Kama hii ndio namna ya profesa kufanya reasoning sijutii kamwe kutokufika chuo kikuu.
Yaani, Profesa Mukandala anaamini kuwa, rais akiondolewa kinga ndio atang'ang'ania madarakani lakini hakuweza kuona kuwa rais akiwekewa kinga anaweza pia kung'ang'ania madarakani kwa kuwa anajua hata jaribio lake likishindwa au kufanikiwa hatashitakiwa na yeyote yule?
Yaani, Profesa Mukandala anashauri zianzishwe taasisi imara na makini za kumshauri rais na bado haoni haja ya rais huyo huyo kubanwa kwa sheria fulani endapo atakataa kusikiliza ushauri wa taasisi hizo!!!
Yaani, Profesa Mukandala anaona kuwa 'kwa kuwa Mwalimu Nyerere alishindwa' basi kila rais ajaye naye anapata haki ya kushindwa na katika hili labda niulize: Mwalimu Nyerere ndio 'marking scheme' ya utendaji wa viongozi wetu wajao?
Hivi profesa anaweza kuainisha hatari za kiusalama na kidemokrasia zinazoikumba Marekani, South Africa na Brazil (kwa kutaja chache) kwa kuwa viongozi wao wa juu wanabanwa na sheria?
Ee Mungu tuhurumie!