataka kulima nyanya ni Ilula ( pande za Lyasa, Image,Namba saba,nane na namba tisa,Kitonga areas), Ruaha Mbuyuni( hapa pana wajanja kidogo be careful), Pawaga ( mashamba ni ya kukodi, hapa sio Kilolo), pia vijiji vya Ndiwili/Ihimbo/Itimbo/Pomern.

Vile vijiji vya ndani sana kama Kising`a hakufai,sababu gharama za usafirishaji. Kama utakuwa tayari, nitakuunganisha na jamaa yangu pale Ilula ili akusaidie kwa usalama zaidi.
 
Bahati nzuri Kilolo naifahamu kwa sehemu, Kilolo ambayo hutapata shida kama utataka kulima nyanya ni Ilula ( pande za Lyasa, Image,Namba saba,nane na namba tisa,Kitonga areas), Ruaha Mbuyuni( hapa pana wajanja kidogo be careful), Pawaga ( mashamba ni ya kukodi, hapa sio Kilolo), pia vijiji vya Ndiwili/Ihimbo/Itimbo/Pomern.

Vile vijiji vya ndani sana kama Kising`a hakufai,sababu gharama za usafirishaji. Kama utakuwa tayari, nitakuunganisha na jamaa yangu pale Ilula ili akusaidie kwa usalama zaidi.

"Shikamoo Malila!",wee jamaa ni noma aisee pawaga ni kwetu kbs eneo ninalotaka kulima ni kihesa mgagao jiran sana pomerin.
Mbegu na madawa ambayo ni lazima niwe nayo ni yapi mkuu maana nahitaji kukopa hayo madawa hvyo nataka nikachukue vyote kwa pamoja. NtakuPM namba zangu mkuu au nitumie nikupgie
 
"Shikamoo Malila!",wee jamaa ni noma aisee pawaga ni kwetu kbs eneo ninalotaka kulima ni kihesa mgagao jiran sana pomerin.
Mbegu na madawa ambayo ni lazima niwe nayo ni yapi mkuu maana nahitaji kukopa hayo madawa hvyo nataka nikachukue vyote kwa pamoja. NtakuPM namba zangu mkuu au nitumie nikupgie

Hapo Mgagao nina mashamba ya misitu, anza kulima july ili upishane na ukungu/theruji. Juzi nilipita hapo, kile kipande cha Magereza kulikuwa na ukungu ile mbaya.

Mbona unateseka na nyanya, lima njegere kule bonde la mtitu au mwombe baba Win akupe kinyungu ulime karoti. Halafu makabichi hapo Mgagao yanamea sana, mbona usilime? Kama una bonde zuri, lima kiazi cha kiangazi ili ukitoe october/november kinalipa sana.
 
Hapo Mgagao nina mashamba ya misitu, anza kulima july ili upishane na ukungu/theruji. Juzi nilipita hapo, kile kipande cha Magereza kulikuwa na ukungu ile mbaya.

Mbona unateseka na nyanya, lima njegere kule bonde la mtitu au mwombe baba Win akupe kinyungu ulime karoti. Halafu makabichi hapo Mgagao yanamea sana, mbona usilime? Kama una bonde zuri, lima kiazi cha kiangazi ili ukitoe october/november kinalipa sana.

Kwny kiazi hapoooo...nlikuwa na options hzo mbili kiazi au nyanya,njegere nimelima ntaanza kuchuma keshokutwa Malila. Ukipita tena huku karibu sana mkuu tuonane JF imeunga undugu
 
Back
Top Bottom