Kitabu kipya: Tanzania na propaganda za udini na prof. Ibrahim Noor



Naona Dr FaizaFoxy at it best.

Jitahidi sana kujaribu kuwaingiza ujinga vijana wasiojishughulisha.

Uarabu ni lugha kwa maana ni lugha ya kiarabu itokanayo na Waarabu.
Utakuwa mmoja wa Waarabu Koko ashkum si matusi!
 
Last edited by a moderator:
Wana jamvi ili kujadili mada hii kwanza tungetafuta hichi kitabu tukaona mwandishi amenena nini na upi ushahidi wake kuhusu alicho andika. Mada inakosa raha kama tutaanza kuzungumzia udini ambao ndio huo unaotajwa katika hicho kitabu.
Pia changamoto hebu tuangalie historia ya hizi Chifdom zili zokuwepo kabla , tuangalie
Machief wa wanyamwezi , unyanyembe kina FUndikira asili yao nini
Tuwaangalie Wangoni na asili yao
Pia wasambaa
Zaramo , kina Bushiri , kinjekitile , mkwawa na wahehe , na tusiishie hapa tuvuke mpaka Uganda kwenye ufalme wa buganda tusome historia yao ...hakika utaona wazi waraabu walifika hapa zamani sana sio kutawala bali kuishi.na waliwakuta wenyeji wa nchi hizi wengi wao wakiwa tayari ni waislam .
Historia ya waoman kufika pwani hii ni ya karibuni sana , na wao hawana athari yoyote katika dini , kwani walikuta tayari wenyeji wamejichanya na waraabu kutoka hejaaz ndio maana madheheb ya huku hayakua ya waoman ambao wengi ni Ibaadhi lKini ni sunni.
Tukitafute hichi kitabu thn tukijadili
 

Muislamu hata asome vipi haelimiki hata siku moja!
 
Mkuu PTER, naomba kutofautiana na wewe, kwa sisi watu wa kutafuta maarifa na kupata ufahamu, kila kinachoandikwa is worth reading, ndio maana kina sisi tumesoma hadi Kuruani na kuidismiss, vivyo hivyo wanazuoni wa Kiislamu wamesoma Biblia na kuidismiss!. Nawashauri wale schollars wetu wa humu, tukisome kitabu kisha ndipo turudi humu with facts.

Mwanzo tuu niliisha smell hiki kitabu is a problem, namna ya ku deal na problem is facing the problem, not running away from the problem, hivyo nashauri tukisome ndipo kisha tuje humu kukibonda!.

Pasco
 
Kitabu kinatuminisha kuwa mapinduzi ya Zanziber hayakuwa halali..kwakuwa Sultan alikuwa mwenyeji kuliko wabantu
 
Naona Dr FaizaFoxy at it best.

Jitahidi sana kujaribu kuwaingiza ujinga vijana wasiojishughulisha.

Uarabu ni lugha kwa maana ni lugha ya kiarabu itokanayo na Waarabu.
Utakuwa mmoja wa Waarabu Koko ashkum si matusi!

Waarabu ni Waarabu kwa kuwa wanaongea Kiarabu. Simpo, si rangi, si taifa, si kabila, ni kama kusema "gypsies".

Maana ya Arabiya ni "Caravan" au msafara, hawa walikuwa ni watu wa misafara toka enzi na enzi na lugha yao ndiyo hicho Kiarabu, ndiyo maana kikazagaa sana Mashariki ya kati na barani Afrika, Magharibi ya Asia walienda tu kwa kuwa kulikuwa hakuna kizuizi cha kuwafikisha huko. Kumbuka kuwa mpaka wa asili wa makotinenti ni bahari, na baina ya Afrika na Asia magharibi kulikuwa hakuna mpaka wa bahari mpaka juzi juzi tu ulipochimbwa mfereji wa Suez.

Waarabu, Afrika na Asia Mashariki hawakuja kama wazungu, Waarabu kwingine ndiyo walikwenda, Afrika na Asia ni "wondering ground" ya misafara "Arabiya" (from time immemorial).
 

Licha ya pwani, naomba unielimishe asili ya Wairaqw (kabla sijauliza asili za wengine), walitokea wapi? walifika lini huko Mbulu?

Hapo sasa!
 
Hapa nimepata definition mpya ya Uarabu, kumbe ni lugha tu, sio kabila wala rangi, kwa hiyo hata wewe kama unazungumza kiarabu basi ni muarabu?, hata mzungu wa ulaya akiwa mzungumzaji wa kiarabu hatumuiti mzungu tena bali anakua ni muarabu?

Kama ni lugha mama kwako, naam, hakuna wakupinga hilo. Lakini kama umejifunza tu kama mimi, hapo ni muhali.
 

Adolay,
Siku zote nimekuomba ushahidi wa tuhuma zako lakini hujaweza kuleta huo
ushahidi.

Unajitisha wewe mwenyewe na unawatisha watu wengine pasi na sababu.
Kwa faida ya wageni wetu hapa Majlis naweka kazi (baadhi) nilizoandika:


1. The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.

2. The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press 2006, Nairobi. (Children's book).

3. Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.

4. Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
5. Uchaguzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.

6. In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
7. Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).

8. Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
9. The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).

10. Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).

11. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).

12. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000' (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15[SUP]th[/SUP] – 17[SUP]th[/SUP] 2003).

13. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27[SUP]th[/SUP] February – 4[SUP]th[/SUP] March 2004).

14. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA)Morogoro 11[SUP]th[/SUP] April 2004).

15. Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8[SUP]th[/SUP] - 10th February 2006).

16. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21[SUP]st[/SUP] Century 1[SUP]st[/SUP] - 3[SUP]rd[/SUP] August 2006, Kenyatta University, and Nairobi.

17. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg. The paper was also presented at Islamic Propagation Centre International (IPCI) Durban.

18. Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.

Visiting Scholar (2011):
University of Iowa, Iowa City, USA
Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin, Germany
 

Ukienda mpaka Afrika ya Kusini unakuta jina Shaka Zulu, kumbuka kuwa "Shaka Zulu" si jina la mtu hiyo ni "title" ina maanisha Sheikh wa Wazulu" neno Shaka ni Sheikh, sasa jiulize kulikoni huyu jemedari mkuu wa Wazulu aitwe Sheikh? Jina lake halisi ni "Shaka" kaSenzangakhona kaJama, hiyo "ka" ni ya heshima Kizulu.

Tuna mengi sana ya kujifunza lakini kuna watu humu muono wao hauzidi urefu wa pua zao, wakishaona jina la Kiislaam basi, wao wanapata mchecheto na kutaharuki bila mfano.

Hiyo ndiyo ukisikia Islamophobia.
 
Kitabu hiki kipigwe marufuku na serikali tukufu ya Tanzania.......ova!!!
Tim Choice,
Kisome kwanza kitabu cha Prof. Noor ikiwa utakiona kuwa hakifai
kusomwa Tanzania basi ndipo utoe ushauri wa kupigwa marufuku.

Hata hivyo dunia ya leo ni taabu sana kupiga marufuku kitabu.
Mtandao umebadilisha mengi.

"Mwembechai Killings..." cha Prof. Hamza Njozi kimepigwa marufuku lakini
hapa nilipo nikiingia Google kitabu tayari ninacho.

Hili la kwanza.
La pili serikali utaitwishwa mzigo wasioweza kuihimili.

Zipo shutuma nyingi dhidi yake kutoka kwa Waislam.

Sasa ikija tena kupiga marufuku kitabu hiki kwa kuwa tu kinarekebisha uongo
katika historia serikali itajiweka pabaya katika macho ya Waislam.

Itabidi pia ipige marufuku kitabu cha Abdul Sykes.
Acha kitabu kisomwe na watu wajadili kwa manufaa ya jamii yetu.

Hiyo "serikali tukufu," ni yetu sote.

Kubwa zaidi wazee wetu walijitolea sana katika kupigania uhuru wa nchi hii
ili sote tuwe huru.

Hawakupigania uhuru wa Tanganyika ili tuje kukaliane vichwani.
 
Mohamed

Hizi historia za ku-brainwash wajinga.

Ujinga na upumbavu wakuchochea ubaguzi na chuki za kidin

Ujinga na upumbavu wa kuongelea wazee wako wa gerezan na K/koo kisha unadiriki kuiita historia ya Tanzania

Ujinga na upumbavu wa kushupalia MOU za wengine ukiulizwa umewezesha MOU ngapi tangia pale Kikwete aliposema ruhusa kwako na kwa yeyote kupeleka MOU Yeye Kikwete atasain-Chaajabu hujatumia elimu yako kuhakikisha unawasilisha MOU mapema na muda upo ukingoni wewe msomi feki unabwabwaja nakulia nahistoria kufanya mambo umeshindwa zaidi ya uchochezi.

Mohamed hunalolote zaidi ya chuki na ubaguzi. Wewe nimsomi mjinga alieathilika vema kwa elimu uloipata utotoni utakufa na wivu, choyo na rohombaya.

Goodday mohamed.


 
Muislamu hata asome vipi haelimiki hata siku moja!

Qur'an 3:66.
Angalieni! Nyinyi mlibishana katika yale mliyo yajua. Mbona sasa mnabishana katika yale msiyo yajua? Na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye, na nyinyi hamjui.
***
 

= aliyeathirika

Mbona povu linakutoka? tatizo lako ni nini?
 

Adolay,
Umeghadhibika na ndiyo maana baada ya kuleta ushahidi niliokuomba umerejea
na tenga la matusi.

Wazee wangu na historia ya Tanganyika...

Unaweza ukaikataa kuwa hiyo siyo historia ya TANU wala si historia ya kupigania
uhuru wa Tanganyika.

Chuo cha TANU Kivukoni waliikataa historia ya akina Abdul Sykes na Sheikh
Hassan bin Amir, Idd Faiz Mafongo na wengineo kuwataja wachache.

Haikuwa kitu.

Kitabu walichoandika bila ya kuwataja wazalendo hawa kipo na kitaendelea
kuwapo na kitasomwa hadi mwisho wa dunia In Sha Allah.

Mimi sikughadhibika kwa nini babu yangu Salum Abdallah hayumo kwenye
historia juu ya mchango na fedha alizotoa kusaidia TANU.

Wengi kama yeye hawakutajwa.
Haijawa neno la watu kutukanana.

Kuwa nina chuki, roho mbaya na wivu huo ni mtazamo wako.

Oxford University Press na wachapaji wengine wananiona ni mwandishi makini na
wananichapa na kuuza vitabu vyangu.

Vyuo Vikuu vingi wananiona ni msomi makini wananialika kwao kuzungumza.

Radio maarufu duniani VOA, BBC na nyiinginezo wanafanya mahojiano na mimi kwa
mada wapendazo...

Sitakujibu kuhusu MoU kwa kuwa haina maana.
Muhimu ni kuwa jitulize punguza hasira.

Hasira ni kitu kibaya kinaharibu chombo kilichokuwa ndani yake.
 
= aliyeathirika

Mbona povu linakutoka? tatizo lako ni nini?
Maalim Faiza,
Siku zote huwaambia kufunya mjadala na Mohamed Said si mchezo kwani
kenda chuoni akiwa na miaka sita wao wanakwenda chuoni watu wazima
weshapea chembelecho FaizaFoxy.

Maana yake hata ile adabu ya mnakasha hana.
Anatukana bila aibu wala uoga.
 
Ukiona kilasiku unaungwa mkono na kundi la walewale ulowabraish ujuwe mjinga tu Wewe.

Mpumbavu mwezio ambaye kwake udini ni sera na kila kitu anasahihisha makosa ya speling kichwan umemjaza ujinga na upumbavu kila unapokanyaga nayeye huyo kafika kukusapoti na kuturekibisha uchapaji nakutetea lolote mjinga wewe unaandika.

Wewe kazi yako kupeperusha madai ya udini muda wote unadhani Taifa hili kila mmoja akifanya madai tutaishi? Jifunze kuvumilia, faham kwamba kila mmoja wetu anamadai mjinga wewe.

Wakristu wakifanya kama wewe zezeta watadai yafutayo
-shule zao zamsingi na sekondari
-hospitali zao
-Ardhi zao nk
Vyote hivyo Nyerere aliwapokonya kwafaida yako, mimi na wengine.

Wasambaa watadai milima ya usambaa

Wachaga watadai mlima kilimanjaro

Budha watasema hapa kuchinja ng'ombe maana ni Mungu wao

Wapagani watapinga uapishwaji kwa kutumia biblia na kuruwan

Kila mmoja anamadai kwa ushenzi wako unachochea ilituvurugane, tuuwane alafu utapata nin wewe mtumwa wa chuki na ubaguzi wakidin?

Unataka ushahidi wakitugan yaani imefikia huna Akili kufaham unafanya nini na historia zako?

Mim naamin kabisa utasumbuka mpaka utakufa utaiacha Tanzania nawatanzani wote kwa ujumla wao (waislam,wakristu, iman zingine nawasioamin) wakiwa salama.

Mungu atakuadhibu maana hawezi acha ukafanya uchochezi kiasi hiki damu za watu wasio nahatia zikamwagika.


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…