Tetesi: Kinana agoma kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya CCM

Tetesi: Kinana agoma kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya CCM

Status
Not open for further replies.
Tayari wameshapokelewa ufipa. Wanangoja kupitishwa kugombea urais. Nimeambiwa (na chanzo cha uhakika), kesho kutwa makamanda watatangaziwa.
 
Ni wazi kwa kitendo cha Mzee Kinana na Mzee Makamba makatibu wakuu wastaafu waliokuwa na mvuto mkubwa kuandika barua ya kujitoa CCM chama chetu kimekutana na dhoruba Kali sawa na kusambaratika.

Nini chanzo cha yote hayo? Bila kupepesa macho ni kitendo cha wao kuhoji kwa nini mtu anayejiita mwanaharakati mtetezi wa Rais Magufuli anawavunjia heshima na kuwatukana na haguswi? Jee anatumwa na Magufuli mwenyewe? Kwa sababu angekuwa hatumwi naye lazima ange shughulikiwa.
Baada ya hapo ndio misukosuko ya ajabu ikaanza.

Sasa jee kweli chama chetu kikongwe kama CCM ambacho kinaheshimika Afrika nzima na hasa kusini mwa Afrika kinaweza kweli kukubali kusambaratishwa na mjinga mmoja kama Musiba na maandiko na kauli zake kwa vile anabebwa?

Na kwa nini mwenyekiti wetu amezungukwa na watu waletao mtafaruku na jamii na hata kusababishia heshima ya chama kupotea naye haambiwi kitu kuhusu watu hao mfano RC Makonda?

Ukiangalia kwa makini tatizo hapa ni mwenyekiti, chama kinageuka kundi LA wahuni na misingi inapotea kabisa.

Kukubali wanachama waandamizi kukikimbia chama ni ujinga mkubwa bora kumtimua madarakani mwenyekiti anayekipoteza chama na kukivuruga. Naamini hata watangulizi wake wote katika hili la kina Kinana hawamuungi mkono na kacheza karata vibaya kabisa.

Kinana nakumbuka ndiye alikuwa Kampeni meneja wa Mkapa kipindi cha pili na JK vipindi vyote viwili jee huyo ndio wa kutumiwa Musiba awatukane?

JPM must go, na inaanzia julai katika kupeperusha Bendera uchaguzi mkuu 2020 then tutamtoa uenyekiti.

Sasa CCM inatakiwa itoke mikononi mwa wasio kijua chama na kurudi mikononi mwa wenyechama yaani wanachama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni afadhali CCM ife izikwe kabisa kuliko kurudi kwenye CCM ya Makamba na Kinana; kuvaa jezi ya Yanga mtaani ilikuwa taabu sana enzi hizo. Siku hizi naziona nyingi tu.
Kwa kuwa demokrasia ilikuwa juu zaidi ya sasa, walizomewa, walitusiwa hata kupigwa, sio leo, ole wake umguse mwenye nguo zile, inamaana wewe ujapata ujumbe?
 
Kwanza mpaka sasa bado hakuna uthibitisho kuwa hili ni kweli, lakini ikitokea likawa kweli, Kinana na Makamba wakajitoa CCM kwasababu ya kile kinyangarika, then huu utakuwa ni uthibitisho kuwa wamegundua kile kinyangarika kinatumwa tuu, hivyo ili kulinda heshima zao, wakaamua kujiepusha na CCM na kumwachia vinyangarika na anayewatuma

Kitendo cha watu waliokipigania chama kwa machozi, jasho na damu katika maisha yao yote, halafu, wakaja kuchafuliwa na kudhalilishwa na kinyangarika fulani ambacho kinatumwa, karma ya Kinana na Makamba ni kubwa, hivyo kama hii ni kweli, then just sit and watch jinsi karma itakavyo kishughulikia hicho kinyangarika na anayekituma!.
P
 
aisee.. hiki chama kinaenda kumfia mtu kabala hata ya kumaliza muda wake, haiwezekani wazee wenye hadhi ya akina kinana ambao wameshiriki kwa kiasi kikubwa kuwaweka watu madarakani eti wakadhalilishwe na vikamati uchwara, ni bora wajivue tu kwani hamna namna!
Na kibaya zaidi malalamiko yao kuhusu kulalamikia kudhalilishwa kwao na huyo mtu anayeitwa Musiba, yakatupwa
 
Jana tarehe 8/2/2020 ndiyo ilikuwa siku tuliyotangaziwa kuwa makatibu wakuu wastaafu wa CCM, Abdrahman Kinana na Yusuph Makamba, watafika mbele ya Kamati ya maadili ya CCM, kuwahoji kwa vitendo vyao vinavyodaiwa kuwa ni kukiuka maadili ya Chama chao cha CCM

Umma wa watanzania walikuwa wametega masikio yao kwa hamu kubwa huko Dodoma kwenye jengo linalofahamika kama "white house" kilikotarajiwa kufanyika kikao hicho ili kujua mbivu na mbichi

Hata hivyo habari zilizotufikia ni kuwa makatibu hao wakuu wastaafu wa CCM "wamegoma" kufika katika kikao hicho ili kuhojiwa.

Tetesi zipo nyingi zinazosemwa, kuhusu sababu za makatibu hao wakuu wastaafu kutohudhuria kikao hicho, miongoni mwake likiwa hili la kujivua uanachama wa CCM

Ndipo hapo tunapomtaka Katibu Mwenezi wa CCM, Humphrey Polepole ajitokeze hadharani na kutujulisha ni nini kimejitokeza hadi kusababisha makatibu hao wakuu wastaafu "kugoma" kuitikia mwito wa Chama chao ili wahojiwe?

Nadhani Katibu mwenszi wa CCM, Humphrey Polepole, atajitokeza hadharani na kulitolea ufafanuzi suala hili nyeti na lenye maslahi mapana kwa Taifa ili kupoza kiu ya mamilioni ya watanzania
Nashukuru niliwahi kushauri wasikubali kuhojiwa, ila wameenda hatua zaidi ya kujivua uanachama, si mbaya, nilisema ni vema wangewafuata na kuongea nao kungejenga zaidi! Sasa pole pole kweli umwite mzee Makamba, kisa madaraka! Naamini adabu ipo chini sana!
 
Wa
Nashukuru niliwahi kushauri wasikubali kuhojiwa, ila wameenda hatua zaidi ya kujivua uanachama, si mbaya, nilisema ni vema wangewafuata na kuongea nao kungejenga zaidi! Sasa pole pole kweli umwite mzee Makamba, kisa madaraka! Naamini adabu ipo chini sana!
Wacha wafu wazikane wenyewe........

Ndiyo hivyo tena, chama kikongwe kabisa barani Afrika cha CCM kimeamua kujizika chenyewe!
 
Kukataa kuhojiwa wameonesha kuwa hawana hoja za kujibu
Ccm hatujawahi kuyumbishwa na viongozi hata siku moja
Jumbe alivuliwa nyadhifa zake zote,zaidi ya nne,Maalim sefu na genge lake walitimuliwa itakua hao wastaafu
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Sijawahi kuona mwanajeshi anaekubali kuburuzwa na asiye mwanajeshi aliyemzidi cheo.

Nionavyo, namna pekee ya kuwahoji hao wazee ni kuwaomba miadi (appointment) na kuwafata majumbani kwao, kwa heshima zote wanazostahiki kwa umri wao na nyadhifa zao walizostaafu, na kufanya nao mahojiano ya kistaarabu.

Huwezi kuwaweka kitimoto hao wakakubali. Hawana cha kupoteza.
Kabisa hawa na wazee na wamekifanyia chama mambo mengi sana hata kabla ya viongozi wa sasa kujiunga na chama leo watoto wanawaita wazee kwa kukosa adabu? hapa ndugu zangu wa CCM wamewakosea sana hawa wazee maana walishapumzika siasa na kubaki kama wanachama tu. Kwa hili ni CCM kuwaomba msamaha hawa wazee sio kinyume chake ni udhalilishaji wa hali ya juu kabisa hata mimi ningekuwa kati ya hawa wazee ningefanya the same.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom