Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu


Lissu akiwa Iramba alikuanika kwamba ulikuwa unamiliki Singida BS na sasa unamiliki Ihefu mambo ambayo wewe umekuwa unakana. Kwa nini tusisieme haya makusanyo ya kodi mnakwenda kuyaficha huko?
 
Mh. Dr. Mwigulu Nchemba kupitia comments hapa jamvini, nadhani unapata picha juu ya utendaji wako . Kwa kifupi watanzania hawaridhiki na utendaji kazi wako. Mkipewa dhamana kusimamia hizi ofisi za serikali, simamia kwa uadilifu, acheni tamaa na upigaji. Mimi nasikitishwa sana na kuporomoka kwa thamani ya pesa yetu. Kingine mnafanya watanzania wanamchukia mh. Rais kwa sababu ya ushauri wenu mbovu.
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6

View attachment 3033852
Kwangu Mimi kama wewe itaendelea kuwepo wizarani nitakua mpkwepa Kodi wa kudumu siwezi kuwafanyeni matajili nyinyi Kisha muendelee kuniita mnyonge sitaki tena sitaki na sitaki
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6

View attachment 3033852
Mh waziri wa fedha @ Mwigulu, Wananchi wanasema

Hakuna maana yoyote kama mwananchi wa kawaida maisha yake yanaendelea kuwa magumu kila kukicha (bidhaa kupanda bei bila nidhamu, gharama za maisha kupaa, uwezo wa mwananchi kujipatia kipato ama kwa njia mshahara, biashara, kilimo nk ni duni sana) huku ninyi mkinufaika na kodi hizo wanazotoa wananchi.

Watumishi wa serikali na umma wakilipwa mishahara ya anasa, wabunge mishahara na posho juu, kununua magari ya kifahari kwa pesa nyingi, viongozi kusafiri sana nje ya nchi bila uwiano wa kile wanachokileta kwa manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla.

Kodi na tozo nyingi wakati mnapokea mikopo na misaadi lukuki isiyo na impact yoyote kwenye maisha halisi ya Mtanzania.

Kulipa madeni kiwango kikubwa nje tena kwa thamani ya dola huku maendeleo yakichechemea bila matumaini ya kukaa sawa.

Makusanyo hayana manufaa yoyote kwa mwananchi wa kawaida zaidi ya kujinufaisha ninyi wenyewe mlioko kwenye dhamana ya uongozi.

Kikokotoo cha wastaafu au kuacha kazi kisimtese mchangiaji michango kwenye mfuko wa jamii maana ni pesa zake kwanini muwapangie namna ya kupata na kiwango gani wakati ninyi wabunge na viongozi wa kisiasa mnalipwa kwa mkupuo na hamlipi kodi yoyote kwenye vipato vyenu?

Kadri makusanyo ya mapato yanavyoongezeka ndivyo wizi, rushwa, ufujaji na ufisadi unavyoongezeka kupitia watumishi wengi wasio waadilifu kazini ambao mnawafahamu lakini hakuna hatua stahiki zinazochukuliwa dhidi yao zaidi ya kulindana.

1. Kodi kero ziondolewe kwenye vipato vya mishahara na biashara
2. Mishahara watumishi wa serikali, umma na sekata binafsi ziboreshwe kulingana na kupanda kwa gharama za maisha
3. Bidhaa zipunguzwe bei kwa serikali kuweka ruzuku kutoka kwenye kodi za wananchi wanazochanga
4. Kikokotoo kilichopo na kilichorekebishwa bila kushirikisha wachangiaji wenyewe kiondoshwe na kupandishwa hadi asilimia 75% na naksi ya kuishi baada ya kustaafu irekebishwe hadi miaka 18 badala ya 12.5
5. Wanafunzi wanaojiunga chuo kikuu kwa shahada katika fani yoyote wapewe mkopo na sharti ya kwamba mwanafunzi aliyesoma shule ya binafsi kidato cha nne kwamba hana sifa ya mkopo iondoshwe ni ubaguzi
nk...................
 
Mhe. Mwigulu.
Nadhani umeona reaction ilivyo humu.

Kama umesoma vizuri maoni ya wanajamvi kuna haja kubwa sana ya kujitathmini na kufanya maamuzi ya haraka.

Serikali hata ikusanye kivipi, Kama mkiendelea kuwa na matumizi ya hovyo hasa katika magari ya kifahari, matumizi yasiyo ya msingi Kama kulipia magoli ya mechi za mpira, kuweka mabango ya Rais kila kona mpaka kwenye mechi za mipira, hasira za wananchi kamwe hazitakoma dhidi yenu.

Ni wakati ya kujitafakari maana kesho yenu itakuwa ngumu sana!

Tanzania ina nafasi kubwa saba ya kuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi Afrika. Ila hamna mipango madhubuti na u serious katika kusimamia mambo ya msingi. Mmekalia uchawa sana na ndo mana nchi yetu ina matatizo lukuki kila siku
 
Matumizi ya serikali yamekuwa hayana nidhamu hata kidogo. Mmeshindwa kuwa na huruma na wanatanzania kabisa, haswa wewe waziri wa fedha
 
Uchumi umesinyaa, pesa mtaani hakuna achilia mbali upatikaji wa fedha za kigeni (US$) imekuwa kizungumkuti ukija kwenye wafanyabiashara wenye zabuni na taasisi za serikali ni kilio malipo hakuna zaidi ya miezi 6 fikiria wengine wamekopa kwenye taasisi za fedha dhamana zao ziko mnadani hivi sasa. Wakati huo wanasiasa mnaendesha maisha ya kifahari mnapitisha billions kwaajili ya manunuzi ya magari ya kifahari ya mwaka 2024 bila soni kwanini msiwe na 'austerity measures' hasa kwenye matumizi huko serikalini kwa kipindi fulani halafu mnakuja hapa na michoro isiyo na uhalisia. Itafika kipindi hata hicho kidgo mtakikosa maana biashara ziko taabani wengi hasa kampuni za kati na ndogo zinapunguza watu nyingine zinafunga biashara sio ishara nzuri kwa uchumi wetu .
 
Huyu haaminiki anaweza akaweka kodi kwa kila thread kabla ya kupost maelezo ya kulipia yanakuja.


Any way acha twende vile mnataka kikubwa nanyi mtapita tukamueni tu.
 
Ng'ombe 🐄 unayemkamua kila siku bila kumpa malisho stahili ipo siku atajifia ...

Punguzeni matumizi ya serikali kwani mzigo mkubwa wa kodi unamwelemea mwananchi asiye na uhakika wa kesho yake.
 
Back
Top Bottom