Kocha Ernest Middendorp: Nimeondoka Singida Fountain Gate kwa kuwa viongozi waliingilia majukumu yangu kwa kiwango kikubwa

Kocha Ernest Middendorp: Nimeondoka Singida Fountain Gate kwa kuwa viongozi waliingilia majukumu yangu kwa kiwango kikubwa

"kesho yake tulikaa kikaoni na uongozi wa Klabu kikiongozwa na Waziri wa Fedha ambaye ndiye bosi wa Klabu"

Mbona huwa anakataa kuwa yeye ndiyo mmiliki huyo Waziri!?
Mambo hadharani, pesa za ufisadi ndio zinazoendesha mpira wetu. Hili la waziri kumiliki timu ya singida tulikuwa tunalijua japo yeye anajaribu kulificha. Msingi nayo ni ya PM ñk.
 
Utakuta humu wale wanaotaka kumpangia Robertinho nao wataishangaa hii habari. Wanauliza kwa nini Phiri hachezi mara kwa nini kocha hafanyi rotation.Kocha analaumiwa kwa matokeo mabaya na sio kwa kumpanga au kutompanga fulani sababu akimpanga huyo unaetaka wewe na matokeo yakawa mabaya nani atawajibika? Mashabiki maandazi punguzeni kelele pia kwa kocha Robertinho.
 
Kumbe bwana. Kodi zetu ndo zinaishia huku. Waziri wa fedha ndo boss wa hii timu. Amejificha weee lakini kafichuliwa
 
Kocha wa singida kafanya maamuzi sahihi,
Sasa singida nao kujiona wakubwa sana kiasi kwamba ushindi wa goli moja wameona hautoshi..!!
 
Mshahara wa waziri Tanzania [emoji1241] kumbe unaweza kuanzisha timu ya mpira????
 
Daaah hii ndio Tanganyika inavyo liwa na waziri kutwa kuongeza mitozo ambayo inapelekwa kwenye timu yake. KIZIMKAZI Wala hajali na hata muda Hana kabisa.
 
Natamani Gamondi nae alijitambue kama huyu msouth,maana pale gongowazi Kuna wapuuzi wanajiona miungu watu na tunajua Wana first eleven Yao.
 
Natamani Gamondi nae alijitambue kama huyu msouth,maana pale gongowazi Kuna wapuuzi wanajiona miungu watu na tunajua Wana first eleven Yao.
Bila kuiongea Yanga maisha yanakua magumu sana
 
"kesho yake tulikaa kikaoni na uongozi wa Klabu kikiongozwa na Waziri wa Fedha ambaye ndiye bosi wa Klabu"

Mbona huwa anakataa kuwa yeye ndiyo mmiliki huyo Waziri!?
Sasa ndo unajuzwa yeye ni mmilikiii.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom