Kinachoendelea Sri Lanka, Tanzania tushukuru kuwa na Rais Samia

Kinachoendelea Sri Lanka, Tanzania tushukuru kuwa na Rais Samia

Rashda Zunde

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2022
Posts
204
Reaction score
231
Ogopa sana taifa ambalo lenye bora kiongozi na sio kiongozi bora. Rais wa Sri Lanka alikua bora kiongozi, yeye alikuwa anafanya mambo kuwafurahisha wananchi bila kuangalia madhara yake hapo mbeleni.

Alikuwa akikopa mikopo mikubwa isiyo na unafuu na kufanya mambo ambayo yameifanya Sri Lanka kuwa na deni kubwa mpaka kufikia hatua ya kushindwa kuhudumia wananchi wake.

Kwa sababu ya janga la COVID-19, mapato kutoka kwa watalii wa kigeni na pesa zinazotumwa kutoka nje zilishuka. Wanauchumi walionya kuwa Sri Lanka huenda isiweze kulipa deni lake la nje na wakahimiza serikali kuwasiliana na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).

Baada ya kuchaguliwa mnamo 2019, Rais Gotabaya Rajapaksa alipunguza ushuru, ambayo ilinyima serikali mapato yanayohitajika sana.

Kama Rais ni vyema ukawa unafanya maamuzi huku ukiangalia muelekeo wa nchi yako. Na hapa ndiyo maana nasema Tanzania tushukuru kuwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwani mikopo inayochukuliwa ni ya nafuu na pia inatumika kwenye mambo muhimu ya maendeleo ya taifa huku ikiendelea kutengeneza fursa na kuweza kupata fedha za kurudishwa mikopo hiyo.

Mnaolalamika kuhusu tozo na ushuru, kumbukeni umuhimu wake katika kuiendesha serikali. Makusanyo ya tozo unaiongezea serikali kipato na kuiwezesha kulipa madeni.

Rais Samia Suluhu amekuwa akiweka wazi umuhimu wa tozo na kufafanua maana ya mikopo hiyo na namna inavyotumika.

Pia hapa tunaweza kuona dhahira umuhimu wa Rais kuwaachia watendaji wake kutekeleza majukumu yao na kujipunguzia majukumu. Rais Samia anafanya kazi zake, Waziri Mkuu naye anafanya majukumu yake, vivyo hivyo wasaidizi wote wa Rais mpaka wabunge.

Lakini kwa serikali ya Sri Lanka, Rais ndiye mkuu wa nchi, serikali na jeshi nchini Sri Lanka lakini anashiriki majukumu mengi ya kiutendaji na waziri mkuu, ambaye anaongoza chama tawala bungeni jambo linalofanya aingilie majukumu ambayo sio yake na kunyima viongozi kutekeleza kazi zao kwa ufasaha.

Wakati tukiiombea Sri Lanka, tukumbuke pia kumuombea Rais wetu na pia kumshukuru Mungu kwa kutupa kiongozi Bora na sio bora kiongozi.

Tanzania ni salama na Samia. KAZI IENDELEE
 
Tumshukuru kwa kwenda kutukopea.

Shida ya wananchi wa Tanzania ni uvumilivu wao tu. Bila uvumilivu hii nchi ingekuwa vipande.

Haiwezekani nchi yenye maziwa, mito, bahari n.k hadi leo kuna shida ya maji. Nani katuloga kama sio hao viongozi?

Sifa za namna yako hutolewa na mtu anae kula na kulala bure.
 
Ogopa sana taifa ambalo lenye bora kiongozi na sio kiongozi bora. Rais wa Sri Lanka alikua bora kiongozi, yeye alikuwa anafanya mambo kuwafurahisha wananchi bila kuangalia madhara yake hapo mbelen...

Tanzania ni salama na Samia. KAZI IENDELEE
 

Attachments

  • F9D6E780-6E03-408F-B670-77037F6F0123.png
    F9D6E780-6E03-408F-B670-77037F6F0123.png
    38.1 KB · Views: 10
Ogopa sana taifa ambalo lenye bora kiongozi na sio kiongozi bora. Rais wa Sri Lanka alikua bora kiongozi, yeye alikuwa anafanya mambo kuwafurahisha wananchi bila kuangalia madhara yake hapo mbeleni...
Mkuu mbona kama unongea kwa mafumbo.

Mikopo tunayokopa kama nchi imefikia wapi?

Kwani Rais wa nchi hii na Waziri Mkuu, wote ni executive, wanateua , wanatema, wanaelekeza mmwelekeo wa uchumi, wanakopa.

Sasa tofauti iko wapi na Sri Lanka.
 
‘Sikio la kufa, alisikii dawa’ Ndugai alishatuonya.

Baada ya kukuza madeni kwa speed ya 5G na kutuongezea tozo kila siku; sasa hivi kaamia kwenye miradi ya mikataba yenye miaka 99 yale yale ya Sri-Lanka na kugawa rasilimali zetu LNG $40 billion dollars. Sidhani kama wengi tunaelewa kitanzi tulichojivisha kwenye huu mradi.

Sasa hivi anatimua yeyote TPA anaeuliza logic ya mkataba wa bandari ya Bagamoyo na China. Nchi ambayo imechangia kuiingiza Sri Lanka katika madeni makubwa na watu ambao mpaka leo wanatudai deni la TAZARA kwa riba kubwa ya mkopo waliotuwekea wakati copper yenyewe inaenda kwao China.

Kudra za mwenyezi mungu mwisho 2025.
 
Mtoa mada huna akili kabisa aisee,
Kwa yanayoendelea nchi mjinga mwingine anaona ni Sawa,
Samia hana uwezo mzuri wa kufikiri,
Nilianza kuona ni mjinga aliporopoka " mwaka huu ni mwaka wa kumekucha kila kitu kitapanda" hajui hii kauli tu pekee imeathiri watanzania wa hali ya chini kwa asilimia kubwa sana,
Kama kiongozi hakutakiwa kusema hivi nalaani sana yeye kuwa rais aisee.
 
Ogopa sana taifa ambalo lenye bora kiongozi na sio kiongozi bora. Rais wa Sri Lanka alikua bora kiongozi, yeye alikuwa anafanya mambo kuwafurahisha wananchi bila kuangalia madhara yake hapo mbeleni...
Hata kama Mwendazake angekuwepo najua shida nyingi za Kiuchumi zingetokea ila kwa alivyokuwa na roho mbaya angewafyeka wote ambao wangethubutu kuandamana..

Na mambo ya kuandamana hapa Tzn ni ngumu kwa sababu hatuna historia ya kudai vitu Kwa nguvu..

Hao Sri Lanka wamepigana vita vya wao Kwa wao Kwa miaka 20 iliyopita na hivyo familia ya Gupta ndio walishinda kwenye Hiyo vita..

Bongo tungenyooka na balaa maana nakumbuka awamu ya Mwendazake mafuta ya diesel/petrol yamewahi adimika kama mara 2 Hivi,sukari ndio ilikuwa kila mwaka na saruji iliadimika 2020..

Kwa uchumi wa hivyo ule wa Mwendazake ndio angekuwepo sasa Hivi Nchi ingekuwa imeshaharibika zamani Sana.
 
Mtoa mada huna akili kabisa aisee,
Kwa yanayoendelea nchi mjinga mwingine anaona ni Sawa,
Samia hana uwezo mzuri wa kufikiri,
Nilianza kuona ni mjinga aliporopoka " mwaka huu ni mwaka wa kumekucha kila kitu kitapanda" hajui hii kauli tu pekee imeathiri watanzania wa hali ya chini kwa asilimia kubwa sana,
Kama kiongozi hakutakiwa kusema hivi nalaani sana yeye kuwa rais aisee.
Kwa hiyo aliposema hivyo wewe kwa akili zako za kuku ndio ukaona hana uwezo sio?

Nakuhakikishia Mungu kaepusha balaa kubwa Sana la Uchumi kwa kufa yule mtu wenu mwongo..

Covid kidogo alianza kupigia magoti wazungu eti wawasamehe kulipa madeni kuliko kwenda Kukopa.
 
Tumshukuru kwa kwenda kutukopea.

Shida ya wananchi wa Tanzania ni uvumilivu wao tu. Bila uvumilivu hii nchi ingekuwa vipande.

Haiwezekani nchi yenye maziwa, mito, bahari n.k hadi leo kuna shida ya maji. Nani katuloga kama sio hao viongozi?

Sifa za namna yako hutolewa na mtu anae kula na kulala bure.
Hawavhmilii bure bali kuna sababu za kuvumilia ..

Nchi gani hapa Africa ina maisha ya afadhari kushinda Tzn?
 
Back
Top Bottom