Kizungumkuti hifadhi ya Burigi

Kizungumkuti hifadhi ya Burigi

Na ndio maana nimewaambia na kuwauliza watetezi wa chato airport watukee business case inayo- justify ujenzi wa chato airport- vinginevyo ni yale yale ya Mobute KUKU banga wa Zabanga... Chato airport ni white elephant project inayomuongezea mlipa kodi mzigo wa operational costs usio wa maana... sijui nako huko wameweka 24/7 immigration officers, air traffic controllers , airport handling etc.. ni mambo mengi sana yanahitajika kuwa na international airport na mzigo huu sijui anaubeba nani kwa hawa watalii wasio zidi 100 kwa wiki ...
Walio wengi wanatetea bila kuwa na hoja za kuutetea huo uwanja.
Wanacho jua ni kutetea na kushangilia na kuwabeza wanao kosoa.
 
Nimepata Bahati Nzuri Ya Kupita Hilo Mbuga

Kutokea Karagwe Kwenda Ngara

Sikukutana Na Wanyama Zaidi Ya Mbweha Watatu Kwa Umbali Tofauti Tofauti.

Pori Ni Kubwa Sana, Lingekuwa Kama Mikumi, Tarangire, Hata Pori La Akiba Pale Lamadi Kwenye Mizani Ukipita Wanyama Unawaona Tu
Kama haukuona nyani na ngedere naweka shilingi mfukoni.!!!!
 
Ndugu hebu tuwekee picha za leo basi.. maana zilizopo na zinazopatika na kuoneshwa ulimwenguni kote, Musoma airport bado haina Lami...
Hao ulimwengu wajue ili iweje?
We hujui msoma kiwanja kitajengwa mda si mrefu na pia kitajengwa kikubwa hapo hapo msoma na kuwa na viwanja viwili?
Kilicho chelewesha ilikuwa ni malipo ya fidia kwa maeneo ya watu.
 
Mleta mada kahakikishe Kwanza ukweli wa mambo uliyoongea. Burigi haipo mkoani Geita isipokuwa kwa sehemu ndogo inaingia mkoani Geita.

Na mapori mengine yote uliyotaja hakuna hata moja liliko Geita labda la Kibanda kama lipo.

Kama ni suala la uwanja wa kuyafikia mapori yote hayo kwa Pamoja uwanja wa Ndege wa Bukoba ungekuwa centre ya kuyafikia kwa urahisi.
Kabisa uwanja wa Omukajunguti ndio ungekuwa sehemu sahihi kujenga uwanja Chato ni matumizi mabaya ya rasilimali mali pesa
 
ingependeza zaidi kuona JPM anafuata watangulizi wake
Anafuata watangulizi wake kwa lipi: safari nyingi za ulaya?, Kwenda kupumzika lushoto?

Unaujua mradi wa maji wa chalinze, unajua mradi wa ujenzi wa bandari ya bagamoyo? Unakumbuka bia za bei nafuu za stela Artois?
 
Hao ulimwengu wajue ili iweje?
We hujui msoma kiwanja kitajengwa mda si mrefu na pia kitajengwa kikubwa hapo hapo msoma na kuwa na viwanja viwili?
Kilicho chelewesha ilikuwa ni malipo ya fidia kwa maeneo ya watu.

Ulisema lami ipo, sasa unasema ni mchakato- kwa nini una shift goal post ndugu...? hiyo hadithi ya ujenzi ni ya muda mrefu sana na mpaka sasa ni utamu kolea.. ni lini itakuwa kweli ? kumbuka, sipingi kiwanja cha chato kuwekewa lami, nacho taka ni usawa wa viwanja vyote nchini kuwa na lami ili kuwezesha private sectors zifanye ndege kuwa kama basi na affordable kwa raia wa kawaida kabisa...

Kwa sasa hakuna business case yoyote inayo -justify uwepo wa chato airport... ukipinga, hebu tuwekee ni watalii wangapi walitembelea hiyo burigi wiki jana... hawazidi hata mia moja kwa maoni yangu na kwa data zinazopatikana toka ICAO... je hao watalii mia moja ndio tuwawekee immigration officers 24/7, airport controlers, na ground operation staff?

Operational costs za Chato ni kubwa kama ukifanya Cost benefist analysis ...na sijui gharama za uendashaji analipa nani, tax payers au JPM mwenyewe au Tanzania airport authorities ? wasije kutuambia kwamba wanapata hasara bila mpango kazi...hasara nyingine ni za kujitakia tu...
Magufuli akiondoka tu, Chato itakuwa kama ile airport iliyojengwa na kuku wa zabanga- Mobutu...white elephant...
 
Kuna kipindi kina simba na Twiga walisafirishwa kwenda kwenye makaazi mapya huko
Watakuwepo ila pori lile ni kubwa mno linagusa Ngara, Karagwe, Biharamulo, Mleba, Chato na linapakana na Rwanda huenda wamepotelea msituni au twiga wameliwa na simba
 
Watakuwepo ila pori lile ni kubwa mno linagusa Ngara, Karagwe, Biharamulo, Mleba, Chato na linapakana na Rwanda huenda wamepotelea msituni au twiga wameliwa na simba
Hivi ni lile pori walipo kuwa wanajificha majambazi walio kuwa wanateka magari hasa mabasi?
 
Tuwekane sawa kidogo kuhusu mambo ya uongo ambayo ameongea ndugu TUNDU LISU mgombea uraisi kwa nafasi kupitia chama Cha demokrasia na maendeleo.

HIFADHI YA TAIFA YA BURIGI
Mwanzo kabisa hi hifadhi ya taifa ya burigi kabla kupandisha hadhi kuwa hifadhi ya taifa ya wanyama pori, Lili kuwa ni pori moja wapo ya mapori ya hifadhi ya serekali ambalo linapatikana mkoa wa Geita, Hili pori lilianzishwa mwaka 1980 Kama pori la hifadhi la akiba.
Katika ukanda huo kwa maana ya mikoa ya Geita na Kagera yalikuwa yanapatikana mapori Kama vile:

Burigi
Kimisi
Biaramulo
Kibanda na
Rumanyika.

Mwaka 2018-2019 kwenye bunge la bajeti,wizara ya utali walipeleka hoja bungeni ya kuomba kupandishwa hadhi baadhi ya mapori ya akiba na kuwa hifadhi za taifa,mapori hayo ni Burigi,Biaramulo,kibanda na rumanyika.

Haya mapori yote yapo katika ukanda muhimu Sana wa ki ikorojia.

Lengo la wizara ya utali kupeleka hiyo hoja ni kwa sababu ya kupanua utali na kuongeza mapato ya taifa ndani ya miaka Saba ili yafikie bill.16 USD yani maana yake wastani wa watali kufikia mil.8 kwa miaka hiyo Saba.

Wa bunge wote wa bunge la Tanzania walipitisha na wakiwemo na wabunge wa Chadema na yule mtoa vimemo vya uongo kwa mgombea wao bwana Mnyika alikuwepo kwenye kupitisha maamuzi hayo.

Lakini wabunge walikubaliana hayo kwa hoja nyingine ya msingi.

Biharamulo,Burigi na Kimisi haya yote yaliunganishwa na kuwa hifadhi ya taifa kwa jina la BURIGI na mapori haya yote yamezungukwa na kata 18 na vijiji 48.

UWANJA WA NDEGE WA CHATO
Kutokana na kupandishwa hadhi mapori hayo na kuwa hifadhi ya taifa kwa namna moja au nyingine ni lazima kuwepo kwa uwanja wa ndege ili uraisishe utali na kupanua wigo wa utali.

Sasa ndio unaona uongo wa huyu mgombea wa Chadema bwana TUNDU LISU kwamba uwanja wa ndege raisi MAGUFULI kajenga kwa ajiri yake.

RAI YANGU KWA WATANZANIA
Tumpinge vikali Sana huyu muongo wa taifa na mchonganishi wa taifa letu kwa huu upotoshaji anaoufanya kipindi cha kuelekea kwenye kampeni za uchaguzi mkuu

Lisu nilidhani ni mwanasheria "Msomi" lakini amekuwa ni mtu wa porojo sana tangu alipoanza ubunge. Hizo mbuga za Burigi zipo siku nyingi sana wakati Magufuli bado yuko sekondari. Eneo hilo linazo mbuga kadhaa kama ulizotaja pamoja na kisiwa cha Lubondo ambazo ni za tangu miaka ya 70 na 80. Hizi kampeini za kueneza uwongo ni za kuogopa sana.
 
Tuwekane sawa kidogo kuhusu mambo ya uongo ambayo ameongea ndugu TUNDU LISU mgombea uraisi kwa nafasi kupitia chama Cha demokrasia na maendeleo.

HIFADHI YA TAIFA YA BURIGI
Mwanzo kabisa hi hifadhi ya taifa ya burigi kabla kupandisha hadhi kuwa hifadhi ya taifa ya wanyama pori, Lili kuwa ni pori moja wapo ya mapori ya hifadhi ya serekali ambalo linapatikana mkoa wa Geita, Hili pori lilianzishwa mwaka 1980 Kama pori la hifadhi la akiba.
Katika ukanda huo kwa maana ya mikoa ya Geita na Kagera yalikuwa yanapatikana mapori Kama vile:

Burigi
Kimisi
Biaramulo
Kibanda na
Rumanyika.

Mwaka 2018-2019 kwenye bunge la bajeti,wizara ya utali walipeleka hoja bungeni ya kuomba kupandishwa hadhi baadhi ya mapori ya akiba na kuwa hifadhi za taifa,mapori hayo ni Burigi,Biaramulo,kibanda na rumanyika.

Haya mapori yote yapo katika ukanda muhimu Sana wa ki ikorojia.

Lengo la wizara ya utali kupeleka hiyo hoja ni kwa sababu ya kupanua utali na kuongeza mapato ya taifa ndani ya miaka Saba ili yafikie bill.16 USD yani maana yake wastani wa watali kufikia mil.8 kwa miaka hiyo Saba.

Wa bunge wote wa bunge la Tanzania walipitisha na wakiwemo na wabunge wa Chadema na yule mtoa vimemo vya uongo kwa mgombea wao bwana Mnyika alikuwepo kwenye kupitisha maamuzi hayo.

Lakini wabunge walikubaliana hayo kwa hoja nyingine ya msingi.

Biharamulo,Burigi na Kimisi haya yote yaliunganishwa na kuwa hifadhi ya taifa kwa jina la BURIGI na mapori haya yote yamezungukwa na kata 18 na vijiji 48.

UWANJA WA NDEGE WA CHATO
Kutokana na kupandishwa hadhi mapori hayo na kuwa hifadhi ya taifa kwa namna moja au nyingine ni lazima kuwepo kwa uwanja wa ndege ili uraisishe utali na kupanua wigo wa utali.

Sasa ndio unaona uongo wa huyu mgombea wa Chadema bwana TUNDU LISU kwamba uwanja wa ndege raisi MAGUFULI kajenga kwa ajiri yake.

RAI YANGU KWA WATANZANIA
Tumpinge vikali Sana huyu muongo wa taifa na mchonganishi wa taifa letu kwa huu upotoshaji anaoufanya kipindi cha kuelekea kwenye kampeni za uchaguzi mkuu
Hoja ni nzuri ila huku mwisho umeiingiza kwenye siasa tena ya chuki kabisa
 
Kama hilo pori lingeweza kuwa mbuga basi wanyama wangejipeleka wenyewe bila kusombwa kwenye magari kutokea serengeti!

Kwanza kitendo cha kuwa na Mbuga artificial kinafanya utalii upungue. Watalii wanataka vitu natural
 
Kulikuwa kuna ulazima gani wa kuweka Lami hapo Chato ilihali Serengeti baba lao hana lami wala Musoma airport lami hakuna mpaka leo... unajibuje hapo?
Hili swari akijibu accordingly basing on his assumption za kuinua sekta ya utalii Tanzania nitakubaliana nae moja kwa moja na alichokisema kuhusu Burigi.
 
Tiz
Ungeweka na idadi ya ndege za kibiashara au za kitalii zinazotua hapo tangu kumalizika kwa uwanja na uwepo wa hiyo hifadhi ya wanyama.

Kama hauna, alichosema TL kitabaki sahihi labda kama kinauma
Tizama hiyo mbuga imefunguliwa hivi karibuni na uwanja umejengwa hivi karibuni biashara ya Utalii siyo kama duka unafungua leo na leo hii unapata wateja inachukua muda baada ya kufanya matangazo na promosheni subiri kidogo utapewa takwimu unazohitaji sijui unafanya utafiti wa utalii, wanyama pori au viwanja vya ndege?
 
Mkuu tatizo letu ni kuwa hatupendi kukosolewa, ukifanya unaambiwa wewe umetumwa na beberu
Tatizo letu kubwa binadamu hasa wa Afrika tumejawa na ubinafsi. Hata hao wanaotetea ni kuwa wameridhika na kubadilisha mboga na viusafiri vyao na watoto wao wakiwa wanasoma shule za binafsi. Hawaangalii hawa binadamu wenzetu vijijini wanavyo shindwa mlo mmoja kwa siku na watoto wao wakiwa wanasoma chini ya miti.
 
Back
Top Bottom