Kisa cha Shariff Abdallah Attas na mwalimu Julius Nyerere ofisi ya TANU baada ya uhuru

Kisa cha Shariff Abdallah Attas na mwalimu Julius Nyerere ofisi ya TANU baada ya uhuru

Nafikiri huyo attas alipaswa kujibu ndio au angemkumbusha hapo .

Mtu kama nyerere anakutana mania ya watu kila siku kwanini asikusahau halafu hakuwa ndugu yake Wa damu .

Mi mwenye kuna watu nilisoma nao siwakumbukj.

Nyerere yawezekana alikuwa hana uhakika kama anafahamu Hugo shekh ndo maana aliuliza sababu pengine alikuwa anapata taswira ama ushawishi kwamba ashawahi kufahamiana na huyo mtu lakini hana uhakika sasa alitaka uthibitisho.

Halafu ungeeleza vizuri uhusika Wa Hugo shekh Attas katika harakati za Uhuru yaaani alishirikiana vipi na Mwalimu?

Sio tu mtu mnaenda nae kula ubwabwa kwa tajiri flani kila siku ndo kutaka akumbukwe kwa kila kitu.

Ni hayo tu
 
Nyiokunda,
Tafadhali hebu nipatie hiyo sehemu nipate kukujibu In Shaallah.
Sijaona mahali neno hili lipo katika uzi huu wa Shariff Attas.
Kuna chapisho ulielezea Mr seleman alivyotolewa minaki ya zamani Na shangazi yake ebu angalia huwa napitia maandiko yako unapoweka link
 
Nafikiri huyo attas alipaswa kujibu ndio au angemkumbusha hapo .

Mtu kama nyerere anakutana mania ya watu kila siku kwanini asikusahau halafu hakuwa ndugu yake Wa damu .

Mi mwenye kuna watu nilisoma nao siwakumbukj.

Nyerere yawezekana alikuwa hana uhakika kama anafahamu Hugo shekh ndo maana aliuliza sababu pengine alikuwa anapata taswira ama ushawishi kwamba ashawahi kufahamiana na huyo mtu lakini hana uhakika sasa alitaka uthibitisho.

Halafu ungeeleza vizuri uhusika Wa Hugo shekh Attas katika harakati za Uhuru yaaani alishirikiana vipi na Mwalimu?

Sio tu mtu mnaenda nae kula ubwabwa kwa tajiri flani kila siku ndo kutaka akumbukwe kwa kila kitu.

Ni hayo tu

Tumeambiwa hapo juu kwamba Nyerere na Attas walikuwa wanatumia muda mwingi kuongea, katika kipindi ambacho nadhani Nyerere alihitaji sana msaada wa wasamaria wema, ukizingatia kwamba ndio kaacha kazi ili akomae na siasa. Siasa ni ngumu, hasa ukiwa mpinzani wa utawala. ilikuwa hivyo wakati ule, na pengine zaidi hivi sasa. Mimi naamini kwamba Nyerere alitakiwa kuwafuatilia wale waliompa tafu enzi hizo na kuwashukuru ipasavyo. kumkumbuka mtu uliyekuwa naye wakati unagaagaa mavumbini, peke yake ni kitendo cha kiungwana na staha, hata kama hujampa chochote.
 
Mzee mohamed bado hujanijibu au nipe maana yake
Nyiokunda,
Hakika sijajibu kwa kuwa katika uzi huu wa Shariff Abdallah Attas
sijaona nilipoandika hiko neno.

Nitajibu In Shaallah nitakapojua ''context,'' ya sentensi.
 
Tumeambiwa hapo juu kwamba Nyerere na Attas walikuwa wanatumia muda mwingi kuongea, katika kipindi ambacho nadhani Nyerere alihitaji sana msaada wa wasamaria wema, ukizingatia kwamba ndio kaacha kazi ili akomae na siasa. Siasa ni ngumu, hasa ukiwa mpinzani wa utawala. ilikuwa hivyo wakati ule, na pengine zaidi hivi sasa. Mimi naamini kwamba Nyerere alitakiwa kuwafuatilia wale waliompa tafu enzi hizo na kuwashukuru ipasavyo. kumkumbuka mtu uliyekuwa naye wakati unagaagaa mavumbini, peke yake ni kitendo cha kiungwana na staha, hata kama hujampa chochote.
Mindi,
Mwalimu Nyerere
alipata kusema watafutwe wazalendo waliojiunga na TANU
kati ya 1954 - 1958 kwa maneno yake alisema kuwa kile kilikuwa kipindi kigumu.

Maneno haya aliyasema Tabora mkutanoni katika sherehe za kuadhimisha miaka
20 ya Azimio la Busara.

Kisa cha Mwalimu kusema maneno yale katika hotuba yake ilikuwa kutokana na
swali alililoulizwa na Ramadhani Singo.

Huyu Ramadhani Singo alikuwa mlinzi wa Nyerere Tabora wakati wa mkutano
ule wa Kura Tatu, akiwa na Mwalimu mchana na usiku akikesha nje ya nyumba
ambayo Nyerere alifikia.

Mwalimu Nyerere alipokutana na wana TANU wa Tabora kundi lile la akina Singo,
Singo alimkabili Nyerere akamwambia, ''Mwalimu mbona umetusahau wenzio?
Angalia hali zetu zilivyokuwa...''

Kundi zima lile la TANU waasisi pale Tabora waliokuwa hai walikuwa mbele yake na
kwa hakika wote walikuwa hali zao taaban kwa kuwaangalia tu.

Singo katika ujana wake alikuwa na sifa ya kupigana na ujasiri na hii ndiyo sababu
ya yeye kupewa kazi ya ulinzi wa Mwalimu Nyerere na bila shaka ndiyo huu ujasiri
wa kumkabili Nyerere na maneno yale.

Ndipo Nyerere alipopanda jukwaani kulihutubia taifa akasema maneno yale.
Shariff Abdallah Attas alikuwa na mengi katika historia ya TANU siku zile za mwanzo.

Kuna kisa cha Mzungu Town Clerk ambalo Kariakoo Market ilikuwa chimi yake na huyu
Mzungu ndiye alikuwa ''boss,'' wa Abdul Sykes na Shariff Attas.

Kisa hiki ametuhadithia Shariff Attas siku ile ya Eid.

Anasema Mzungu zimemfikia taarifa kuwa Abdul anauza kadi za TANU ofisini kwake.

Mwingireza akamvamia Abdul ofisini kwake na akazikuta kadi tena Abdul kazitoa
mwenyewe katika mtoto wa meza akaziweka juu ya meza yake huku maneno yakimtoka
kuwa asimtishe TANU ni chama halali na mtu yeyote anaweza kuwa na kadi za TANU
popote.

Abdul anamjibu Muingereza Town Clerk ''boss,'' wake kwa ile ''perfect English,'' yake.
Sifa moja kubwa ya Abdul Sykes ilikuwa kuzungumza Kiingereza vizuri.

Mawazo Shomvi, huyu alikuwa mchezaji mpira wa Yanga katika miaka ya 1960 ananambia,
''Mimi iko siku nilikwenda ofisini kwa Abdul Sykes nikamkuta anazungumza Kiingereza na
mtu, nilipigwa na butwaa jinsi alivyokuwa anazunguza vizuri lugha ile.''

Muingereza na Abdul wakabwatizana hadi nje ya ofisi watu wakajazana kumtazama Abdul
anavyopimana ubavu na Muingereza.

Shariff Attas akamgeukia Kleist akamwambia, ''Baba yako alikuwa jeuri wakati mwingine.''

Wafanyabiashara wa Kariakoo Mshume Kiyate, Shariff Mbaya Mtu na wenzao wakakutana
ghafla kufanya kisomo cha kuchinja ili Muingereza asije kusababisha Abdul afukuzwe kazi kwa
ajili ya TANU.

Kisa hiki pia alipata kunihadithia George Kissaka mtoto wa Mzee Kissaka ambae alikuwa
akifanya kazi pale sokoni chini ya Abdul Sykes.

George anasema baba yake alipata kumuhadithia kisa hiki.

Stori za TANU miaka ile ya mwanzo zinasisimua sana na kama alivyosema
Baba wa Taifa, kile kilikuwa kipindi kigumu sana.


Soko la Kariakoo kama lilivyokuwa katika miaka ya 1950

Kwa taarifa zaidi za historia ya Soko la Kariakoo wakati wa kuaisisi TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika ingia hapo chini:
Mohamed Said: KARIAKOO MARKET 1949 MOJA YA KITUO CHA HARAKATI ZA SIASA DAR ES SALAAM
 
Kuna chapisho ulielezea Mr seleman alivyotolewa minaki ya zamani Na shangazi yake ebu angalia huwa napitia maandiko yako unapoweka link
Nyiokunda,
Kupata kitu kama hicho katika maktaba yangu inataka muda.
 
Nafikiri huyo attas alipaswa kujibu ndio au angemkumbusha hapo .

Mtu kama nyerere anakutana mania ya watu kila siku kwanini asikusahau halafu hakuwa ndugu yake Wa damu .

Mi mwenye kuna watu nilisoma nao siwakumbukj.

Nyerere yawezekana alikuwa hana uhakika kama anafahamu Hugo shekh ndo maana aliuliza sababu pengine alikuwa anapata taswira ama ushawishi kwamba ashawahi kufahamiana na huyo mtu lakini hana uhakika sasa alitaka uthibitisho.

Halafu ungeeleza vizuri uhusika Wa Hugo shekh Attas katika harakati za Uhuru yaaani alishirikiana vipi na Mwalimu?

Sio tu mtu mnaenda nae kula ubwabwa kwa tajiri flani kila siku ndo kutaka akumbukwe kwa kila kitu.

Ni hayo tu
Mazigazi,
Umesema kweli hakika si rahisi kukumbuka kila mtu.
Sijui kwa nini umekuja na hii lugha ya ''kula ubwawabwa kwa tajiri fulani...''

Unadhani Nyerere alikuwa anakwenda ''kula ubwabwa,'' kwa tajiri?

Unadhani Abdul Sykes na Nyerere na mafungamano yao yalikuwa ya
''mafadhili,'' na ''mfadhiliwa?''

Mzee Abdallah alikuwa, ''messenger,'' katika ofisi ya Market Master na mimi
nilifanyanae mahijiano kuhusu siku zile za siasa akiwa na Abdul Sykes.

Alininambia kuwa alikuwa akichinja kuku 20 kwa siku akipeleka nyumbani kwa
Abdul Sykes kwa ajili ya kitoweoa cha wana TANU.

Hii haina maana kazi ya Abdul ilikuwa kufadhili wana TANU.

Kitu kikubwa zaidi ndicho kilichokuwa kikiwaunganisha wazalendo hawa nacho
ni kuijenga TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Chief Kidaha Makwaia akila sana nyumbani kwa Abdul kila akija Dar es Salaam
kutoka Shinyinga kuja kuhudhuria vikao vya Baraza la Kutunga Sheria.

Sasa tuseme na Chief Kidaha alikuwa anakula ubwawa kwa Abdul Sykes?
Ingia hapa kuna mengi ya kujifunza katika uhusiano baina ya watu katika
kupambana na ukoloni:
Mohamed Said: KUTOKA JF: MAMA DAISY NA HISTORIA YA CHIEF DAVID KIDAHA MAKWAIA
 
Nyakaonda,
Mpaka nipate hapo nilipoandika hilo neno.
Cha kushangaza kila nikitafuta kwa sasa siioni kwa sasa ila Mzee umeandika ila hutaki kunifafanulia.OK tuishie hapo nitatafuta kwa MTU mwingine ani habarishe.
 
Cha kushangaza kila nikitafuta kwa sasa siioni kwa sasa ila Mzee umeandika ila hutaki kunifafanulia.OK tuishie hapo nitatafuta kwa MTU mwingine ani habarishe.
Nyiokonda,
Ungejua kiasi cha maneno na makala ninayoandika usingesema
hivyo.

Tabu kukumbuka kitu nilichoandika hata mwaka mmoja uliopita.
 
Cha kushangaza kila nikitafuta kwa sasa siioni kwa sasa ila Mzee umeandika ila hutaki kunifafanulia.OK tuishie hapo nitatafuta kwa MTU mwingine ani habarishe.
Wanamajlis,
Kuna ndugu yangu hapa Barzani jina lake Jackline1.

Sina kawaida ya kufanya nongwa lakini kwa hili ningependa kumsikia
kuhusu, ''admissions'' mbili za Abdul Sykes, Makerere na Princeton
University, New Jersey.

Aliniandikia kuhusu hizo, ''admission,'' kama vile mimi ni muongo kwa
kusema kuwa taarifa hizo anazisikia kwangu tu.

Kusema kweli niliumia sana na hii ndiyo sababu nareja kwake na kwenu
nimsikize kama baada ya kumjibu na kumwekea rejea mbili ingawa zote
ni zangu mwenyewe, nini sasa maoni yake?

Naweka hapa na picha nikiwa New Jersey:

vRfPSpZCJZOvHP2ltbzELdEWPMqo5ydk6sG09VcexjPhTzUmbt_pw0iNEASSLsJLMweCO4Wv1EvG9CkF-kVdDat3RZrEXIaSHGXRwW5nGOeHEc_TbCHNZ7auwO9mkRGDoPU8DwEYEtQ5c7A-_C0jK55TWzUkuPJyGuQudRpppMTqKFejNQbM10pGABQP0gbKM5YDQT97NPEAaOFNuxjUSAiKoNFUeYoCg07S0Q2eUjOcavqGOzSgmBJWhYsdH0W6GoNUpdTaca94BZRvnzTnBOFwkVF6bplRVzUQ22z7iT6ZkKRFNJEc7r0DQ915iTaJ3-JVxsOq7vgXndk0mhxNYewoAIiPPRCkWT3NRV4SSmxWKpYowq6JVKTzBUrlSd7YIb4OGSEjfPEsha_I3jPGNEOMpDLkHO_9Ulgq0SgKxbxN42FPFmp3NjLDy5t6saXnp8Z4NZEX1GDVNfP1w7KelphF5zWwyZMRIlaOKTlKHPWNW_bh2Dh1rxkFOYuQKRBkMxQu8ETe5RsFcJ2Y5h2iNQgkcnT_fXzwgIn4N0beSZWRjXUih52bG4rTLPQIQaHhRSeM84nWDiv0_01k2gZ1oEXn4SjEAR6KcTquqPHYCTGdFGm4=w876-h657-no
 
Cha kushangaza kila nikitafuta kwa sasa siioni kwa sasa ila Mzee umeandika ila hutaki kunifafanulia.OK tuishie hapo nitatafuta kwa MTU mwingine ani habarishe.
Nadhani hujamtendea haki Sheikh Mohamed Said. ingetosha tu kama ungesema "Inshaalah nasubiri utapopata nafasi, nitazamie". hata kama ungeuliza wengine, ingekuwa siyo tatizo.
 
Mindi,
Mwalimu Nyerere
alipata kusema watafutwe wazalendo waliojiunga na TANU
kati ya 1954 - 1958 kwa maneno yake alisema kuwa kile kilikuwa kipindi kigumu.

Maneno haya aliyasema Tabora mkutanoni katika sherehe za kuadhimisha miaka
20 ya Azimio la Busara.

Kisa cha Mwalimu kusema maneno yale katika hotuba yake ilikuwa kutokana na
swali alililoulizwa na Ramadhani Singo.

Huyu Ramadhani Singo alikuwa mlinzi wa Nyerere Tabora wakati wa mkutano
ule wa Kura Tatu, akiwa na Mwalimu mchana na usiku akikesha nje ya nyumba
ambayo Nyerere alifikia.

Mwalimu Nyerere alipokutana na wana TANU wa Tabora kundi lile la akina Singo,
Singo alimkabili Nyerere akamwambia, ''Mwalimu mbona umetusahau wenzio?
Angalia hali zetu zilivyokuwa...''

Kundi zima lile la TANU waasisi pale Tabora waliokuwa hai walikuwa mbele yake na
kwa hakika wote walikuwa hali zao taaban kwa kuwaangalia tu.

Singo katika ujana wake alikuwa na sifa ya kupigana na ujasiri na hii ndiyo sababu
ya yeye kupewa kazi ya ulinzi wa Mwalimu Nyerere na bila shaka ndiyo huu ujasiri
wa kumkabili Nyerere na maneno yale.

Ndipo Nyerere alipopanda jukwaani kulihutubia taifa akasema maneno yale.
Shariff Abdallah Attas alikuwa na mengi katika historia ya TANU siku zile za mwanzo.

Kuna kisa cha Mzungu Town Clerk ambalo Kariakoo Market ilikuwa chimi yake na huyu
Mzungu ndiye alikuwa ''boss,'' wa Abdul Sykes na Shariff Attas.

Kisa hiki ametuhadithia Shariff Attas siku ile ya Eid.

Anasema Mzungu zimemfikia taarifa kuwa Abdul anauza kadi za TANU ofisini kwake.

Mwingireza akamvamia Abdul ofisini kwake na akazikuta kadi tena Abdul kazitoa
mwenyewe katika mtoto wa meza akaziweka juu ya meza yake huku maneno yakimtoka
kuwa asimtishe TANU ni chama halali na mtu yeyote anaweza kuwa na kadi za TANU
popote.

Abdul anamjibu Muingereza Town Clerk ''boss,'' wake kwa ile ''perfect English,'' yake.
Sifa moja kubwa ya Abdul Sykes ilikuwa kuzungumza Kiingereza vizuri.

Mawazo Shomvi, huyu alikuwa mchezaji mpira wa Yanga katika miaka ya 1960 ananambia,
''Mimi iko siku nilikwenda ofisini kwa Abdul Sykes nikamkuta anazungumza Kiingereza na
mtu, nilipigwa na butwaa jinsi alivyokuwa anazunguza vizuri lugha ile.''

Muingereza na Abdul wakabwatizana hadi nje ya ofisi watu wakajazana kumtazama Abdul
anavyopimana ubavu na Muingereza.

Shariff Attas akamgeukia Kleist akamwambia, ''Baba yako alikuwa jeuri wakati mwingine.''

Wafanyabiashara wa Kariakoo Mshume Kiyate, Shariff Mbaya Mtu na wenzao wakakutana
ghafla kufanya kisomo cha kuchinja ili Muingereza asije kusababisha Abdul afukuzwe kazi kwa
ajili ya TANU.

Kisa hiki pia alipata kunihadithia George Kissaka mtoto wa Mzee Kissaka ambae alikuwa
akifanya kazi pale sokoni chini ya Abdul Sykes.

George anasema baba yake alipata kumuhadithia kisa hiki.

Stori za TANU miaka ile ya mwanzo zinasisimua sana na kama alivyosema
Baba wa Taifa, kile kilikuwa kipindi kigumu sana.


Soko la Kariakoo kama lilivyokuwa katika miaka ya 1950

Kwa taarifa zaidi za historia ya Soko la Kariakoo wakati wa kuaisisi TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika ingia hapo chini:
Mohamed Said: KARIAKOO MARKET 1949 MOJA YA KITUO CHA HARAKATI ZA SIASA DAR ES SALAAM
Ahsante sana Sheikh, katika kujibu maswali unazidi kudondoza asali, Mwenyezi Mungu akujalie zaidi na zaidi
 
Nadhani hujamtendea haki Sheikh Mohamed Said. ingetosha tu kama ungesema "Inshaalah nasubiri utapopata nafasi, nitazamie". hata kama ungeuliza wengine, ingekuwa siyo tatizo.
Mzee mohamed ameshanielewa Na ana busara
 
Wanamajlis,
Kuna ndugu yangu hapa Barzani jina lake Jackline1.

Sina kawaida ya kufanya nongwa lakini kwa hili ningependa kumsikia
kuhusu, ''admissions'' mbili za Abdul Sykes, Makerere na Princeton
University, New Jersey.

Aliniandikia kuhusu hizo, ''admission,'' kama vile mimi ni muongo kwa
kusema kuwa taarifa hizo anazisikia kwangu tu.

Kusema kweli niliumia sana na hii ndiyo sababu nareja kwake na kwenu
nimsikize kama baada ya kumjibu na kumwekea rejea mbili ingawa zote
ni zangu mwenyewe, nini sasa maoni yake?

Naweka hapa na picha nikiwa New Jersey:

vRfPSpZCJZOvHP2ltbzELdEWPMqo5ydk6sG09VcexjPhTzUmbt_pw0iNEASSLsJLMweCO4Wv1EvG9CkF-kVdDat3RZrEXIaSHGXRwW5nGOeHEc_TbCHNZ7auwO9mkRGDoPU8DwEYEtQ5c7A-_C0jK55TWzUkuPJyGuQudRpppMTqKFejNQbM10pGABQP0gbKM5YDQT97NPEAaOFNuxjUSAiKoNFUeYoCg07S0Q2eUjOcavqGOzSgmBJWhYsdH0W6GoNUpdTaca94BZRvnzTnBOFwkVF6bplRVzUQ22z7iT6ZkKRFNJEc7r0DQ915iTaJ3-JVxsOq7vgXndk0mhxNYewoAIiPPRCkWT3NRV4SSmxWKpYowq6JVKTzBUrlSd7YIb4OGSEjfPEsha_I3jPGNEOMpDLkHO_9Ulgq0SgKxbxN42FPFmp3NjLDy5t6saXnp8Z4NZEX1GDVNfP1w7KelphF5zWwyZMRIlaOKTlKHPWNW_bh2Dh1rxkFOYuQKRBkMxQu8ETe5RsFcJ2Y5h2iNQgkcnT_fXzwgIn4N0beSZWRjXUih52bG4rTLPQIQaHhRSeM84nWDiv0_01k2gZ1oEXn4SjEAR6KcTquqPHYCTGdFGm4=w876-h657-no
ni ngumu kumeza kuhusu hizo admissions-hasa sababu unatumia ujanja wa lugha ya ku convince ili mradi kutuambia kwamba hawa watu Nyerere aku waacha sana kiupeo na kielimu
 
Back
Top Bottom