Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

Na kwanini tukihitaji maelezo kuhusu kodi hii ya majengo kila idara inajifanya haijui...

TANESCO na TRA wanasema hawajui na hawahusiki...

Je huu ni mwendelezo wa kutuona sisi watanzania wa kawaida ni wehu na kwamba hatuna uwezo wa kuwafanya chochote au nini?
 
Maswali muhimu kama haya hatayajibu.

Waziri pekee anajiamini na kujitambua,, mwenye uthubutu wa kujibu hoja hapa jamvini ni Dr. Dorothy Gwajima pekee.
Hawa wengine wako kisiasa zaidi.
Huyu ameweka hili bandiko akilenga uchaguzi ujao.
Kama kalenga uchaguzi ndiyo anatakiwa zaidi ajibu,tena ajibu kwa ufasaha ili azidi kujenga heshima yake kwa wapiga kura.
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6

View attachment 3033852

Hongera, but kuna mapungufu kwenye graphical presentation/displays of revenue collection data..!

Graph hazina uhalisia, mfano, toka tshs 22 trilioni hadi 27 trilioni is an increase of tshs 5 trilioni, ila graph ya Tshs. 27 trilioni ni kubwa mara 3 ya 22 trilioni, yaani graph ya tril 27 inaonyesha kama graph ya 22 x 3 = 66 trilioni

So hizo graph hazijafuata uhalisia mmeweka kubwa sanaaaa..!!

Wekeni graph halisi to show from 22 to 27 trilioni kuna increase of 5 tril or 5/22 x 100% = 22.7% increase in Revenue Collection

Sasa 22.7% ya Revenue Collection, for 2 years graph yake iongezeke at that proportion of 22.7 %, ila hapo graph ya mwisho ni kubwa mara 3 zaidi ya graph ya 22 tril, rekebisheni..!!
 
Hii serikali ya awamu hii mimi std7 nina uwezo wa kuiongoza vizuri zaidi ya hawa wachumi-a-tumbo
Huko shuleni mlienda kusomea ujinga?

20240702_072327.jpg
 
Mhe. Waziri, kwanza tunashukuru umeshiriki nasi hapa. Binafsi nina jambo moja ambalo ni nje ya mada hii ila wewe kama Waziri mwenye dhamana linakuhusu.

Mhe, kuna hii mikopo ya online ambayo licha ya kutoza riba kubwa, lakiini wanakiuka mikataba baina yao na wateja wao mfano ni kuanza kudai marejesho siku ya 5 badala ya siku ya 7 tena kwa vitisho na lugha za hovyo. Kibaya zaidi ni kusambaza taarifa zla watu wanaowadai mitandaoni kisa tu mu amechelewa kulipa kwa siku 1 au 2 wakati utaratibu ukichelewa ni kulipa faini sio kumdhhalilisha mteja.

Jambo moja la kushangaza ni nyie kama serikali kushindwa kuyabaini haya makampuni yanayokopesha mitandaoni wakati transactions zao zote za kutoa mikopo na kulipwa/kupokea fedha zao(lmarejesho) hufanyika kwa kutumia mitandao ya simu ya humu nchini(Mpesa, tigo pesa, Airtel money, n.k). Hii ina maana wamesajliwa katika hii mitandao wanatumia Lipa namba na hiki ndio kinachofanyika.

Sasa swali wangu ni hili:

Kama kweli haya makampuni hayana vibali (leseni kutoka BOT), kwanini serikali isiagize mara moja haya makampuni ya simu yaache kushirikiana kibiashara na haya makampuni ya kitapeli?

Au kama kweli mna lengo la kubaini haya makampuni, kwanini Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na BOT, wasiyabane makampuni ya simu yawasaidie kuwapata wenye haya makampuni maana wameyasajili kwenye mitandao yao ya simu.

Ili upate "Lipa namba" ya kampuni kwenye mitandao ya simu, si ni shariti usajiliwe? Na ili usajiliwe, si ni shariti kampuni iwasilishe vielelezo muhimu kama leseni ya biashara, anuani ya makazi, n.k?

Katika hili, Mhe. Waziri, binafsi naona hakuna dhamira ya dhoti ya kupambania na haya makampuni na ndio maana kila siku yanaongezeka wakati serikali na vyombo vyake kama Jeshi la Polisi, TCRA na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi(PDPC) vipo.

Pathetic!
 
Tumepata privilege ya kutembelewa na waziri wa fedha badała ya kutuelezea mipango yake kabambe iliyopo kwenye budget yake kuchagiza new business start up kwenye secondary production, mipango ya kukuza sector ya uzalishaji kwa ujumla.

Anakuja na post ya kukua kwa kodi kitu ambacho chawa yeyote angeweza post.

Mtu mkubwa kama waziri akitutunuku ku-post kwa ID yake we expect more and depth explanation ya sera, sio kuleta sifa za kitoto.
 
Punguzeni matumizi yenu ya kila siku aisee na vitendo vya rushwa na ufisadi vilivyokithiri kwenye serikali yenu, ili na sisi wananchi tupate nguvu ya kuilipa hiyo kodi.
 
Tumepata privilege ya kutembelewa na waziri wa fedha badała ya kutuelezea mipango yake kabambe iliyopo kwenye budget yake kuchagiza new business start up kwenye secondary production, mipango ya kukuza sector ya uzalishaji kwa ujumla.

Anakuja na post ya kukua kwa kodi kitu ambacho chawa yeyote angeweza post.

Mtu mkubwa kama waziri akitutunuku ku-post kwa ID yake we expect more and depth explanation ya sera, sio kuleta sifa za kitoto.
Dr. Mwigulu Nchemba
 
Mnakata mitaji yetu mkuu, wala sio kodi stahiki hizo. Haha
Kila la kheri na mwaka mpya wa fedha.
 
Back
Top Bottom