Kocha Ernest Middendorp: Nimeondoka Singida Fountain Gate kwa kuwa viongozi waliingilia majukumu yangu kwa kiwango kikubwa

Kocha Ernest Middendorp: Nimeondoka Singida Fountain Gate kwa kuwa viongozi waliingilia majukumu yangu kwa kiwango kikubwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
F5SBPRwW0AAnpOk.jpeg
Muda mfupi baada ya kuondoka Singida Fountain Gate FC, Kocha Ernest Middendorp ameweka wazi sababu ambayo imemuondoa kwenye klabu hiyo.

Akizungumza katika mahojiano na Mtangazaji Robert Marawa ambayo yamerushwa na 947 Joburg, kocha huyo amesema:

Baada ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, kesho yake tulikaa kikaoni na uongozi wa Klabu kikiongozwa na Waziri wa Fedha ambaye ndiye bosi wa Klabu, akaeleza kutofurahishwa na uwezo wa timu na jinsi kikosi kilivyopangwa, alivuka mipaka ya majukumu yake.

Licha ya kwamba yeye ni Waziri wa Fedha lakini ilikuwa 'too much', nina taaluma najua ninachokifanya, ndio maana mtu akiingilia majukumu yangu namuachia afanye yeye hiyo kazi.

Madai ya kuhojiwa kuhusu wachezaji
Ndio, kulikuwa na hoja hizo, mchezaji hapangwi kwa kuangaliwa anapendwa na mmiliki au historia, kikosi kinatokana na mazoezi ya wakati husika.

Kupigiwa simu wakati wa mapumziko
Hapana sikupigiwa simu, ingetokea hivyo ningeondoka muda huohuo.

Kuandika barua ya kujiuzulu
Niliondoka kikaoni baada ya kuona wanazidi kuvuka mipaka, walinihoji mambo ambayo waliingilia taaluma yangu na nikaweka wazi mbele ya viongozi wote kuwa sitaendelea na majukumu, sikuandika barua ya kujiuzulu na niliona hakuna umuhimu wa kufanya hivyo kwa kuwa nilitamka mbele yao.

Sikutaka kudai fedha na wala uwepo wangu haukuwa umeshawishiwa na fedha, wanaweza kuzitumia katika miradi mingine.

Makocha wengine wanafanya kazi kwa mtindo huo wa kupangiwa timu na kuingiliwa majukumu ya taaluma zao lakini kwangu mimi hilo haliwezekani

Makocha Wasaidizi
Kocha huyo wa zamani wa Kaizer Chiefs na Moroka Swallows amesema makocha wasaidizi ambao alikuwa akifanya nao kazi “Bado wana mikataba na ni juu yao kuamua kama waendelee kubaki au wataondoka.”

Afisa Habari wa Singida
Hussein Masanza alipoulizwa amesema “Tumeona taarifa zake lakini kama klabu hatujapata taarifa rasmi kuhusu maelezo yake, bado ni kocha wa klabu yetu na tunajua yupo Afrika Kusini, kama kukiwa na lolote atatupatia taarifa ya maandishi.”
 
Ajabu hapo ndio wameshinda bao moja na wamempa too much pressure kocha mpaka ka quit. Kuna timu imefungwa nyumbani na kutolewa michuano hiyohiyo lakini hata kumsema kocha wameshindwa.
 
Mwisho wa Singida umefika.
Muda mfupi baada ya kuondoka Singida Fountain Gate FC, Kocha Ernest Middendorp ameweka wazi sababu ambayo imemuondoa kwenye klabu hiyo.

Akizungumza katika mahojiano na Mtangazaji Robert Marawa ambayo yamerushwa na 947 Joburg, kocha huyo amesema:

Baada ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, kesho yake tulikaa kikaoni na uongozi wa Klabu kikiongozwa na Waziri wa Fedha ambaye ndiye bosi wa Klabu, akaeleza kutofurahishwa na uwezo wa timu na jinsi kikosi kilivyopangwa, alivuka mipaka ya majukumu yake.

Licha ya kwamba yeye ni Waziri wa Fedha lakini ilikuwa 'too much', nina taaluma najua ninachokifanya, ndio maana mtu akiingilia majukumu yangu namuachia afanye yeye hiyo kazi.

Madai ya kuhojiwa kuhusu wachezaji
Ndio, kulikuwa na hoja hizo, mchezaji hapangwi kwa kuangaliwa anapendwa na mmiliki au historia, kikosi kinatokana na mazoezi ya wakati husika.

Kupigiwa simu wakati wa mapumziko
Hapana sikupigiwa simu, ingetokea hivyo ningeondoka muda huohuo.

Kuandika barua ya kujiuzulu
Niliondoka kikaoni baada ya kuona wanazidi kuvuka mipaka, walinihoji mambo ambayo waliingilia taaluma yangu na nikaweka wazi mbele ya viongozi wote kuwa sitaendelea na majukumu, sikuandika barua ya kujiuzulu na niliona hakuna umuhimu wa kufanya hivyo kwa kuwa nilitamka mbele yao.

Sikutaka kudai fedha na wala uwepo wangu haukuwa umeshawishiwa na fedha, wanaweza kuzitumia katika miradi mingine.

Makocha wengine wanafanya kazi kwa mtindo huo wa kupangiwa timu na kuingiliwa majukumu ya taaluma zao lakini kwangu mimi hilo haliwezekani

Makocha Wasaidizi
Kocha huyo wa zamani wa Kaizer Chiefs na Moroka Swallows amesema makocha wasaidizi ambao alikuwa akifanya nao kazi “Bado wana mikataba na ni juu yao kuamua kama waendelee kubaki au wataondoka.”

Afisa Habari wa Singida
Hussein Masanza alipoulizwa amesema “Tumeona taarifa zake lakini kama klabu hatujapata taarifa rasmi kuhusu maelezo yake, bado ni kocha wa klabu yetu na tunajua yupo Afrika Kusini, kama kukiwa na lolote atatupatia taarifa ya maandishi.”

Mwisho wa Singida umefika, wameisha.
 
Ajabu hapo ndio wameshinda bao moja na wamempa too much pressure kocha mpaka ka quit. Kuna timu imefungwa nyumbani na kutolewa michuano hiyohiyo lakini hata kumsema kocha wameshindwa.
Achana na hyo timu ilianzishwa ili kutupa sisi wabaeba viroba vya ngano furaha sio ninyi wakaa ofisini
 
Singida FG wanadai hawana taarifa hiyo ya kocha kuachana nao,wabongo wamezidi uongo uongo....hata yule Hans walidai ameomba kupumzika kumbe walimtimua.

Watu wenye kujielewa ndio Kama hao sio kila kitu unapangiwa na watu wasiokuwa na taaluma husika....Hawa jamaa na wenyewe wameanza uswahili.
 
Muandishi umepotosha, jamaa hajamtaja waziri wa fedha, nimechek full interview

Kuna watu huwa mnajifanya mnajua kila kitu, sipendi kuwajibu lakini kwako wewe nimeona nikujibu kwa faida ya wengine wenye kidomodomo kama wewe. KULA CHUMA.........
 
Back
Top Bottom