Habari za asubuhi watu wa Mungu nyie siyo watu wangu
😎 😎
Leo nimewaza sana kwamba kuna vitu fulani au tabia fulan tunazo maishani zinatufanya tutumie hela rafu na kujikuta mwaka unaisha maisha yako yapo kama ya mwaka uliopita. Kuna baadhi ya mambo yanapelekea tunatumia fedha kidogo tunazopata kuyafanya na kujikuta hatusogei kabisa kimaisha.
Sitoi lecture namna ya kutumia pesa zako. Kwa mimi ntataja baadhi ya vitu vinavyomaliza pesa zangu.
1.0 Gari
Haka kagari yaani kanakula sana sehemu kubwa ya fedha zangu ambazo kananisaidia kuzipata yaani tunaenda paso kwa paso
mafuta, service, urembo( Kila kinachopendezesha gari nikikiona lazima nikitafute kwa garama yoyote, Sport Rims, Profile tyres, Android radio NK.
2.0 Gambe
Yaani nikipata pesa ambayo haikuwa kwenye official mishe zangu lazima niitie kiberiti naweza kupata 70k mchana ikifika usiku nina 10.
3.0 Wanawake
Kuna kipindi nilikuwa na mahusiano na wanawake wa4 aisee, yaani ni kama wana majini siku nikipata hela tu ndio siku hiyo nakumbukwa na kila mmoja, nikipigwa mizinga ya 20k tu kwa kila mmoja 80k ishadondoka nkaachana na watatu amebaki mmoja tu mtarajiwa tu
😎
Ukipata demu mpya lazima utumie zaidi ya ulichopanga yaani kukutana na demu mara moja tu ni matumizi hayapungui 70+
(sipeleki demu kwangu so lodge inahusika + vinywaji+chakula na posho+ usafiri). Siku hizi hawanipi shida sana kwa kuwa naweza kuchepuka mara moja tu ndani wiki6 mi saivi sio mtumwa saaaana wa sex haya nimemwachia
Zero IQ.
4. Bando
Haka kaeneo nako kanachangia sana maana siwezi kutokuwepo hewani maana net pia kwa sehemu flani inaendesha maisha yangu nje ya ajira.
Kuna mengine mengi ila kwa leo haya yanatosha kuyafanya maisha yangu kutosogea kwa kasi ninayoipanga.
Hebu tutajie nini kinarozotesha kasi ya maendeleo yako?