Joseverest
JF-Expert Member
- Sep 25, 2013
- 52,812
- 71,392
Naaaaam Barabara kabisa,
Ndugu wadau wa Michezo wa hapa Jamiiforums na kwingineko karibuni katika Live updates(Matukio Mubashara) kutokea hapa Kinshasa katika Dimba la Stade De Martyrs, uwanja wa nyumbani wa Timu ya AS VITA CLUB ambapo kuna "patashika nguo kuchanika" au unaweza kusema kipute cha ligi ya mabingwa hatua ya makundi katika Kundi A baina ya Wenyeji AS VITA ya hapa Congo na Simba Sports Ckub kutokea Tanzania.. Mechi hii itachezwa Saa Mbili usiku ( Kwa saa za hapa DR Congo na Saa 4 usiku kwa saa za Tanzania)
Kikosi cha Simba kilisafiri kutoka Tanzania jumanne kuja hapa DR Congo na kilitua salama, kikipokelewa salama na wenyeji na jopo la viongozi. Walikaribishwa na wakaendelea na mazoezi siku inayofuata.. Wapinzani wengine kwenye kundi hili A, ni Al Ahly ya Misri na El Mereikh ya Sudan ambao nao watapapatuana keshokutwa 16/2/2021
Kuelekea Mchezo huu Muhimu kwa timu zote, Timu ya Simba itawakosa nyota wake wanne kwa sababu mbalimbali ambao ni Erasto Nyoni/John Bocco (Majeruhi) David Kameta (Timu ya taifa U-20) Pamoja na Perfect Chikwende(Sheria za CAF hazimruhusu). Kocha wao Didier Gomes amesema kuwa wanahitaji kushinda magoli mengi kadiri wawezavyo kulingana na nafasi wapatazo ili kujiweka salama kwa mchezo ujao (Japo anajua Kutoka pale ni ngumu)
Kwa upande wa AS VITA kocha wao Florent Ibenge amesema kuwa itakuwa ni mechi ngumu baina ya timu hizo na amesema chochote kinaweza kutokea, ila amejizatiti kimbinu kushinda mechi hiyo muhimu
Kikosi cha As Vita kilichoibugiza Simba mabao matano kwa sufuri sio hiki kinachocheza leo kwa kuwa wachezaji wengi wameuzwa akiwemo Makusu, Tinombe Mukoko, Tuisila Kisinda, Ngoma n.k na Kile cha Simba sio hiki japo kuna baaadhi ya wachezaji walikuwepo wakiwemo Aishi Manula, Chama Cleotus, Kagere, Mkude, Wawa, Dilunga na wengineo
Kumbukumbu za Head to Head
Hii sio mara ya kwanza kwa timu hizo kucheza, huku Simba ikienda na 'kumbukumbu mbaya' ya kuchabangwa "Hamsa" yaani goli 5 bila majibu mnamo mwaka 2019.
2012 : Simba 1 : 1 As Vita Club
January 19 2019 AS VITA 5 : SIMBA 0
Machi 16, 2019 SIMBA 2 : AS VITA 1
Kwenye kundi lao Simba alifanikiwa kupita ila alitolewa hatua ya Robo fainali
Vikosi vya Timu zote mbili vitawekwa hapa kadiri muda utakavyokwenda......
--------------‐---‐-----------------------
Updates on starting XI (Huenda ikawa/Sio Rasmi)
AS VITA CLUB; Assie Koua, Ebunga Simbi, Makabi Lilepo, Masasi, Fiston Mayele, Medjo Simon Loti, Ouattara, Shabani Djuma, Tulengi Sindani, Wamba Merveille, Yacouba Sidi
SIMBA SPORTS CLUB; Manula, Kapombe, Zimbwe, Wawa, Mkude,Lwanga, Chama, Bwalya, Miquissone,
Mugalu, Kagere
Vikosi rasmi vitawekwa vikishatangazwa hapo baadae
----------------------------------------
Confirmed Mechi kwa watakaotizama itaoneshwa saa 4 usiku kupitia Channel ya ZBC2 inayopatikana kupitia Kisimbuzi cha Azam Tv
View attachment 1700848
Wale wa DSTV CHANNEL NAMBA 270 KBC 1
--------------------‐---------------------
Vikosi Rasmi ( CONFIRMED)
Simba XI: Manula Aishi, Kapombe Shomari, Mohamed Hussein (Nahodha), Onyango, Wawa Sergi, Lwanga Thadeo, Chama Cleotus, Mzamiru Yassin, Mugalu Kopa, Bwalya Larry na Miquissone Luis
Substitutes: Kakolanya, Gadiel, Kennedy, Ndemla, Kagere, Morisson, Kahata
AS VITA XI:
AS Vita Club [emoji1078] lineup:
Simon Omossola (GK) [emoji1062]
Djuma Shabani [emoji1078] (Captain)
Ousmane Ouattara [emoji1081]
Vivien Assié Koua [emoji1081]
Ernest Luzolo Sita [emoji1078]
Papy Tshishimbi [emoji1078]
Amedé Masasi [emoji1078]
Sidi Yacoub [emoji1163]
Jéremie Mbuyi [emoji1078]
Glody Mokabi Lilepo [emoji1078]
Fiston Mayele Kalala [emoji1078]
#TotalCAFCL #ASVSSC
_______________________________________
Mpira utaanza muda wowote kuanzia sasa, vikosi rasmi vinaingia dimbani, wanajipanga kwa picha na matukio mengine
Kickoff
00 + 1' Mpira umeanza rasmi na Simba ndio wanasukuma 'gozi la ng'ombe' kutokea kusini kuelekea Vita club waliopo lango la kaskazini
3' Simba wanalisakama lango la Vita ila mipango inakwama.. Vita wanarudi mchezoni... wanapata faulo inapigwa inaokolewa
7' Simba wanacheza vizuri, wanaonana vyema ila mipango yao inatibuliwa pale..aiseee
8' Vita wanapata faulo....inapigwa inaenda nje pale daaah
10' Kona fupi kwa Vita.. wanacheza vizuri ila inatoka nje Papy Tshishimbi anaitoa nje
13' Timu zote zashambuliana kwa Zamu kwa mashambulizi ya kushtukiza, Simba bado beki hazijatulia wakati huohuo Lwanga anafanyiwa faulo na Papy Kabamba, Papy anaonywa
17' Simva wanapata kona ya kwanza, wanaanzishiana fupi..inatolewa nje
20' luis Miquissone anashambulia lango la Vita, bahati mbaya anaushika mwamuzi anapuliza kipyenga..faulo
22' Miquison anatoa mpira inakuwa ni kona kwa Vita, mchezaji wa Vita anapiga kichwa mpira unatoka sentimeta chache langoni
25' Mpira umesimama Lwanga amechezewa faulu, anagangwa kidogo mpira unaendelea
30' Simba wanatengeneza mipango mizuri lakini namna gani pale Bwalya anajichanganya Vita wanaupata mpira
32' Djuma wa As Vita anadondoshwa na Lwanga ila refa anakataa mpira waendelea na kuwa kona ya kurusha kwa Vita
35' Vita wanapata faulo, mita kama 27 kutoka langoni, inapigwa moja kwa moja ila Manula anaidaka
40' Simba wanamiliki mpira ila wanakosa umakini Safu ya Kiungo Mzamiru Bwalya na Chama wanakosa mawasiliano sahihi, Vita wanapata faulo inapigwa lakini Manula anainyaka vyema
42' Bado ngoma Mbichi 0-0, Simba wanapiga counter attack lakini wanashindwa pale, daah nafasi nzuri
45' Dakika moja ya nyongeza kuelekea mapumziko, timu zimekamiana sana
45+1 Mpira ni mapumziko,
tukishuhudia matumizi makubwa ya nguvu, tunaweza kusema kuwa mechi imebalance ila Simba wanakosa umakini sana na Pia AS Vita wanashambulia sana lango la Simba ila hawajafanikiwa kwa kiasi kikubwa
.....Tukutane kipindi cha pili
____________________________________________________________________________
Naaam Kipindi cha pili kimeanza Vita 0 Simba 0
45-46' Mpira umeanzishwa na Vita wakiwa Lango la Kusini la uwanja wa Martyrs wakipeleka mashambulizi kunako lango la Simba lililopo Kaskazini
Tuendelee......huku timu zote hakuna mabadiliko
47' Djuma anamuona kipa wake pale baada ya Simba kushambulia.. Anakwenda chama ila anapoteza mpira
50' J. MBUYI wa Vita anatoa mpira baada ya kubambikiziwa na Chama
52' Simba wanashambulia kupitia chama, wanaanza haraka haraka ila Miquison anapiga shuti dhaifu linazuiwa na ukuta wa vita
54' Kona AS vita wanapata inapigwa ndefu inawahiwa kwa kichwa ila Goal kick mpira unatoka nje
56' Mabadiliko kwa Vita, Mumbere In Papy shishimbi out... mukokyani in Mayele out
58' Simba wanapata penalti baada ya mchezaji wa AS Vita kuunawa/Kuushika katika harakati za kuokoa mpira ule... Naona Mugalu kaushika mpira bila shaka ndie mpigaji
Wakati huo Simba wanafanya mabadiliko
Bwalya Rally nje , Kahata Francis ndani
59 ' Penalti inapigwa pale..... Goooooooaal Mugalu anapata penalt
AS Vita 0 Simba 1
62' Simba wanakosa goal kupitia Mzamiru baada ya kutengeneza chance moja nzuri ila bahati haiko kwao
Sub kwa vita Tulenge Sindani In, Glody Out
65' AS vita wanapoteza nafasi za wazi hapa huku wakisakama lango la Simba kwa udi na uvumba
68' Lwanga anapata kadi ya njano baada ya kumchezea rafu jezi namba 6 wa Vita
70' AS vita 0 Simba 1 , As vita wanasakama lango la Simba , Simba kama wamerudi nyuma hivi kulinda ushindi
Sub kwa vita (double)
Moloko D, Zemanga Soze in
Yacoub and Kalenda J. out
75' Bado 0 kwa vita na 1 kwa Simba
Juma shaban anapenya ngome ya Simba ila anakowa bahati pale daah
77' Mugalu anakamatwa na misuli sijui kama ataendelea... Anaingia Medie Kagere
80' Kona kwa Vita, inaokolewa Simba wanapiga counter attack wanashindwa kuelewana hapa
83' Vivien anapewa kadi ya njano kwa kumchezea rafu kagere
84' AS VITA wanaliandama sana Lango la Simba, huyu beki Djuma Shabani analeta mushkeli kidogo kwa mabeki wa Simba
86' Kona kwa Simba, inapigwa ndeefu Simba wanaokoa hatari ile
Wawa kapewa kadi ya njano kwa kupoteza muda
87' Sub kwa Simba Chama out, Kennedy Juma In
90' Dakika 4 za nyongeza As vita 0 Simba 1
91' Mchezaji wa As Vita - Mayamba anapiga tik taka inaenda nje
90+2' Kennedy Juma anatoa nuksi golini kwao na kuwaweka salama Simba
90+3' AS VITA Wanasakama goli la Simba ila Simba wanasimama imara na kuzuia mashambulizi japo wanachezewa nusu uwanja
90+4' Full time AS VITA 0 SIMBA 1
Simba wanapata ushindi wa kwanza wa hatua ya makundi kwa kuifunga AS Vita bao 1 sifuri kupitia Penalti ya Mugalu Chris Kope ya dakika 59 kuelekea 60
Ahsanteni kwa kunifatilia kuanzia mwanzo hadi mwisho!
Ndugu wadau wa Michezo wa hapa Jamiiforums na kwingineko karibuni katika Live updates(Matukio Mubashara) kutokea hapa Kinshasa katika Dimba la Stade De Martyrs, uwanja wa nyumbani wa Timu ya AS VITA CLUB ambapo kuna "patashika nguo kuchanika" au unaweza kusema kipute cha ligi ya mabingwa hatua ya makundi katika Kundi A baina ya Wenyeji AS VITA ya hapa Congo na Simba Sports Ckub kutokea Tanzania.. Mechi hii itachezwa Saa Mbili usiku ( Kwa saa za hapa DR Congo na Saa 4 usiku kwa saa za Tanzania)
Kikosi cha Simba kilisafiri kutoka Tanzania jumanne kuja hapa DR Congo na kilitua salama, kikipokelewa salama na wenyeji na jopo la viongozi. Walikaribishwa na wakaendelea na mazoezi siku inayofuata.. Wapinzani wengine kwenye kundi hili A, ni Al Ahly ya Misri na El Mereikh ya Sudan ambao nao watapapatuana keshokutwa 16/2/2021
Kuelekea Mchezo huu Muhimu kwa timu zote, Timu ya Simba itawakosa nyota wake wanne kwa sababu mbalimbali ambao ni Erasto Nyoni/John Bocco (Majeruhi) David Kameta (Timu ya taifa U-20) Pamoja na Perfect Chikwende(Sheria za CAF hazimruhusu). Kocha wao Didier Gomes amesema kuwa wanahitaji kushinda magoli mengi kadiri wawezavyo kulingana na nafasi wapatazo ili kujiweka salama kwa mchezo ujao (Japo anajua Kutoka pale ni ngumu)
Kwa upande wa AS VITA kocha wao Florent Ibenge amesema kuwa itakuwa ni mechi ngumu baina ya timu hizo na amesema chochote kinaweza kutokea, ila amejizatiti kimbinu kushinda mechi hiyo muhimu
Kikosi cha As Vita kilichoibugiza Simba mabao matano kwa sufuri sio hiki kinachocheza leo kwa kuwa wachezaji wengi wameuzwa akiwemo Makusu, Tinombe Mukoko, Tuisila Kisinda, Ngoma n.k na Kile cha Simba sio hiki japo kuna baaadhi ya wachezaji walikuwepo wakiwemo Aishi Manula, Chama Cleotus, Kagere, Mkude, Wawa, Dilunga na wengineo
Kumbukumbu za Head to Head
Hii sio mara ya kwanza kwa timu hizo kucheza, huku Simba ikienda na 'kumbukumbu mbaya' ya kuchabangwa "Hamsa" yaani goli 5 bila majibu mnamo mwaka 2019.
2012 : Simba 1 : 1 As Vita Club
January 19 2019 AS VITA 5 : SIMBA 0
Machi 16, 2019 SIMBA 2 : AS VITA 1
Kwenye kundi lao Simba alifanikiwa kupita ila alitolewa hatua ya Robo fainali
Vikosi vya Timu zote mbili vitawekwa hapa kadiri muda utakavyokwenda......
--------------‐---‐-----------------------
Updates on starting XI (Huenda ikawa/Sio Rasmi)
AS VITA CLUB; Assie Koua, Ebunga Simbi, Makabi Lilepo, Masasi, Fiston Mayele, Medjo Simon Loti, Ouattara, Shabani Djuma, Tulengi Sindani, Wamba Merveille, Yacouba Sidi
SIMBA SPORTS CLUB; Manula, Kapombe, Zimbwe, Wawa, Mkude,Lwanga, Chama, Bwalya, Miquissone,
Mugalu, Kagere
Vikosi rasmi vitawekwa vikishatangazwa hapo baadae
----------------------------------------
Confirmed Mechi kwa watakaotizama itaoneshwa saa 4 usiku kupitia Channel ya ZBC2 inayopatikana kupitia Kisimbuzi cha Azam Tv
View attachment 1700848
Wale wa DSTV CHANNEL NAMBA 270 KBC 1
--------------------‐---------------------
Vikosi Rasmi ( CONFIRMED)
Simba XI: Manula Aishi, Kapombe Shomari, Mohamed Hussein (Nahodha), Onyango, Wawa Sergi, Lwanga Thadeo, Chama Cleotus, Mzamiru Yassin, Mugalu Kopa, Bwalya Larry na Miquissone Luis
Substitutes: Kakolanya, Gadiel, Kennedy, Ndemla, Kagere, Morisson, Kahata
AS VITA XI:
AS Vita Club [emoji1078] lineup:
Simon Omossola (GK) [emoji1062]
Djuma Shabani [emoji1078] (Captain)
Ousmane Ouattara [emoji1081]
Vivien Assié Koua [emoji1081]
Ernest Luzolo Sita [emoji1078]
Papy Tshishimbi [emoji1078]
Amedé Masasi [emoji1078]
Sidi Yacoub [emoji1163]
Jéremie Mbuyi [emoji1078]
Glody Mokabi Lilepo [emoji1078]
Fiston Mayele Kalala [emoji1078]
#TotalCAFCL #ASVSSC
_______________________________________
Mpira utaanza muda wowote kuanzia sasa, vikosi rasmi vinaingia dimbani, wanajipanga kwa picha na matukio mengine
Kickoff
00 + 1' Mpira umeanza rasmi na Simba ndio wanasukuma 'gozi la ng'ombe' kutokea kusini kuelekea Vita club waliopo lango la kaskazini
3' Simba wanalisakama lango la Vita ila mipango inakwama.. Vita wanarudi mchezoni... wanapata faulo inapigwa inaokolewa
7' Simba wanacheza vizuri, wanaonana vyema ila mipango yao inatibuliwa pale..aiseee
8' Vita wanapata faulo....inapigwa inaenda nje pale daaah
10' Kona fupi kwa Vita.. wanacheza vizuri ila inatoka nje Papy Tshishimbi anaitoa nje
13' Timu zote zashambuliana kwa Zamu kwa mashambulizi ya kushtukiza, Simba bado beki hazijatulia wakati huohuo Lwanga anafanyiwa faulo na Papy Kabamba, Papy anaonywa
17' Simva wanapata kona ya kwanza, wanaanzishiana fupi..inatolewa nje
20' luis Miquissone anashambulia lango la Vita, bahati mbaya anaushika mwamuzi anapuliza kipyenga..faulo
22' Miquison anatoa mpira inakuwa ni kona kwa Vita, mchezaji wa Vita anapiga kichwa mpira unatoka sentimeta chache langoni
25' Mpira umesimama Lwanga amechezewa faulu, anagangwa kidogo mpira unaendelea
30' Simba wanatengeneza mipango mizuri lakini namna gani pale Bwalya anajichanganya Vita wanaupata mpira
32' Djuma wa As Vita anadondoshwa na Lwanga ila refa anakataa mpira waendelea na kuwa kona ya kurusha kwa Vita
35' Vita wanapata faulo, mita kama 27 kutoka langoni, inapigwa moja kwa moja ila Manula anaidaka
40' Simba wanamiliki mpira ila wanakosa umakini Safu ya Kiungo Mzamiru Bwalya na Chama wanakosa mawasiliano sahihi, Vita wanapata faulo inapigwa lakini Manula anainyaka vyema
42' Bado ngoma Mbichi 0-0, Simba wanapiga counter attack lakini wanashindwa pale, daah nafasi nzuri
45' Dakika moja ya nyongeza kuelekea mapumziko, timu zimekamiana sana
45+1 Mpira ni mapumziko,
tukishuhudia matumizi makubwa ya nguvu, tunaweza kusema kuwa mechi imebalance ila Simba wanakosa umakini sana na Pia AS Vita wanashambulia sana lango la Simba ila hawajafanikiwa kwa kiasi kikubwa
.....Tukutane kipindi cha pili
____________________________________________________________________________
Naaam Kipindi cha pili kimeanza Vita 0 Simba 0
45-46' Mpira umeanzishwa na Vita wakiwa Lango la Kusini la uwanja wa Martyrs wakipeleka mashambulizi kunako lango la Simba lililopo Kaskazini
Tuendelee......huku timu zote hakuna mabadiliko
47' Djuma anamuona kipa wake pale baada ya Simba kushambulia.. Anakwenda chama ila anapoteza mpira
50' J. MBUYI wa Vita anatoa mpira baada ya kubambikiziwa na Chama
52' Simba wanashambulia kupitia chama, wanaanza haraka haraka ila Miquison anapiga shuti dhaifu linazuiwa na ukuta wa vita
54' Kona AS vita wanapata inapigwa ndefu inawahiwa kwa kichwa ila Goal kick mpira unatoka nje
56' Mabadiliko kwa Vita, Mumbere In Papy shishimbi out... mukokyani in Mayele out
58' Simba wanapata penalti baada ya mchezaji wa AS Vita kuunawa/Kuushika katika harakati za kuokoa mpira ule... Naona Mugalu kaushika mpira bila shaka ndie mpigaji
Wakati huo Simba wanafanya mabadiliko
Bwalya Rally nje , Kahata Francis ndani
59 ' Penalti inapigwa pale..... Goooooooaal Mugalu anapata penalt
AS Vita 0 Simba 1
62' Simba wanakosa goal kupitia Mzamiru baada ya kutengeneza chance moja nzuri ila bahati haiko kwao
Sub kwa vita Tulenge Sindani In, Glody Out
65' AS vita wanapoteza nafasi za wazi hapa huku wakisakama lango la Simba kwa udi na uvumba
68' Lwanga anapata kadi ya njano baada ya kumchezea rafu jezi namba 6 wa Vita
70' AS vita 0 Simba 1 , As vita wanasakama lango la Simba , Simba kama wamerudi nyuma hivi kulinda ushindi
Sub kwa vita (double)
Moloko D, Zemanga Soze in
Yacoub and Kalenda J. out
75' Bado 0 kwa vita na 1 kwa Simba
Juma shaban anapenya ngome ya Simba ila anakowa bahati pale daah
77' Mugalu anakamatwa na misuli sijui kama ataendelea... Anaingia Medie Kagere
80' Kona kwa Vita, inaokolewa Simba wanapiga counter attack wanashindwa kuelewana hapa
83' Vivien anapewa kadi ya njano kwa kumchezea rafu kagere
84' AS VITA wanaliandama sana Lango la Simba, huyu beki Djuma Shabani analeta mushkeli kidogo kwa mabeki wa Simba
86' Kona kwa Simba, inapigwa ndeefu Simba wanaokoa hatari ile
Wawa kapewa kadi ya njano kwa kupoteza muda
87' Sub kwa Simba Chama out, Kennedy Juma In
90' Dakika 4 za nyongeza As vita 0 Simba 1
91' Mchezaji wa As Vita - Mayamba anapiga tik taka inaenda nje
90+2' Kennedy Juma anatoa nuksi golini kwao na kuwaweka salama Simba
90+3' AS VITA Wanasakama goli la Simba ila Simba wanasimama imara na kuzuia mashambulizi japo wanachezewa nusu uwanja
90+4' Full time AS VITA 0 SIMBA 1
Simba wanapata ushindi wa kwanza wa hatua ya makundi kwa kuifunga AS Vita bao 1 sifuri kupitia Penalti ya Mugalu Chris Kope ya dakika 59 kuelekea 60
Ahsanteni kwa kunifatilia kuanzia mwanzo hadi mwisho!