Mvinyo mpya
JF-Expert Member
- Aug 24, 2013
- 1,052
- 2,866
Zanzibar ni sehemu ya serikali ya muungano....Wao hawajali kwa kuwa huo Mkopo unalipwa na utalipwa na Watanganyika ....!!
Imagine Afya si swala la Muungano ... sijui inakuwaje serikali ya Muungano inakopa kwenda kujenga Hospital Zanzibar. Kweli Wajinga ndiyo waliwao.
Tanganyika.Nani analipa huo mkopo kama sio Tanganyika
Serikali moja ni sawa lakini tuanze na Mama aendelee kutawala mpaka 2035.Zanzibar tena? Atakayelipa mkopo ni URT au visiwa? Kama tulikuwa na serikali moja isngekuwa hivi ni suala la muda tu
Ni balaa aiseKwani huduma za afya ni mambo ya Kimuungano?
Yaani tunakopa Tanzania Bara halafu Hospitali inaenda kujengwa Zanzibar?
Deni tunakuja kulipa Tanzania Bara π
It's unfair aisee π
Ingekuwa ni la Muungano asingekuwepo waziri wa Afya wa Zanzibar, hapa tumepigwa waziwazi!Naomba kueleweshwa kwa anaeelewa.
Hivi mambo ya afya ni jambo la muungano au sio.
Halafu kulipa tunalipa sote?! Changu changu chenu chetu?!
Na daraja la Tanganyika hadi Zanzibar linaendeleaje huko? πExim Bank ya Korea imeikopesha Serikali ya Tanzania zaidi ya Bilioni 400 Kwa Ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kisasa na Chuo Cha Mafunzo(Mfano wa Muhimbili-Mlonganzila) Zanzibar.
---
Serikali ya Tanzania imepokea mkopo wa Dola za Marekani 163.6 milioni (Sh427.8 bilioni) kutoka Benki ya Exim ya Korea, kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Binguni Zanzibar pamoja na kituo cha mafunzo ya utabibu.
Mkataba wa mkopo huo umesainiwa leo Juni 5, 2024 kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Natu Mwamba na Mkurugenzi Mtendaji Mwandamizi wa Benki ya Exim ya Korea, Hwang Kiyeon na kushuhudiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais wa Zanzibar, Fedha na Mipango, Dk Saada Mkuya.
Mkataba huo wa mkopo umetiwa saini wakati Rais Samia Suluhu Hassan akiendelea na ziara yake ya siku sita nchini Korea.
Chanzo: Mwananchi
My Take
Tunawashukuru watu wa Korea. Mcheza kwao hutunzwa, turudi nyumbani kumenoga.
Pia soma RC Chalamila: Hospitali ya Muhimbili itabomolewa yote na kujengwa upya kwa msaada wa Korea Kusini alipokwenda Rais Samia
Pia someni hapa Tanzania Kushirikiana na Korea Kusini Kujenga Bandari ya Uvuvi Bagamoyo. Itagharimu Bilioni 400
Tatizo ni pale ambapo Zenji hawaruhusiwi kukopa wenyewe bila Tanganyika.Swala sio wao kushindwa kujenga Bali ukumbuke hospitali itajengwa Zanzibar na mkopo utalipwa kwa jasho la watanganyika kwa jina la Tanzania.
Hawa Viongozi wameshindwa kutofautisha kabisa mambo ya Muungano na yasiyo ya Muungano.Ni balaa aise
Imekula kwetu aise! Tumeshikilia kisu upande wa makali.Hawa Viongozi wameshindwa kutofautisha kabisa mambo ya Muungano na yasiyo ya Muungano.
Hili la Afya ni mambo yasiyo ya Muungano, lakini Mkopo tunaenda kulipa Tanzania Bara π
Je afya ni swala la muungano?Exim Bank ya Korea imeikopesha Serikali ya Tanzania zaidi ya Bilioni 400 Kwa Ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kisasa na Chuo Cha Mafunzo(Mfano wa Muhimbili-Mlonganzila) Zanzibar.
---
Serikali ya Tanzania imepokea mkopo wa Dola za Marekani 163.6 milioni (Sh427.8 bilioni) kutoka Benki ya Exim ya Korea, kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Binguni Zanzibar pamoja na kituo cha mafunzo ya utabibu.
Mkataba wa mkopo huo umesainiwa leo Juni 5, 2024 kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Natu Mwamba na Mkurugenzi Mtendaji Mwandamizi wa Benki ya Exim ya Korea, Hwang Kiyeon na kushuhudiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais wa Zanzibar, Fedha na Mipango, Dk Saada Mkuya.
Mkataba huo wa mkopo umetiwa saini wakati Rais Samia Suluhu Hassan akiendelea na ziara yake ya siku sita nchini Korea.
Chanzo: Mwananchi
My Take
Tunawashukuru watu wa Korea. Mcheza kwao hutunzwa, turudi nyumbani kumenoga.
Pia soma RC Chalamila: Hospitali ya Muhimbili itabomolewa yote na kujengwa upya kwa msaada wa Korea Kusini alipokwenda Rais Samia
Pia someni hapa Tanzania Kushirikiana na Korea Kusini Kujenga Bandari ya Uvuvi Bagamoyo. Itagharimu Bilioni 400