Kizungumkuti hifadhi ya Burigi

Kizungumkuti hifadhi ya Burigi

Labda ungetufafanulia unadhani kipi kinapaswa kuanza?? Kujengea uwanja ndio ndege zitue au ndege zitue Kwanza afu ndo uwanja ujengwe??

Uwanja huu na hifadhi hizi bado ni mpya. Tunahitaji muda wa kuboresha miundombinu ya kuhudumia watalii ndio utaona wanatua hapo. Miundombinu hiyo ni pamoja na Mahoteli, viwanja vya ndege na barabara ndani ya hifadhi. Hivyo, ndugu zangu haya Mambo hayatokei overnight. Ni busara Kabla mtu hajaanza kuongea hovyo kwa maneno yakulishwa, tutumie akili zetu kufikiri.
Kuna mbuga kibao kongwe na maarufu ila hazina miundombinu miaka na miaka. Kwenda zako. Kama lengo ndio hilo lako kwa nini asingeanza na kuboresha hifadhi zilizopo kabla ya kushughulika na mpya.
 
..mbuga ya wanyama na uwanja wa ndege ni kwa ajili ya hoteli yake aliyojenga huko.

..wako wanaodai pale alipoapishwa Mwigulu Nchemba ni hotelini kwa bwana mkubwa.
Unamaanisha wananchi wengine hawataruhusiwa kutua kwenye uwanja huo?? Naomba ufafanuzi Kiongozi.

Mimi nadhani badala ya kupiga majungu, tulipaswa tufurahie uwekezaji wa watanzania kwenye nchi yao. Sasa Kama Sugu na Mbowe wanahoteli zao? Mnashangaa nini Kwa Rais wa Nchi kuwa na Hoteli? (Hata kama ni Kweli)? Au Mhe. Rais hapaswi kumiliki Hotel? Haya Mambo mengine mnalalama naweza sema ni Wivu ila hakuna hoja za Msingi.
 
We tuliza domo. Kuna mbuga kibao kongwe na maarufu ila hazina miundombinu miaka na miaka. Kwenda zako. Kama lengo ndio hilo lako kwa nini asingeanza na kuboresha hifadhi zilizopo kabla ya kushughulika na mpya. Acha mahaba ya MATAGA
Hujajibu Maswali niliyokuuliza na usinifokee. Twende hoja Kwa hoja Hadi tutoane Kwa hoja sio kwa vihoja.

Kwa ujumla naweza sema mnatumika kisiasa. Tafuteni hoja zenye Mashiko. Kabla ya Hifadhi ya Mwl. Nyerere na Ruaha kuwa hifadhi kubwa, Hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania ilikuwa ni Serengeti. Je, Uliwahi kujiuliza ni Kwanini uwanja wa kimataifa unaohudumia watalii wa Serengeti upo Mkoani Kilimanjaro?? Ukijibu Hilo Akili inaweza ikazibuka ukaanza kufikiri wewe kama wewe.

Miundombinu mbalimbali nchini imejengwa kimkakati. Ni watu wa ajabu ndio wanaweza ainisha miundombinu na Ukabila. Kwamba Miundombinu huu umejengwa kuhudumia watu wa Kabila Fulani
 
Tuwekane sawa kidogo kuhusu mambo ya uongo ambayo ameongea ndugu TUNDU LISU mgombea uraisi kwa nafasi kupitia chama Cha demokrasia na maendeleo.

HIFADHI YA TAIFA YA BURIGI
Mwanzo kabisa hi hifadhi ya taifa ya burigi kabla kupandisha hadhi kuwa hifadhi ya taifa ya wanyama pori, Lili kuwa ni pori moja wapo ya mapori ya hifadhi ya serekali ambalo linapatikana mkoa wa Geita, Hili pori lilianzishwa mwaka 1980 Kama pori la hifadhi la akiba.
Katika ukanda huo kwa maana ya mikoa ya Geita na Kagera yalikuwa yanapatikana mapori Kama vile:

Burigi
Kimisi
Biaramulo
Kibanda na
Rumanyika.

Mwaka 2018-2019 kwenye bunge la bajeti,wizara ya utali walipeleka hoja bungeni ya kuomba kupandishwa hadhi baadhi ya mapori ya akiba na kuwa hifadhi za taifa,mapori hayo ni Burigi,Biaramulo,kibanda na rumanyika.

Haya mapori yote yapo katika ukanda muhimu Sana wa ki ikorojia.

Lengo la wizara ya utali kupeleka hiyo hoja ni kwa sababu ya kupanua utali na kuongeza mapato ya taifa ndani ya miaka Saba ili yafikie bill.16 USD yani maana yake wastani wa watali kufikia mil.8 kwa miaka hiyo Saba.

Wa bunge wote wa bunge la Tanzania walipitisha na wakiwemo na wabunge wa Chadema na yule mtoa vimemo vya uongo kwa mgombea wao bwana Mnyika alikuwepo kwenye kupitisha maamuzi hayo.

Lakini wabunge walikubaliana hayo kwa hoja nyingine ya msingi.

Biharamulo,Burigi na Kimisi haya yote yaliunganishwa na kuwa hifadhi ya taifa kwa jina la BURIGI na mapori haya yote yamezungukwa na kata 18 na vijiji 48.

UWANJA WA NDEGE WA CHATO
Kutokana na kupandishwa hadhi mapori hayo na kuwa hifadhi ya taifa kwa namna moja au nyingine ni lazima kuwepo kwa uwanja wa ndege ili uraisishe utali na kupanua wigo wa utali.

Sasa ndio unaona uongo wa huyu mgombea wa Chadema bwana TUNDU LISU kwamba uwanja wa ndege raisi MAGUFULI kajenga kwa ajiri yake.

RAI YANGU KWA WATANZANIA
Tumpinge vikali Sana huyu muongo wa taifa na mchonganishi wa taifa letu kwa huu upotoshaji anaoufanya kipindi cha kuelekea kwenye kampeni za uchaguzi mkuu
Muelimisheni huyo ndugu muhisika kwani elimu ni bahati haina mwisho. Asante kwa kutuelewesha. Tusiporomoshe matusi si busara
 
Tuwekane sawa kidogo kuhusu mambo ya uongo ambayo ameongea ndugu TUNDU LISU mgombea uraisi kwa nafasi kupitia chama Cha demokrasia na maendeleo.

HIFADHI YA TAIFA YA BURIGI
Mwanzo kabisa hi hifadhi ya taifa ya burigi kabla kupandisha hadhi kuwa hifadhi ya taifa ya wanyama pori, Lili kuwa ni pori moja wapo ya mapori ya hifadhi ya serekali ambalo linapatikana mkoa wa Geita, Hili pori lilianzishwa mwaka 1980 Kama pori la hifadhi la akiba.
Katika ukanda huo kwa maana ya mikoa ya Geita na Kagera yalikuwa yanapatikana mapori Kama vile:

Burigi
Kimisi
Biaramulo
Kibanda na
Rumanyika.

Mwaka 2018-2019 kwenye bunge la bajeti,wizara ya utali walipeleka hoja bungeni ya kuomba kupandishwa hadhi baadhi ya mapori ya akiba na kuwa hifadhi za taifa,mapori hayo ni Burigi,Biaramulo,kibanda na rumanyika.

Haya mapori yote yapo katika ukanda muhimu Sana wa ki ikorojia.

Lengo la wizara ya utali kupeleka hiyo hoja ni kwa sababu ya kupanua utali na kuongeza mapato ya taifa ndani ya miaka Saba ili yafikie bill.16 USD yani maana yake wastani wa watali kufikia mil.8 kwa miaka hiyo Saba.

Wa bunge wote wa bunge la Tanzania walipitisha na wakiwemo na wabunge wa Chadema na yule mtoa vimemo vya uongo kwa mgombea wao bwana Mnyika alikuwepo kwenye kupitisha maamuzi hayo.

Lakini wabunge walikubaliana hayo kwa hoja nyingine ya msingi.

Biharamulo,Burigi na Kimisi haya yote yaliunganishwa na kuwa hifadhi ya taifa kwa jina la BURIGI na mapori haya yote yamezungukwa na kata 18 na vijiji 48.

UWANJA WA NDEGE WA CHATO
Kutokana na kupandishwa hadhi mapori hayo na kuwa hifadhi ya taifa kwa namna moja au nyingine ni lazima kuwepo kwa uwanja wa ndege ili uraisishe utali na kupanua wigo wa utali.

Sasa ndio unaona uongo wa huyu mgombea wa Chadema bwana TUNDU LISU kwamba uwanja wa ndege raisi MAGUFULI kajenga kwa ajiri yake.

RAI YANGU KWA WATANZANIA
Tumpinge vikali Sana huyu muongo wa taifa na mchonganishi wa taifa letu kwa huu upotoshaji anaoufanya kipindi cha kuelekea kwenye kampeni za uchaguzi mkuu
Viwanja vya ndege vilivyopo vina hali mbaya na vinahitaji matengenezo makubwa kwanini kujenga uwanja wa kimataifa mahali ambapo hakuna shughuli za kimataifa zinaendelea?
 
Mimi kwangu sioni kama ni upendeleo as long kilichofanyika ni kitu cha kuwaletea watu maendeleo. Ningeona ni upendeleo iwapo angekuwa amegawa pesa bure au huduma zote za kijamii zinapatikana bure au hata kodi hawalipi. Sasa kujenga uwanja wa ndege Chato ni upendeleo? Au kuipa Burigi hadhi ya mbuga imekuwa upendeleo kweli?
Mbona viwanja vya ndege vipo Mbeya, Mtwara, Bukoba, Iringa, n.k huko hawajapendelewa? Kuna mbuga nyingi tu zilipandishwa hadhi kuwa hifadhi za Taifa, hizo je?
Mi ndio maana nasema haya ni mawazo ya kimasikini na kupandikiza chuki tu kusiko na sababu.
Sio tu kimasikini, ni mawazo ya Kifukara.

Walipaswa wajadili baada ya Uwanja wa Chato kukamilika wanadhani ni mkoa gani mwingine uwe na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa.

Uwanja upo ndani ya nchi yao wenyewe, watakaotumia uwanja huo ni wao wenyewe bado wanalaumu. Nadhani wengi wao hawapandagi ndege ndo mana hawaoni umuhimu wa kuwa na hiyo facility ndani ya nchi yao. Wangekuwa ni frequent flyers wa maeneo ya huko wangeipongeza serikali Kwa kuwafikishia huduma hiyo hadi mlangoni.
 
Tatizo letu kubwa binadamu hasa wa Afrika tumejawa na ubinafsi. Hata hao wanaotetea ni kuwa wameridhika na kubadilisha mboga na viusafiri vyao na watoto wao wakiwa wanasoma shule za binafsi. Hawaangalii hawa binadamu wenzetu vijijini wanavyo shindwa mlo mmoja kwa siku na watoto wao wakiwa wanasoma chini ya miti.
Ndio wanajengewa mazingira Ili na wao wapate shughuli za kuwaingizia kipato kupitia sekta ya utalii Ili wale na wao milo mitatu.
 
Mleta mada, kipi kilianza, Chattle International Airport, au kupandishwa hadhi hayo mapori??
Kama umejichanganya vile??

Everyday is Saturday.......................... 😎
 
Hakuna mapato yeyote huko. Ni kuongeza tu matumizi yasiyo na maana. Mbuga mbili tu ndo zinaingiza pesa nyingi zaidi ya mapato. Ngorongoro na Serengeti. Hizo nyingine pesa za kuendeshwa zinatokana na Serengeti na Ngorongoro. Fanya research uache upuuzi
Unafahamu mapato yatokanayo na Mlima Kilimanjaro?? Nadhani huna taarifa za kutosha.

Kwa hiyo unamaanisha tufute Mbuga nyingine zote tubakishe Serengeti na Ngorongoro? Labda unachopaswa ufahamu ni kuwa hatuhifadhi Kwa ajili ya kuvutia watalii Tu.

Hifadhi na mapori yetu yana kazi nyingine muhimj zaidi ya utalii. Na huenda fedha zinazopatikana kutokana na huduma nyingine za kiikolojia no zaidi ya zile zitokanazo na utalii.

Unafahamu kuwa vyanzo vingi vya maji vipo kwenye hifadhi zetu? Pori linaweza lisitembelewe na watalii lakin uwepo wake Una umuhim mkubwa Sana Kwa maisha ya wananchi wanaozunguka Pori Hilo. Je likifutwa Kwa sababu hakuna mtalii anayekuja wananchi watapata wapi maji??

Unafadham faida inayochangiwa na hifadhi kwenye huduma ya uchavushaji (Pollination Service). Ukiona unakula tunda Huku mjini jua kuna Uchavushaji umetokea. Na bila mchavushaji kimsingi hakuna maisha hapa duniani. Hifadhi zetu zinasaidia Sana kwenye kuhifadhi viumbe wachavushaji kama nyuki, popo, bettles na vipepeo.

Itoshe kusema, faida za uwepo wa hizi hifadhi ni zaidi ya kuvutia watalii. Naweza kusema kuvutia watalii ni faida ndogo kabisa ya uwepo wa hizi hifadhi. Hivyo mnavyojadili mada hii ya uanzishwaji/upandishwaji hadhi wa hifadhi ni vyema mkawa na uelewa wa kutosha kuhusu faida zake.
 
Kwa nini useme Burigi ipo Geita ingali ina-cover maeneo ya Biharamulo?
Kwa ufupi hifadhi ya taifa ya burigi iliunganisha mapori matatu: Burigi ambayo ipo Mleba, Biharamulo lililopo biharamulo na kimisi lililopo karagwe, kwa muunganiko huo wakalipatia jina Burigi kutoka na ziwa burigi. Pori la Biharamulo lilijumuisha maeneo yote ya pori hilo kabla Biharamulo haijagawanywa na kuzaa wilaya mpya ya chato. Baada ya kugawanywa kipande cha pori la biharamulo kilienda wilaya ya chato hasa maeneo ya katete.

Hivyo burigi kipekeee ni eneo la mleba isipokuwa imebeba jina la muunganiko kutokana na ziwa. Ofisi kuu zipo biharamulo na mlango mkuu upo Nyungwe/ Nyakahura wilayani biharamulo na kambi kuu ipo Nkonji.
 
Ukweli ni kwamba hizo hifadhi zimeanzishwa kisiasa kwa maslahi ya watu au mtu kwa mitazamo yao au yake. Nia haikua mbaya ila uanzishwaji wake kwangu nauona una mashaka. Hayo mapori yalikua machafu toka miaka na miaka na uanzishwaji wake umekua niwaharaka sana ukilinganisha na hali halisi. Hadi sasa Tanapa ina hifadhi nyingi tegemezi sasa kuwaongezea hizo mbuga tena kwa haraka nikuwaongezea mzigo usio wa lazima.

Nakuhakikishia ata ilazimishwe vip hizo hifadhi hadi zifikie daraja la kati lakuingiza ata wageni 200 kwa mwaka sio chini ya miaka 20.Nakama lengo lilikua nikuongeza idadi ya wageni suluhisho la kwanza lisingekua kuanzisha hifadhi mpya bali kuboresha kwanza zilizopo kwa maana ya zile zinazozalisha vizuri(serenget, tarangire, kilimanjaro, ngorongoro, manyara n.k) zizalishe zaidi kisha kugeukia zisizozalisha vizuri(ruaha, mkomaz, kitulo, rubondo, mahale, gombe, odzungwa, mikumi n.k) zifikie kuzalisha vizuri kisha ndo wazo lakuanzisha hizo nyingine lingekuja, tena ilitakiwa zipande moja baada ya nyingine.
Hizi hifadhi hazijaanzishwa, zilikuwepo over 40 years now. Kilichofanyika ni kuzipandisha hadhi, kuziongezwa ulinzi na kuongeza fursa Kwa wazawa. Huko nyuma zilipokuwa Mapori ya Akiba, wazawa hawakuwa na uwezo kisheria kutumia rasilimali ya humo ndani mana ni Uwindaji wa Kitalii tu ndio uliokuwa unaruhusiwa.

Kuhusu suala la kuboresha zilizopo Kwanza. Nakubaliana na wewe, lakini unadhan ni Bora watu wa Burigi wasubirie kwanza had Tarangire itengamae? Itachukua miaka mingapi?? Kama haya ndo mawazo yako, basi ni Bora kilichofanyika mana Kwa utaratibu huo watanzania wa maeneo mengine hawataona maendeleo had wanaingia kaburini. Yaani watakufa wkt wanasubiria kwingine kukamilike kwanza kimaendeleo.
 
Hakuna pori linaitwa biharamuro..
Pori linaitwa Kasindaga game reserve
Ila lipo biharamuro..
 
Mbona Mkapa alikuwa karibu na Selous lakin hajaweka. Wew haujielewi. Hata jiografia ya kuka hauijui vzr wengine ni wazaliwa kabisa wa uko. Unachekwa kichina. Aliyekuandaa kijibu hoja ya Lisu mwambie akuweke vzr zaid alaf tutakuja kuambia ukweli. Kwa taarifa yako baada ya Mzee Baba kumaliza mda wake ule uwanja yatakuwa machungio ya mbuz kama ilivyo ya Mobutu Seseco wa Zaire DRC sas
Kwani Daraja la Mkapa halisaidii kuboresha utalii kusini mwa Tanzania? Naimani wakati Mkapa anajenga Daraja lile wapo waliobeza juhudi hizo. Leo hii mnasifu na kusahau masimango aliyoyapata miaka hiyo Daraja lile linajengwa.

Mimi naomba tuweke kumbukumbu vzr, zitasaidia Sana huko mbeleni.

Uwanja ule ukishindwa kutumika uzembe ni wetu Sisi watanzania mana ndio tunapaswa kuchangamkia fursa hiyo. Tunapiga porojo na kubeza huku badala ya kutangaza vivutio vya Burigi na kuleta watalii nchini.

Watalii huenda Mbuga za Kaskazini Kwa vile zinauzwa/zinatangazwa zaidi. Watalii hawasemi Tu wenyewe wanataka kwenda sehem flan. So tupambane tupeleke watalii Burigi.
 
Kuna mbuga kibao kongwe na maarufu ila hazina miundombinu miaka na miaka. Kwenda zako. Kama lengo ndio hilo lako kwa nini asingeanza na kuboresha hifadhi zilizopo kabla ya kushughulika na mpya.
Zitaje,
 
Sawa, Ngoja nikubaliane na wewe. Tunza post yako, Mungu akitujalia uhai, uje na takwimu ni watumiaji wangapi watakuwa wameutumia uwanja huo wa chato toka sasa hadi 2025. Hawatafika hata Milioni moja... mark my word.
Kiongozi inaonekana hata hujui kinachoendelea kwenye hii sekta ya Utalii. Kwahiyo unategemea Hifadhi ya Burigi itapokea watalii million moja ndani ya miaka mitano?? Ni vyema ukafahamu kuwa toka Tanzania upate Uhuru ni mwaka Jana ndio tumepokea watalii 1.5m Kwa Mwaka Kwa mara ya Kwanza. So watalii wanaotembelea nchini mwetu sio wengi kihivyo. So tuna kazi kubwa mbele yetu ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu kama hivi ilivyofanyika kwenye Ujenzi uwanja wa ndege Chato.
 
Kwani Daraja la Mkapa halisaidii kuboresha utalii kusini mwa Tanzania? Naimani wakati Mkapa anajenga Daraja lile wapo waliobeza juhudi hizo. Leo hii mnasifu na kusahau masimango aliyoyapata miaka hiyo Daraja lile linajengwa.

Mimi naomba tuweke kumbukumbu vzr, zitasaidia Sana huko mbeleni.

Uwanja ule ukishindwa kutumika uzembe ni wetu Sisi watanzania mana ndio tunapaswa kuchangamkia fursa hiyo. Tunapiga porojo na kubeza huku badala ya kutangaza vivutio vya Burigi na kuleta watalii nchini.

Watalii huenda Mbuga za Kaskazini Kwa vile zinauzwa/zinatangazwa zaidi. Watalii hawasemi Tu wenyewe wanataka kwenda sehem flan. So tupambane tupeleke watalii Burigi.
Sifa pekee ya hifadhi ya Burigi Ina Twiga weupe ambao huonekana kwa nadra na hawapatikani kokote duniani zaidi ya Burigi
 
Kiongozi inaonekana hata hujui kinachoendelea kwenye hii sekta ya Utalii. Kwahiyo unategemea Hifadhi ya Burigi itapokea watalii million moja ndani ya miaka mitano?? Ni vyema ukafahamu kuwa toka Tanzania upate Uhuru ni mwaka Jana ndio tumepokea watalii 1.5m Kwa Mwaka Kwa mara ya Kwanza. So watalii wanaotembelea nchini mwetu sio wengi kihivyo. So tuna kazi kubwa mbele yetu ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu kama hivi ilivyofanyika kwenye Ujenzi uwanja wa ndege Chato.
[emoji16][emoji119]
 
Duuh! Ukisikia mtu kajibiwa kwa hoja ndiyo hivi Sasa. Huyu mleta mada hawezi kupangua hoja hizi.
Hakuna hoja ya maana hapo. Hivi anajua ukanda ule wa Kaskazin Magharibi kuna hifadhi ngapi ambazo watalii wake watahudumiwa na kiwanja kile? Angelijua Hilo asingelinganisha na Iringa, Mara, Kigoma, Katavi na kwingineko.

Lakini afahamu kuwa ukanda wa nyanda za juu kusini tayari kuna Songwe International Airport. Ukanda wa Mashariki kuna JNIA, Ukanda wa Kaskazini kuna KIA. Hivyo si busara kuongeza uwanja mwingine wa kimataifa katika kanda hizi.
 
Haya mafua ya mara kwa mara tunayopataga, nahisi kuna watu huwa wanapenga ubongo badala ya kamasi.
 
Sifa pekee ya hifadhi ya Burigi Ina Twiga weupe ambao huonekana kwa nadra na hawapatikani kokote duniani zaidi ya Burigi
Hivi una taarifa za kutosha kusema hayo eddy? Acha uvivu tafuta taarifa sahihi. Neno kivutio Lina maana pana Sana. Inawezekana Burigi kuwa Chato ni kivutio pia mana ndo Nyumban Kwa Mhe. Rais. Kitu kuwa kivutio inategemea namna tunavyokipackage.
 
Back
Top Bottom