Kitendo cha Jaji Mkuu kutambua nafasi ya Makamu wa Rais Bara kama Makamu wa Pili; Je, ni bahati mbaya ama?

Wasalaam,

Ni zaidi ya mara tano Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma Juma anatamka au kutaja kwa nafasi zao Makamu wa Rais kuwa Makamu wa pili wa Rais .

Je, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuna Makamu mmoja tu wa Rais ;

Kwa mjibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara 47.-(1) inasema; "Kutakuwa na Makamu wa Rais ambaye atakuwa
ndiye Msaidizi Mkuu wa Rais kuhusu mambo yote ya Jamhuri ya Muungano kwa jumla",

Sheria ya 1994Na.34 ib.1,
Sheria ya 2000Na.3 ib.9.
"MKAMU MMOJA
WA RAIS",

Katika hii video Profesa Ibrahim Juma Juma kwa nyakati tofauti amekuwa akimtaja Makamu wa Rais wa Tz kama Makamu wa pili wa Rais.

Amefanya hivyo kwa Rais Samia akiwa Makamu wa Rais wa Hayati Magufuli na amefanya hivyo kwa Dkt Isdor Mpango na kumtaja kuwa Makamu wa pili wa Rais.

Je ni ulimi kuteleza ?
Ni Makusudi
Au anajua sana Katiba na sheria zake mbona amekuwa akitaja bila woga?

Hii hapa video

Your browser is not able to display this video.
 
We unapoona rais wa zanzibar ameanza kumwakilisha rais wa jamuhuri huku makamu wa rais yupo unaelewa nini
Kipindi cha kimoja , Rais wa Zanzibar alikuwa makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu alikuwa makamu wa pili wa Rais... Mh. John Samwel Maleccela ndio alikuwa Waziri Mkuu wa mwisho kuwa na cheo hicho cha Makamu wa pili wa Rais.I stand to be corrected.
 
Anajua anachokifanya wamchokoze waone.

Joka ukilifuga mwenyewe....
 
Jaji wa hivi anaweza kukufunga kifungo cha maisha au hata kunyongwa kwa sababu ya Slip of the Tongue
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…