Kiranga na jamaa zake wanaweza wasionekane kwenye thread mbalimbali lakini uzi wowote unaomsifia Mungu huwakosi

Hakuna cha fulani ndio wanatumia akili, kila siku watu hubadilisha mitazamo kama atheist anakuwa agnostic na agnostic anakuwa theist na kinyume chake ni mitazamo tu. Kuwa atheist au agnostic nako unaenda KULAZIMIKA kukataa uwepo wa vitu vingi sana zaidi ya Mungu/miungu tu ambapo ni kufuata mkumbo pia.
 
Umesoma haya maneno 👉(iwe amefikia itinisho au la bado anajitafuta) umeyaelewa maana yake ?
 
Sio kweli kwamba agnostic anaamini Mungu anaweza kuwepo au asiwepo, tofauti ya atheist na agnostic ni hayo madai ya atheist kujifanya anajua kiuhakika kuwa hakuna Mungu wakati agnostic anaona hakuna namna ya kuweza kujua kiuhakika kuwa Mungu yupo au hayupo.
 
Umesoma haya maneno 👉(iwe amefikia itinisho au la bado anajitafuta) umeyaelewa maana yake ?
Huwezi kusema kuwa atheist au agnostic ndio kujitafuta kwa sababu hata wenye kuamini Mungu sio wote wapo sawa wapo wenye mitazamo tofauti kwa sababu ya kujitafuta, sasa wewe wenye kuamini Mungu unaona wote ni wamoja na ni wapumbavu halafu hao waliyokimbilia kwenye atheism na agnosticism ndio wanatumia akili na wanajitafuta wakati kiuhalisia wamejitupa huko.
 
Wewe kichwa chako kina akili ? Rudi nyuma kasome nilicho andika ..kuna makundi mawili ya wanao amini uwepo wa mungu ...rudi nyuma kasome kwanza siyo unadandia tu mijadara usiyo jua imetokea wapi
 
UHURU JR Soma kuanzia hapa nimeeleza yote unayo yasema
 
Hoja haijengwi kwa kusema 'wenzetu wanafanya, basi na sisi tufanye,' bali kwa kuleta uthibitisho wa wazi wa msimamo wako. Je, unaweza kuthibitisha kwa mantiki kuwa Mungu hayupo badala ya tu kusema kwamba kuna mafundisho yanayodai yupo?
 
Mambo ya kiimani hayahitaji logic za kina Kiranga au wanasayansi, yanahitaji usitumie logic zako sababu wewe ni kondoo au bibi harusi.

Ushasema ni imani, wao wakija na fact wewe simama na imani yako.

Biblia inakuambia Yona kamezwa na samaki, wao wakija kuchambua kutowezekana kwa hilo jambo kitaalam wewe simama na imani.

Umesahau YESU alivyoona majaribu ya shetani yanavuka mipaka alimjibu nini?
 
Umempasua au tumekupuuza huna hojatumeamua kukalia chimyaaa
 
Pili, kwa kujibu swali la "watu walitoka wapi", naweza kuwa sina jibu kamili la watu walitoka wapi lakini nikajua kuwa hawakuumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.
Unasema hujui watu walitoka wapi, lakini unasema unajua Mungu siyo chanzo chao. Hii ni argument from ignorance – unadai kitu fulani si sahihi pasipo kutoa uthibitisho wa mbadala. Kama hujui jibu sahihi, kwa mantiki huwezi kuwa na uhakika kwamba Mungu siyo chanzo. Unawezaje kuwa na uhakika kuwa Mungu hayupo kama hujui chanzo cha uhai?
Unapinga wazo la Mungu kwa sababu halina uthibitisho wa moja kwa moja, lakini unakubali wazo la evolution hata kama unasema ni gumu na lina controversy. Kwa nini unapendelea shaka upande mmoja lakini si mwingine?"
 
Kipi kinafanya uone sijakuelewa?
Nilisema tokea mwanzo kuwa wanao amini katika mungu wapo makundi mawili wenye kutumia akili kufikia imani hiyo na wasio tumia akili ...nikasema hao ndiyo kundi la 1 na la 3 ..kisha nikaja kwa hao wa kundi la 2 wasio amini ...wewe umekuja kunikosoa kuwa hata wanao amini wapo wanao tumia akili jambo ambalo mimi pia nimelielezea vizuri tu
 
Mungu hayupo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika yupo.

Hakuna uhakika, ushahidi wala uthibitisho wowote ule wa kwamba Mungu yupo.

Hivyo Mungu hayupo.

Sasa wewe unakataa kwamba Mungu hayupo, Halafu umeshindwa kumthibitisha yupo.

Sasa unataka nini zaidi?
 
Sasa mkuu, wadau wawachore tu, mkiwa mnalishana matango pori?.....🤔🤔
 
Point uliyoiruka ni kwamba agnostic wanasema hakuna njia ya kuweza kujua kuwa Mungu yupo au hayupo, kwahiyo theist akisema Mungu yupo agnostic atahoji amewezaje kujua? Na atheist akisema huyo Mungu hayupo pia agnostic atahoji amewezaje kujua?

Chengine ni kwamba si kuwa hakuna uthibitisho wa kuwepo Mungu tu bali pia hadi sasa hakuna ushahidi uliyoweza kuonyesha kutokuwepo kwa huyo Mungu, najua suala la uthibitisho linakupa shida kulielewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…