Uchaguzi 2020 Kishindo cha Tundu Lissu chatikisa Zanzibar, Maandalizi ya ujio wake usipime

Unajua kuna watu hawafahamu kwamba si rahisi kushindana na aliyejaaliwa , huyu Lissu baada ya Mungu kumfufua alimpangia kuwa Rais wa Tanzania 2020 , hili hakuna binadamu yeyote au kibwengo chochote kitakachozuia .
Na wewe ni msomi?
Wasomi wa Tanzania, Wakati mwingine mmejaa Ujinga usiotokana na akili zenu!!

Eti Mungu kampangia awe Raisi??🤣
 
Mimi ningewashauri muwe watulivu tu hata hizo form angepita kuzijaza kimya kimya tu

Ina madhara makubwa kwenda kimya kimya, bora hivi mubashara tunafuatilia kila hatua na kujiridhisha uhai wa chama amasivyo tutawekwa kundi moja kupitia propaganda za CCM kuwa sisi ni sawa na TLP, TADEA, CHAUMA n.k vyama vya msimu wa uchaguzi.

Kubwa katika hili hatuvunji sheria na ktk kutafuta wadhamini lazima watu wawepo na pia kumbuka shughuli ni watu.

CCM Mpya wanajitia wapo kimya, huu ni mtego wa kisiasa wa CCM tuwaigize ili watu-brandi CHADEMA imekufa. Leo si umeona na wao baada ya kugundua mtego wao wa kimya kimya umeteguliwa nao wamejitokeza kinamna uwanja wa Uhuru.
Wanatesti mitambo uwanja wa uhuru
Source: Global TV online
CCM wametumia sikukuu ya NANENANE Wakulima, Kongamano la Kinamama, TAHALISO Dodoma, Kongamano la Kanisa la TAG , TBC Channel Ten, Uhuru Redio /TV n.k halafu wanajifanya wapo kimya kimya, ogopa sana mbinu za chama hili kongwe CCM ukiwaigiza unajimaliza kisiasa.

15 August 2020
Angalia jinsi MAELEZO (CCM) wanavyohangaika kutangaza mafanikio kimyakimya
DKT ABBAS:"BILIONEA LAIZER ILIISHANGAZA DUNIA, ANA ZAIDI YA Sh. Bilioni 10/NI MAONO YA SERIKALI"
Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt Hassan Abbas amesema kuwa kisa cha mchimbaji madini Ananiu Laiser cha kupata madini na kulipwa na seriakli zaidi ya shilingi bilioni 10, ni maono na mabadiliko makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Magufuli katika sekta ya madini nchini.. Source : Global TV online
 
Kwa kweli Lissu na Chadema watashinda sana kwenye mitandao ila siyo kwenye uchaguzi. Jiandaeni kisaikolojia hasa Lissu maana anaweza akapata degedege akashindwa kabisa kutembea baada ya matokeo kutangazwa huku akiwa amembulia asilimia 20% ya kura zote.
 
Sio huu mwaka labda na 25 ndio atafikiriwa ila huu mwaka angekaa kimya tu hatoweza kushinda .
 
Lisu wa mitandaoni sounds amazing 😉
 
Kanda ya Kaskazini wametuangusha kwenye habari za Lissu, Viva kanda ya serengeti
 
Angeshinda Kama angegombea Tanzania Visiwani, Huku bara ni Jpm
 
Shambulizi la ofisi liliharibu kila kitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…