Kiswahili: Matumizi ya Herufi “L” na “R”

Kiswahili: Matumizi ya Herufi “L” na “R”

Watu wanaosema ulasimu badala ya urasimu, Dal es saram badala ya Dar es Salaam, ulojo badala ya urojo, talatibu badala ya taratibu na michanganyiko mingine kama hiyo huwa wana tatizo gani hasa?

Siku hizi karibuni sio tu kutamka maneno yenye L na R imekuwa changamoto kubwa bali hata kuandika nalo limekuwa tatizo kubwa. Unaweza kuta tangazo limeandikwa tunauza tofari badala ya tofali, kujigalagalaza bada ya kujigaragaza, mchere badala ya mchele n.k Hivi kama kutamka ni shida hata kuandika ambapo mtu unatumia muda mwingi kufikiri bado nako hakusaidii?!

Michanganyo hii kwa sasa imeshika kasi hadi kwa watangazaji kwenye vyombo vya habari. Unakuaje mtangazi kama huwezi kutamka maneno ya lugha yako kwa ufasaha?

Hili tatizo la kuchanganya L na R linatokana na nini na linatatuliwa vipi kwa watu walioweza kulitatua?
 
Tatizo kwenye kuandika ni elimu, lakini kwenye matamko ni mtu na jamii iliyomzunguka. Mfano watu wa Mara hawana L, watu wa nyanda za juu kusini hawana R. Hii hutokana na mazingira.

Kisayansi inasemwa mtoto kabla hajaweza kusema anakuwa anatoa sauti zote. Za kichina, kijerumani, R na L. Jamii inamshape.
 
Kwenye uandishi unaweza kusema tatizo ni elimu na uwezo.

Ila kwenye mazungumzo hali ni tofauti kwasababu mara nyingi lugha huwa zinaathiriwa na lugha mama.

Mfano, Mkurya kutamka L utamuonea tu au Jaluo kutamka R ni ngumu.

Mara ya kwanza nimeenda Bukoba nilikuwa nashangaa, maana Wahaya huwa ni ngumu sana kutamaka NG' hata Ng'ombe wanaweza kusema Ngombe.

Sentenzi za Kiingereza zinazoishia na ......ing mfano She is going, wanatamka 'She is goingi.

Na hii iko dunia nzima, tafuta Mhindi aongee Kiingereza au Mzungu aongee Kiswahili utaiona athari ya lugha mama kwenya matamshi.
 
Hapana. Sioni kama kuna lugha ambayo ni sahihi kuliko nyingine. Ukiona hivyo kiswahili si lugha yao ya asili. Wanaotumia R au L wako sahihi tu....hiyo ni free style
 
Mfano Malaria anatamkaje vile? Honestly nikisoma maandishi yalivochanyanywa R ilipokuwa itumike L huwa naishia hapo. Inaudhi sasa ukute ndo anaandika kwa lugha ya malkia ndo itabidi urudie rudie. Sijaelewa hata kama ni accent ndo ifikie hatua mpaka maandishi?
 
Vipi wazaramo na watu wengine wa pwani ambao wanachanganya hizo herufi?Mkuu mimi sizungumzii watu ambao wanakosea herufi fulani katika matamshi yao, nazungumzia hawa wanaochanganya hizi herufi, sehemu ya R anaweka L na ya L anaweka R
Tatizo kwenye kuandika ni elimu, lakini kwenye matamko ni mtu na jamii iliyomzunguka. Mfano watu wa Mara hawana L, watu wa nyanda za juu kusini hawana R. Hii hutokana na mazingira.

Kisayansi inasemwa mtoto kabla hajaweza kusema anakuwa anatoa sauti zote. Za kichina, kijerumani, R na L. Jamii inamshape.
 
Watu wanaosema ulasimu badala ya urasimu, Dal es saram badala ya Dar es Salaam, ulojo badala ya urojo, talatibu badala ya taratibu na michanganyiko mingine kama hiyo huwa wana tatizo gani hasa?

Siku hizi karibuni sio tu kutamka maneno yenye L na R imekuwa changamoto kubwa bali hata kuandika nalo limekuwa tatizo kubwa. Unaweza kuta tangazo limeandikwa tunauza tofari badala ya tofali, kujigalagalaza bada ya kujigaragaza, mchere badala ya mchele n.k Hivi kama kutamka ni shida hata kuandika ambapo mtu unatumia muda mwingi kufikiri bado nako hakusaidii?!

Michanganyo hii kwa sasa imeshika kasi hadi kwa watangazaji kwenye vyombo vya habari. Unakuaje mtangazi kama huwezi kutamka maneno ya lugha yako kwa ufasaha?

Hili tatizo la kuchanganya L na R linatokana na nini na linatatuliwa vipi kwa watu walioweza kulitatua?
Nadhani tatizo linatokana na lugha za asili. Mfano R inawekwa na watu wengi toka Kagera. L inawekwa sana na Wanyakyusa.

Lakini tatizo halipo kwenye R na L tu.
 
Man Mvua


1624080209083.png
 
Vipi wazaramo na watu wengine wa pwani ambao wanachanganya hizo herufi?Mkuu mimi sizungumzii watu ambao wanakosea herufi fulani katika matamshi yao, nazungumzia hawa wanaochanganya hizi herufi, sehemu ya R anaweka L na ya L anaweka R
Kwenye kutamka au kuandika.
 
Nadhani tatizo linatokana na lugha za asili. Mfano R inawekwa na watu wengi toka Kagera. L inawekwa sana na Wanyakyusa.

Lakini tatizo halipo kwenye R na L tu.
Hujaelewa wazo la msingi na swali la mleta-mada.
 
Ni Kama S na Z Kwa wachaga S ina nguvu zaidi.
Hiyo ni athari ya lugha mama Katika kiswahili.
Unakuta lugha ya kabila husika haitumii sauti hiyo /l, r au z/hivyo inakuwa ngumu Kwa mzungumzaji kuitumia anapojifunza kiswahili.

Ni Sawa na sisi Waswahili tunapozungumza kiingereza Kwa kuweka sauti /j/ Katika maneno Kama Jesus, Joseph,July n.k,kwenye kiingereza Haipo kabisa hiyo, badala yake hutamkwa /dz/ ila na sisi kwasababu hiyo dz/ Haipo kwenye kiswahili tunashindwa kuitumia kirahisi
 
Kwa nini kuna wanyakyusa wameishi maisha yao yote Dar es Salaam wanachanganya R na L halafu kuna Wanyakyusa wameishi maisha yao yote Mbeya na wanaweza kutofautisha hizo herufi?
Nadhani tatizo linatokana na lugha za asili. Mfano R inawekwa na watu wengi toka Kagera. L inawekwa sana na Wanyakyusa.

Lakini tatizo halipo kwenye R na L tu.
 
Nadhani tatizo linatokana na lugha za asili. Mfano R inawekwa na watu wengi toka Kagera. L inawekwa sana na Wanyakyusa.

Lakini tatizo halipo kwenye R na L tu.
Did you know, a bad speaker wa lugha fulani si lazima awe mwandishi mbovu vilevile!???
 
Kuna wale wa "H" & "U"

Hilo la R & l hata mimi kuna baadhi ya maeneo linanitatiza, sio mother tongue(matamshi) ila kuna baadhi ya sehemu nashindwa kujua hapa inayotumika ni R au L..

Mfano wa sehemu ambazo nachanganyaga ipi itumike ni Neno Mahari na Mahali,
Haya yote ni maneno sahihi ila inategemea umelenga nini.

Kuna wengine shida inaazia kwenye kutamka.
 
Nadhani tatizo linatokana na lugha za asili. Mfano R inawekwa na watu wengi toka Kagera. L inawekwa sana na Wanyakyusa.

Lakini tatizo halipo kwenye R na L tu.
Walikosea sana kuita wilaya yao Rungwe, hamnaga jina la kinyakyusa linaanza na R. Lakini ukienda kwa wahaya unakuta Kagera, karagwe, ngara, kyerwa, katerero nk
 
Vipi wazaramo na watu wengine wa pwani ambao wanachanganya hizo herufi?Mkuu mimi sizungumzii watu ambao wanakosea herufi fulani katika matamshi yao, nazungumzia hawa wanaochanganya hizi herufi, sehemu ya R anaweka L na ya L anaweka R
Nani kakwambia Wazaramo au watu wa Pwani ndio wanaoongea Kiswahili sanifu ?

Lahaja ya Kiunguja na Kimtang'ata* nadhani ndio lahaja za Kiswahili sanifu.

Utamkaji mwingine wowote ni kupuyanga tu.
 
Kwa nini kuna wanyakyusa wameishi maisha yao yote Dar es Salaam wanachanganya R na L halafu kuna Wanyakyusa wameishi maisha yao yote Mbeya na wanaweza kutofautisha hizo herufi?
Swali hapa si geographical upbringing, bali makuzi. Je alifundishwa kutamka na kutofautisha hizo herufi!??? HIli ni suala litokanalo na kukosa mafunzo sahihi utotoni ama kutoweka juhudi za kurekebisha ukubwani.
 
Tatizo kwenye kuandika ni elimu, lakini kwenye matamko ni mtu na jamii iliyomzunguka. Mfano watu wa Mara hawana L, watu wa nyanda za juu kusini hawana R. Hii hutokana na mazingira.

Kisayansi inasemwa mtoto kabla hajaweza kusema anakuwa anatoa sauti zote. Za kichina, kijerumani, R na L. Jamii inamshape.
Mimi naungana na ww kabisa. Kutamka ni mazingira yanasababisha,lakini kuandika ni UDUNI WA ELIMU. Mikoa kama Kilimanjaro, Arusha Mara, Kagera, Tabora,Singida Manyara n.k wanatumia herufi vizuri kutamka na kuandika ila Dar ndio wanakosea sana kwenye mambo yote. Mbeya,Iringa Dodoma n.k wao kwenye kuongea tu ila kuandika kidogo afadhali
 
Back
Top Bottom