Kingunge: Mchakato wa kumpata Mgombea Urais CCM ulikuwa batili! Lowassa si fisadi kama inavyodhaniwa

Kingunge: Mchakato wa kumpata Mgombea Urais CCM ulikuwa batili! Lowassa si fisadi kama inavyodhaniwa

Kingunge ameamua kusema Ukweli na ukweli pekee ndio unaweza kuwaweka huru wanaCCM. Japokuwa simuungi Mkono Lowassa lakini hakutendewa haki kabisa.

Kama kweli Lowassa na wenzake wenye nguvu na ushawishi ndani ya CCM waliokuwa wanagombea walikuwa hawafai, ilikuwa ni busara sana kuwapa nafasi wajumbe wa Kamati kuu, Halmashauri Kuu au Mkutano Mkuu kuamua hilo na sio kuwakata majina yao kwenye kamati ya Maadili kinyume kabisa na kanuni, taratibu na Katiba ya CCM.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Hicho mnachokiita KITENGO kilifanya what had to be done kwa maslahi ya CHAMA.
Msifumbie macho mikakati miovu ya EL na genge lake hasa kipindi hiki cha kuomba udhamini.
Wametembeza hela.
Tunakaa na watu wanaotusimulia namna hela yao ilivyopotea kwa jina la EL kukatwa...msijifanye hamuoni hilo.
Tusijifanye pia kuwa tumesahau uchaguzi wa CCM wa 2012 ulijaa rushwa na kupanga timu.
Huku Kamati kuu, NEC na Mkutano mkuu pesa ilishatembea.
Viongozi si wapuuzi wapeleke jina huko tayari watu walishanunuliwa!!!
Genge hili lilisha-manupulate mfumo uliopo, zikiwemo kanuni kwa pesa ndio maana walikuwa na jeuri ya kudai hawaoni wa kukata jina-limekatwa sasa kwa maslahi ya CHAMA!!!
Cha msingi tunachopaswa kujifunza toka Dodoma sio kulilia ukatwaji wa watu; cha msingi ni kujifunza kuwa kuna wakati inabidi kufanya lolote kunusuru.
CCM baada ya miaka mingi imetoa mgombea ambae hakununua uongozi na hilo ndio muhimu...Wote mnaolia, pamoja na Kingunge mkumbushwe uongozi haununuliwi!!!!
Kama mtu huyo ana uwezo kama mnaodai, hapakuwa na sababu ya kutumia hela zote zile kumnadi kuchukua tu fomu...pesa hizo wakati hospitali wajawazito wanalala chini!!!
Umefika wakati muwe wazalendo
 
na sasa hivi wamemkimbia mzee wa watu....wakati ule angekuwa amezungukwa kila kona



attachment.php

Anatia huruma ...
 
Mnao mdharau Mzee Kingunge hamjui kitu na mpo kama bendera fuata upepo! Kingunge ni mzee makini sana na mnaofurahia jambo hili mtakuja jutia siku moja!

Umakini wake kwa kumtetea luwasa tu?
Kwani luwasa pekee ndio aliekatwa hakukuwa na wagombea wengine walio katwa mbona hatujamsikia akiwatetea au kuwataja?
Hana umakini wowote zaidi kajidhalilisha na kutuonyesha udhaifu wake.
Mzee kingunge kakosa kujijua na kujua nafasi yake aliyo nayo ktk chama na taifa kwa ujumla.
Kama angejijua na kujua nafasi yake aliyo nayo asingethubutu kuegemea kwa mgombea yeyote ktk wagombea wote waliochukuwa form .
Kwa kuegemea kwa mgombea mmoja ndio jambo lililo mpunguzia sifa zote alizokuwa nazo.
Nahivi anavyo zidi kusemasema ndio zaidi anavyo zidi kujishushia heshima.
Mshaurini akae kimya mm ningemuelewa pale alipo kuwa ktk bunge na dr mwakyembe anasoma taarifa ya uchunguzi wa richmond angesimama akamtetea luwasa lakini ALIUFYATA leo tutamuelewaje anapo mtetea luwasa wakati luwasa mwenyewe aliomba ajiuzu.
anamtetea mtu baada miaka 3 alikuwa wapi muda wote huo?
Afahamu sifa ya mgombea urais sio kupendwa na watu tu au kutokuwa mla rushwa au fisadi.
Arudi asome tena sifa za mgombea urais kwa tiket ya ccm.
 
hakika wazee wa kamati ya maadili ni wahuni. kweli siasa ni uhuni
 
Mzee kaishia kubaya, na bado anazidi kujichanganya. Bora angejinyamazia kama swahiba wake luwasa
 
Ukiachilia mbali mahaba ya Kingunge kwa Lowassa na sababu zake za utetezi ambazo sizo at least kwa dhana aliyojengewa mgombea wake na kushindwa kujitofautisha yeye mwenyewe ndio kabisa; wachina wanamsemo wao bora ukae kimya wakufikirie mpumbavu, kuliko kufungua mdomo wako na kuwthibitishia upumbafu wako. Timu ya Lowassa kuelekea uchaguzi ndio imetufanya wengi kukubali tuhuma zinazotolewa juu yake, binafsi nimeshangaa kuona Karamagi bado anaingia NEC.

Having said that bado hoja yake ya mchakato ulivyoenda ndivyo-sivyo inabaki ni ya msingi sana ndani ya chama chao na inabidi wakae wafikirie wakikutana wanasawazisha vipi kwenda mbele. Kanuni na sheria zipo kwa sababu ya maelekezo ya ufanyaji mambo na uwezi badilisha kwa manufaa yako things dont work that way or else utazua migogoro tu na watu wa nje kuwaombea hiyo migogoro ijitokeze kwa faida yao.

Hakuna kipindi kigumu kwenye chama chochote cha siasa duniani kama wakati wa kubadili leadership ya juu, kazi yote ya kamati ya maadili, sijui whips huko dunia zingine wanavyoitana ni kuhakikisha chama kinabaki salama kipindi kama hiki maana makundi ayakosekani.

CCM mbona kasheshe lake dogo sana kipindi hiki kulinganisha na migogoro inayozuka China tofauti yao na CCM labda wao wakishaamua huyu ndio wetu kama ukileta ukaidi awasubiri muda wa kuchagua kiongozi ufike uyumbishe chama chenye wanachama zaidi ya millino saba hiyo kamati yao ya maadili inaanza na wewe kabla awajafikia hatua hizo.

Lowassa na Apson nawafananisha na 'Bo Xilai' ambaye alikuwa ni challenger 'Xi Jinping' na 'Zou Yongkang' ex spy no suprises kwa sababu ya utawala wa vyama vya kijamaa. Na issue ni hii hii Sura ya chama jamaa walivyoleta ukaidi wala hakuna haja ya kukatana wakijua wanasupport ya wanachama wanaweza leta migogoro 'Bo Xilai' anaozea jela sasa hivi na mkewe ana suspended death sentences; huyo wausalaa walimvutia muda na yeye sasa hivi lupango makosa yao ushahid wa ufisadi wa zamani.

Chama akiwezi tishiwa nyau na makada wake ndio maana kuna kamati za maadili ambazo kazi yake ni kuhakikisha wanachama wanaowania nafasi za juu wanasifa sahihi na vision sahihi na kuna muda mrefu sana wakufikia hatua za kufikirwa kutokana na groomed procedure na mafanikio yako sio tu kwenye kufanya kazi bali uwezo wako wa kukiunganisha chama na wanachama wakisema huyu ni kuwa ana tick all the boxes sio tu hana makundi ndani ya chama.

Huu mchakato uligubikwa na majungu, poor succession planning ambayo aijulikani nani anafaa kwa sifa zipi kutokana na mahitaji ya watanzania na kukijenga chama, binafsi nina mashaka sana na uwezo wa Magufuli kama raisi nilitegemea zaidi ya uchapakazi bali vision pia.

In short the whole thing and several part machines needs services na Kingunge anaposema muundo wa chama umewekwa majaribuni nakubaliana naye kabisa. Way forward ni kuacha kufanya vitu kwa mazoea tu ya kuendesha nchi na previlege za usalama walizonazo hila CCM inabidi ijipange upya na iangalie safu yake ikibidi watu kama kina Wilson Mkama warudi tu kama awapo kwa sasa bado skills zao zinahitajika na kupanga safu mpya yenye mawazo mapya kwa sasa hawa watu wengi wafanya maamuzi na strategists are weak na namna alivyoenguliwa Lowassa sio ingawa end justifies the means that the only justification of the their wrong doings.
 
yaan Leo ningekuwa mm n lowasa ningehama chama yaan hakuna dhambi mbaya kama uwoga
 
Hicho mnachokiita KITENGO kilifanya what had to be done kwa maslahi ya CHAMA.
Msifumbie macho mikakati miovu ya EL na genge lake hasa kipindi hiki cha kuomba udhamini.
Wametembeza hela.
Tunakaa na watu wanaotusimulia namna hela yao ilivyopotea kwa jina la EL kukatwa...msijifanye hamuoni hilo.
Tusijifanye pia kuwa tumesahau uchaguzi wa CCM wa 2012 ulijaa rushwa na kupanga timu.
Huku Kamati kuu, NEC na Mkutano mkuu pesa ilishatembea.
Viongozi si wapuuzi wapeleke jina huko tayari watu walishanunuliwa!!!
Genge hili lilisha-manupulate mfumo uliopo, zikiwemo kanuni kwa pesa ndio maana walikuwa na jeuri ya kudai hawaoni wa kukata jina-limekatwa sasa kwa maslahi ya CHAMA!!!
Cha msingi tunachopaswa kujifunza toka Dodoma sio kulilia ukatwaji wa watu; cha msingi ni kujifunza kuwa kuna wakati inabidi kufanya lolote kunusuru.
CCM baada ya miaka mingi imetoa mgombea ambae hakununua uongozi na hilo ndio muhimu...Wote mnaolia, pamoja na Kingunge mkumbushwe uongozi haununuliwi!!!!
Kama mtu huyo ana uwezo kama mnaodai, hapakuwa na sababu ya kutumia hela zote zile kumnadi kuchukua tu fomu...pesa hizo wakati hospitali wajawazito wanalala chini!!!
Umefika wakati muwe wazalendo

Kwa hiyo huko CCM Fisadi ni Lowasa peke yake ni watu wangapi tunasikia tetesi zao kama anavyochafuliwa Lowasa peke yake bila ushahidi wowote kuwa wamekwapua hiki na kile kuanzia Mkuu wa Kaya mpaka mawaziri wake lakini hatusikii wakiimbwa kama EL?Pinda hajawa na kashfa ya Sukari,Mkulu hajatajwa kwenye Escrow,Membe hajatajwa kwenye kashfa ya Libya,Magufuli hajatajwa kwenye kashfa ya Nyumba pamoja na wizara yake?kama ni hivyo inakuwaje leo hii aonekane Lowasa ndio dampo la kila baya la Nchi hii,umesema kwenye mchakato wa udhamini amenunua watu,je una ushahidi gani au kisa alikuwa anapata watu wengi kuliko wenzake?. Acheni unafiki,kila mtu alifanya rafu kuanzia familia kuu kumbeba mtu mmoja mpaka kuhonga watu hela,kilichotakiwa ni usawa na haki kwa kila mgombea na ndicho Mzee Kingunge analia nacho.
 
Kingunge wachane maccm yanaonea watu.Ccm wamezoea magoli ya mikono leo msikubali pambana mpaka Lowasa apate haki yake.ccm ni mafisadi na wadhurumu haki
 
Mzee kingunge pambana mpaka haki ipatikane.Sisi waislam hatutaki Pombe iende ikulu.Mzee pambana haki itendeke Lowasa wetu arudi kugombea.
 
Makubwa haya, sasa ni dhahiri CCM vipande vipande.

Namshauri huyu Mzee (Dingi) akapumzike, yeye na Lowasa ni mafisadi hivyo wanaelea chombo kimoja baharini, wanalindana. Eti huyu alikuwa mfuasi wa Nyerere kiasi cha kutoamini dini yoyote. Wanahabari walipaswa kumuuliza juu ya ufisadi mkubwa alioufanya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani, tena kwa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Aende zake kaishiwa cha kuongea.
 
Kwa hiyo huko CCM Fisadi ni Lowasa peke yake ni watu wangapi tunasikia tetesi zao kama anavyochafuliwa Lowasa peke yake bila ushahidi wowote kuwa wamekwapua hiki na kile kuanzia Mkuu wa Kaya mpaka mawaziri wake lakini hatusikii wakiimbwa kama EL?Pinda hajawa na kashfa ya Sukari,Mkulu hajatajwa kwenye Escrow,Membe hajatajwa kwenye kashfa ya Libya,Magufuli hajatajwa kwenye kashfa ya Nyumba pamoja na wizara yake?kama ni hivyo inakuwaje leo hii aonekane Lowasa ndio dampo la kila baya la Nchi hii,umesema kwenye mchakato wa udhamini amenunua watu,je una ushahidi gani au kisa alikuwa anapata watu wengi kuliko wenzake?. Acheni unafiki,kila mtu alifanya rafu kuanzia familia kuu kumbeba mtu mmoja mpaka kuhonga watu hela,kilichotakiwa ni usawa na haki kwa kila mgombea na ndicho Mzee Kingunge analia nacho.

Mmmh kumbe walioumia ni wengi aseee, poleni bana ndio hivyo.
Lakini mbona mnalalamika wakati jamaa ni mtu wa maamuz magumu????
Halafu imekuaje amekatwa wakati alishasema hakuna wakumkata!!!!!
Mh hatari
 
Kwa hiyo huko CCM Fisadi ni Lowasa peke yake ni watu wangapi tunasikia tetesi zao kama anavyochafuliwa Lowasa peke yake bila ushahidi wowote kuwa wamekwapua hiki na kile kuanzia Mkuu wa Kaya mpaka mawaziri wake lakini hatusikii wakiimbwa kama EL?Pinda hajawa na kashfa ya Sukari,Mkulu hajatajwa kwenye Escrow,Membe hajatajwa kwenye kashfa ya Libya,Magufuli hajatajwa kwenye kashfa ya Nyumba pamoja na wizara yake?kama ni hivyo inakuwaje leo hii aonekane Lowasa ndio dampo la kila baya la Nchi hii,umesema kwenye mchakato wa udhamini amenunua watu,je una ushahidi gani au kisa alikuwa anapata watu wengi kuliko wenzake?. Acheni unafiki,kila mtu alifanya rafu kuanzia familia kuu kumbeba mtu mmoja mpaka kuhonga watu hela,kilichotakiwa ni usawa na haki kwa kila mgombea na ndicho Mzee Kingunge analia nacho.

Mzee kingunge amuthubutu kuongea Ukweli na Ukweli unauma sana, Hata watu wakimkejeli vipi ukweli umejulikana mchakato wote ulibugikwa na hujuma kubwa mfano kamati batili ya maadili ilipeleka majina 5 yakiwemo bilali na makongoro , lakini Nape na JK wakayakata kienyeji wakawaweka Membe na January Makamba huu ni mojawapo ya mapungufu ya cc. Mzee kingunge si Mnafiki kaanika ukweli pasipo kujali matokeo yake .
 
Mmmh kumbe walioumia ni wengi aseee, poleni bana ndio hivyo.
Lakini mbona mnalalamika wakati jamaa ni mtu wa maamuz magumu????
Halafu imekuaje amekatwa wakati alishasema hakuna wakumkata!!!!!
Mh hatari

Ni bora ukweli ubakie kuwa wazi kuliko kukaa na hayo mapungufu ya cc moyoni kisha tunaendeleza unafiki japo Nape atakuja na majibu mepesi dhidi ya Ukweli lakini wenye Akili zao wameshajua kilichofanyika Hata Nape aseme nini itakuwa Kama kuweka maji kwenye Tenga.
 
Namshauri huyu Mzee (Dingi) akapumzike, yeye na Lowasa ni mafisadi hivyo wanaelea chombo kimoja baharini, wanalindana. Eti huyu alikuwa mfuasi wa Nyerere kiasi cha kutoamini dini yoyote. Wanahabari walipaswa kumuuliza juu ya ufisadi mkubwa alioufanya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani, tena kwa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Aende zake kaishiwa cha kuongea.

Tuhuma za ufisadi si kigezo cha kumzuia Kingunge kusema Ukweli , Tambua kuwa ccm hakuna Msafi Hata mmoja wote ni Mafisadi wale wote 38 waliochukua form ya kuwania urais ni mafisadi , ufisadi wao unajulikana hakuna Msafi ccm kiasi cha kumnyooshea mwenzake kidole, Mzee kasema Ukweli jinsi magumashi yalivyofanyika sasa wenye Akili zao wameshajua lakini wabishi mtabaki kumkejeli .
 
Back
Top Bottom