Kisa cha rafiki yangu wa Mafia

Kisa cha rafiki yangu wa Mafia

Kwanza ni kweli kabisa asie kua muislam ni kafiri.
Lakin uislam umekataza kumfanyia ubaya kafiri asie udhuru uislam, na umehusia kuwafanyia wema majirani zako, na katika watu wawili ambao wataipata adhabu ya Mungu ni mwenye kuuvunja undugu na jirani muovu

Na jirani bila kujali ni muislam au siyo muislam ana haki zake mbele ya muislam, Muislam yeyote haruhusiwi kumfanyia uadui jirani yake bila kujali Iman.

Hivyo ukimfanyia ubaya mtu asie kua musilam hali ya kua yeye hajakufanyia ubaya basi utahesabiwa umetenda dhambi.
ila asie Amini Mungu ni mmoja hakuzaa wala hakuzaliwa, na akaamkaamini ktika miungu watatu au vinginevyo huyo atahesabika kama KAFIRI na tutamuombea ili siku moja atoke katika huo Ukafiri.
Vile mwafrika alivyokuwa brainwashed..inashangaza sana.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaona unapofeli hapo?! Kwahiyo Al Shabaab kusema waliyosema kwako ndo reference ya kufanya conclusion?!

Hebu twende taratibu! Kwanza kabisa neno Jihad ambako umewatoa hao uliowaita Jihadists, ni neno ambalo limekuwa corrupted sana kiasi kwamba wengi mnaamini Jihad is nothing but war! Lakini hata tukichukua hiyo tafsiri yenu mnayoipenda sana, hebu tuangalie aya zinazotumiwa sana na hao mnaowaita Jihadists!!

QURAN 2:190 inasema:-

Na 191 Inasema:-

Na 192 inasema:-

Na mwisho inasema:-



Kwanza kabisa, kuzielewa hizo aya ni lazima uwe umesoma au uwe na mwanga wa theology tofauti na wengi wenu mnavyoingia tu Google na kuokoteza aya halafu eti ndo mnajiona mnaijua Quran...

...Yaani Quran ile ile ambayo watu wanatumia miaka na miaka kuisoma, watu mnaielewa ndani ya dakika 1... you guys are geniuses!

Lakini pamoja na umuhimu wa teolojia ili uweze kuelewa msingi wa aya za Quran na hata zile za Bible, lakini hebu zisome kwa makini hizo sehemu zilizo-highlight!

Piganeni na wale WANAOKUPIGENI, na wala MSIVUKE MIPAKA!

Hivi hapo unapata picha gani? Ni kwamba Waislamu wameambiwa Wabebe silaha wakaue watu wasio wa imani yao au wameambiwa WAKIWAANZA, FIGHT BACK?!

Hivi kwenye hayo mataifa ya Kikristo, WAKIANZA KUPIGWA, ina maana hawapigani? Kama hawa-fight back, unaweza ku-declare hapa kwamba Crusade ilikuwa UNHOLY War?


Na hapa wala sitaki kuwa mnafiki... Ukiacha wale Waarabu wala neema kule Gulf Countries, Waislam duniani kote akili zetu tunazijua wenyewe!! Huwa hawataki ujinga!!

Hata ukikaa chini ukapiag mahesabu tawala zilizowahi kufurumishwa madarakani just kwa watu kuingia barabarani tu... utakuta nchi zenye Waislamu wengi ndo zinaongoza!! Hata kule West Africa ambako ukizingua tu watu wanakupandia na mashine huko huko Ikulu, nyingi ni zile zenye waislamu wengi!

Hata hawa ma-CCM yanayotusumbua ni kwa sababu yanajua kuna akina Chaliifrancisco wengi ambao Mzungu ili kuhakikisha anakula neema za Afrika bila wenge, akawaambia Bwana Kasema "Mtu akikutandika kofi mkono wa kushoto, mgeuzie na la kulia..." (Don't mind, hii ni furahisha genge tu)

But look CCM Zanzibar wanavyoikumbatia bara... wale wanajua kabisa CCM Bara wakisema "sasa kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake katika kutafuta utawala", huo utakuwa ndio mwisho wa CCM ZNZ!

Mtasema sana... hamjasoma, vibarakashia, sijui kunywa kahawa vibarazani, lakini UJINGA KWETU, NOI!

Tuache hayo "mazungumzo baada ya habari"

Sasa ni kwanini nilisema kuzielewa hizo aya ni lazima uwe na mwanga wa teolojia!

Unlike Moses and Jesus, Muhamad aliitangaza imani yake kwa taabu kweli kweli! Yeye na wafuasi wake ilikuwa mara kwa mara wanashambuliwa na hata kuuawa! Wakati mwingine mateso waliyokuwa wanayapata yalikuwa yanatoka kwa watu wa ukoo wake mwenyewe!

Mambo yalipozidi kuwa magumu, ikabidi Muhammad na Wafuasi wake watoroke Makkha usiku usiku na kukimbilia Madina!! Lakini wakati wote huo, ilikuwa wakishambuliwa, jamaa hawajibu mapigo na wakabaki kumlilia Mwenyezi Mungu awanusuru na madhira waliyokuwa wanakutana nayo!

Kutokana na hayo, ndipo zikashuka hizo aya kuwaambia "Acheni uf'ala nyie , wakiwapiga, fight back! Wakiwaua, nanyi ueni! Kama waliwatoa sehemu zenu, fight hard kukomboa hizo sehemu"

Sasa je, hao Magaidi ambao mnapenda sana kuwatumia kama reference, ndivyo wanavyofanya?! Kule Msumbiji walikoenda kuua watu, unaamini kabisa actions zao zinaendana na hizo aya?! Wale wauaji wanaojiita Boko Haram, hivi kabla hawajaanza ule unyama wao ulishawahi kusikia Waislamu Nigeria wamepigwa na Wakristo hatimae Boko Haram wakapata uhalali wa ku-fight back

Na kabla hujaanza kulalamika kuhusu neno kafiri lililotumika hapo, nikujuze tu kwamba Kafiri sio TUSI na wala sio NENO LA KASHFA kama ambavyo mnadhanii! KAFIRI NI MTU ASIYEAMINI UNACHOKIAMINI! Hata Mwislamu ni KAFIRI mbele ya jicho la Mkristo! Hata kwenye Bible hilo neno limetumika sana!!!

Lakini hata ukija kwenye kamusi,
View attachment 2096949
Hiyo ni kamusi ya Kizungu ambayo kuna 90% imeandikwa na Christians! Wao wanakuambia:-

Kwa Mkristo: Kafiri ni yule asiyeamini, especially MUSLIM, wakati kwa Waislam, Kafiri asiyeamini katika Uislamu bila kujali kama ni Mkristo, Pagan, Myahudi or anyone!!

Merriam Dictionary nao:-
View attachment 2096953

Hilo nimeamua kuweka wazi mapema kwa sababu wangekuja wengine hapa wakaanza kutoa mapovu kwa sababu tu aya ya 191 imetaja Makafiri! Tena nadhani ukifahamu maana ya Kafiri basi Mkristo ataona fahari kuitwa Kafiri na Mwislamu! Kwanini asione fahari kuambiwa anaamini Yesu alikufa na kufufuka? Kwanini asione fahari kuaambiwa haamani Quran?!
umeupiga mwingii umeelezea kwa kina sanaa [emoji3059][emoji3059]
 
Habari zenu wakuu, rafiki yangu wa mafia ananiambia hivi.

Mimi nimezaliwa na kukulia kisiwani mafia, shuleni kwetu tangia naanza darasa la awali mpaka namaliza darasa la saba, hapakuwahi kuwa na mwanafunzi mkristo, sote tuliwa wa imani ya uislamu. Aliwahi kuja mwalimu mmoja wa imani ya ukristo lakini hakukaa sana akaondoka.

Kwa ufupi sisi tangu utotoni katika ukuaji wetu tulifundishwa kwa msisitizo sana kuwa mtu ambaye si wa imani yetu, huyo mtu haifai hata kumsogelea kwa namna yoyote ile, mtu ambaye si muislamu ni sawa au ni zaidi ya nguruwe au mbwa. Mara kadhaa walipokuja watalii wa kizungu, hao ndiyo tuliaminishwa kabisa ni watu wanaopigana na Mungu anayetupatia uwezo wa kuishi. Alipopita mzungu tulikuwa tukitema mate kwa nyuma kuashiria ni kitu ambacho hata kukiona ni dhambi.

Mimi nilipomaliza darasa la saba nilitafutiwa uhamisho na nikahamia Vikindu, na hapo nilianza kidato cha kwanza. Kwakweli niliteseka sana siku za mwanzo pale shuleni, maana nyumbani Mafia nilifundishwa kuwa mtu asiye wa imani yangu ni haramu na haitakiwi hata nimsogelee.

Darasani nilipangwa dawati moja na mkristo, aliyeitwa Yohana Frank, kwakweli nilikaa naye kwa taabu sana nikiamini kukaa dawati moja na yeye natenda madhambi na nitaikosa pepo. Baada ya kuzoea mazingira ya shuleni nilipata rafiki wa imani yangu aliyeitwa Omari.

Cha kusikitisha huyo Omari alikuwa na marafiki wa imani ya kikristo, na walikuwa wakigawana vyakula pale shuleni. Mimi kwa mazingira niliyokulia na mafundisho niliyofundishwa tangu utotoni nilikuwa na wakati mgumu sana pale shuleni. Watu nilioaminishwa ni haramu na haitakiwi hata kuwasogelea, iweje leo nikae nao meza moja na kula pamoja nao?

Kwakweli nilikuwa nikijiuliza maswali mengi sana, na nikaanza kuyafikiria upya mafundisho yote niliyofundishwa tangu utotoni ikiwa yana mantiki au la! Nilianza kuifikiria imani yangu yote kwa ujumla. Mpaka leo nimeanza kufikiria kama kweli Mungu yupo? Huyu Mungu niliyefundishwa tangu utotoni yupo? na vipi kuhusu hawa miungu wa imani nyingine tofauti na imani yangu?
huu ndio ukweli mchungu: katika baadhi ya maeneo ya imani hiyo anayoiongelea wanaamini kuwa maovu yote yanafanywa na wasio na imanai yao. Wanaaminini kuwa wao ni wasaafi - hii ndiyo ajabu yenyewe
 
Habari zenu wakuu, rafiki yangu wa mafia ananiambia hivi.

Mimi nimezaliwa na kukulia kisiwani mafia, shuleni kwetu tangia naanza darasa la awali mpaka namaliza darasa la saba, hapakuwahi kuwa na mwanafunzi mkristo, sote tuliwa wa imani ya uislamu. Aliwahi kuja mwalimu mmoja wa imani ya ukristo lakini hakukaa sana akaondoka.

Kwa ufupi sisi tangu utotoni katika ukuaji wetu tulifundishwa kwa msisitizo sana kuwa mtu ambaye si wa imani yetu, huyo mtu haifai hata kumsogelea kwa namna yoyote ile, mtu ambaye si muislamu ni sawa au ni zaidi ya nguruwe au mbwa. Mara kadhaa walipokuja watalii wa kizungu, hao ndiyo tuliaminishwa kabisa ni watu wanaopigana na Mungu anayetupatia uwezo wa kuishi. Alipopita mzungu tulikuwa tukitema mate kwa nyuma kuashiria ni kitu ambacho hata kukiona ni dhambi.

Mimi nilipomaliza darasa la saba nilitafutiwa uhamisho na nikahamia Vikindu, na hapo nilianza kidato cha kwanza. Kwakweli niliteseka sana siku za mwanzo pale shuleni, maana nyumbani Mafia nilifundishwa kuwa mtu asiye wa imani yangu ni haramu na haitakiwi hata nimsogelee.

Darasani nilipangwa dawati moja na mkristo, aliyeitwa Yohana Frank, kwakweli nilikaa naye kwa taabu sana nikiamini kukaa dawati moja na yeye natenda madhambi na nitaikosa pepo. Baada ya kuzoea mazingira ya shuleni nilipata rafiki wa imani yangu aliyeitwa Omari.

Cha kusikitisha huyo Omari alikuwa na marafiki wa imani ya kikristo, na walikuwa wakigawana vyakula pale shuleni. Mimi kwa mazingira niliyokulia na mafundisho niliyofundishwa tangu utotoni nilikuwa na wakati mgumu sana pale shuleni. Watu nilioaminishwa ni haramu na haitakiwi hata kuwasogelea, iweje leo nikae nao meza moja na kula pamoja nao?

Kwakweli nilikuwa nikijiuliza maswali mengi sana, na nikaanza kuyafikiria upya mafundisho yote niliyofundishwa tangu utotoni ikiwa yana mantiki au la! Nilianza kuifikiria imani yangu yote kwa ujumla. Mpaka leo nimeanza kufikiria kama kweli Mungu yupo? Huyu Mungu niliyefundishwa tangu utotoni yupo? na vipi kuhusu hawa miungu wa imani nyingine tofauti na imani yangu?

Tafuta Kanisa zuri karibu yako; wakristo wanafundishwa Upendo, Ila usiende Kwa Manabii Na wapiga ramli
 
Huyo mleta mada ama nae ni MUONGO au ni mtu kutoka vijijini, na wala asiseme "kwetu Mafia tunafundishwa...." bali aseme "kwenye familia yao wanafundishwa..."
Sawa, lakini "dini" haifundishwi kwenye familia pekee, naamini yukosahihi 100%
 
Sawa, lakini "dini" haifundishwi kwenye familia pekee, naamini yukosahihi 100%
Yuko sahihi fundisho lipi?

1. Kwamba Uislamu unakataza Mwislamu kukaa karibu na Mkristo kwa sababu Mkristo ni zaidi ya nguruwe au mbwa,

2. Au yupo sahihi kwamba Ukristo unakataza kukataza karibu na Mwislamu kwa sababu utapata majini, au

3. Ay yupo sahihi kwa yote hayo?
 
Nimejisikia vizuri sana aliposema ameanza kufikiria ikiwa kweli Mungu yupo?

Bila shaka hivi karibuni atatambua Mungu wa imani yake hayupo, wala Miungu wa imani nyingine tofauti na imani yake hawapo.
Namtakia kila la kheri.
Mbona unajijibu mwenyewe? Umesahau kuswitch id siyo
 
Yuko sahihi fundisho lipi?

1. Kwamba Uislamu unakataza Mwislamu kukaa karibu na Mkristo kwa sababu Mkristo ni zaidi ya nguruwe au mbwa,

2. Au yupo sahihi kwamba Ukristo unakataza kukataza karibu na Mwislamu kwa sababu utapata majini, au

3. Ay yupo sahihi kwa yote hayo?
Na.2 na 3 umetengeneza ya kwako, huenda unauelewa juu ya hayo.
Na 1 ndicho alichosema: harafu unajua na unajifanya hujui, poor you.
 
Upo sahihi sana Mkuu ,hakuna dini inayofundisha kumchukia jirani yako haijalishi tofauti ya imani yake bali aya mambo yametokea sababu ya mitazamo ya wanazuoni mbalimbali katika kuendelea ku exist

Wakristo tulikuwa na mitazamo tofauti kwa waislamu katika kuonyesha sisi ni bora zaidi yao ndio maana kulikuwa na kejeli mbalimbali mfano: tulikuwa tunasema waislamu hawali nguruwe sababu mt.Muhamad maiti yake ililiwa na nguruwe na kwavile tulikuwa watoto tuliami kabisa

Pia kwa upande wa waislamu ni ivyo ivyo, hasa miaka ile 90's ya mihadhara kulikuwa na upinzani mkubwa sana ,Mimi binafsi nimeshawai kubaguliwa sababu ni mkristo jamii tuliyokuwa tunaishi ni mchanganyiko maeneo ya Temeke, sasa nilikuwa na rafiki yangu mmoja anaitwa Rajabu ambae ni muislamu tulikuwa tunasoma wote primary siku moja tunarudi home tukapita karibu na chuo chao madrasa ndipo tukakutana na kundi la watoto wenzake wa chuo ,wakaanza kumuuliza Rajabu rafiki yako anaitwa nani ,akawa kama anasita kujibu ndipo mimi nikaropoka jina la kikristo hauwezi amini (labda kwavile tulikuwa watoto) pale pale walianza kumwambia Rajabu kwanini anakuwa na rafiki mkristo kafiri na maneno mengine mengi siyakumbuki ,nilijisikia vibaya sana ingawa rafiki yangu Rajabu aliniambia niachane nao baada ya kutoka pale

Hivyo ni visa vichache katika jamii zetu, ingawa tuliishi vizuri mpaka Leo bila ubaguzi wowote kwenye sikukuu zetu tunaleteana mapilau mfano kwa upande wetu wakristo ikifika sikukuu zetu tunatafuta muislamu atuchinjie kuku ili iwe rahisi kwetu kuwapelekea vyakula ivyo

Rajabu mpaka Leo ni rafiki yangu na tumeshakuwa wakubwa ingawa sasa ivi tupo mikoa tofauti katika kutafuta maisha
 
Unaona unapofeli hapo?! Kwahiyo Al Shabaab kusema waliyosema kwako ndo reference ya kufanya conclusion?!

Hebu twende taratibu! Kwanza kabisa neno Jihad ambako umewatoa hao uliowaita Jihadists, ni neno ambalo limekuwa corrupted sana kiasi kwamba wengi mnaamini Jihad is nothing but war! Lakini hata tukichukua hiyo tafsiri yenu mnayoipenda sana, hebu tuangalie aya zinazotumiwa sana na hao mnaowaita Jihadists!!

QURAN 2:190 inasema:-

Na 191 Inasema:-

Na 192 inasema:-

Na mwisho inasema:-



Kwanza kabisa, kuzielewa hizo aya ni lazima uwe umesoma au uwe na mwanga wa theology tofauti na wengi wenu mnavyoingia tu Google na kuokoteza aya halafu eti ndo mnajiona mnaijua Quran...

...Yaani Quran ile ile ambayo watu wanatumia miaka na miaka kuisoma, watu mnaielewa ndani ya dakika 1... you guys are geniuses!

Lakini pamoja na umuhimu wa teolojia ili uweze kuelewa msingi wa aya za Quran na hata zile za Bible, lakini hebu zisome kwa makini hizo sehemu zilizo-highlight!

Piganeni na wale WANAOKUPIGENI, na wala MSIVUKE MIPAKA!

Hivi hapo unapata picha gani? Ni kwamba Waislamu wameambiwa Wabebe silaha wakaue watu wasio wa imani yao au wameambiwa WAKIWAANZA, FIGHT BACK?!

Hivi kwenye hayo mataifa ya Kikristo, WAKIANZA KUPIGWA, ina maana hawapigani? Kama hawa-fight back, unaweza ku-declare hapa kwamba Crusade ilikuwa UNHOLY War?


Na hapa wala sitaki kuwa mnafiki... Ukiacha wale Waarabu wala neema kule Gulf Countries, Waislam duniani kote akili zetu tunazijua wenyewe!! Huwa hawataki ujinga!!

Hata ukikaa chini ukapiag mahesabu tawala zilizowahi kufurumishwa madarakani just kwa watu kuingia barabarani tu... utakuta nchi zenye Waislamu wengi ndo zinaongoza!! Hata kule West Africa ambako ukizingua tu watu wanakupandia na mashine huko huko Ikulu, nyingi ni zile zenye waislamu wengi!

Hata hawa ma-CCM yanayotusumbua ni kwa sababu yanajua kuna akina Chaliifrancisco wengi ambao Mzungu ili kuhakikisha anakula neema za Afrika bila wenge, akawaambia Bwana Kasema "Mtu akikutandika kofi mkono wa kushoto, mgeuzie na la kulia..." (Don't mind, hii ni furahisha genge tu)

But look CCM Zanzibar wanavyoikumbatia bara... wale wanajua kabisa CCM Bara wakisema "sasa kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake katika kutafuta utawala", huo utakuwa ndio mwisho wa CCM ZNZ!

Mtasema sana... hamjasoma, vibarakashia, sijui kunywa kahawa vibarazani, lakini UJINGA KWETU, NOI!

Tuache hayo "mazungumzo baada ya habari"

Sasa ni kwanini nilisema kuzielewa hizo aya ni lazima uwe na mwanga wa teolojia!

Unlike Moses and Jesus, Muhamad aliitangaza imani yake kwa taabu kweli kweli! Yeye na wafuasi wake ilikuwa mara kwa mara wanashambuliwa na hata kuuawa! Wakati mwingine mateso waliyokuwa wanayapata yalikuwa yanatoka kwa watu wa ukoo wake mwenyewe!

Mambo yalipozidi kuwa magumu, ikabidi Muhammad na Wafuasi wake watoroke Makkha usiku usiku na kukimbilia Madina!! Lakini wakati wote huo, ilikuwa wakishambuliwa, jamaa hawajibu mapigo na wakabaki kumlilia Mwenyezi Mungu awanusuru na madhira waliyokuwa wanakutana nayo!

Kutokana na hayo, ndipo zikashuka hizo aya kuwaambia "Acheni uf'ala nyie , wakiwapiga, fight back! Wakiwaua, nanyi ueni! Kama waliwatoa sehemu zenu, fight hard kukomboa hizo sehemu"

Sasa je, hao Magaidi ambao mnapenda sana kuwatumia kama reference, ndivyo wanavyofanya?! Kule Msumbiji walikoenda kuua watu, unaamini kabisa actions zao zinaendana na hizo aya?! Wale wauaji wanaojiita Boko Haram, hivi kabla hawajaanza ule unyama wao ulishawahi kusikia Waislamu Nigeria wamepigwa na Wakristo hatimae Boko Haram wakapata uhalali wa ku-fight back

Na kabla hujaanza kulalamika kuhusu neno kafiri lililotumika hapo, nikujuze tu kwamba Kafiri sio TUSI na wala sio NENO LA KASHFA kama ambavyo mnadhanii! KAFIRI NI MTU ASIYEAMINI UNACHOKIAMINI! Hata Mwislamu ni KAFIRI mbele ya jicho la Mkristo! Hata kwenye Bible hilo neno limetumika sana!!!

Lakini hata ukija kwenye kamusi,
View attachment 2096949
Hiyo ni kamusi ya Kizungu ambayo kuna 90% imeandikwa na Christians! Wao wanakuambia:-

Kwa Mkristo: Kafiri ni yule asiyeamini, especially MUSLIM, wakati kwa Waislam, Kafiri asiyeamini katika Uislamu bila kujali kama ni Mkristo, Pagan, Myahudi or anyone!!

Merriam Dictionary nao:-
View attachment 2096953

Hilo nimeamua kuweka wazi mapema kwa sababu wangekuja wengine hapa wakaanza kutoa mapovu kwa sababu tu aya ya 191 imetaja Makafiri! Tena nadhani ukifahamu maana ya Kafiri basi Mkristo ataona fahari kuitwa Kafiri na Mwislamu! Kwanini asione fahari kuambiwa anaamini Yesu alikufa na kufufuka? Kwanini asione fahari kuaambiwa haamani Quran?!
Wape elimu hao wasioujua Uislamu ni nini?

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Na.2 na 3 umetengeneza ya kwako, huenda unauelewa juu ya hayo.
Na 1 ndicho alichosema: harafu unajua na unajifanya hujui, poor you.
Eti ndicho ulichosema...

Usichojua ni kwamba Post #2 kai-edit na akafuta aliposema Wakristo wanafundishwa wasikae na Waislamu kwa sababu watapata majini!

Na kama ndivyo alivyosema, ilikuaje anijibu:-
Imani za ukristo na uislamu wote wanafundisha chuki dhidi ya wenzao, ni vile tu kila dini inafundisha chuki kwa aina yake.
aise,

How come umefuta post yako ulipoandika habari za Wakristo kufundisha watoto wao kwamba wasikae na Waislamu kwa sababu watapata majini? Mbona umefuta simulizi za rafiki yako Swaumu na kwamba ukawa unahisi vyote vina majini?

NI kwamba ulidanganya sio?

Wewe unayejiita Gama siwezi kukushangaa kwa sababu nilishawahi kukutana na wewe kwenye mjadala mmoja uliokuwa unatetea mauaji ya Rohingya na bila aibu ukasema kwanza hao Waislamu wa Rohingya kule Myanmar sio kwao, wamefuata nini!!

Nilipokuambia wewe mwenyewe kwa hilo jina utakuwa Mngoni, na Wangoni Tanzania wamekuja tu kutoka SA, je itakuwa sahihi tukianza mauaji dhidi ya Wangoni... ukakimbia, na hukurudi tena!

Na kama wewe ni Mkristo kweli, utakubali angalau nafsini mwako kama utaona aibu kukiri hadharani kwamba nilichosema hapo juu ni KWELI KWA 100%!

Nimekukumbusha hayo ili kukuambia ACHA CHUKI!!!
 
NI kwamba ulidanganya sio?

Wewe unayejiita Gama siwezi kukushangaa kwa sababu nilishawahi kukutana na wewe kwenye mjadala mmoja uliokuwa unatetea mauaji ya Rohingya na bila aibu ukasema kwanza hao Waislamu wa Rohingya kule Myanmar sio kwao, wamefuata nini
Inawezekana wewe hupenda kunukuu na hujibidishi kubeba meaning ya content
 
Haya mambo yapo sana kuna Mwalimu wangu mmoja kwenye miaka ya mwanzoni mwa 2000 alipangiwa kazi huko Mbozi ndani ndani. Anafika kwenye huo mji yeye pekee ndio alikua Muislamu, kutokana na maelezo yake watu walikua wanamshangaa.

Kuna siku jioni yupo kwake akaja mzee mmoja na kumuuliza "Kijana nasikia wewe ni Muislamu". Jamaa akajibu "Ndio mzee mimi ni Muislamu". Mzee akauliza tena "Mbona upo kama sisi tu, hauna tofauti yoyote kabisa? Kwa maana tumekua tukiambiwa waislam sio watu kama sisi, wana manyoya mwili mzima na ni watu hatari sana". Ticha alibaki kushangaa tu.


Kutokana na mahali ulipozaliwa na kukulia unaweza kujikuta na mtazamo wa ajabu sana kuhusu watu wa jamii nyingine.
 
Inawezekana wewe hupenda kunukuu na hujibidishi kubeba meaning ya content
NImekuuliza, unafahamu kwanini alisema dini zote zinafundisha chuki?!

Use your common sense kijana! Wewe umeukutia uzi ukiwa na posts kadhaa wakati mimi nimeukuta ukiwa bado page ya kwanza! Unaona sina akili hadi nizungumzie kitu ambacho hakuandika?

Au angalia post yangu #11 yenye sehemu inayosema:-
Au tuseme katika maisha yako hujawahi kukaa na Mwislamu?! Inawezekana hivyo? Au ukigundua tu kwamba Mwislamu unamkimbia kwavile ulifundishwa (according to mtoa mada ambae umeamua kumwamini) ukikaa na Mwislamu utapata majini?!
Umeiona hiyo blacket?! Inakupa ishara gani?! Na ili usidhani kama nime-edit, angalia post #12 ambayo Khantwe alini-quote, na utaiona hiyo bracket! Unataka kusema sina akili hadi nikasema according to mtoa mada!

Na ndo hivi sasa naanza kumwelewa Khantwe kwanini alinihoji "Ni kitabu cha dini gani kimeandikwa kuwa watoto wao wakikaa na waislamu wanapata majini?"

Inawezekana nae alikuta jamaa kesha-edit sehemu ambayo jamaa aliandika "Kuna dini inafundisha watoto wao wasikae na Waislamu kwa sababu watapata majini"!!

Ni kutokana na hicho kipengele ndo maana post from my quote above niliweka bracket na kusema "according to mtoa mada..."!

Mwambie aise kama ana ujasiri aje hapa akatae kwamba hakuzungumzia suala la dini zingine kufundisha watoto wao wasikae na Waislamu ili wasije wakapata majini! Kama alivyoleta simulizi za Yohana, hapo akaleta simulizi za rafiki yake aliyekuwa anaitwa Swaumu!!!
 
Kiukweli Mafia mnayoisema mie siielewi ni ya wapi? Mie ni mkristo na nilipoenda mafia sikutegemea hata kitimoto ningeikuta Ila wazee Kuna pub na jamaa anatengeneza mbuzi katoliki safi sana na Kuna mangi mmoja anachoma mbuzi safi kabisa pale Mafia.

Haya mengine ni maneno ya kipuuzi ubaguzi huwa unakuwepo tu sababu ya kutozoea aina fulani ya maisha hata jamii ya kikristu huwabagua wengine sababu wanakuwa na Ile cultural shock ni Jambo la kawaida ambapo baada ya muda unakuja kuzoea tu.

Huu mchanganyiko wa jamii ndio husababisha watu kuzoeana na kuchukuliana na kuheshimiana Kama jamii iliyostaarabika ndio maana mzungu alipokuja alipewa maeneo na akakaribishwa akae wakajiweka kwenye maeneo yao kwa kuwa wenyeji wakiona Kama life ya wazungu ni tofauti.

Hata wahindi walipokuja nao walijitenga maeneo yao ya uhindini na wao kwa wao walijitenga unakuta wabohora Wana mtaa wao, jamatii Wana mtaa wao, waishamilia Wana mtaa wao, wasunni hivyohivyo basi ni ilikuwa wanaishi sababu ya kutozoea imani na maisha ya kila mwenzie.

Ila Mafia nguruwe nyama ipo Safi anayebisha aseme so huo ubaguzi wa kidini sijui na kama upo basi wa kawaida kwa familia na familia usigeneralize sheikh.
 
baada ya kumchunguza mtoa maada nimeona kuwa

YEYE SIO MUISLAM NA HAKUWAHI KUWA MUISLAM HATA SEKUNDE MOJA,
WALA SIO MKRISTO.
NI KAFIRI LILILOAMUA KUCHAFUA MAZINGIRA YA WATU, ILI WATU WAPIGISHANE MAKELELE.
VIZURI KULIPUUZA KAFIRI HILI LISILOKUWA NA NINI YOYOTE.
JAAHILI
 
Mkuu kubali ukatae ni kwasababu tu kuna sheria za nchi la sivyo ungeshuhudia mambo ya ajabu sana. Angalia mfano jihadists mafundisho yao ambayo wanafundisha vijana.

Reference ya karibu kabisa angalia lile tukio la West Gate Nairobi. Wale jamaa walikuwa wakikukuta wanakuambia recite shahadah (kwamba unamkiri Allah na unamtambua Mohamed kuwa ni mtume wa Allah) na kama hujui ulikuwa unakula risasi.

Sasa imagine kungekuwa hakuna hizo sheria za nchi zinazozuia mauaji unadhani watu ambao hawaamini Islam wangepona?
Kwani huko Nairobi/Kenya hawana sheria za nchi? Kama wanayo unafikiri kuwa na sheria ndo kunazuia kutokea mambo ya ajabu. Ugaidi unatumia mwamvuli wa dini kupandikiza chuki tu kwa interest za watu wachache.
Chuki inaweza kupandikizwa hata kwa makundi mbalimbali iwe ya kisiasa au jamii ya watu flani dhidi ya jamii nyingine au chama kingine na chuki siku zote huleta machafuko rejea hata vita vya rwanda.
Hivyo kitu chochote kinachoenezwa au kutangazwa kwa chuki nicha kuwanacho makini. Naamini Maandiko yote Matakatifu yanisisitiza upendo kama msingi mkuu wa maisha.
N.b Lengo la huyu mleta mada nayo ni kuleta na kuchochea chuki ya kidini
 
Back
Top Bottom