Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

bc sawa najua kama nina pkpk hanipati
Labda kama kuna pikipiki za auto sikuizi, yaaani uwe unasubiriwa tu umalize kufanya gear shift kutoka #1 hadi 4... Nadhani pikipiki ni hatari zaidi kuliko gari. Utadokolewa tu miguuni au mgongoni
 
Ukweli ni kwamba madirisha ya Aluminium yasipofungiwa nyavu ni hatari,huyu Koboko aliingilia dirishani akaenda kujibanza kwenye kabati ya nguo.
View attachment 772131

Kuna kipindi aliwahi kuingia room moja (chemba) katika shule ya sekondari Malangali ilikua mida ya jioni akajiviringisha kwenye nondo za dirishani akatulia kuna mwanafunzi aliingia bila ya kumuona akaazake mezani anakula kumbe nyoka yupo dirishani katulia, sasa ghafla akaja mwanafunzi mwingine akamuona nyoka yupo dirishani kajaa kwenye nondo za dirisha ndipo alipopiga kelele na wote wakatoka mbio yule nyoka alishuka pale nakuanza kuwafukuza walipotoka nje akarudi ndani na kukimbilia kwenye bomba lililokuwemo mmle ndani ambalo kwa upande wa pili lilitokea kwenye jengo la karakana ya shule kwakua yule nyoka alikua mrefu sana kama (3m) walimuwahi na kumshika mkia na kuanza kumponda kwa mipini ya majembe na mawe huku wanamvuta atoke kwenye bomba lile, alivyokaribia kumalizika kutokaakajirusha wakamwachia nakukimbia ila kwakua walishamvunja baadhiya pingili zake kwa kipigo alipokua ndani ya bomba hakuweza kupambana tena akabaki anagaagaa hapo sakafuni wakamshambulia kwa mawe na fimbo mpaka wakamuua, baada ya hapo alitembezwa madarasani kwakua ilikua mida ya jioni karibu na muda wa prepo keshoyake alipasuliwa na kukutwa amewameza panya watatu wamenyooka ndani ya tumbo lake, pia alipimwa na kukutwa na urefu zaidi ya mita tatu a rangi yake ilikua ni ya kijivu tumboni kama nyeupe flani
 
keshoyake alipasuliwa na kukutwa amewameza panya watatu wamenyooka ndani ya tumbo lake, pia alipimwa na kukutwa na urefu zaidi ya mita tatu a rangi yake ilikua ni ya kijivu tumboni kama nyeupe flani
Koboko kwenye msosi huwa hajivungi kuna video moja anagonga na kula panya watatu,kuna kisa kingine walimkuta kammeza kasuku mkubwa.
 
Haha acha kabisa uyo mdudu ata tukiua nikimshika na mjiti huwa bado nasisimka kwa ile ngozi yake ilivyo siwezi
Unajua wengi hawafahamu kuwa baada ya kuamini kuwa umemuuwa kumbe bado yupo hai
Yaani kuna wakati unamkata mpaka kichwa lakini huwa bado ana uwezo wa kugonga
Sio wa kuamini kabisa hawa
 
Koboko wnapatikana hata huko mpanda katavi kwa sasa yaani huyo nyoka ana hasira siyo za dunia hii akifanikiwa kuingia ndani ya nyumba hataki kuguswa na chochote yaani kila mwili wake ukigusana hata na kikombe au sufuria yeye anagonga tu ukisikia ko ko ko ujue Mzee WA kazi kazama ndani tayari hapo shughuli mnayo Kuna jamaa yangu allikuwa amepanda mitini anakata Kuni mchana mara koboko anarudi kwenye mawindo yake halafu shimoni anamokaa liko jirani na huo mti Bwana we tulimsikia jamaa anapiga kelele kama kafumaniwa maana Yule nyoka akishakomaa anapotembea anatoa milio ya kutosha utasikia shiiiiiiiiiiiii ujue anakuja alizama shimoni tukawai kuweka magogo na mipira tukawasha Moto akaungua tukachimba pembeni ya shimo tukamtoa akiwa hajiwezi daa hatari Yule nyoka
Huyo ni kawaida yake kugonga vyombo vya ndani, ukitaka kumtoa kiurahisi we usihangaike tu, washa moto kisha chukua chumvi ile ya mawe tia kwenye moto ikianza kulia ile Ta ta ta taa taa utaona linavyotoka nduki, yaani hapo ndo utajua huyu Nyoka anambio namna gani kisha na wewe ndo utakapoanza kuchukua mazoezi ya kufukuzana nae, ila usimkimbize umbali mrefu maana mlio utakapokoma madikioni mwake na yeye atakugeuzia kibao
 
Koboko kwenye msosi huwa hajivungi kuna video moja anagonga na kula panya watatu,kuna kisa kingine walimkuta kammeza kasuku mkubwa.
Ila nimeona video moja Youtube kaingia kwenye kiota kakuta vifaranga vya ndege kavitishia tishia mara huyo kageuza na kuondoka zake bila kuvitafuna!!
 
Ila nimeona video moja Youtube kaingia kwenye kiota kakuta vifaranga vya ndege kavitishia tishia mara huyo kageuza na kuondoka zake bila kuvitafuna!!
Inawezekana alikuwa ameshiba,sasa alikuwa anajihakikishia kuwa supermaket yake ina stock za kutosha.
 
na je ina maana ana ugumu wa aina gan kias ata akanyagwe na gar hafi ???? na nilickia pia wanamhusisha na nguvu za giza.....kiumbe wa ajabu je ni kwel??

Huyu nyoka nilishamkanyaga kwa pikipiki bila ya kumpasua na alidunda na kuruka kwakua nilikua spidi sana nilisimama mbali kwa woga nika iacha pikipik nikaikagua sikumuona niliporudi mahali nilipomkanyaga sikumkuta hata damu hamna so inawezekana ni mgumu sana
 
Huyu ndege akimuona Koboko huwa anamzonga na kupiga makelele mpaka Koboko huwa ana amua kuondoka.
75351781-1200px.jpg

Starling Bird
 
Hivi kwani hizo mita mia anazotumia si ndio max speed kumbuka yeye anatumia misuli na oxygen hivyo kama ni max speed tegemea itapungua tuu ni tofauti na chombo cha moto, ata kama anatumia sec kadhaa je anauwezo wa kumantain speed hiyo hiyo kwa mita ata 500 kama itatokea amekimbizwa na nyoka?

Yale ni mashindano mi siamini kama binadamu anaweza maintain maximum speed yake kwa umbali wa zaidi ya mita 100 hapo ni lazima agongwe tuu
Mbio zamashindanon tena mkiwa uwanjan nitofaut nambio yakukimbizwa tena porin, ukchanganya woga,mawenge namajan huchukui round ushakula kiss of death
 
Huyu anafaa kufugwa maeneo yenye koboko
Wataalam wamejaribu kumdunga nyoka huyu na kila aina ya Sumu ya nyoka waliopo duniani lakini hakuna sumu hata moja iliyomlaza huyu nyoka.
 
Back
Top Bottom