Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

Ni sawa kodi ni maendeleo ya nchi,bila kupunguza matumizi ya anasa hakika tutapiga hatua mwendo wa konokono.

Manunuzi ya magari mengi ya gharama kubwa L/C V8,Nissan.... ni kaburi la kodi za walipa kodi.

Mikutano,Makongamano,Warsha na safari za hovyo hovyo hakika ni matumizi ya hovyo ya fedha za umma.

Kuuziana Magari ya thamani kubwa ya serekali kwa bei ya nyanya kunawakatisha tamaa walipa kodi.

Serekali ni lazima ibane matumizi si kuongeza na kubuni kila uchao vya kodi.

Kuhusu makusanyo ya kodi naomba kutofautiana na wewe.

Ongezeko la kodi pia linatokana na makusanyo ya TANAPA,TAWA,Ngorongoro kuingizwa kama kodi wakati hizi taasisi zilitakiwa kuachiwa fedha zake na kuilipa gaiwo kama ilivyo bandari,CRDB,NMB,NHC......

Kifupi hesabu za TRA hazina ukweli kwakuwa fedha za TANAPA &Ngorongoro si kodi bali ni mapato ya hizo taasisi.

Nashangaa CAG alishalitolea ufafanuzi suala hili lakini bado serekali inaendelea kuwadanganya wananchi na kuirundukia sifa TRA bila sababu za msingi.

Nina uhakika high season inayoanza mwezi 7 hadi 10 TRA itabebeshwa sifa za uongo kupitia mgongo wa TANAPA & Ngorongoro.

Ngongo kwa sasa Kibanda maiti.
Hii Serikali na hasa huyu Raisi ni mtu wa matumizi ya Anasa sana, anaamini kwenye matumizi ya anasa.
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6

View attachment 3033852
Hatuna shida na kodi,infact tunataka wigo wa ukusanyaji kodi uongezeke na wala hatukatai kulupa kodi,shida ni kodi zetu manzitumia hovyo kwa manufaa yenu binafsi na kisiasa.
Huku walipa kodi wakibaki na maumivu na uchungu wa maisha.

Pia jaribuni kuwakumbuka nakuwamwagia sifa kedekede walipa kodi wa nchi hii sio kila jambo sifa kwa Samia bila kukumbuka samia hana hela yake kwenye mkoba anayotoa ya maendeleo bali ni fedha za walipakodi wa nchi hii.
 
Kila siku mnatukata pesa kwenye miamala ya simu, mwanzo ulikuwa ukituambia makusanyo yamepatikana kiasi gani, na mapato yake yataelekezwa wapi.

Kwanini siku hizi uko kimya, unakusanya tu lakini hutuambii chochote?

Ukimya wako tukiuchukulia kama dalili ya wizi wa pesa za makusanyo yetu tutakuwa tunakuonea?

Anza tena kutangaza makusanyo na utuambie matumizi yake, ili mwisho wa siku tupime kama kweli makusanyo yetu yanatumika ipasavyo.
 
Maendeleo yanaletwa na uzalishaji na kuuza nje kwa wingi sio kodi kandamizi, kwakua viwanda ni vya kuhesabu kwa vidole serikali ingeweka nguvu kubwa kwenye kilimo mazingira yawe rafiki ili Kila mmoja atamani kufanya kilimo cha biashara tuuze nje serikali ichukue chake na wenye nchi tuchukue chetu

lakini wewe kila mara unakuja na kodi mpya bila kusahau mikopo alafu unatuambia eti Kodi ndio maendeleo unashindwa kuelewa kadri unavyo zidi kumfinya mlipa kodi ndivyo makusanyo yatapungua kwa sababu kuna ambao watashindwa kuhimili watakwepa
Lakini hamjali kwa sababu hizi Kodi haziwagusi tunao umia ni walala hoi kugharamia maisha yenu
 
2025 is loading
 

Attachments

  • 20240705_051403.jpg
    20240705_051403.jpg
    166.2 KB · Views: 1
Karibu tena Mkuu, baada ya kuadimika humu Kwa kipindi kiasi..

Umekuwa Serikalini ukihudumu nafasi mbalimbali kwenye Baraza la Mawaziri

Swali langu; Kipi kimefanya kiwango cha Kodi tunachokusanya kipande awamu hii kulinganisha na awamu iliyopita?

Swali la pili, pamoja na makusanyo ya kikodi kuwa makubwa kwanini bado tunaendelea kukopa?
Maswali muhimu kama haya hatayajibu.

Waziri pekee anajiamini na kujitambua,, mwenye uthubutu wa kujibu hoja hapa jamvini ni Dr. Dorothy Gwajima pekee.
Hawa wengine wako kisiasa zaidi.
Huyu ameweka hili bandiko akilenga uchaguzi ujao.
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6

View attachment 3033852
Kodi mnatukamua na kuzichezea mtakvyo kifisadi. Mnamiliki mali ambazo hamuwezi kuzitolea maelezo jinsi zilivyo patikana. Ipo siku Mungu anaingilia kati kutuokoa
 
Dr. Mwigulu Nchemba ni kweli, ni kwa maendeleo yenu msiolipa kodi maana haiwezekani pamoja na maslahi ya spika kuwa juu bado inachukuliwa kwamba hawezi kumudu gharama za makato ya miamala ya simu.

Screenshot hiyo inaonesha muamala wa spika hauchangii chochote kwa maendeleo ya taifa bali ni mmoja wa wafujaji kupitia utaratibu uliorasimishwa kisheria bila haki.

Acheni kuwaona wananchi kama majuha.

20240701_144755.jpg
 
Maswali muhimu kama haya hatayajibu.

Waziri pekee anajiamini na kujitambua,, mwenye uthubutu wa kujibu hoja hapa jamvini ni Dr. Dorothy Gwajima pekee.
Hawa wengine wako kisiasa zaidi.
Huyu ameweka hili bandiko akilenga uchaguzi ujao.
Umesema sahihi Mkuu 🙏

Hata wakati ule alipokuwa active hapa jukwaani ilikuwa ni miaka ile ya 2013-15 ambapo ndiyo alianza na ile Kampeni yake kutaka achaguliwe Kwa nafasi Kubwa Kwa kujichora kwenye mawe ya barabara kubwa zote hadi kule Mlima Kitonga 🙌

Binafsi namtakia Kila la heri kwenye kutimiza ndoto yake, ila sio vibaya akajifunza Kwa waliomtangulia akina Edo.

Wapi walipatia na wapi walikosea...
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6

View attachment 3033852
Hakuna mtu asiyetaka kulipa kodi...

Lakini kwanini mtubambikie kodi zisizotuhusu?

Ni wewe na watu wako mlipanga kodi ya majengo mwezi huu iwe ni 2000 kwa nyumba za kawaida na kuanzia 6000 kwa nyumba ya ghorofa...

Kwanini tuliopo kwenye nyumba za kawaida mnatulipisha 6000 ya kodi ya majengo?

Mheshimiwa Mwigulu nakuheshimu sana, kwasababu wewe ni mtanzania mwenzangu lakini kwenye hili unajidharaulisha sana...

Hivi mnatuona watanzania ni wehu au nini mheshimiwa?
 
Back
Top Bottom