Korea yaikopesha Tanzania Shilingi Bilioni 400 za kujenga Hospitali ya Rufaa Zanzibar

Korea yaikopesha Tanzania Shilingi Bilioni 400 za kujenga Hospitali ya Rufaa Zanzibar

Hii ni sawa, pesa imekopwa na muungano sio Tanganyika, na kwa vile TRA kuna Kodi inakusanya Zenj na kuziweka hazina BOT dar, hii ni sawa tu
Fedha zimekopwa na Zanzibar kwa jina la Tanzania ndiyo maana Saada Mkuya yupo na inakwenda kujenga Hospitali Zanzibar.

Hakuna fedha kutoka TRA inayovuka bahari hata senti tano! kama ipo tuambie mwaka 2023/2024 kiasi gani kililetwa
Katika Takwimu za kila robo mwaka za BoT lini uliona mapato ya Zanzibar.

Hizi fedha zimekopwa ili kujenga Hospitali kwa ajili ya AFCON. Moja ya masharti ni kuwa na Hopsitali katika viwango vya Kimataifa. Ile ya V.I. Lenini au Mnazi mmoja ipo chini ya kiwango ndio maana inajengwa hii ya rufaa

Hakuna tatizo Zanzibar kukopa, kuna tatizo moja hakuna anayejua mkopo wa Zanzibar unalipwaje.
Ukisoma Bajeti ya SMZ hakuna sehemu ya malipo ya mikopo!
Kwa maneno mengine Tanganyika kwa jina la Tanzania ndiyo italipa katika mtindo ule ule wa madeni ya Umeme

Zanzibar wanataka kila formula ya kugawana nafasi za ajira, misaada , mikopo . Hutawasikia wakitoa formula ya kuchangia muungano au formula ya kulipa madeni!

Hili deni mtalipa Watanganyika kwa jina la Tanzania! ndio msemo wao siku hizi, kila Mzanzibar ni Mtanzania lakini si kila Mtanzania ni Mzanzibar!
 
Kwani huduma za afya ni mambo ya Kimuungano?

Yaani tunakopa Tanzania Bara halafu Hospitali inaenda kujengwa Zanzibar?

Deni tunakuja kulipa Tanzania Bara 🙆

It's unfair aisee 🙌
Mkuu mbona kwenye ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato, wazanzibari walichangia kupitia kodi zao na si jambo la muungano na hawakulalamika??? Punguza chuki, subiri awamu ya 7 Mkuu!
 
Mkopo wa kijinga hiyo hospitali ya Zanzibar itakosa wateja

Population ndogo sana wangeendelea tu kuja Muhimbili kama kukihitajika huduma za kibingwa kama ambavyo wamekuwa wakifanya miaka yote

Wangeimarisha tu huduma za hospital ya Mnazi mmoja Zanzibar

Mabilioni yote hayo kuwekeza Zanzibar ni mkopo usio na tija huo heri ungekopwa labda hata kukopesha wavuvi wanunue meli kubwa za uvuvi za kisasa ili.kushiriki kikamilifu uchumi wa Blue

Ujinga mtu serikali imefanya kulipa huo mkopo

Uswahili tu umetumika hapo kuwa bara Kuna hospital ya rufaa na chuo kikuu Cha afya Muhimbili Kwa hiyo na Zanzibar inabidi iwepo .Utoto na ujinga mtupu

Muda utaongea
Mkuu maneno yako anaonesha jinsi ulivyo Jawa na chuki na kukosa utu! Acha ukoloni wako huko, kwani wao sio watanzania wanaostahili tiba nzuri na ya kisasa!
 
Hawa Viongozi wameshindwa kutofautisha kabisa mambo ya Muungano na yasiyo ya Muungano.

Hili la Afya ni mambo yasiyo ya Muungano, lakini Mkopo tunaenda kulipa Tanzania Bara 🙌
🤣 🤣 🤣
 
Mkuu mbona kwenye ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato, wazanzibari walichangia kupitia kodi zao na si jambo la muungano na hawakulalamika??? Punguza chuki, subiri awamu ya 7 Mkuu!
Hakuna hela ya Zanzibar inakuja kujenga miradi huku Bara, isipokuwa hela za Bara ndiyo zinaenda kujenga miradi ya afya Zanzibar

Huoni kwamba ni unfair kutumia hela za Zisizo za Muungano kutumika kwenye mambo ya Muungano

Tanzania Bara tunanyonywa
 
Hii ni sawa, pesa imekopwa na muungano sio Tanganyika, na kwa vile TRA kuna Kodi inakusanya Zenj na kuziweka hazina BOT dar, hii ni sawa tu
Huo Mkopo anaenda kulipa Zanzibar ama Tanzania Bara?
 
Yaani hapo ni sawasawa wanakopa Kenya hospitali inajengwa tanzania
Halafu nashangaa Kuna watu humu wanaona hilo ni jambo la kawaida 🙌

Suala la Muungano linatuumiza Tanzania Bara
 
Tanganyika imeingizwa kingi kweli kwenye huu muungano wa mchongo! Yaani mkopo wamechukua Zanzibar lakini wadhamini Tanganyika!
Zanzibar iachwe ikope na ijidhamini yenyewe.
 
Hapana.
Afya siyo suala la muungano ndiyo sababu Znz wana wizara yao ya Afya.


Duh,
Ajabu sana.
Awamu hii Tanganyika itakamuliwa hadi damu
Bahati mbaya hakuna anayeweza kusimama na kulikemea hili, amejaribu Tundu Lissu ikaonekana eti ni Mbaguzi

Hii Nchi haina mwenye uchungu nayo 🙌
 
Hakuna mwenye uchungu na Tanganyika yetu

Wenyewe pamoja na uwingi wetu Bungeni na Serikalini lakini tumeshindwa kufurukuta 🙌
Watanganyika wana uchungu sana broo, sema walio kwenye nafasi za kusikika kirahisi wanahofia kufanywa kama Ndugai, so wanaufyata kulinda ugali wao!
 
Watanganyika wana uchungu sana broo, sema walio kwenye nafasi za kusikika kirahisi wanahofia kufanywa kama Ndugai, so wanaufyata kulinda ugali wao!
Siku hizi tuna Viongozi Cowards wengi, walamba miguu ya wakubwa ndiyo maana hawana ujasiri wa kumshauri Mkuu pamoja na kufanya maamuzi mazito

Kweli tuna hali mbaya kama Taifa 🙌
 
Hawa Viongozi wameshindwa kutofautisha kabisa mambo ya Muungano na yasiyo ya Muungano.

Hili la Afya ni mambo yasiyo ya Muungano, lakini Mkopo tunaenda kulipa Tanzania Bara 🙌

Alesema mkpo munaenda kulipa nyinyi ni nani? Acheni kukariri story za vibarazani wakuu
 
Back
Top Bottom