Kisarawe: DC Magoti apiga marufuku shughuli za ngoma kuhusisha wanafunzi

Acheni kashfa zenu kwa stori mnazopeana vijiweni,inawezekanaje mtu amtake mwanamke yeyote tu hata akiwa mke wa mtu na lazima eti huyo mwanamke akubali? Ukiona jambo kama hilo huyo mwanamke atakuwa amekubali mwenyewe labda kwa sababu ya umalaya wake tu na hakuna kitu kinaitwa sijui chakala chakala mikoroshini sema sehemu yoyote ya starehe na kwenye matamasha labda kutokana na ulevi mihemko ya ngono hujitokeza sana na watu hujikuta wanafanya matendo ya ovyo hata huko kwenye masherehe yenu nyie wenzetu mnaojiona mna mila nzuri mambo hayo hujitokeza na sisi tunayajua.
 
Acha ujinga
 

Ushawahi kushiriki ukaona?
 
Tamaduni zinafundishwa hadi mashuleni yeye anakataza vipi? Kwa maana hiyo mitaala ibadilishwe pia?
Hawa wajinga ndio wanamuangusha Rais, mbaya zaidi halioni hilo.
Yaani mambo mengine ni basi tu.
Yaani tukose pa kupumulia siyo?
Maisha na ugumu wake mliotusababishia, halafu hadi kwenye starehe zetu mnakuja kutuwekea kauzibe?
 
Wengi mnamshambulia kwa mihemko. Labda tumkosoe hilo la kutoboa matairi kwani kufanya hivyo ni jinai.
 
Huyu ndiye DC Mpya wa Kisarawe aliyeaminiwa na Mamlaka ya Uteuzi, Angalieni vipaumbele vyake.

View attachment 3025814View attachment 3025815

Yaani unateua mtu hata miiko ya uongozi hajui! Hivi hii nchi imeishiwa watu wa kuteuliwa?
Nimecheka sana,eti badala ya kutafakari waanzishe miradi ya kiuchumi ili kupunguza umaskini unapoteza muda kuanza kukimbizana na wapiga ngoma,wapiga ngoma hiyo ndio starehe yao ya kujiliwaza na umaskini walionao.
Yaani wakati matajiri wanakwenda kuburudika Serena hotel na Mlimani City hao maskini wa kisarawe starehe yao ndio hiyo ngoma.
Sitetei watoto kwenda ngomani au kupewa mimba ila kuna namna ya kufanya ili watoto wawe bize shuleni na kuisahau ngoma automatically na sio kwa kukimbizana na wapiga ngoma
 
Mtani pigeni busha la kilo tatu huyo 🤣🤣🤣haiwezekani bwana awakataze watani wangu kujinafasi na mila zao.
 
Le

Huyu jamaa hana weledi wowote wa uongozi! Kapewa nafasi tu ya upendeleo kutokana na ulemavu wake
 
Kwa jinsi walivyo nalo watalihusisha na dini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…