Mwalamsha mkuu,
Kwa nchi zenye malengo ya kupiga hatua ni lazima zishirikiana na private sector hasa kwenye sector nyeti kama nishati, lakin kwetu sisi mafuta na gesi ni completely zimehodhiwa na private sector, kwa miaka ya hv karibuni angalau kidogo serikali yetu kupitia TPDC wameanzisha TANOIL kujaribu kuweka kaushindani na private sector, lkn kana nguvu ndogo mnoo its like wanajaribu.
Sector ya usafirishaji ndio kabisa hali tete, ma UDA yaliyokuwepo machache yanaozea huko kwenye mayadi mbagala, treni zetu ndio hivyo tena, badala ya kuweka njia mbili, wameweka njia moja, ina maana likienda inabidi usubiri lirudi. Sawa na mzungu mmoja akajisemea NO HURRY IN AFRICA.
Kwa sehem kubwa sisi Watanzania tunauongelea uchumi midomoni, lkn hatujui uchumi unaendana na muda.
Kama hatujui kutunza muda, uchumi utaimalikaje?
Mtu uko Dar lkn cha kutoka mbande, Chanika au Tegeta unatumia masaa matatu barabarani, ina maana ukienda na kurudi masaa sita hadi saba.
kazin unatakiwa ukae masaa nane, na wafanyakazi wadanganyifu wanachukua na time sheet ya overtime kabisa.
Kwa hesabu hiyo ya siku kwa masaa 24, masaa 14 yametumika kwa kazi na barabarani, katika masaa 24 yanasalia masaa 10 tu.
Katika hayo masaa kumi ufanye ibada, ukae na familia, upumnzike, usome vitabu na magazeti nk, then unataka innovation kwenye kazi kweli?