Wana bodi!
Hali ya CCM ni mbaya sana. Hawakutegemea kabisa kuwa watanzania watawakataa kama inavyotokea sasa. Na katika ku-panic na kuonyesha taharuki wamejikuta wanafanya mambo yanayozidi kuwafumbua wananchi macho na kuiona CCM ni kundi la matapeli:
1; Matusi ndio imekuwa ilani yao ya uchaguzi.
2: Magufuli ameshindwa kujinadi kwa kutumia jina la CCM na badala yake anajinadi kama mgombea binafsi.
3: Na kali ya funga kazi ni hii iliyotokea leo: wamekuja na mpango wa maandalizi ya ilani mpya huku ile ya zamani wakiwa wameitupa. Hebu oneni huu utapeli:
My take: CCM wanazidi kuonyesha utapeli, ulaghai na kuwa ni wale wale wala hawakuwa wamejiandaa. Hivi kweli inaweza kuingia akilini mtu kusema Chama kilichotawala muda wote huu haya mambo kilikuwa hakiyajui na sasa ndio wameshtuka na wanaanza kuchunguza? Si ni kwasababu wameona hali ni mbaya ndio maana wanakuja na mipango mipya huku hata iliyopo kwenye ilani haijatekelezwa?