Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #181
Samcezar,Aaaah bwana weeee hebu tupishe zako bwana. Aaaaakh.
Mambo gani unatuletea hapa ya kipuuzi. Hao wanaodhurumiwa wanadhurumiwaje, mimi nina marafiki kibao wapo kwenye maisha mazuri na ni waislam kama wewe....
Wewe ndio wale waliokuwa wanatoroka shule kushinda madrasa maisha yamekuwa magumu unaanza kuongea upuuzi wa miaka kenda na wajua haina faida..... Cha zaidi ni hauna jipya
Sent using Jamii Forums mobile app
Samcezar,
Mkuu Mohamed Said, ni kweli kuwa Dr. Vedasto Kyaruzi hakuwa muasisi wa TAA japo ungekuwa muungwana kwa kukiri kuwa alionyesha mchango mkubwa ktk kui-shape TAA.Mag 3,
Unaandika huku umejawa na ghadhabu.
Katika hali kama hiyo kwa kawaida akili hupoteza umakini.
Umenitukana kwa kuniita mpuuzi na sifa nyingine mbaya na kusema kuwa nipuuzwe.
Mimi si mpuuzi na ndiyo maana wewe umeshindwa kunipuuza umekuwa ukinisoma siku zote.
Mimi si mpuuzi na ndiyo maana unaona nimeweza kuandika vitabu kadhaa na vikachapwa na wachapaji wa sifa kama Oxford University Press.
Unaumizwa kwa jinsi kitabu cha Abdul Sykes kilivyobadili historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
Unasema ati Cecil Matola ndiye aliyeanzisha African Association nk. nk.
Lakini huna ushahidi wa hilo.
Nenda Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana kasome Seminar Paper ya mwaka wa 1968 iliyoandikwa na Aisha "Daisy"Sykes, ''Kleist Sykes (1894 - 1949),'' mwanafunzi wa gwiji wa historia ya Tanganyika John Iliffe, inayotokana na mswada wa kitabu alioandika babu yake Kleist Sykes kabla hajafariki mwaka wa 1949.
Humo utapata historia yote ya uasisi wa African Association 1929, kwa majina ya waasisi wake: Cecil Matola (Rais), Kleist Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Zibe Kidasi, Ibrahim Hamisi, Ali Said Mpima, Suleiman Majisu, Raikes Kusi na Rawson Watts.
Utapata pia historia ya kuasisiwa kwa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Kleist Sykes 1933 Kleist akiwa Secretary na Mzee bin Sudi akiwa Rais.
Kleist anaeleza pia na utasoma humo kuwa kabla ya kuasisiwa kwa African Association, Waafrika walikuwa wakiwakilishwa na Mzungu Father Gibbons kutoka Pugu Mission na Wakristo wakionywa wasijiingize katika siasa.
Hii ndiyo sababu ya kuona waasisi wa African Association wengi wao ni Waislam.
Haya si maneno yangu bali ni maneno ya Kleist Sykes ndani ya mswada wake ambao sasa ni sura katika kitabu alichohariri John Iliffe (1973).
Isingewezekana kwa hali hii kwa Cecil Matola kuwa kinara wa harakati hili achilia mbali ile hali ya siasa ya Dar es Salaam ya miaka ile ambayo Wakristo walipangiwa hadi maeneo ya kuishi na wakoloni.
Cecil Matola akiishi Mission Quarters sehemu ambako kulikuwa na kanisa pekee Kariakoo.
TANU ilipokuja kuundwa mwaka wa 1954 hali haikubadilika Waislam walikuwa mstari wa mbele.
Umeandika na unasema kuwa mimi nawahalalisha Wazulu, Wanubi na Wamanyema waliongizwa Tanganyika na Wajerumani kama askari mamluki kuja kuwasaidia Wajerumani katika vita yao na wananchi wa Tanganyika waliokuwa wakipigana dhidi ya ukoloni chini ya viongozi wao Mtwa Mkwawa na Bushiri bin Salim Al Harith.
Haya ni matokeo ya ukoloni na mimi nimeeleza historia hii si kwa nia yoyote ya kutukuza dhulma.
Katika hawa mamluki walioingizwa Tanganyika mwishoni mwa miaka ya 1800 alikuwapo babu yangu mkuu, Abdallah Samitungo Muyukwa kutoka Belgian Congo.
Lakini watoto wa hawa askari mamluki ndiyo waliowasha cheche za ukombozi wa Tanganyika.
Historia ya Kleist Sykes na wanae hivi sasa si ngeni katika ukombozi wa Tanganyika.
Babu yangu Salum Abdallah ni mmoja katika wanachama wa TAA na ni muasisi wa TANU Tabora 1954 na mwaka wa 1955 aliasisi Tanganyika Railways African Union (TRAU) akiwa Rais na Kassanga Tumbo Secretary.
Mchango wa babu yangu katika vyama vya wafanyakazi wa Tanganyika ni mkubwa sana ingawa historia bado haijamtambua.
View attachment 1312692
Kushoto ni Salum Abdallah Rais wa TRAU akivishwa mgolole kama ishara ya kiongozi wa mapamabano na wa mwanzo kulia Christopher Kassanga Tumbo Katibu wa TRAU
Salum Abdallah aliongoza migomo mitatu ya wafanyakazi wa reli na migomo hii ikaenea nchi nzima dhidi ya wakoloni 1947, 1949 na 1960, mgomo wa mwaka wa 1960 ukidumu kwa siku 82 rekodi ambayo bado haijavunjwa inawezekana Afrika nzima kwani mgomo mkubwa na mrefu ulikuwa siku 62 ulioongozwa na Makhan Singh, Kenya.
Nina mswada wa Dr. Vedasto Kyaruzi katika Maktaba yangu, ''The Muhaya Doctor.''
Hakuna popote amasema kuwa yeye aliasisi TAA.
TAA hakikuwa chama kipya bali ni ile ilie African Association ilibadilishwa jina mwaka wa 1948 ili kuitofautisha na African Association ya Zanzibar.
Ungependa na kwa hakika nafsi yako na wengi wanatamani kama labda Dr. Kyaruzi angeanzisha TAA kama chama kipya na Nyerere akawa muasisi pekee wa TANU lakini majaaliwa hayakuwa hivi.
Ushahidi wa historia hii unasema vinginevyo.
Historia ya vyama hivi viwili nimeiandika kutokana na Nyaraka za Sykes na sasa imetiwa katika Dictionary of African Biography (DAB) mimi nikiwa mwandishi.
Ikiwa wewe hukubaliani na historia hii itabidi uje na ushahidi kuthibitisha hayo unayoyatamani yawe.
Kunishambulia mimi kama mtu binafsi badala ya kuleta ushahidi wa hiyo historia unayotamani iwe hakutobadilisha ukweli wa historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
Sent using Jamii Forums mobile app
Iselamagazi,Mkuu Mohamed Said, ni kweli kuwa Dr. Vedasto Kyaruzi hakuwa muasisi wa TAA japo ungekuwa muungwana kwa kukiri kuwa alionyesha mchango mkubwa ktk kui-shape TAA.
Kwanza alikuwa Katibu wa TAA Tawi la Makerere mwanzoni mwa mwaka 1942 wakati akiwa Uganda kwa ajili ya masomo.
Kipindi hicho Mwl. Nyerere hakuwa active kisiasa na wote wawili walikuja kutana pale Makerere University mwaka uliofuata - 1943.
Pia Dr. Kyaruzi aliporudi Tanganyika 1948 aliendekea kuwa mwanachama hai wa TAA na alikuta chama kimepooza sana kikiwa kimejaa wazee wa kiswahili na illiterate wasiokuwa na mikakati madhubuti ya kumuondoa mkoloni. Hakuna vikao vya kimkakati vilivyokuwa vikiendelea na wazee hao walijitenga na wasomi - akina Dr. Kyaruzi na wenzake wachache.
Baada ya rais wa TAA wakati huo Dr. Luciana Tsere mnamo mwaka 1950 kuhamishiwa Tanga, Dr. Kyaruzi alichukuwa urais wa TAA wakati huo wazee wakikataa vikao halali.
Hata hivyo, Dr. Kyaruzi alifanyiwa figisu na wakoloni baada ya kuona TAA imetekwa na wasomi na aliambiwa akasome kule Ulaya.
Hakwenda na bado alipewa transfer kwenda Morogoro ktk gereza la Kingolwira kama MO in-charge.
Mwl. Nyerere ndipo alipoingia TAA na kuwa rais akipewa kijiti na Dr. Kyaruzi (RIP).
Mkuu Mohamed Said, kama hutambui mchango wa Dr. Kyaruzi ktk kuijenga TAA sema.
Sent using Jamii Forums mobile app
You've posted this shit ad nauseam miaka na miaka hadi inatia huruma. Kwa kifupi, umeishiwa Mzee Mohamed Said. Huna uwongo mpya.Inawezekana tatizo ni kuwa hatufahamiani.
Inaelekea wengi wenu ndiyo kwanza mnasoma historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kama nilivyoaindika miaka 22 iliyopita na ndiyo maana mmepata mshtuko mkubwa ambao kwa bahati mbaya imesababisha taharuki kwenu kupelekea kuandika katika njia si ya kiungwana na pia kutoa vitisho dhidi yangu na kuitaka serikali ifanye kadha wa kadha dhidi yangu.
Mnadhani kuwa sifahamiki.
Ingekutosheni tu kwa kuona kuwa naandika kwa jina langu halisi na picha zangu zipo mnaziona.
Ombi langu kwenu ni kuweni watulivu someni historia hii kwani kuna wengi wamenufaikanayo.
Tufahamiane:
- PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
- The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
- The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
- Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
- Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
- Uamuzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
- Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam.
- Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
- Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigani Uhuru wa Tanganyika Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaaam
- Watu Mashuhuri Katika Kuulingania Uislam Tanzania, Sheikh Ilunga, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
- Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam
- The School Trip to Zanzibar, Africa Proper Education Network 2020, Dar es Salaam
- In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
- Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
- Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
- The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
- Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
- The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
- Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
- Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
- Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
- Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
- Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
- 14. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
- Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
- Awards: Several Awards
- Visiting Scholar: (2011)
- University of Iowa, Iowa City, USA
- Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
- Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin.
- OTHER COUNTRIES VISITED
- Zambia, Ethiopia, Great Britain, Swaziland, Msumbiji, Zimbabwe, Zambia, Sudan, Egypt, Saudi Arabia, United Arab Emirates, Oman, Yemen, Uganda, Switzerland, Iran, France, Netherlands, Turkey and Abu Dhabi.
Ndjabu...You've posted this shit ad nauseam miaka na miaka hadi inatia huruma. Kwa kifupi, umeishiwa Mzee Mohamed Said. Huna uwongo mpya.
Wengi tushakuzoea Mzee Mohamed Said. Umeishiwa huna jipya sasa unakuja na promo ya hii "The School Trip To Zanzibar". Sarakasi hizi.Ndjabu...
Hapana haja ya kutukana.
Nitaweka mara nyingi kwa kuwa wako wengine ndiyo leo ananisoma na hujua huyu mgeni kutokana na maswali na namna anavyoandika.
Hii ndiyo sababu najirudia.
Niko hapa kusomesha na mwalimu siku zote hurrudia masomo yake kwa wanafunzi wapya.
Kuishiwa si kweli nimeongeza vitabu sita nilivyoandika na vimetoka mwezi uliopita viezi vitano na cha sita kimetoka siku ya mwaka mpya 2020:
- Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam.
- Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
- Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigani Uhuru wa Tanganyika Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaaam
- Watu Mashuhuri Katika Kuulingania Uislam Tanzania, Sheikh Ilunga, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
- Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam
- The School Trip to Zanzibar, Africa Proper Education Network 2020, Dar es Salaam
Ndjabu...Wengi tushakuzoea Mzee Mohamed Said. Umeishiwa huna jipya sasa unakuja na promo ya hii "The School Trip To Zanzibar". Sarakasi hizi.
Ndjabu...Wengi tushakuzoea Mzee Mohamed Said. Umeishiwa huna jipya sasa unakuja na promo ya hii "The School Trip To Zanzibar". Sarakasi hizi.
The boy tz,Sitaki kuifundisha serikali kazi yake sisi tunasambaza upendo wengine wanasambaza udini na chuki kuna watu wameota mapembe ni yakukata sasa.
Bagamoyo,Maswali mengi sana kwa Mohamed Said, mimi kama kijana naona ktk majibu yako mengi huku ukutumia utulivu mkubwa nikupongeze, ila naona kila namna ya watu wametoa mchango wao ktk uhuru wa Tanganyika.
Wapo Wazulu toka Mozambique / South Africa , wapo 'Wanyasa' wa Malawi, Wadengereko, waSomali, Wahindi, Watu wa Kigoma , watu wa Kaskazini mwa Tanganyika, watu wa Nyanda za juu Kusini, WaComoro , WaZanzibari n.k ila hili la kuwafuta asili yao na kuwaweka ktk makundi ya udini wao ndiyo umeharibu hali ya hewa ktk kazi yako nzuri. Wengine walibadili dini ili wazee wake au makazi mjini au nafasi za masomo n.k
Maana kwa kuweka majina yao na asili yao unaweza kuwatambua mchango wao ila kwa kuweka dini yao na kuficha asili/maeneo watokayo hujaitendea haki historia.
Bagamoyo,
Haikuwa kila mtu kama unavyosema.
Kila mtu ilikuja baada ya Uchaguzi wa Kura Tatu mwaka wa 1958.
Juu ya haya yote hata kama wewe na wengineo haiwapendezi mchango wa Waislam haukuwa na mfanowe.
Huu ndiyo ukweli na ndiyo historia ilivyokuwa.
Sasa ikiwa historia hii imefutwa ndiyo ilitakiwa mimi niiache ipotee?
Bahati nzuri historia hii ya TANU na uhuru wa Tanganyika ni historia ya wazee wangu sikuweza kustahamili kuona imefanyiwa khiyana ilikuwa lazima niiandike.
Sasa kuandika historia hii lakini niache vitu muhimu kwa kuhofu ati nisieleze historia kama ilivyokuwa hili kwangu halikuwezekana.
Sent using Jamii Forums mobile app
Bagamoyo,Mohamed Said,
Swali moja Maalim, swali ni nini kilikusukuma kufuta asili ya hawa wapigania uhuru na kuwatambulisha kwa 'dini za kuja' wakati sisi ni watu huru wenye historia ya majina yetu, asili zetu, tamaduni zetu, mila na desturi .
Kuweka nyuma asili zetu Huoni unautia doa uhuru waliogombania mababu hawa ambao walijitambua kama waTanganyika lakini unafuta asili zao na kuwatambua kwa kuwatia uasili wa Mashariki ya Kati chimbuko la dini hizi?
Bagamoyo,January 6, 2020
Ujiji, Kigoma
Mzee Juma Ambrose na Simulizi za vuguvugu la kutambuliwa uasili wao kuelekea Uhuru
Wabembe na Wagoma wa Ujiji wakataa kutupa utambulisho na utamaduni wao mbele ya Waarabu.
Mzee Juma Ambrose asilimulia jinsi wazee wa Ujiji walivyowadindia Waingereza na Waarabu, kisa majina yao kutotamkwa vyema na haiwezekani washurutishwe watupe Miungu yao ya kiasili kirahisi na kukumbatia Miungu ya Dini za kuja.
Wazee wa Kigoma Ujiji wanasema Miungu yao ya Asili ndiyo kitambilisho chao, mfumo wao na ndiyo salama yao. Nyumba maarufu ya Tanganyika House na milango ya vyumba vyake asili yake ni nini. Magonjwa ya Mizimu ya Kale dini hizi za kuja haziwezi kuyapoza lazima utaratibu wa mila ufuatwe Mzee Juma Ambrose anaendelea ktk simulizi sahihi za sisi ni kina nani kama waTanganyika...na matokeo yanakuwa mazuri watu wanaishi salama bila bughudha za dini za kuja...
Mambo haya ya asili yanatuunganisha kwani yanafanana ktk jamii ya kiTanganyika hata unaweza kukabidhiwa mikoba uwashikie watani zako kujilinda hawa watu wa kuja na mashua wakikubadilikia anaendelea kuelezea umuhimu kuweka asili mbele Mzee Juma Ambrose...wa Ujiji Kigoma Tanganyika.
Sasa natambua kwanini waTanzania wanakuja juu kutambulishwa kwa makundi ya dini za kuja badala ya mchango wao kama wao ktk kuunda nchi huru Tanzania.
Source: Dar24 Media
Kwa hiyo naweza kwenda Saudia tena Maka nikafungua Kanisa na kuanza kueneza Injili kwa vibali pasipo kujali katiba yao inasema nini na wakanikubalia?Bagamoyo,
Katika Uislam hakuna kushurutishana katika mambo ya dini.
Bwana Ambrose ana haki ya kuamini akitakacho na hairuhisiwi kumbughudhi madam yeye hajawafanyia uadui wengine.
Haya ndiyo mafunzo ya Uislam.