Kitu gani kilikuwa kinamfanya Magufuli amheshimu Edward Lowassa?

Kitu gani kilikuwa kinamfanya Magufuli amheshimu Edward Lowassa?

unakataa ukweli ambao upo uchi kabisa... unadhani kwa nini mbowe alimkubali lowassa akaona slaa aende zake tu? lowassa alikuwa na nguvu sana na baada ya hapo aliachana na siasa kabisa. alishakata tamaa hakutegemea tena. na haitatokea tena cdm ikawa vile ilikuwa mwaka 2015

Mbowe alimkubal Lowassa maana alimpa hela, Slaa alikuwa na hela gani ya kumpa Mbowe? Lowassa hakuacha siasa kwa kupenda bali afya mgogoro.
KuP kurudi kwa mfumo wa vyama vingi,Hakuna mgombea kutoka upinzani aliyewahi kupata kura nyingi kwenye uchaguzi kumzidi Lowasa. Kidogo labda Mrema na kwa mbali Lipumba,hawa kina Slaa walipata kidogo sana.
Kwa hiyo huwezi kuponda Mbowe kumleta Lowasa, ukweli Lowasa alikuwa asset kwa wakati huo.
Hizi habari za ufisadi ni uzushi tu, kwani hata Magufuli alipong'ang'ana kujenga mahakama ya mafisadi watu wengi waliamini ni kwa ajili ya Lowasa, lakini hakuna aliyemgusa, mahakama ikakosa wateja na sijui kama iliwahi kupata ukiondoa kesi ya mchongo ya Mbowe.
Magufuli alikuwa anajua kwa hakika nguvu ya Lowasa ndio sababu alifanya juu chini kuhakikisha anamrudisha ccm,na yeye mwenyewe anampokea pamoja na kamati kuu nzima.

Narudia tena, kama aliweza kuleta kura 6m akiwa na miezi miwili, sema alileta kura ngapi akiwa na mwaka mmoja. Kura za cdm zilipatikana kwa juhudi za cdm wenyewe kutokana na kufanya kazi yake ya siasa. Naona wote mnazunguka tu hakuna anayeonyesha nguvu ya Lowassa baada ya uchaguzi.

Magufuli hakuwahi kupambana na mafisadi, bali alikuwa anakomoa na kulipa visasi kwa aliohitilafiana nao kabla hajawa rais. Alimpokea Lowassa kwenye kampeni yake ya kujibrand ya kuunga juhudi, na sio kwamba alikuwa anamuheshimu. Labda ww ndio ulikuwa unaona ni bonge ya fahari kupokelewa na Magufuli. Isitoshe hiyo mahakama ya mafisadi hakuwa na nia nayo, bali alipora ajenda ya cdm ili kulazimisha kukubalika na umma. Hakuna mtu anayepambana na ufisadi akawa adui wa vyombo vya habari. Sana sana Magufuli alipambana na matumizi ya neno fisadi na sio ufisadi.
 
My God hii I'd inedukuliwa , hopefully sio wewe

USSR

Ni mimi na sijawahi kubadilika kwenye hili toka Lowassa apokelewe ndani ya cdm, au unadhani na mimi ni bendera fuata upepo kama ww?
 
Mbowe alimkubal Lowassa maana alimpa hela, Slaa alikuwa na hela gani ya kumpa Mbowe?
Hapa unakiri kabisa Mbowe alipewa hongo ili kumpitisha Lowassa agombee Urais, hii inaonyesha Cdm sio wa kuamini kuwapa nchi.

Halafu unapodai ndiyo nguvu ya Cdm pekee iliyovutia wapiga kura wengi 2015, Ina maana na wafuasi wa Lowassa (ambao sio Cdm akiwemo) ila walimpa kura akiwa Cdm nao walivutiwa na Cdm na sio Lowassa ?

Huamini kuna maeneo mlipata kura za huruma sababu ya mgombea wenu na sio mvuto wa chama chenu ?
 
hizi stories za kwenye bao na kahawa... zipo versions nyingi sana na hazi make sense kuna urais wa miaka 3? kwa katiba ipi? huwa mnadanganyana hata kuhoji hamjui? hiyo walau wa miaka mitatu kuna urais wa miaka mitatu tanzania? jamani acheni uzuzu
Akisema mwenyewe,labda kwa kujua afya yake kwamba hatoweza dumu kwa awamu yote/zote
 
Hapa unakiri kabisa Mbowe alipewa hongo ili kumpitisha Lowassa agombee Urais, hii inaonyesha Cdm sio wa kuamini kuwapa nchi.

Halafu unapodai ndiyo nguvu ya Cdm pekee iliyovutia wapiga kura wengi 2015, Ina maana na wafuasi wa Lowassa (ambao sio Cdm akiwemo) ila walimpa kura akiwa Cdm nao walivutiwa na Cdm na sio Lowassa ?

Huamini kuna maeneo mlipata kura za huruma sababu ya mgombea wenu na sio mvuto wa chama chenu ?

Hiyo paragraph ya kwanza sijui unamaanisha nini, maana kama hongo inazuia kuwa rais, basi aliyestahili kuwa rais wa nchi hii ni Nyerere tu. Na kwa bahati mbaya uadilifu sio kigezo cha kumnyima mtu uongozi ndani ya nchi hii, na ushahidi upo, labda kama kwenye hili unaoongozwa na ushabiki na unataka uonekane una hoja.

Para ya pili, mimi binafsi kura yangu ya urais niliwapa cdm na sio Lowassa, kwani najua kura ya urais inachangia kupata viti maalum vingi. Nadhani na wapiga kura wengi wenye mtazamo kama wangu walifanya hivyo hivyo. Sitaki kuwasemea wengine maana mimi sio msemaji wao.

Para ya mwisho, Kura za huruma kila mtu anaweza kupata eneo fulani, lakini ushawishi hasa wa kisiasa ndio hutoa kura za uhakika za kupata ushindi. Na kwa upande huo cdm walikuwa nao miaka zaidi ya miwili kabla ya uchaguzi wa 2015.
 
Hapa unakiri kabisa Mbowe alipewa hongo ili kumpitisha Lowassa agombee Urais, hii inaonyesha Cdm sio wa kuamini kuwapa nchi.

Halafu unapodai ndiyo nguvu ya Cdm pekee iliyovutia wapiga kura wengi 2015, Ina maana na wafuasi wa Lowassa (ambao sio Cdm akiwemo) ila walimpa kura akiwa Cdm nao walivutiwa na Cdm na sio Lowassa ?

Huamini kuna maeneo mlipata kura za huruma sababu ya mgombea wenu na sio mvuto wa chama chenu ?
Mvuto wa chama ndiyo jibu tosha ukitaka kujua kuwa CHADEMA ina mvuto Tanzania ona Magufuri badala ya kuwaletea wananchi maendeleo alikuwa anapambana na CHADEMA utafikiri ni Urusi na Ukraine.
 
Dr. Slaa ndio aliyekuwa sahihi, Lowassa alikuja na utapeli kuwa alikuwa aje na wabunge 50 toka CCM kitu ambacho si kweli. Ifahamike CHADEMA ndio chama kilichofanya kazi ya kisiasa kuanzia 2010 baada ya uchaguzi mpaka 2015. Ndio chama kilichofanya mikutano mingi nchini kuliko chama chochote cha siasa ikiwemo ccm. Ndio kilichotoa elimu ya uraia kuliko chama chochote cha siasa. Hayo yote yalifanyika Lowassa akiwa ccm. Kama ni rahisi kupata kura 6m+ ukiwa na miezi miwili kwenye chama, Lowassa angeenda TLP au NCCR kisha apate kura zile. Msitake kumpa Lowassa sifa asiyostahili hata kidogo.
Hakika umenena! Huwa siwaelewi na huyo Lowassa.
 
unakataa ukweli ambao upo uchi kabisa... unadhani kwa nini mbowe alimkubali lowassa akaona slaa aende zake tu? lowassa alikuwa na nguvu sana na baada ya hapo aliachana na siasa kabisa. alishakata tamaa hakutegemea tena. na haitatokea tena cdm ikawa vile ilikuwa mwaka 2015
Ni vigumu watu kuukubaki ukweli huu hasa kama ulikuwa na imani zote kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA wa wakati ule.

Ni kweli chama hicho kilijijenga kabla ya uchaguzi wa 2015, lakini turufu ya Lowasa ilikuwa dhahiri, kwa mwanasiasa anayeamini hakuna rafiki wala adui wa kudumu katika mchezo huu, kuchukua maamuzi aliyoyachukua Mbowe kumkaribisha Lowasa na kumpa nafasi ya kugombea, kila mwanasiasa angechukua uamuzi huo ikiwa ni lengo la kujihakik8shia kushinda uchaguzi.

Hata Mh. Dr. Slaa alishiriki katika mpango ule wa kumkaribisha ila kamamabavyo hakuna mtu katika siasa asiyefika bei, nae bei yake ilifika kwa CCM kumvuta baada ya kuonekana hakuridhika na maamuzi ya chama. Kama kweli mh. Dr. Slaa angekuwa na dhamira ya kweli wala asingekikimbia chama na kulamba matapishi yake kule CCM alikokup8ga kwa zaidi ya miongo miwili!

Tatizo kubwa kwa sisi mashabiki wa siasa hatuangalii hesabu za kisiasa, tunaamini kila ambacho tunakisimamia lazima tuendelee kukisimamia hata kwamba wakati, nyakati na mfumo unapokuwa haupo upande wa chama tukipendacho.

CHADEMA kilijitanua na kupata umaarufu nabupenzi zaidi ya wakati wowote kipindi cha Lowasa!

Tuchukie, tukasirike, tususe.
Huu ndio ukweli
 
Nguvu ya Lowassa ingeanza kwa kuleta hao wabunge wa ccm aliosema ataondoka nao. Cdm ilikuwa na nguvu kutokana na kazi ya siasa iliyoifanya toka 2010-2015. Nionyeshe nguvu ya Lowassa baada ya uchaguzi akiwa na zaidi ya mwaka, na sio nguvu ya miezi miwili wakati alikuta chama tayari kina hamasa ya kutosha.
Mkuu Tindo

Je ni kweli kwamba mathalani Lowasa angeenda ACT na CHADEMA mngemsimamisha Dr. Slaa ni dhahiri kwamba CHADEMA kingepata kura zaidi ya 6m na kumshinda CCM?
 
Hiyo paragraph ya kwanza sijui unamaanisha nini, maana kama hongo inazuia kuwa rais, basi aliyestahili kuwa rais wa nchi hii ni Nyerere tu. Na kwa bahati mbaya uadilifu sio kigezo cha kumnyima mtu uongozi ndani ya nchi hii, na ushahidi upo, labda kama kwenye hili unaoongozwa na ushabiki na unataka uonekane una hoja.
Uliposema Mbowe alipewa hela ili ampitishe Lowassa, inaonyesha mwenyekiti wa Cdm ndio mwenye kauli ya mwisho, ndio maana mlikubali hilo japo baadhi yenu mlifahamu kwamba amepokea mlungula wa Lowassa, huo ni udhaifu mkubwa kwa Cdm.


Para ya pili, mimi binafsi kura yangu ya urais niliwapa cdm na sio Lowassa, kwani najua kura ya urais inachangia kupata viti maalum vingi. Nadhani na wapiga kura wengi wenye mtazamo kama wangu walifanya hivyo hivyo. Sitaki kuwasemea wengine maana mimi sio msemaji wao.
Kusema uliwapa kura urais Cdm na sio Lowassa eti sababu ya viti maalumu ni kujikanganya, ingetokea mfano Lowassa angeshinda na kuwa Rais bado ungebaki na huu mtazamo kwa Urais ni wa Cdm na sio wa Lowassa ?

Kwani ukikiri kwamba kwa upepo uliokuwepo kipindi hicho na mvuto aliokuwa nao kuanzia ndani ya chama chake (japo alitoswa), mpaka kwa wapiga kura uliwanufaisha pakubwa mtapungukiwa nini ?.... Kura za Urais mlizopata (za kihistoria) huwezi kupuuza mvuto wake (japo hakuwa mzungumzaji mzuri ).
 
Pia Magufuli alipoingia Ikulu akagundua Richmond ilikuwa ya Kikwete na Lowassa alichafuliwa tu.
Kupitia issues kama hizi ndiposa mwenye akili hutulia kuzifikilisha akili zake juu ya mustakabali wa taifa.

Wengi wetu ni kama upepo likija jambo hatutaki kutulia, mfano iba, ua, vunja, fanya lolote baya ila kula na waswahili, hao hao ndiyo watakutetea, ooh huyu anaonewa huyu, ooh huyu hapana.

But stand out of them na fanya jambo la maana pasi kula nao uone!.
 
Mkuu Tindo

Je ni kweli kwamba mathalani Lowasa angeenda ACT na CHADEMA mngemsimamisha Dr. Slaa ni dhahiri kwamba CHADEMA kingepata kura zaidi ya 6m na kumshinda CCM?

Cdm sio kura 6m+ tu, walikuwa na uwezo wa kupata zaidi ya hizo, na kubwa kuliko yote cdm wangebaki na haiba yao ya kupinga ufisadi. Tena hizo 6m ni zile ambazo zingetangazwa na tume isiyo huru ya uchaguzi. Lowassa hakutaka kwenda vyama vingine nje ya cdm maana anajua angechafuka zaidi, achia mbali kura za aibu ambazo angepata. Watu walichukua vitambulisho vya kura kwa hasira kwa ajili ya Lowassa, ila siku ya disko ikabidi walicheze hivyo hivyo hata baada ya kukuta DJ ni Lowassa, maana watu walikuwa na kiu ya mabadiliko kuliko kawaida.
 
Uliposema Mbowe alipewa hela ili ampitishe Lowassa, inaonyesha mwenyekiti wa Cdm ndio mwenye kauli ya mwisho, ndio maana mlikubali hilo japo baadhi yenu mlifahamu kwamba amepokea mlungula wa Lowassa, huo ni udhaifu mkubwa kwa Cdm.



Kusema uliwapa kura urais Cdm na sio Lowassa eti sababu ya viti maalumu ni kujikanganya, ingetokea mfano Lowassa angeshinda na kuwa Rais bado ungebaki na huu mtazamo kwa Urais ni wa Cdm na sio wa Lowassa ?

Kwani ukikiri kwamba kwa upepo uliokuwepo kipindi hicho na mvuto aliokuwa nao kuanzia ndani ya chama chake (japo alitoswa), mpaka kwa wapiga kura uliwanufaisha pakubwa mtapungukiwa nini ?.... Kura za Urais mlizopata (za kihistoria) huwezi kupuuza mvuto wake (japo hakuwa mzungumzaji mzuri ).

Alipewa mlungula hilo halina mjadala, nimekuambia hakuna taasisi isiyofanya makosa. Ila uchaguzi wa 2020 kosa lile halikuridiwa tena ndio maana mgombea wa urais alipitishwa na mkutano mkuu wa chama na sio kigenge kidogo. Na kwa kuangalia tu Mbowe alimtaka Nyalandu zaidi, lakini alikosa nguvu kwa wanachama baada ya Lisu kupitishwa na akakaa kwa kutulia.

Naona unanichukulia kwa urahisi, kwa taarifa yako Lowassa angekuwa rais mimi ni moja kati ya wafuasi wa cdm ambao tungekuwa mstari wa mbele kumkataa. Simkatai Lowassa kwa bahati mbaya boss, nalimkataa maana nilijua sio mtu sahihi. Kama tu hata wakati wa uchaguzi nilikuwa nasema kabisa tumeingia cha kike, ndio itakuwa yeye kuwa rais? Kura yangu ya urais niliitoa kwa cdm kama chama, na sio kwa kumkubali Lowassa. Unaweza kwenda kwenye nyumba ya ibada na kutoa sadaka, sio kwa kuwa unamkubali mchungaji, jitahidi kujua mambo haya. Kwa kukusaidia tu, cdm ilikuwa na mvuto maradufu kuliko Lowassa. Lowassa kugombea kupitia cdm ilikuwa ni kama kuokota dodo chini ya mnazi. Lowassa kama alikuwa na mvuto wa kweli angeenda TLP, UPDP apate hata kura 1m ndio ungekuwa na hoja.
 
Alikuwa anajua kuwa bila Lowasa, yeye E3 asingekuwa Rais.

Ufahamu kuwa utawala ulimwandaa Membe kuwa Rais. Wakakata majina ya wote ambao wangesababisha ushindani kwa Membe. Wakamwekea membe washindani dhaifu, wale ambao waliamini wajumbe wa mkutano mkuu, hawawezi kuwachagua. Mmoja wa hao dhaifu kabisa alikuwa ni Magufuli. Mwenye nguvu kubwa aliyekatwa alikuwa ni Lowasa.

Waliotaka kumpa kura Lowasa, wakazira kupiga kura, wakatoka nje ya ukumbi. Baadaye wakaambiwa kuwa wenzao waliobaki ndani ya ukumbi wameanza kugawiwa karatasi za kupigia kura. Wakajadili, na haraka wakakubaliana kuwa kura zao wampe yule asiyetakiwa kabisa ili kumkomoa Jakaya. Na mtu huyo alikuwa ni Magufuli. Wakafanya hivyo.

Kwa ufupi, kura alizozipata Magufuli ndani ya CCM zilikuwa za Lowasa, na Magufuli alilijua hilo.
Muongo ww.....unajua waliopigiwa kura ni wangapi?....kati ya watatu walio pigiwa kura jina la membe lilikuwepo?
 
Back
Top Bottom