Kiswahili fasaha kinatoweka

Kiswahili fasaha kinatoweka

Kuna wale wa "Nyimbo mpya ya" Chino wana man huku wanalamba lips, wanazingua sana kudadek zao
 
Kama tunavyosema hapa, unaweza kushangazwa sana unapokutana na taasisi kubwa kama TUKI nayo inaboronga Kiswahili.

Wamekosea, hilo si neno sahihi.
Oxford nao wamekosea?

Hapana, wote hawajakosea. Wako sahihi.

Pia, zote, ‘onyesha’ na ‘onesha’ ni sahihi.

Kwa nini zote ni sahihi? Jibu ni lahaja.

Kiswahili kinazungumzwa Afrika Mashariki na Kati.

Hili ni eneo kubwa. Hivyo suala la lahaja za lugha haliepukiki.

Kimvita [Kiswahili cha Mombasa na pwani ya Kenya] kina tofauti za hapa na pale katika matamshi na tahajia za maneno na Kiswahili cha bara.

Mfano, ile mboga uijuayo wewe kama ‘biringanya’, kule Mvita na baadhi ya sehemu za Congo, inaitwa ‘biringani’.

Kuna baadhi ya maeneo namba 0 huitwa ‘sufuri’ na kwingineko huitwa ‘sifuri’.

Hata Kisukuma kina lahaja. Kinyantuzu, Kisukuma cha wenyeji wa Simiyu, kina utofauti na Kisukuma cha wenyeji wa Shinyanga

Mfano, kijiji cha ‘Gambosi’, watu wa nje huwa wanakiita ‘Gamboshi’.

Matamshi yote yanakubalika.

Hata Kiingereza kiko hivyo hivyo.

Mfano, neno ‘schedule’, kwa Marekani hutamkwa tofauti na litamkwavyo Uingereza na kwingineko kutumiako Kiingereza cha Uingereza.

Hata kwenye tahajia, kuna maneno huandikwa tofauti. ‘Center’ na ‘centre’ yote ni sahihi.

‘Defense’ na ‘defence’ yote ni sahihi pia.

Hivyo, ‘onyesha’ na ‘onesha’ nayo yote ni sahihi. Ni suala la lahaja tu.

Na ndo maana yote yapo kwenye kamusi zote za Kiswahili sanifu [ambazo ninazo na ambazo nimewahi kuziona].

Sikuwa na nia ya kujivika ualimu wa isimu matumizi. Ila, wakati mwingine inabidi tu iwe hivyo ili kutoa somo ambalo linaonekana kuwaepa watu wengi.

Kamusi hutungwa na wataalamu wa lugha waliofanya tafiti za kutosha. Sidhani kabisa kama wataalamu wote hao wa Kiswahili, kutoka Afrika Mashariki na Kati, wakakosea kuliweka neno ‘onyesha’ na kutoa fasili yake, katika hizo kamusi za Kiswahili.

Kwenye lugha, neno moja kuwa tofauti katika matamshi na tahajia, ni jambo la kawaida sana, kwa kuzingatia muktadha wa lahaja.
 
Maneno mazuri ya kiswahili yamepindishwa kiasi inaleta kichefuchefu hata kusikiliza. Hapa nitaweka baadhi ya maneno.

Alikuwa = alikua
Kwa hiyo = ko
Baadhi = baazi
kufanikiwa = kujipata
sasa = saivi
Ndio hivyo = ndoivo
Ndio nini = ndonini
serikali = serekali/selekale
yaani = yani
mtaa = kitaa/kitaani
kwa sababu = co

Pasipo kuchukuliwa hatua za makusudi lugha hii inaelekea kupotea.
Sikiliza hii video kuanzia dakika ya 1:26 hadi 2:06 jiulize public kiasi gani inaharibiwa [WARARAMIKAJI]


View: https://www.youtube.com/watch?v=61ES1Sgksoo
 
Oxford nao wamekosea?

Hapana, wote hawajakosea. Wako sahihi.

Pia, zote, ‘onyesha’ na ‘onesha’ ni sahihi.

Kwa nini zote ni sahihi? Jibu ni lahaja.

Kiswahili kinazungumzwa Afrika Mashariki na Kati.

Hili ni eneo kubwa. Hivyo suala la lahaja za lugha haliepukiki.

Kimvita [Kiswahili cha Mombasa na pwani ya Kenya] kina tofauti za hapa na pale katika matamshi na tahajia za maneno na Kiswahili cha bara.

Mfano, ile mboga uijuayo wewe kama ‘biringanya’, kule Mvita na baadhi ya sehemu za Congo, inaitwa ‘biringani’.

Kuna baadhi ya maeneo namba 0 huitwa ‘sufuri’ na kwingineko huitwa ‘sifuri’.

Hata Kisukuma kina lahaja. Kinyantuzu, Kisukuma cha wenyeji wa Simiyu, kina utofauti na Kisukuma cha wenyeji wa Shinyanga

Mfano, kijiji cha ‘Gambosi’, watu wa nje huwa wanakiita ‘Gamboshi’.

Matamshi yote yanakubalika.

Hata Kiingereza kiko hivyo hivyo.

Mfano, neno ‘schedule’, kwa Marekani hutamkwa tofauti na litamkwavyo Uingereza na kwingineko kutumiako Kiingereza cha Uingereza.

Hata kwenye tahajia, kuna maneno huandikwa tofauti. ‘Center’ na ‘centre’ yote ni sahihi.

‘Defense’ na ‘defence’ yote ni sahihi pia.

Hivyo, ‘onyesha’ na ‘onesha’ nayo yote ni sahihi. Ni suala la lahaja tu.

Na ndo maana yote yapo kwenye kamusi zote za Kiswahili sanifu [ambazo ninazo na ambazo nimewahi kuziona].

Sikuwa na nia ya kujivika ualimu wa isimu matumizi. Ila, wakati mwingine inabidi tu iwe hivyo ili kutoa somo ambalo linaonekana kuwaepa watu wengi.

Kamusi hutungwa na wataalamu wa lugha waliofanya tafiti za kutosha. Sidhani kabisa kama wataalamu wote hao wa Kiswahili, kutoka Afrika Mashariki na Kati, wakakosea kuliweka neno ‘onyesha’ na kutoa fasili yake, katika hizo kamusi za Kiswahili.

Kwenye lugha, neno moja kuwa tofauti katika matamshi na tahajia, ni jambo la kawaida sana, kwa kuzingatia muktadha wa lahaja.
Siwezi kubisha sana kwenye hili, lakini ukweli kabisa, mzizi sahihi wa Kitenzi ONA ni "ON".

Kutoka kwenye "ON" ndipo unapoweza kukinyumbua kitenzi kwenda kwenye muelekeo uutakao.

Kama ni lahaja sijui, na sijaelewa hii lahaja ya "ONYESHA" ni ya nchi gani au eneo lipi la kijografia!

Lakini pia, kabla na baada ya uhuru tulipitia mchakato wa USANIFISHAJI WA KISWAHILI ambapo lahaja zote za Kiswahili zilisawazishwa (standardized) tukapata lahaja ya sasa ya KISWAHILI SANIFU ambayo ilitolewa kwa kiasi kikubwa kutoka kwenye Kiunguja.

Hivyo, lahaja zingine zilififishwa na kutotambulika rasmi.

Na kwa ufahamu wangu usio na mashaka wala ubabaishaji, neno SANIFU ni ONESHA.

Hapa sasa nazungumza kama mtaalamu wa Lugha na sio Kanjanja. Tunaweza kubishana katika usahihi wa lugha na ndio utamu wa utaalamu. Kubishana na kukinzana.

Lakini pia ONYESHA linaweza kuwa sawa kwa hoja ulizozitoa. Lugha inapanuka na kukubalika kulingana na mazingira au mazoea.

Sipingi. Mimi nitaenda na ONESHA.
 
Sio vizuri kuwa na kaida katika lugha ya mazungumzo . Lugha sanifu inaweza kutumika katika maandishi na katika maandiko rasmi. Ukiongea Kama Kiswahili kinavyotakiwa kuandikwa utaongea Kama kingereza Cha watanzania they talk like a book Yani wazungu wanashangaa Sana😆 afu utakuta lijitu linajinasibu linajua kingereza kumbe linaongea lugha ya kiuandishi😆
Unatutusi kaka, na kweli ukicheki movie jinsi wenye lugha yao wanavyoongea na kina sie wa kidum na fagio ni tofauti kabisa 😂😂.

Lugha yoyote ngeni kwako ni lazima tu utafamu zaidi ile formal/ya kiofisi zaidi ile ya mtaa mtaa utaijua ukiwa unaongea na watu wanaoijua vyedi lugha hiyo la sivyo ndo ivo unakua unaongea kama kitabu.
 
Siwezi kubisha sana kwenye hili, lakini ukweli kabisa, mzizi sahihi wa Kitenzi ONA ni "ON".

Kutoka kwenye "ON" ndipo unapoweza kukinyumbua kitenzi kwenye muelekeo uutakao.

Kama ni lahaja sijui, na sijaelewa hii lahaja ya "ONYESHA" ni ya nchi gani au eneo lipi la kijografia!

Na ukumbuke pia lahaja zote za Kiswahili zilisawazishwa (standardized) tukapata lahaja ya sasa ya KISWAHILI SANIFU.

Na kwa ufahamu wangu usio na mashaka wala ubabaishaji, neno sahihi ni ONESHA.

Lakini pia ONYESHA linaweza kuwa sawa kwa hoja ulizozitoa. Lugha inapanuka na kukubalika kulingana na mazingira au mazoea.

Sipingi. Mimi nitaenda na ONESHA.
Ukitumia ‘onesha’, ni sahihi:

Atakayetumia tumia ‘onyesha’, naye atakuwa sahihi.

Sijui uko wapi. Ila kama upo Tanzania, kama unaweza, nunua kamusi ya Kiswahili sanifu, hususan ya toleo lililo jipya [2023/2024], halafu uyaangalie hayo maneno usome na maelezo yake.

Ukikuta ni tofauti na maelezo niliyokupa, rudi hapa unitafute 😀.

Jingine, lahaja huwezi kuzisawazisha. Kinachofanyika ni kuzikubali tu tofauti zilizopo. Na ndo maana kwenye Kiingereza, kwa mfano, ukilitamka neno schedule kama ‘skedyul’ au ‘shedyul’, vyote ni sawa tu maana matamshi yote ni sahihi.

Lugha na misamiati yake husawazishwa na matumizi ya watumiaji wake. Siyo taasisi.

Kwani unadhani Kiingereza walichokuwa wanaongea Waingereza miaka 800 iliyopita ni sawa na Kiingereza cha leo?

Hata Kiswahili cha leo si sawa na Kiswahili cha miaka 200 iliyopita na hakitakuwa sawa na Kiswahili cha miaka 200 ijayo.

Lugha huwa ina evolve.
 
Ukitumia ‘onesha’, ni sahihi:

Atakayetumia tumia ‘onyesha’, naye atakuwa sahihi.

Sijui uko wapi. Ila kama upo Tanzania, kama unaweza, nunua kamusi ya Kiswahili sanifu, hususan ya toleo lililo jipya [2023/2024], halafu uyaangalie hayo maneno usome na maelezo yake.

Ukikuta ni tofauti na maelezo niliyokupa, rudi hapa unitafute 😀.

Jingine, lahaja huwezi kuzisawazisha. Kinachofanyika ni kuzikubali tu tofauti zilizopo. Na ndo maana kwenye Kiingereza, kwa mfano, ukilitamka neno schedule kama ‘skedyul’ au ‘shedyul’, vyote ni sawa tu maana matamshi yote ni sahihi.

Lugha na misamiati yake husawazishwa na matumizi ya watumiaji wake. Siyo taasisi.

Kwani unadhani Kiingereza walichokuwa wanaongea Waingereza miaka 800 iliyopita ni sawa na Kiingereza cha leo?

Hata Kiswahili cha leo si sawa na Kiswahili cha miaka 200 iliyopita na hakitakuwa sawa na Kiswahili cha miaka 200 ijayo.

Lugha huwa ina evolve.
Nimehariri ujumbe wangu wa juu hapo, kuna jambo ukilisoma upya utanielewa uzuri zaidi.

Usawazishaji wa Kiswahili hapa Afrika Mashariki ama kama wengi wanavyoita Usanifishaji wa Kiswahili, sio HADITHI, ni mchakato rasmi uliofanywa na Wajerumani na ukaendelezwa baada ya uhuru baada ya kuzuka mtafaruku wa kimawasiliano hususani pale ambapo Wajerumani walitaka kukitumia Kiswahili mashuleni.

Kwahiyo, usawazishaji wa Kiswahili ni kitu halisi kilichofanyika, na kwa minajili hiyo, Lugha sanifu ya Kiswahili iliyotambulika ni ile ya lahaja ya Kiunguja na marekebisho yake machache.

Lahaja zingine ziliendelea kubaki na kutumika lakini hazikutambulika kama lahaja sanifu.

Na nikurudie tena kwa kusema kwamba, "onesha" na "onyesha" yote yaweza kuwa sahihi, lakini pia kuna uwezekano TUKI wakawa wamekosea pia. Sijasema wamekosea, nimesema wanaweza kuwa wamekosea.

Lolote linawezekana, lakini mimi kama mtaalamu wa lugha asiye na ukanjanja, siku zote ninaamini kuwa, MZIZI WA KITENZI ndio msingi wa usanifu wa kitenzi hicho pamoja na unyumbuaji wake.

Maneno ya mfano uliyoyataja hapo juu ni NOMINO si Vitenzi, kwahiyo ni vigumu kubaini au kupinga usahihi wa lahaja za NOMINO kuliko usahihi wa lahaja za VITENZI kwa sababu VITENZI vinapimwa usahihi wake kwenye MIZANI MADHUBUTI YA MNYUMBULIKO WA VITENZI.

Kama mzizi wa neno "ONA" ni "ONY" basi uko sahihi, Lakini kama mzizi wa neno ONA ni "ON" basi nitakuwa sahihi.

Unaweza ukasema "gari limeONYekana? HAUWEZI!

Kwanini? Kwa sababu huo si mzizi sahihi wa kitenzi "ONA". Na kwa sababu hiyo, mzizi huo hauwezi kunyumbulika kwenye maneno mengine pia kama "oNYesha".
 
Lugha sio kitabu cha dini, ni muhimu ibadilike kutokana na wahitaji na mazingira husika. Hicho kiswahili mnachosema ni sahihi,ni sahihi kwa mantiki ipi na vilizingatiwa vitu gani kufikia kwenye usahihi huo.
 
Nimehariri ujumbe wangu wa juu hapo, kuna jambo ukilisoma upya utanielewa uzuri zaidi.

Usawazishaji wa Kiswahili hapa Afrika Mashariki ama kama wengi wanavyoita Usanifishaji wa Kiswahili, sio HADITHI, ni mchakato rasmi uliofanywa na Wajerumani na ukaendelezwa baada ya uhuru baada ya kuzuka mtafaruku wa kimawasiliano hususani pale ambapo Wajerumani walitaka kukitumia Kiswahili mashuleni.

Kwahiyo, usawazishaji wa Kiswahili ni kitu halisi kilichofanyika, na kwa minajili hiyo, Lugha sanifu ya Kiswahili iliyotambulika ni ile ya lahaja ya Kiunguja na marekebisho yake machache.

Lahaja zingine ziliendelea kubaki na kutumika lakini hazikutambulika kama lahaja sanifu.

Na nikurudie tena kwa kusema kwamba, "onesha" na "onyesha" yote yaweza kuwa sahihi, lakini pia kuna uwezekano TUKI wakawa wamekosea pia. Sijasema wamekosea, nimesema wanaweza kuwa wamekosea.

Lolote linawezekana, lakini mimi kama mtaalamu wa lugha asiye na ukanjanja, siku zote ninaamini kuwa, MZIZI WA KITENZI ndio msingi wa usanifu wa kitenzi hicho pamoja na unyumbuaji wake.

Maneno ya mfano uliyoyataja hapo juu ni NOMINO si Vitenzi, kwahiyo ni vigumu kubaini au kupinga usahihi wa lahaja za NOMINO kuliko usahihi wa lahaja za VITENZI kwa sababu VITENZI vinapimwa usahihi wake kwenye MIZANI MADHUBUTI YA MNYUMBULIKO WA VITENZI.

Kama mzizi wa neno "ONA" ni "ONY" basi uko sahihi, Lakini kama mzizi wa neno ONA ni "ON" basi nitakuwa sahihi.

Unaweza ukasema "gari limeONYekana? HAUWEZI!

Kwanini? Kwa sababu huo si mzizi sahihi wa kitenzi "ONA". Na kwa sababu hiyo, mzizi huo hauwezi kunyumbulika kwenye maneno mengine pia kama "oNYesha".
Sipo nyumbani sasa hivi. Nikirudi nitakuwekea picha ya ukurasa yenye neno ‘onyesha’ na fasıli yake toka kamusi tatu tofauti zilizochapiswa na taasisi tofauti.

Ni vigumu sana mimi kukubali kwamba, wataalamu tofauti wa lugha ya Kiswahili, kutoka taasisi tofauti tofauti, wote wakosee katika kuliweka hilo neno kwenye kamusi walizozichapisha na kuzihariri.

Uzuri wa hizi kamusi, huwa zinachapisha majina ya wataalamu waliohusika katika kuzitengeneza.

Nitakuwekea picha ya kurasa zenye majina yao.

Ni watu wenye shahada za juu za lugha ya Kiswahili. Ni watu waliofanya tafiti na kuandika juu ya lugha ya Kiswahili.

Kwa ufupi, ni wataalamu wa lugha ya Kiswahili. Hivyo, ni watu ambao wanatambulika kama mamlaka katika fani zao.

Wataalamu wa Kiswahili kutoka chuo kikuu cha Oxford, kutoka chuo kikuu cha Nairobi, kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, wote hawa wakosee katika kuliweka kwenye kamusi hilo neno?

Au siku hizi kamusi siyo kitabu cha mamlaka na marejeo katika kutafuta fasili na maana za maneno?

Anyway, nitarudi na screenshots. Ngoja nimalizie kubeba boksi kwanza.
 
Kwa utafiti wangu mdogo hakujawahi kutokea matumizi mabovu ya lugha ya kiswahili kama muda huu tulionao.

Kibaya zaidi hata baadhi ya vyombo vya habari vikubwa vinashiriki dhambi hii.

Maneno mazuri ya kiswahili yamepindishwa kiasi inaleta kichefuchefu hata kusikiliza. Hapa nitaweka baadhi ya maneno.

Alikuwa = alikua
Kwa hiyo = ko
Baadhi = baazi
kufanikiwa = kujipata
sasa = saivi
Ndio hivyo = ndoivo
Ndio nini = ndonini
serikali = serekali/selekale
yaani = yani
mtaa = kitaa/kitaani
kwa sababu = co

Pasipo kuchukuliwa hatua za makusudi lugha hii inaelekea kupotea.

Chanzo kikuu cha haya ni uholela wa vyombo vya habari hasa habari za mtandaoni.

Nashauri mambo makubwa mawili yafanyike kwa haraka.

Kuwe na takwa la lazima kwa waleta habari kwa jamii wote kuwa na ufaulu mzuri wa lugha hii

vyombo vya habari vyote yaani vya kawaida na mitandaoni lazima visajiliwe kwanza na mamlaka za kiserikali kabla ya kuanza kupeleka habari yoyote kwa jamii.

Tuungane pamoja kuinusuru tunu yetu kuu ya lugha ya kiswahili
Kwa hiyo iwe "kwahiyo'. Ni neno moja
 
Back
Top Bottom