Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

1. Mwigulu lipa mkopo wa HESLB wadogo zetu wasome
2. Mnakopa sana, mnakusanya sana kodi ila hatuoni maendeleo, watoto wanakaa chini, vyoo shuleni changamoto, huku mkinunua ma V8 na kujenga mahoteli nchi jirani.
3. Hivi kuna haja gani ya kununua V8 mpya kila mwaka kwaajili ya wakuu wa mikoa, mawaziri na wabunge katika nchi masikini kama hii ambapo kodi zinazo kusanywa zinaishia mifukoni mwenu viongozi wa umma?
Kuna haja gani kwa nchi masikini kama hii kuwa na mtumishi wa umma analipwa zaidi milioni mbili kwa mwezi kama siyo ubinafisi na ufisadi? matumizi ya anasa na makubwa ya hovyo pamoja na wizi wa mali za umma.
 
Kuna haja gani kwa nchi masikini kama hii kuwa na mtumishi wa umma analipwa zaidi milioni mbili kwa mwezi kama siyo ubinafisi na ufisadi? matumizi ya anasa na makubwa ya hovyo pamoja na wizi wa mali za umma.
Wewe unaona TShs. 2milioni ni mshahara mkubwa??? Watu wanakusanya mamilioni ya fedha kila mwezi, halafu wewe unazungumzia Milioni mbili!!?
Wapo baadhi ya maafisa wa Serikali kila mwezi wanakusanya zaidi ya Tshs. 24milioni zikiwa kama ni Malipo ya posho tu ya mwezi mmoja, mbali na mshahara wake wa kila mwezi.
 
~~~Ongezeni taratibu nzuri zaidi katika mikopo ya wanafunzi wa vyuo, kwani fedha nyingi zinapotea kwa kushindwa kuajiri wahitimu aidha wengi kutokomea, zidisheni conditions, kwa ajili ya kupata mikopo hiyo, ikiwemo udhamini wa mashamba, mali mbalimbali na vinginevyo visivyohamishika ili kulazimisha wahitimu hao kurejesha fedha za umma. ~~~~
 
Wewe unaona TShs. 2milioni ni mshahara mkubwa??? Watu wanakusanya mamilioni ya fedha kila mwezi, halafu wewe unazungumzia Milioni mbili!!?
Wapo baadhi ya maafisa wa Serikali kila mwezi wanakusanya zaidi ya Tshs. 24milioni zikiwa kama ni Malipo ya posho tu ya mwezi mmoja, mbali na mshahara wake wa kila mwezi.
Ndiyo hayo mkuu sasa tunaongea hiyo milioni 24 ingeweza kuajiri watanzania 48@500,000 badala ya kulipa mtu mmoja na badala lake tungepunguza tatizo la ajira kwa ndugu zetu sehemu kubwa sn, tena hawa wangejituma kupita kiasi, huyo anayelipwa milioni 24 unaweza kukuta kazi yake kubwa ni kuzunguka kwenye vikao badala ya kuzalisha. Shame on us
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6

Mhe. Dr. (Ph.D), binafsi nimefarijika sana na rejeo lako JF. You might be the highest GOT high rank official, to appear humu jf in person, this is the type of boldness we need it up there!. Kuna kitu niliwahi kusema kukuhusu wewe, Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa! kitu hicho bado unacho and the room is still there, and the door wide open.
Thanks for being who you are.
P
 
Hapa umeleta takwimu za makusanyo. Kesho tunaomba za matumizi ya hovyo na zinazoibwa wakati wa kutumia. Au bado unasimamia kauli yako hakuna wizi serikalini?
Matumizi ya Hovyo ndio yakoje hayo? Serikali si Ina matumizi ya Fedha clear kabisa kwenye Bajeti Kuu inaonesha na Bajeti za Kila Wizara.
 
Mh Dr Mwigulu kwanza nikupongeze kwa kuchapa kazi.

Pamoja na kuwa Nchi yetu bado ina sua sua kwenye swala la maendeleo licha ya kukopa sana tangu tupate uhuru.

Umetuwekea Takwimu ya kiwango cha makusanyo ya Kodi inayopatikana ktk Time Frame hapo juu.

Lakini Mh Dr Mwigulu ingekuwa vema utuwekee hizo takwimu ukilinganisha na Ongezeko la Wananchi kwa idadi yao na walipa kodi.

Kama mwaka 2021 idadi ya watanzania ilikuwa Milioni 10 mathalani idadi ya walipa kodi ikawa milioni 2 then mwaka 2024 idadi ya watu huongezeka na idadi ya walipa kodi inaongezeka vile vile..

Kwa hiyo ongezeko linaoonekana hapo linaweza kuwa Net gain ni Zero ukilinganisha na Idadi ya watu wanaoingia kwenye kundi la walipa kodi pamoja na matumizi.

Jambo lingine kama Ushauri tu, acheni kununua magari ya kifahari mtumie magari binafsi kama watumishi wengine wa umma ili pesa iwekwe kwenye maendeleo zaidi.

Kwani Mwl wa sekondari ambaye anatumia baiskeli yake mbon anasomesha vizuri na wanafunzi wanaelewa.

Wewe Mh Dr Mwigulu umeenda bungeni kusoma Bajeti ukiwa na msururu wa Magari kwenye msafara. Hili jambo sisi walipa kodi hatukulifurahia.

Bajeti yenyewe imejaa mikopo na misaasa ya wafadhili sasa wakituona tunafanya anasa watatukopa tena?

Nakutakia kazi njema ya kulijenga Taifa.

Pamoja sana Mzalendo Dr Mwigulu Nchemba.
Kwani Kila ongezeko la watu manake ni ongezeko la walipa Kodi? Poor reasoning 😁😁
 
Karibu tena Mkuu, baada ya kuadimika humu Kwa kipindi kiasi..

Umekuwa Serikalini ukihudumu nafasi mbalimbali kwenye Baraza la Mawaziri

Swali langu; Kipi kimefanya kiwango cha Kodi tunachokusanya kipande awamu hii kulinganisha na awamu iliyopita?

Swali la pili, pamoja na makusanyo ya kikodi kuwa makubwa kwanini bado tunaendelea kukopa?
Hawezi kuja kujibu Kila mtu hapa ila Mimi naweza kujibu Baadhi ya sababu .
1.Mama amefungua Nchi,ishu ya kwanza kabisa ilikuwa kurejesha Imani ya wawekezaji na wafanyabiashara Kwa Serikali na mnakumbuka hatua mbalimbali zilifanyika ikiwemo ziara za Nje,kurudisha pesa za walioporwa na kuacha kutumia task force au kufungua accounts.Waliofungiwa accounts Kwa Sasa ni wale wanaodaiwa.

2.Utalii.Ishu ya Royal tour imeirejesha Tzn kwenye ramani ya Utalii,ni sekta imefanya vizuri Sana na kuweka rekodi kubwa kuwahi tokea.

3.Sekya ya Madini.Sekta ya Madini imekua sana awamu hii ya sita Kwa sababu ya uratibu mzuri,udhibiti na kuwajali wawekezaji wadogo na wakubwa.Mfano wawekezaji wadogo wamepewa Mitaji,umeme na mitambo Baadhi ya maeneo.

4.Sekta ya Ujenzi,viwanda na Uchukuzi imeimarika sana awamu ya 6.

5.Kekta ya Kilimo.Licha ya kwamba Bado inachangia kiwango ambacho sio kikubwa sana ila imechangia zaidi ya hapo awali.

Mazao kama ufuta,avocado,mazao ya nafaka na ya biashara hasa tumbaku yameleta pesa nyingi sana Nchini Kwa sababu ya sera na uwekezaji wa Serikali kwenye kilomo.Kumbuka mama ameweka pesa mara dufu kwenye Kilimo.

Kwa maoni yangu nilivyofuatilia nimebaini sekta hizo ndio maana mabenki na bima wamepata mabilioni Kwa mabilioni ya faida kushinda wakati mwingine wowote.
 
Hawezi kuja kujibu Kila mtu hapa ila Mimi naweza kujibu Baadhi ya sababu .
1.Mama amefungua Nchi,ishu ya kwanza kabisa ilikuwa kurejesha Imani ya wawekezaji na wafanyabiashara Kwa Serikali na mnakumbuka hatua mbalimbali zilifanyika ikiwemo ziara za Nje,kurudisha pesa za walioporwa na kuacha kutumia task force au kufungua accounts.Waliofungiwa accounts Kwa Sasa ni wale wanaodaiwa.

2.Utalii.Ishu ya Royal tour imeirejesha Tzn kwenye ramani ya Utalii,ni sekta imefanya vizuri Sana na kuweka rekodi kubwa kuwahi tokea.

3.Sekya ya Madini.Sekta ya Madini imekua sana awamu hii ya sita Kwa sababu ya uratibu mzuri,udhibiti na kuwajali wawekezaji wadogo na wakubwa.Mfano wawekezaji wadogo wamepewa Mitaji,umeme na mitambo Baadhi ya maeneo.

4.Sekta ya Ujenzi,viwanda na Uchukuzi imeimarika sana awamu ya 6.

5.Kekta ya Kilimo.Licha ya kwamba Bado inachangia kiwango ambacho sio kikubwa sana ila imechangia zaidi ya hapo awali.

Mazao kama ufuta,avocado,mazao ya nafaka na ya biashara hasa tumbaku yameleta pesa nyingi sana Nchini Kwa sababu ya sera na uwekezaji wa Serikali kwenye kilomo.Kumbuka mama ameweka pesa mara dufu kwenye Kilimo.

Kwa maoni yangu nilivyofuatilia nimebaini sekta hizo ndio maana mabenki na bima wamepata mabilioni Kwa mabilioni ya faida kushinda wakati mwingine wowote.
Umejitahidi kujibu swali la kwanza Mkuu, japo hujawasilisha jibu la swali la pili.

Kwamba pamoja na makusanyo hayo makubwa ya Kodi, kwanini tunaendelea kukopa?
 
Mkuu Mwigulu hebu hizi kodi ziweke kwa dola katika miaka yake jinsi rate ya dola ilivyokuwa. Unaweza ukute hakuna kilichoongezeka isipokuwa shilingi imeshuka thamani tu na tena unaweza kuta mwaka 2021 tulikusanya zaidi kuliko 2023......
 
Back
Top Bottom