Kingunge: Bila tume huru, wapinzani wasahau kuingia Ikulu

Kingunge: Bila tume huru, wapinzani wasahau kuingia Ikulu

Ajenda kuu ya upinzani na hasa ukawa ni lazima iwe tume huru ya uchaguzi kama kweli tunataka haki yetu ya ushindi ilindwe
Mkuu unaweza ukawa na Tume huru lakini kusiwepo Uhuru wa Tume kumbuka na ilo
 
isitoshe mpaka hivi majuzi tuu wakati wa bunge la katiba, wote hao EL, Sumaye, Kingunge walikuwa against UKAWA, nashindwa kuelewa hii nguvu wanaipata wapi.?

siasa za Tanzania ni za kinafiki sana na zenye kuangalia maslahi binafsi. halafu eti wanasiasa wanafiki wa aina hii ndo wanataka tuandamane tuvunjwe miguu kwa ajili yao, mi nasema hivi yeyote anayeingia madarakani ndo ninamuunga mkono.

wadhulumiane huko wawezavyo, yule mdhulumaji anayewazidi nguvu wadhulumaji wenzie mi ndio namuunga mkono, sitaki stress mie maisha yenyewe mafupi haya. akhaaaa.!
wew kama Mimi Safi sna mkuu
 
hahahahah alishindikiza .au.alishindikizwa mkuu? ilkuwa.lazma mult party system iazishwe mkuu na sio nyerere
Na yote hiyo ni kulingana na wakati. Hivyo kubadilika sio jambo la ajabu
 
Ni mnafiki, mbona Ukawa walipotoka yeye hakutoka kama kweli alikuwa na nia njema na taifa letu?
Mwalimu Nyerere alisema mpinzani wa kweli atatoka CCM, hata hivyo Mwalimu Nyerere ndie aliyefuta mfumo wa vyama vingi baada ya Uhuru na pia ndie aliyependekeza na kuurudisha mfumo wa vyama vingi miaka ya 90 kiasi kwamba kila mtu anamsifu Mwalimu Nyerere hadi leo ,sasa iweje tumbeze Kingunge?
 
Siku ambayo Tanzania itatengeneza katiba mpya na kupatikana kwa Tume huru ya Uchaguzi basi CCM itaondoka madarakani mchana kweupe
hahahah ni rahisi mno kuandika ila ni vigumu.mno kuamini ulicho andika,usifute j ibu lako mkuu hlo ndo sahihi .

Yesu ataludi ?
 
Guys,mzee Kingunge has nothing to lose at his current age kafanya mengi kapata mengi kama tunashindwa kuona umuhimu wake kwa upinzani basi tujitafakari ni aina gani ya upinzani tunataka, je upinzani wa kushiriki chaguzi kila baada ya miaka mitano au upinzani wa kuleta mbadala wa CCM,lazima tukumbuke kuwa asilimia kubwa ya viongozi wapinzani nchi hii kwa namna moja au nyingine wametokea CCM .
 
Kwa serikali hii ya chama cha mapinduzi kukubali tume huru ya uchaguzi hakuna tofauti na tajiri kuuona ufalme wa mbinguni ngumu, ni rahisi kwa ngamia kupenya katika tundu la sindano kuliko tajiri kuuona ufalme wa mbinguni.
 
CCM wenzangu angalieni, fanyeni tafiti kujua ktk vijana wenye age ya 13, 14, 15, 16 na 17 kwa asilimia wangapi wanaunga mkono CCM na wangapi wako upinzani. Mwaka 2020 ndio wataamua nani awe rais wa Tanzania.
 
Kwa jinsi Mazingira yanavyokwenda, na Mchezo mchafu sana Unaosukwa na Magufuli na CCM, hali sio nzuri kabisa kwa Ukawa 2020.

Mtego Mkubwa uliopo ni kuwa Wabunge wengi Siasa ubunge kwao ni sehemu ya Ajira. Hata tume na katiba ikiwa mbovu kiasi gani, Ili mradi kuna uwezekano wa wao kushinda ubunge, ukiwakataza Kugombea Ubunge watakimbilia CCM wapo wachache Majasiri, Lakini Wasaliti kama Joshua Nasari watakimbilia CCM kwa Speed ya supper sonic.

Pia huo ni mtego Mbaya sana Kwani Tumeona CCM ni kama mafisi wasiojali kula kiungo cha Myama ambaye bado anatembea au nyama ya Mzoga ambao umeoza kiasi cha kutoa usaha! Kugomea Uchaguzi kwao itakuwa ni sherehe na njia ya Mkato ya Kuiua Chadema. Na kwa Chadema kushiriki Uchaguzi Kutakuwa ni Mhururi wa Kuwasafishia CCM ushindi haramu wa urais ambao sina shaka watajitangazia hata kama kura za Urais watapata tano. Mfano halisi ni Zanzibar. Hata hivyo kama Chadema hawako tayari kufanya mambo kadhaa Muhimu, Ninaona ni Bora washiriki Uchaguzi hivyo hivyo. Lakini Pia hofu mbaya zaidi Ni kuwa Magufuli kwa kukataza mikutano na akaona no body pushed away hard enough, msishangae bila aibu 2020 akalazimisha wagombea wa CCM watangazwe washindi majimbo ya Upinzani hata kama mpizani ameshinda kwa asilimia 98 na yule wa CCM asilimia 2.
If a man will swim with crocodiles and they do nothing, he will be used of it! CCM na Magufuli wameget away na Uhuni Mwingi, kunyanganya Komputer za Ukawa 2015 Kimya, Kufuta Matokeo ya Zanzibar, Kimya, Kukataza Mikutano ya Vyama Kimya, Kumsindikiza na Polisi Lipumba Kuvunja Ofisi za Cuf, Kimya. Tutashuhudia Vituko 2020.
Mimi Nina Suluhisho la Uhuni huu, Bila Shuruti CCM wenyewe wataomba iwepo Katiba mpya na Tume mpya ya Uchaguzi, Nitawatafuta Ukawa- Chadema only once, wakipuuza thats it. Baada ya hapo wanitafute wao au 2020 wabakie na Wabunge Watatu (3)
 
Bado hata tukipata tume huru kushika hii nchi bado...maana chama chetu hakina mikakati na kimeanza kupoteza umakini...mfano ukiwa unakunywa maziwa akakutana na funza ndani yake...hata ukipewa siku nyingine maziwa lazima utakumbukia yale yenye funza hapo itabidi uamue kunywa kigumu au usilazimishe...ndani ya chama penyewe hatutumii katiba kumpata mgombea...hata katiba yetu tunaikiuka sana
 
Wenzetu husema "it is better late than never". Wangeangalia mbele wangeona lakini ukiwa mtawala unafikiria jinsi ya kuhadaa wapinzani wako unasau huenda siku moja ukawa mpinzani. EL, FS, KNM na Masha nao ni zamu yao kujua mabaya ya kile walichokua wanasimamia-safari hii tunaisoma wote namba lakini waliobaki huko CCM wasipoangalia iko siku zamu yao itafika. Bado namuunga mkono hata kama alichelewa.
Muunge tu mkono mkuu. Ni haki yako. Ila kwa hii mianasiasa ya Bongo michumia tumbo hii you will be disappointed again and again. I am sorry but psychologically it gonna be a bumpy ride for you.
 
Mkuu naona mabwana wanavyochangamkia chai bila hata itifaki,wanaiwahi chai kabla hata ya mwenyekiti!
Chai ya ikulu tamu wewe. Hebu muone Prof. alivyo makini utafikiri hajawahi kunywa chai maishani. Badala ya kusubiri mwenyeji aionje kwanza ili kuhakikisha haina sumu, wenyewe hata wafe sawa tu.
 
huyu mzee ni mnafiki. hivi umuhimu wa tume huru ya uchaguzi ameuona leo? huyu na lowasa wote walikuwa wajumbe wa bunge la katiba. je walifanyaje? japo alichoongea kina ukweli.
 
Nyie ni watu sio mawe hivyo watu wanatakiwa kubadilika kutokana na wakati. Ni aibu mtu uliyesoma kumlaumu mtu eti mbona zamani alikuwa na msimamo ule na leo ana msimamo huu.
Mwanzilishi wa sheria ya muundo wa utawala wa Chama kimoja ni Mwalimu Nyerere, lakini ndiye huyohuyo aliye shinikiza kuwa sasa wakati umefika kuwa na vyama vingi. Mbona hamkumshangaa
Mkuu najua wewe ni mfia chama ila tuweke uzalendo kidogo. Hawa akina Kingunge hawa? Umesahau hasira zake zilianzia wapi? Akina Mahanga? Umemsahau mkuu? Masha? Muulize Wenje! Mmekatisha wengi tamaa! Wengi wasiojua muda utaongea tu. Tatizo si kukosea ...bali baada ya makosa mnafanya nini! Ukisoma historia ya kanisa unakumbuka hakuna mtikisiko mkubwa uliopasua kanisa kama ule wa Martin Luther ....pamoja na Kanisa kuamini Luther alikosea lakini walijitathimini na kufanya marekebisho pale walipoona kulikuwa na hoja. Chadema inapaswa kufanya marekebisho makubwa yatakayorudisha mwamko upya. Tuache kutetea kila kitu tuseme ukweli chama kipone...
 
Huyu mzee si alikuwa kwenye bunge la katiba, wanazingua, waongee wengine si hawa

Kingunge na Lowassa wake waache unafiki au wanadhani kila mtu ni mjinga? Walihonga kila kona kuhakikisha rasimu ya Warioba inapigwa chini ili ile rasimu yao na Chenge ipite wakiimini Lowassa atakuwa rais! Sasa wanadai nini? Wavune walichopanda.
 
Huyu babu anahasira na stendi ya ubungo tu!
 
Back
Top Bottom