Kitwanga: Kuna kundi linalomshauri vibaya Rais Samia

Kitwanga: Kuna kundi linalomshauri vibaya Rais Samia

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Kitwanga anasema kuna kundi ambalo limejipenyeza kwa rais na kila mahala linamshauri vibaya Rais.

==========

Kitwanga.jpg

WAZIRI wa zamani wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, amesema kuna kundi linalomzunguka Rais Samia Suluhu Hassan ambalo limekuwa likiweka vigingi kwa watu, wakiwamo wataalamu, wanaotaka kushauri kuhusu mambo mema ya kuipeleka nchini pazuri zaidi.

Kitwanga amesema mbali na kuweka vigingi kwa watu wenye nia njema, kundi hilo limekuwa likiwaona tishio, hivyo kuwachafua, ili kulinda masilahi binafsi. Amemwomba Rais kuwa makini na kundi hilo.

Kitwanga alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo mbalimbali yanayoendelea nchini na kwamba ameona kuna umuhimu wa kumshauri Rais Samia kupitia vyombo vya habari.

Alisema kundi hilo limejipenyeza katika kila sekta zikiwamo taasisi za umma na kwamba lengo lake ni kuharibu nchi kwa maslahi binafsi.

Chanzo: Nipashe
 
Na kama Rais kila mara anakubali huo ushauri mbaya, basi naye ndie hafai kabisa, ametokea kukiamini kikundi cha watu wachache no matter what bado anaendelea kukiamini tu, anajiharibia kabisa.

Anaonekana ameshikiwa akili, na members wa hicho kikundi nao sasa wanajua wamemshika akili, hivyo wanafanya watakavyo, matokeo yake nao sasa wamejigeuza "marais" kwenye idara zao.

Hayo ndio matokeo ya kuwa na Rais dhaifu, ni sawa na baba nyumbani asiewakanya wanae, anawaacha wafanye vile watakavyo, matokeo yake kila mtoto atajiamulia cha kufanya.
 
Anataka wakashauri jinsi ya kuteka watu, kuwatisha ama kuwamaliza kwa risasi kabisa!!

Hicho kipindi cha uhuni na uuaji kimepita na kuzikwa chato!! Wamwache mama aongoze nchi!!

Aliyepita ndo walishauri wapeleka kuficha hela China?
 
Bwana kitwanga fanya home work yako.

Hebu weka hizo list ya shauri mbaya alizoshuriwa na majina ya waliomshauri.

Halafu pia weka mapendekezo ya shauri ambazo wewe unaona ni nzuri na list ya watu ambayo wewe unadhani wanafaa kumshauri rais
 
Hakuna wa kumshauri vibaya Rais! Yanayo endelea ni matokeo ya uwezo wake na utendaji wake na fikra zake tusiwasingizie watu!
Yani rais hata kama kweli anashauriwa vibaya, akiukubali ushauri, kosa ni lake.

Rais anatakiwa kuwa na njia za kuhakiki ushauri anaopewa.

Nyerere alishauriwa na washauri wake ataifishe maduka yote, yani maduka yote mpaka ya Uswahilini yawe ya ushirika au chama.

Akamfuata Mzee mmoja anaitwa Songambele, Mzee wa Dar tu wa chama, yani hakuwa hata katika washauri rasmi wa rais. Lakini Nyerere alimfuata kama Mzee wa kitaa anayeyajua mambo ya kitaa.

Nyerere akamwambia Mzee Songambele, nimeshauriwa hivi na washauri wangu, kwamba tuyafanye maduka yote yawe ya umma, unaonaje?

Mzee Songambele akamwambia chonde chonde usifanye hivyo baba, tutaadhirika mtaani, wenyewe tunajua tunavyojistiri kwenye viduka vyetu hivi, usifanye hivyo. Hao washauri wako hawajui maisha ya mtaani.

Nyerere akautupa ushauri aliopewa na washauri wake wasomi, akaenda na maneno ya Mzee Songambele, Mzee wa Dar ambaye yuko connected kitaa.

Hapo utaona rais kajiwekea namna ya kuhakiki ushauri anaopewa, hakubali kila kitu anachoshauriwa.

Rais akikubali ushauri mbaya, kosa ni la rais, kwa sababu rais anatakiwa kuhakiki ushauri kabla ya kuukubali.
 
Yani rais hata kama kweli anashauriwa vibaya, akiukubali ushauri, kosa ni lake.

Rais anatakiwa kuwa na njia za kuhakiki ushauri anaopewa...

Mazee hii story nimewahi isikia only nilitajiwa jina la Mzee Tabu Mangara..aliekuwa Mwenyekiti Yanga ......kila kitu the same na ulivyoeleza... except jina la huyo Mzee.
 
Mara nyingi ipo hivyo. JK pia alizungukwa hivyo na mambo yakaenda mrama kupitiliza hadi kuelekea awamu yake ya pili akaanza mkakati wa kujichomoa.

Hata mama itafika sehemu atajiondoa kwenye mikono ya hawa wajanjawajanja ingawa si kazi rahisi hasa kwa uzoefu waliopata kuanzia awamu ya JK , JPM na sasa.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom