Kisa cha Shariff Abdallah Attas na mwalimu Julius Nyerere ofisi ya TANU baada ya uhuru

Mzee Mohamed Said umenifunza mengi juu ya historia yetu. Labda sijapekua sana lakini ningependa kujua historia yako pia.
 
Bukyanagandi,
Mzee Chihota
alikuwa Meneja wa Arnatouglo Hall nadhani alipotoka yeye
ndiye akaja Denis Phombeah, Mnyasa.

Mzee Chihota alikwenda masomoni Uingereza na huko mauti yakamfika na
alizikwa huko huko.

Hii ilikuwa miaka ya mwanzoni 1950s.
Kuna mtaa Temeke unaitwa, ''Chihota,'' kwa heshima yake.

Kulikuwa na Norman Chihota bingwa wa 100 metres na Raymond kaka
yake.

Hawa walitoka Rhodesia.

Gershom Chihota nilisomanae St. Joseph's School na tukicheza mpira sote
na kupiga muziki yeye akipiga bass guitar.

Baada ya uhuru kupatikana walirudi kwao na huko Raymond alifariki.
Huyu alisoma Urusi na alioa Mrusi.

Raymond alipomaliza shule Aga Khan alifanyakazi TBC kama mtangazaji na
allikuwa na kipindi, ''Teenagers Time,'' akipiga pop music akina Cliff Richard,
Helen Shapiro, Elvis Presly, Beatles, Rolling Stones etc.

Ray kama alivyokuwa akijulikana alikuwa mmoja wa ''Chipukizi,'' na akina Henin
Seif, Abdul Nanji, Badrin,
Salum Hirizi, Yusuf Ramia, Hussein Shebe, Cuthbert Sabuni,
Sauda Mohamed, Maryam Zialor
na vijana wengi wa Dar es Salaam.

Salim Hirizi akijulikana kama Sammy Davis.

Ray alikuwa mwimbaji mzuri wa nyimbo za Kizungu na Chipukizi na yeye kwa
msaada wa David Wakati wakaanzisha kipindi RTD, ''Chipukizi Club.''


Kulia Raymond Chihota, Henin Seif, Hussein Shebe
Nyuma ya Hussein Shebe Mbaraka Bata, Nyuma ya Henin Seif Hussein


Kipindi hiki kilipendwa sana na vijana hadi pale kilipokuja kupigwa marufuku na
Regiional Commissioner wa Dar es Salaam, Mustafa Songambele kwa sabau ati
kinatukuza utamaduni wa nje.

Songambele hakupendezewa na zile nyimbo za Kizungu bendi ile ya Chipukizi
walizokuwa wakipiga.

Chipukizi walikuwa wakipiga pamoja na vijana wa Kigoa wakijiita ''The Blue Diamonds.''
Walikuwa na wapiga magitaa hodari sana.

Hii ilikuwa 1963/64.

Ray
na Yusuf Baruti wakaenda kusoma Urusi na ''members,'' wengi wa Chipukizi wakaondoka kwenda
nje.

Hussein Shebe akaenda Nairobi kujiunga na Ashantis kama muimbaji na kwa kweli
aliipaisha ile bendi na hawakukaa sana Nairobi wakenda Addis Ababa wakawa
wanapiga Wabe Shebelle Hotel, hotel kubwa sana wakati ule.

Sal Davis ndiye aliyemchukua Hussein kumpeleka Nairobi.

Sal alikuja Dar es Salaam na alifanya show moja na Chipukizi Radio Tanzania na hapo
ndipo alipomsikia Hussein akiimba.

Badrin na Nanji wao walikwenda America.

Sabuni na bendi yake, ''The Flaming Stars,'' akiwa na Peter Kondowe (Peco) na
George Mzinga wao wakaenda Mombasa.

Miaka mingi baadae nilifika Addis Ababa na nilikaa Wabe Shebelle lakini hoteli ilikuwa
taaban, imechoka.

Nakumbuka nililetewa Coke lakini sikuweza kuitambua chupa jinsi ilivyokuwa imesagika.

Hii ilikuwa 1989 enzi ya Mengitsu Haile Mariam na Hussein Shebe na Ashanti
wamekimbia wanapiga muziki wao Italy.

Nakumbuka Ray aliporudi alikaribishwa Radio Tanzania English Service kwa mahojiano
katika kipindi cha muziki.

katika nyimbo alizochagua apigiwe moja naikumbuka kwa kuwa nami nikiipenda,
''Let The Good Times Roll,'' ya Ray Charles.

Mwaka wa 1993 nilikwenda Harare na nilimtafuta Gershom na Norman na bahati
nzuri nilikutananao.

Nina picha nikizipata nitaziweka hapa In Shaallah.

Baada ya miaka mingi sana nilikutana na Hussein Shebe kwenye boat tunakuja Dar es
Salaam kutoka Zanzibar nilikuwa na rafiki yangu Tamim Faraj.

Tulikumbusha mengi na akanipa cassette yake na Ashanti.

Hivi sasa Hussein amepumzika muziki na akiwa na nafasi hupita nyumbani kwangu
kunijulia hali kila anapokuja kutoka Zurich anakoishi na mkewe Mswiss na wanae na kila
siku ananikaribisha Switzerland.

Ingia You Tube ustaladhi na muziki wa Hussein Shebe.

Katika mahojiano nliyofanya na Hussein ananambia kuwa siku alipomwabia Meneja wake
kuwa yeye muziki basi alishtuka na akambembeleza sana.

Hussein hajatazama nyuma.
Mke wake anasema, ''Huyu Hussein toka amerudi kwenye Uislam wake...''

Siku moja nafanya mahojiano na Hussein.
Ghafla ananyanyuka ananambia, ''Mohamed Maghrib sasa tuswali kwanza...''

Machozi yalinilengalenga...
Tulikuwa nyumbani kwa rafiki yake toka udogo wao - Henin Seif.

Kakutana na mke wangu msikitini Maamur anamwambia, ''Mohamed si rafiki
yangu ni ndugu yangu...''

Ingia hapo chini kuangalia picha:
Mohamed Said: KUTOKA JF: CHIPUKIZI CLUB WATOTO WA MJINI DAR ES SALAAM 1964
 
Mzee wangu Mohamed nimekunyooshea mikono.
Ila changamoto iliyoko Sasa, kadiri unavyojitahidi kuwaelewesha vijana juu ya Historia ya Tanzania na vijana wa wakati huo, hawataki kabisa kukuelewa.

Unatoa hadi ushahidi wa picha lakini hawataki kuelewa.

Lakini siku moja mzee wangu utakumbukwa sana sana.

Mungu akujalie mapenzi yake na rehema zake.
 
Nkuba25,
Allahuma Amin.
 
Mzee Mohamed Said umenifunza mengi juu ya historia yetu. Labda sijapekua sana lakini ningependa kujua historia yako pia.
Window7,
Mie nitakuwa na historia gani ya maana hadi mtu atake kuisoma kaka.
Mimi ni mtu wa Dar es Salaam ndiko nilikozaliwa.

Sina mambo muhimu kaka tupo tupo tu.
Nikifanya kazi bandarini sasa nimestaafu naishi Magomeni Mapipa.
 
Maneno meeengi...hayana maana...nyie waandishi ndio magufuli hawataki...
Mnoel,
Mtu wa maana nitakuwa mie kaka?
Mbona unauliza jibu?

Shukuru Mungu wewe kakupa akili pevu ukawa na uwezo wa kusoma kitu
ukakichambua ukajua kama hiki cha maana na huu upuuzi.

Si kila mtu kajaaliwa kama wewe ndugu yangu.
Nistahamile ndugu yangu hivyo hivyo,
 

Wanamajlis na Mnoel,
Asubuhi hii wakati napitapita katika maktaba yangu nimekutana na nyaraka
hiyo hapo chini ya TAA ya mwaka wa 1953:



Hapo chini ni picha ya Dome Okochi Budohi mmoja wa viongozi wa TAA ambae sahihi yake
ipo kwenye hiyo nyaraka hapo juu:



Katika kitabu changu ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1928) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism'' London 1998, ambacho kilikuja kufasiriwa na kuitwa ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes Historia iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza'' Nairobi 2002 nimeandika maneno hayo hapo chini kuhusu Dome Budohi:

''Familia yangu ilifahamiana na Dome Budohi, mmoja wa wanaharakati kutoka Kenya. Wakati ule wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika alikuwa akiishi Dar es Salaam. Budohi alikuwa mmoja wa wazalendo walioasisi TANU na kadi yake ya uanachama ni nambari sita aliyopewa Julai 1954. Mwaka 1955 alikamatwa na serikali ya kikoloni kwa tuhuma ya kuwa mmoja wa askari wa Mau Mau harakati za wazalendo takriban wengi wao wakulima wadogo waliokuwa wakipigana na ukoloni wa Waingereza nchini Kenya. Ninazo kumbukumbu nyingi za utoto nikimtembelea Budohi ndani ya selo yake Kituo Cha Kati cha Polisi. Hivi sasa jengo hilo ni Makao Makuu ya Shirika la Reli la Tanzania. Wakati huo mimi nilikuwa mtoto, si zaidi ya miaka minne hivi. Jambo la kwanza ninalokumbuka kuhusu Budohi ni kuwa kila mara tulipokwenda kumtembelea tulimkuta anasoma gazeti. Baadae Budohi alihamishiwa Kenya na aliwekwa kizuizini katika kisiwa cha Lamu.

Alipofunguliwa toka kizuizini mwaka wa 1963 miezi michache kabla ya uhuru wa Kenya, Budohi alikwenda Uganda na akaajiriwa na gazeti la Uganda Argus. Hivi sasa ninaelewa kwa nini siku zile kila mara nilikuwa namkuta amezama ndani ya gazeti kila tulipokwenda kumtembelea pale rumande mjini Dar es Salaam. Niliweza kwa msaada wa rafiki yake Maxwell aliyelowea Tanganyika, kumpata Budohi mjini Nairobi mwaka 1972. Nilimtembelea mjini Nairobi wakati huo alikuwa akiishi Ruiru maili chache kutoka Nairobi mjini. Budohi alikuwa ametundika picha ya Nat King Cole sebuleni kwake. Mwaka 1974 nilimtembelea tena, safari hii katika nyumba yake ya Ngei Estate. Budohi alikuja kuwa mtu wa kwanza kabisa kunipa habari kuhusu historia ya harakati za Tanganyika dhidi ya ukoloni wa Waingereza. Hata hivyo wakati ule nilikuwa bado sijapata hamu wala kuwa na hamu ya kuandika kitabu kuhusu uhuru wa Tanganyika.

Kulikuwepo na wazalendo kutoka nchi jirani ya Kenya kama vile Dome Okochi Budohi na Patrick Aoko ambao walikuwa wanajua vyema siasa za walowezi za kupora ardhi za wananchi. Kutoka kwa wazalendo kama hawa, Abdulwahid alipata usikivu wa mawazo yake ya kuigeuza TAA kuwa chama cha siasa chenye nguvu. Lakini mara tu baada ya kuundwa kwa TANU wazalendo hawa wa Kenya wakakamatwa na serikali. Kwa miezi sita walihojiwa na kuwekwa rumande Central Police Station huku wamefungwa minyororo. Budohi na Aoko walikuwa wakifuatwa na makachero (Special Branch) toka mwaka wa1952 baada ya hali ya hatari kutangazwa Kenya. Inasemekana Dome Budohi aliponzwa na barua iliyotoka Kenya ambayo ilikamatwa na makachero. Barua hii ilikuwa inamuhusisha Budohi na Mau Mau. Inasemekana Budohi alisalitiwa na Mkenya mwenzake aliyeitwa Martin[1]ambaye alikuwa pamoja naye katika Blackbirds. Martin alikuwa akipuliza tarumbeta.

Askari waliokuwa wakiwalinda kule rumande walitoa habari kwa TANU kuwa kulikuwa na mpango wa kuwapa sumu wafungwa wale, Budohi na mwenzake Aoko. Baadaye wafungwa hawa walihamishiwa Handeni ambako kulikuwa na kambi ya kuwafunga watuhumiwa wa Mau Mau. Kawawa alikuwa amehamishiwa hapo kutoka Dar es Salaam. Baadhi ya wafungwa walikuwa wananachama wa TAA na baada ya kuundwa TANU wakawa wanachama wa TANU. Kawawa alikuwa akifahamiana na wengi kati ya wafungwa wale. Budohi na Aoko waliwahi kuwa viongozi wa TAA. Kawawa aliwaangalia wafungwa hawa kwa moyo wa huruma akijaribu kupunguza shida zao pale kambini kila alipopata mwanya wa kufanya hivyo. Budohi aliwahi kucheza senema ya Kiswahili na Kawawa iliyoitwa Mgeni Mwema iliyokuwa imetayarishwa na Community Development Department. Idara hii ilitengeneza filamu kadhaa ambazo Kawawa alicheza kama nyota wa mchezo. Katika senema zote alizocheza, iliyopata umaarufu na kupendwa zaidi ilikuwa Muhogo Mchungu ambalo ndiyo lilikuwa jina la Kawawa katika filamu hiyo.

Minongíono ilikuwa ikisikika kutoka kanda ya ziwa kuwa kiongozi wa wapiganaji wa Mau Mau, Dedan Kimathi alikuwa anaonekana mjini Mwanza. Wakati ule pale Mwanza kulikuwa na Wakikuyu wengi wakifanya biashara sokoni. Ilivumishwa kuwa Dedan Kimathi alikuwa akiwasiliana na Wakikuyu wenzake na wao walikuwa wakimkusanyia fremu za baiskeli za zamani ili zitumike kutengenezea magobole ili zitumiwe misituni dhidi ya majeshi ya Waingereza. [1] Mapigano yalipoonza kati ya Mau Mau na Waingereza kulikuwa na Wakikuyu kama elfu kumi na sita wakiishi na kufanya kazi kaskazini ya Tanganyika. Kama tahadhari, Wakikuyu wachache walioonekana kuunga mkono Mau Mau, walikamatwa na kupelekwa Kenya ambako waliwekwa kizuizini katika kambi mbali mbali. Wakati Budohi na Wakenya wengine walipopita Korogwe wakati wakirudishwa Kenya kupitia Taveta, Ally Sykes, ambaye alikuwa amehamishiwa Korogwe, alikwenda hadi stesheni ya reli kuwaaga. Watuhumiwa hawa wa Mau Mau walikuwa wametiwa katika mabehewa ya kubebea ng'ombe huku wamefungwa minyororo. Dome Budohi na wazalendo wengine waliwekwa kizuizini kwa miaka saba.

Katika wale walioasisi TANU, ni wale tu aliokuwa makao makuu ya TAA ndiyo wanaoweza kueleza historia ya kweli ya chama hiki. Hawa ni John Rupia, Dossa Aziz, Tewa Said Tewa, Julius Nyerere, Dome Budohi, Abdulwahid na Ally Sykes.

Miaka mingi baada ya kutoka kizuizini kisiwa cha Lamu, Budohi bado alikuwa ma mfundo na Martin na kila alipozungumza kuhusu yeye na mwandishi,alionyesha chuki ya kupindukia.

Wazalendo wa Kenya waliokuwa katika harakati nchini Tanganyika hawakuwa na uhusiano na TANU baada ya uhuru na wala chama hakikufanya juhudi kuwasiliana nao. Dome Budohi alijaribu mara nyingi kuomba kukutana na Nyerere alipozuru Nairobi lakini ilishindikana. Budohi hafahamu kama maafisa wa serikali ya Tanzania walimzuia wao tu au walifanya hivyo kwa amri ya Nyerere. Hadi anafariki Dome Budohi hakuwahi kuonana na Nyerere ambae wakati wa enzi za TAA na TANU walikuwa wakifahamiana vizuri.

Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa. Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama. Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo. Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7. Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Tosiri kadi nambari 25.

Mwezi June 1953, makao makuu ya TAA yalitangaza kamati yake ya utendaji: J. K. Nyerere, Rais, Abdulwahid Sykes, Makamu wa Rais; J. P. Kasella Bantu, Katibu Mkuu; Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz, Katibu wa pamoja wa muhtasari; Wajumbe wa kamati: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.[1]Muundo wa uongozi katika TAA unaonyesha ule mshikamano wa Afrika ya Mashariki uliokuweko wakati wa harakati za uhuru. Wazalendo wa Kenya walichaguliwa kama viongozi wa TAA bega kwa bega na Watanganyika.''

Nimenyanyambua vipande hivyo kutoka sehemu tofauti ya kitabu changu ili kutoa picha na kujaza habari katika historia ya TANU na harakati za kudai uhuru. Mengi ya haya hayajulikani na wengi na hivyo kuathiri sana kufahamika na kuheshimu historia ya uhuru wa Tanganyika na mashujaa wake.
 
Umejua kuitumia vyema lugha kiswahili
Kweli watu Wa pwani ni wakarim
 
Nashindwa kuelewa,kujua kwote huku,you seems to be in the know in many aspects-kitu ambacho Tazania ina lack sana, how come you never hit the heights katika nchi hii. AU from the word go walikustukia utageuza ofisi kuwa place of worship??

AU kitu gani bwana jf inatosha sana watu matumbo yanawazuka, mezeni tu hata kama chungu ndio sifa ya ukweli
 

Mzee Mohamedi Said mm, nina babu yangu hapa mzaliwa wa Tanga, amezaliwa kati ya 1927 au 28, ananihadithia muda huo alikuwa akifanya biashara ya maembe kutoka kaskazini kuja kuuza hapo kariakoo ananiambia soko lilikuwa banda la sio lile la leo, leo ndio nimeliona kwenye picha hapo juu. Huyu mzee ni kaka nne wa bibi yangu mzaa baba. ninae hapa dsm kwa kweli na ameniambia niandike kitabu kuhusu ujio wa watu katik kijiji chetu huko tanga yeye anayajua mengi kwani amehadithiwa na wazee wake na mengine kayaona kwa macho yake.

Kitu ninachomfanya asikie uchungu sana ni kwamba, kwa sasa huko kwetu kuna watu wageni sana walipokewa katika mji huo lakini sasa wanajifanya wenyeji na kuwatukana wazee wa mji ule. Hamasa yakuandika kitabu hiki ili kutunza historia ile imetokana na kukusoma wewe SHEIKH wangu nikahisi naweza mkosa huyu mzee kisha mambo adimu yakakosekana.
 

eleza basi hiyo 80% ilikuwaje wakati hata kula alikuwa hatimizi??
 
Maneno meeengi...hayana maana...nyie waandishi ndio magufuli hawataki...

hahahahahahahahahaha, si yeye tu hata wewe na wengine wengiiiiiiiiiiiii, jamani dunia hii si yenu pekeyenu, mnataka kusikia mazuri yenu,mabaya yenu hamuwezi kuyasema ndio twawasemea, tamu meza chungu sukutua tema,
 
Window7,
Mie nitakuwa na historia gani ya maana hadi mtu atake kuisoma kaka.
Mimi ni mtu wa Dar es Salaam ndiko nilikozaliwa.

Sina mambo muhimu kaka tupo tupo tu.
Nikifanya kazi bandarini sasa nimestaafu naishi Magomeni Mapipa.
weka hapa watu waisome;sasa ukizaliwa dar ndo unakosa historia???

unakazana kila mtu atajwe mpaka aliyekuwa anafagia ofisi za TANU,au aliyekuwa anaosha vyombo mwl akimaliza kula!;huo uandishi wa wapi???si utajaza dunia yote sasa ukianza kutoa shukrani,unataja watu wachache tu huo ndo uandishi!

>>>>LAKINI WEWE ULIVYOKUWA MWANDISHI UCHWARA UNATAKA MPAKA WOTE WALIOKUWA WANAUZA KAHAWA NA MWL ALIKUWA AKIPITA KUNYWA WATAJWE SIO????

##>>>HUO UDINI UNAOKUSUMBUA LAZIMA UFE KIHORO!

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…