Kiongozi makini na anayejali wananchi wake asingekubali zaidi ya bil 11 kutumika kutengeneza filamu ya namna hii badala ya kuboresha huduma za afya

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Ilikuwa ni jambo la kutumia kamera za Tbc taifa na kutengeneza filamu ambayo ingewekwa kwenye masoko mtandao ingeuzika na kuenea dunia nzima.

Hayo mabilioni yaliyotumika yangeimarisha huduma za afya huko vijijini maana vituo vya afya na Zahanati nyingi hazina madawa na vifaa tiba.

Hakuna kitu kipya hii filamu iliyogharimu pesa nyingi itabadili kwa sekta ya utalii. Mkuu wa nchi alipaswa kuwa na uchungu na taifa lake na wananchi wake.

Mkuu wa nchi anashiriki kutwanga vitu vizito kichwani raia wake!
 
Wewe na watu wenye mtizamo kama wako, hawapaswi kulaumiwa maana tatizo lao ni uelewa na exposure. Kumlaumu mtu ambaye akili yake imefikia kimo cha kufikiri ni kumuonea bure.

Kwa lugha rahisi hiyo ni investment ambayo itazalisha. Kwa lugha rahisi zaidi ni mbegu ambayo itazalisha 1000x. .....

Sasa wewe ushauri wako ni kuwa ni bora tungekula mbegu. Mama alipaswa aongoze watoto kula mbegu ili aonekane anajali. Hahaahahah

Kuongoza nchi yenye watu wengi wenye uelewa wa namna hii, you must be very tricky! Vinginevo unaweza ukajikuta unaweka mbegu mezani kweli.
 
Ahaaa. Sidhani kama hata la saba ulimaliza.
 
Nakuunga mkono asilimia zote Hawa ndio wale wa kutafuta doa kwenye chochote kinachofanywa na mtu wanayemchukia
 
Akili zako ni tofauti na wanadamu wengine.
Anyway ngoja nikuache

Sent from my SM-G973U using JamiiForums mobile app
 
Anaekuchukia hakosi jambo na huo ndio ukweli wenyewe,bi mkubwa hatafanya jema wakaliona.
 
Kufanya kazi za maendeleo ni kula mbegu?
 
Nitoe mfano mmoja tu / muigizaji filamu wa kibongo akipata fursa ya kuigiza na Silvester Stalline ( Rambo) au aigize na wa hapa hapa.
Atapata milege (mafanikio ya kimataifa) na nani?
Mara nyingine unahitaji kugharamia ili utangaze na ufanye biashara.
Mfano tangaza biashara zako wakati wanacheza mpira kwenye Azam Tv Ihefu na Mbeya City au Simba na Yanga !!! Utasikika na kujulikana wapi zaidi???
Na je utangaze Kupitia mechi Ya Liverpool vs Man City.
Mifano mingi sana . Mafanikio ni gharama pia.
 
Unajitambua? Umepost nini?
 
Unaweza kuwa na hoja, hivi ule uwanja wa ndege uliojengwa bila idhini ya bunge sio matumizi mabaya,
Ulikuwa mtetezi mkubwa,
 
Mwaka huu lazima uokote makopo,chuki zako kwa Rais Samia zimepitiliza. Sukuma Gang kubalini matokeo tu kutesa kwa zamu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…