Kitu gani kilikuwa kinamfanya Magufuli amheshimu Edward Lowassa?

Ni hivi,wafanyabiashara ndiyo wapo nyuma ya kundi likijulikana mtandao 1995,kwa kuwa lowasa alikua na doa,mtandao ukamweka mbele jk,jk alinitumia mtandao Kama ngazi ya kufikia ndoto yake,kwa ahadi akitoka yeye atafata mmasai,jk akatumia dola kumshinda mmasai na wafanya biashara wake 2015,ndiyo maana mmasai alikua anataka urais walau wa miaka mitatu ili kupitia bandari warudishe pesa zao
 
Show ya IT ilimalizwa na mafundi wa IT toka NASA,baada ya jk kuomba tafu kwa mjaluo,ndiyo maana jiwe alikua anasema bila jakaya asingekua rais
 
hebu tupe ushahidi kwa hicho unachokisema isije kuwa ni stori za kwenye kahawa
 
Afadhali wewe umesema ukweli, tukisema sisi mnatuporomoshea matusi. Hiyo kitu ilinifanya niachane kabisa na chadema maana ilikuwa ni unafiki wa hali ya juu.

Uporomoshewe matusi na nani, ukweli ni ukweli, lakini ukileta upotoshaji unarejeshwa kwenye mstari.
 
Mwizi mwenzie
 

Nguvu ya Lowassa ingeanza kwa kuleta hao wabunge wa ccm aliosema ataondoka nao. Cdm ilikuwa na nguvu kutokana na kazi ya siasa iliyoifanya toka 2010-2015. Nionyeshe nguvu ya Lowassa baada ya uchaguzi akiwa na zaidi ya mwaka, na sio nguvu ya miezi miwili wakati alikuta chama tayari kina hamasa ya kutosha.
 
hizi stories za kwenye bao na kahawa... zipo versions nyingi sana na hazi make sense kuna urais wa miaka 3? kwa katiba ipi? huwa mnadanganyana hata kuhoji hamjui? hiyo walau wa miaka mitatu kuna urais wa miaka mitatu tanzania? jamani acheni uzuzu
 
unakataa ukweli ambao upo uchi kabisa... unadhani kwa nini mbowe alimkubali lowassa akaona slaa aende zake tu? lowassa alikuwa na nguvu sana na baada ya hapo aliachana na siasa kabisa. alishakata tamaa hakutegemea tena. na haitatokea tena cdm ikawa vile ilikuwa mwaka 2015
 
Mwizi mwenzie.
 
My God hii I'd inedukuliwa , hopefully sio wewe

USSR
 
Hapo umedanganya ndugu yangu,kilichomponza Mbowe ni UKAWA ya Katiba kuona kuwa ukawa inaweza kuwaangusha ccm,sasa pale kulikuwa na vigogo wawili ambao kila mmoja alikuwa anataka urais kwa lazima ambao ni Wilbrod Slaa na Ibrahim Lipumba.Kama mmojawapo kati ya hao UKAWA ingempitisha mgombea Urais 2015 basi mwingine angejiuzulu na kuivuruga vibaya ukawa,hivyo ili kuweka status quo Mbowe akaingia kichwa kichwa kumuweka Lowasa kuwa mgombea urais ambalo lilikuwa kosa la karne.
 
dr slaa na lipumba hamna mgombea urais hapo.... hao wote hamna kitu. lowassa ndo alikuwa karata
 
dr slaa na lipumba hamna mgombea urais hapo.... hao wote hamna kitu. lowassa ndo alikuwa karata
Angekuwa karata vipi wakati alikuwa hajulikani ukawa,labda tunabishana na mtoto aliyezaliwa 2000 mpaka 2004.lakini kama ni mtu mzima huwezi sema bila Lowasa ukawa isingeenda.
 
Tangu kurudi kwa mfumo wa vyama vingi,Hakuna mgombea kutoka upinzani aliyewahi kupata kura nyingi kwenye uchaguzi kumzidi Lowasa. Kidogo labda Mrema na kwa mbali Lipumba,hawa kina Slaa walipata kidogo sana.
Kwa hiyo huwezi kuponda Mbowe kumleta Lowasa, ukweli Lowasa alikuwa asset kwa wakati huo.
Hizi habari za ufisadi ni uzushi tu, kwani hata Magufuli alipong'ang'ana kujenga mahakama ya mafisadi watu wengi waliamini ni kwa ajili ya Lowasa, lakini hakuna aliyemgusa, mahakama ikakosa wateja na sijui kama iliwahi kupata ukiondoa kesi ya mchongo ya Mbowe.
Magufuli alikuwa anajua kwa hakika nguvu ya Lowasa ndio sababu alifanya juu chini kuhakikisha anamrudisha ccm,na yeye mwenyewe anampokea pamoja na kamati kuu nzima.
 
Lowasa alikuwa na ushawishi gani kama ana ushawishi aanzishe chama ndiyo tugundue kuwa ana ushawishi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…