Kitendo cha Jaji Mkuu kutambua nafasi ya Makamu wa Rais Bara kama Makamu wa Pili; Je, ni bahati mbaya ama?

Kitendo cha Jaji Mkuu kutambua nafasi ya Makamu wa Rais Bara kama Makamu wa Pili; Je, ni bahati mbaya ama?

Mh. John Samwel Maleccela ndio alikuwa Waziri Mkuu wa mwisho kuwa na cheo hicho cha Makamu wa pili wa Rais.I stand to be corrected.
Kwa kuwa rais alikuwa Mwinyi toka Zanzibar, waziri mkuu toka bara alikuwa makamu wa kwanza.

Wa mwisho kushika wadhifa huo alikuwa Cleopa Msuya baada ya Malecela kuondoshwa kwa shinikizo la Nyerere.
 
nchi hii inachosha sana. ninaomba Mungu wanangu wasiiahi nchi hii yenye watawala wapuuzi.
 
  • December 9 2020
  • February 19 2021
  • May 17 2021
  • October 11 2021
Jaji Mkuu katika tarehe hizo hapo juu kuwatambua makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ( Mgombea Mwenza wa Rais JMT ktk uchaguzi) kama makamu wa pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Ukijenga muungano juu ya udongo na mchanga(pun😀😀) lazima mbele ikuletee shida
 
☝☝☝☝
Hapa inabidi wamkaribishe wakili msomi Tundu Antipas Lissu aje atufafanulie kauli ya Jaji Mkuu wa Tanzania kuhusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia 2020 kuwa na Makamu wa Pili wa Rais ktk serikali ya Muungano wa Tanzania.

Je rais wa Zanzibar SMZ aliye mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar BLMZ walimshindikiza hayati mwendazake John Pombe Magufuli kutambua ukubwa wa Rais wa SMZ aliye mwenyekiti w BLMZ katika serikali ya Muungano wa Tanzania?

Na ndiyo maana Hayati rais John Magufuli wala Mh. Samia Suluhu Hassan rais wa Jamhuri ya Muungano hawajatia neno kuhusu Jaji Mkuu wa Tanzania kutambua uwepo wa kiaina wa Makamu wa Pili wa Rais ktk serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka hapo katiba itapobadilishwa na kutambua uwepo wa Makamu wa Kwanza na Makamu wa Pili wa Rais ktk serikali ya Muungano wa Tanzania ili kumuweka panapostahili kiitifaki / kiprotokali Rais wa SMZ ktk Setikali ya Muungano wa Tanzania.


Haiwezekani rais wa SMZ atambulike kama mjumbe aliye na wadhifa wa uwaziri ktk mkutano wa baraza la mawaziri wa Muungano ( kabineti). Wakati rais wa serikali ya SMZ kiitifaki kwa sasa ni mkubwa kuliko Makamu wa Rais wa JMT pia ni mkubwa kuliko Waziri Mkuu wa JMT.

Rais wa SMZ anaongoza nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano, ana bendera ya rais wa SMZ ana vikosi maalumu, KMKM na valantia katika nchi ya Zanzibar, ana uwezo wa kuvunja Baraza la Uwakilishi Zanzibar pia kuitisha uchaguzi Zanzibar wakati kwa mfano Makamu wa Rais JMT na waziri mkuu wa JMT hana madaraka hayo wala wadhifa unaokaribia U-Amiri Jeshi wa Majeshi ktk nchi.
 
We unapoona rais wa zanzibar ameanza kumwakilisha rais wa jamuhuri huku makamu wa rais yupo unaelewa nini
Filipo ni version ya pili ya Ghalib Bilali....
Mimi siamini kama ni bahati mbaya, kuna master mind wa mchezo huu, ipo siku atakulikana!
 
We unapoona rais wa zanzibar ameanza kumwakilisha rais wa jamuhuri huku makamu wa rais yupo unaelewa nini
Mkuu madaraka yanapatikana kwa mujibu wa sheria siyo kwa itifaki.

Hebu tuonyeshe sharia ipi inayosema rais wa Zanzibar ni makamu wa rais au wapi inasema akimuwakilisha rais nje ya nchi anakuwa makamu wa rais?
 
We unapoona rais wa zanzibar ameanza kumwakilisha rais wa jamuhuri huku makamu wa rais yupo unaelewa nini
hivi Makamu wa Rais, na Rais wa Zenji, nani mkubwa? mbona sijaelewa hapo.
 
Sio kweli. Marekebisho ya Katiba ya 1992 yaliyoruhusu Mfumo wa Vyama Vingi yalimuondoa Rais wa Zanzibar kama Makamu wa Rais. Sasa hivi anatambulika kama RAIS WA ZANZIBAR, MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI ZANZIBAR NA MJUMBE WA BARAZA LA MAWAZIRI LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.
kwahiyo huyu Ibrahim juma tumfanyeje ?
 
Acha kupotosha, Rais wa Zanzibar anakuwa mjumbe wa baraza la mawaziri kwa nafasi yake kama rais wa Zanzibar yeye sio sawa na mawaziri wengine wa kisekta ambao ndio wapo chini ya Waziri Mkuu.
Na wakifuata rank anaanza Rais, Makamu wa rais, Rais wa Zanzibar na anayefuata ndio Waziri Mkuu.
Hapa kuna utata wa kikatiba.

Rais wa Zanzibar mamlaka yake yako limited kwa Zanzibar peke yake na Waziri mkuu ana mamlaka kwa Jamhuri ya Muungano iweje kiitifaki rais wa Zanzibar awe juu ya waziri mkuu ???
 
Uko sahihi Mkuu. Lakini, out of good will, wakati wa vikao vya Baraza la Mawaziri, kulia kwa Rais akikaa Makamu wa Rais basi kushoto kwake anakaa Rais wa Zanzibar. The reverse is true.
Unafanyika kiitifaki tu lakini kikatiba kuna utata
 
Naomba nikusahihishe. Katiba inawataja Rais, Makamu wa Rais, Spika wa Bunge na Jaji Mkuu ndio wanaoweza kuongoza nchi kama mmoja hayupo kwa mfuatano nilivyoandika. Waziri Mkuu hayumo!
Kifungu kipi cha katiba mkuu ?
 
____________________________________________________________________
Katiba ya Zanzibar ya 1984
SURA YA KWANZA
ZANZIBAR

Sehemu ya Kwanza
Zanzibar
1. Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la
Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka
na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
2.Zanzibar ni miongoni mwa Nchi mbili zinazounda Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
2A. Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali, Rais
aweza kuigawa Zanzibar katika Mikoa, Wilaya na maeneo mengineyo
kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Baraza la
Wawakilishi.
3.(1) Kutakuwa na Muhuri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
ambao alama yake itakuwa kama itavyokubaliwa na sheria iliyotungwa
na Baraza la Wawakilishi.
(2) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itakuwa na uwezo wa
kuweka kitu chochote kitachokuwa kielelezo cha Serikali kama
itavyokubaliwa na sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
4. Katiba hii ni Katiba ya Zanzibar na itakuwa na nguvu za kisheria
nchini kote na isipokuwa kutokana na kifungu 80 ikiwa sheria yoyote
inatofautiana na Katiba hii, basi Katiba hii ndiyo itayokuwa na nguvu
na sheria hiyo itakuwa batili kwa kiwango kile ambacho kinahitilafia

Soma zaidi :

Source : Katiba ya Zanzibar, toleo la 1984 pamoja na masahihisho ya 2010
 
SURA YA NNE
Serikali
Sehemu ya Kwanza
Rais

26.(1) Kutakuwa na Rais wa Zanzibar ambaye atakuwa Mkuu
wa Nchi ya Zanzibar, Kiongozi Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
(2) Mtu yeyote anaweza kufaa kuchaguliwa kuwa Rais ikiwa:
(a) ni Mzanzibari wakuzaliwa; na
(b) ameshatimia umri wa miaka 40; na
16


Soma zaidi source :

Katiba ya Zanzibar, toleo la 1984 pamoja na masahihisho ya 2010
 
Yawezekana ndivyo anavyoelewa, ambapo ni tofauti na katiba.
Labda alikariri kabla ya mabadiliko.
Aulizwe mwenyewe atoe ufafanuzi.
Ni sawa na juwauliza watu kwa nini mtu fulani anasema 1+1=3, watakujibu nini?
 
Mimi naona ni bora hivyo maana huyu makamu wa rais tuliye nae huku ni kichekesho tosha
 
Hapa kuna utata wa kikatiba.

Rais wa Zanzibar mamlaka yake yako limited kwa Zanzibar peke yake na Waziri mkuu ana mamlaka kwa Jamhuri ya Muungano iweje kiitifaki rais wa Zanzibar awe juu ya waziri mkuu ???
Hata huyo waziri mkuu mamlaka yake yanaishia Tanganyika kule Zanzibar hana ubavu wa kumwajibisha yeyote.
Zamani Rais wa Zanzibar ilikuwa akitaka kugawa mipaka upya ya wilaya na mikoa basi lazima ashauriane na Rais wa muungano lakini baadaye wakafanya marekebisho ya katiba wameondoa kipengele hicho sasa anaamua bila ya kushauriana na Rais wa muungano, yaani kwa ujumla muungano wetu hauweleweki kabisa.
 
Back
Top Bottom