Korogwe: Bodaboda wadaiwa kuchoma basi la Saibaba baada ya mwenzao kugongwa

Korogwe: Bodaboda wadaiwa kuchoma basi la Saibaba baada ya mwenzao kugongwa

Basi la Kampuni ya Sai Baba linalofanya Safari kutoka Dar es Salaam kuelekea Mkoani Arusha limeteketezwa kwa Moto mara baada ya kusababisha Ajali kwa kumgonga Dereva wa Bodaboda na kudaiwa kusababisha kifo kwa dereva huyo wa Bodaboda katika eneo la Msambiazi wilayani Korogwe mkoani Tanga leo Februari 27, 2024.

Waendesha Pikipiki (Bodaboda) katika eneo hilo wamejichukulia sheria mkononi mara baada ya kushuhudia ajali hiyo ikitokea kwa kulichoma basi hilo moto kwa kutumia mafuta ya Petroli.





View attachment 2918376View attachment 2918378View attachment 2918377
Hakuna habari za "kudaiwa" tena mkuu yote uliyosema ni kweli kabisa
 
Wewe kama sio dereva hauwezi kuona kero za bodaboda hawa jamaa ni hatari sana na hakuna wanachojua zaidi ya breki na kukanyaga mafuta Tu...ukiona Hadi bungeni nako wameanza kuwa na mashaka dhidi ya bodaboda ujue hapo kuna shida
Kwa wabunge wapi?
 
Basi la Kampuni ya Sai Baba linalofanya Safari kutoka Dar es Salaam kuelekea Mkoani Arusha limeteketezwa kwa Moto mara baada ya kusababisha Ajali kwa kumgonga Dereva wa Bodaboda na kudaiwa kusababisha kifo kwa dereva huyo wa Bodaboda katika eneo la Msambiazi wilayani Korogwe mkoani Tanga leo Februari 27, 2024.

Waendesha Pikipiki (Bodaboda) katika eneo hilo wamejichukulia sheria mkononi mara baada ya kushuhudia ajali hiyo ikitokea kwa kulichoma basi hilo moto kwa kutumia mafuta ya Petroli.





View attachment 2918376View attachment 2918378View attachment 2918377
Hawa vijana wasipokamatwa na kufungwa basi binaadamu hatutokuwa salama maana leo saibaba kesho mimi na wewe maana ajali hakuna anayepanga , polisi hapo waonyeshe mfano kwamba uhalifu haukubaliki iwe onyo kwa boda wengine kenge kabisa
 
Sawa hao bodaboda wamekosea kuchoma hilo basi ila madereva wa mabasi ni washenzi sana yaani wanacheza rafu barabarani hatari. mimi nikiona basi naweka chombo yangu pembeni namuachia njia nyeupe.
Mimi nimeendesha pikipiki for more than 15 years... Huwa nawaambia bodaboda kila siku wakiwa highway wawe makini sana na madereva wa mabasi maana ndiyo wanaongoza kwa kuvunja sheria za usalama barabarani. Ukishindana na hao madereva unajitafutia mauti au ulemavu, yaani ukiona anakuja bora umpishe uingie porini kwa sababu ni wapumbavu sana. Shida ya bodaboda wengine ni kujiona wana haki sawa barabarani na magari mengine, kitu ambacho si kweli kwa sababu chassis au body ya bodaboda ni yeye mwenyewe. RIP bodaboda... Tukirudi kwenye hao waliochoma Bus nao ni wapumbavu pia kwa sababu itabidi wakimbie, waache kazi zao na familia zao na pia lazima kuna watakaokamatwa wejiingiza kwenye shida ya kujitakia.
 
Nawalaani kwa nguvu zote waliohalalisha pikipiki kubeba abiria, nawalaani askari wa usalama barabarani kwa kutofuatilia na kuangalia mwenendo wa bodaboda hapa nchni, nawalaani wanasiasa wote hasa wa ccm kuwatumia bodaboda kisiasa. Majanga wanaosababisha bodaboda na hayaripotiwi Au kuupuuziwa na mamlaka ni makubwa mno
Unabii wa Lema umeuelewa si ndiyo mkuu? Nakuunga mkono mkuu tena si kwa bodaboda tuu bali hata bajaj na NOA kuzifanya means of public transport.
 
Huo ni unyasaji wa kijinsia hata km umegongwa Sawa lakini haikufaa kufanya Jambo km hilo wanakuaje km vichaa namna hio unachomaje Gari unajua gharama yake wewe?

Hio clip ionyeshe pia waliofanya tukio hilo alafu Jeshi la Polisi lidili nao hao vichaa waliojificha kwenye kichaka cha ubodaboda
 
Basi la Kampuni ya Sai Baba linalofanya Safari kutoka Dar es Salaam kuelekea Mkoani Arusha limeteketezwa kwa Moto mara baada ya kusababisha Ajali kwa kumgonga Dereva wa Bodaboda na kudaiwa kusababisha kifo kwa dereva huyo wa Bodaboda katika eneo la Msambiazi wilayani Korogwe mkoani Tanga leo Februari 27, 2024.

Waendesha Pikipiki (Bodaboda) katika eneo hilo wamejichukulia sheria mkononi mara baada ya kushuhudia ajali hiyo ikitokea kwa kulichoma basi hilo moto kwa kutumia mafuta ya Petroli.





View attachment 2918376View attachment 2918378View attachment 2918377
Jeshi la policcm lilikuwa wapi yote haya yakijiri?

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Juzi tu hapo tuliwapa cheo as maafisa usafirishaji na wengi vichwa vilijaa maji kwa sababu ya aliyewapa jina.

Haya hao maafisa usafirishaji a.k.a vibaka na wauaji wamefanya yao na bahati mbaya hapo kijijini kwa wiki au mwezi hawataonekana kwa uharibifu wa mali.

Watetezi wao waibuke tuone.
Kuna wanaomuita Lema ni nabii. Sasa tunaona kile alichokiita 'laana'!

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Dah! Wasambaa wenzangu mmeniabisha kwa kweli! Hapo itabidi mkajifiche tu milimani ili kuepuka kukamatwa na polisi kutokana na huo upuuzi mlio ufanya.

Mbaya zaidi unaweza kukuta makosa yalikuwa ni ya huyo bodaboda mwenzenu! Maana wengi wenu huwa hamzingatii kabisa sheria za usalama barabarani.
 
Wewe kama sio dereva hauwezi kuona kero za bodaboda hawa jamaa ni hatari sana na hakuna wanachojua zaidi ya breki na kukanyaga mafuta Tu...ukiona Hadi bungeni nako wameanza kuwa na mashaka dhidi ya bodaboda ujue hapo kuna shida
Madereva wa magari wengi nao ni shida ktk uendeshaji tumeona,kwa hali ya kawaida hao boda mwenzao angekuwa amekosea wasingefanya chochote wangenyamaza inawezekana huyo gari kubwa alikosea kwa makusudi.Lkn all in all madereva wa magari na pikpik wengi hawafuati taratibu wawapo barabarani.
 
Hao wapuuzi sana. Juzi kuna mmoja kaja kunigonga mi nikiwa na gari. Jamaa nimemuona toka mbali akikimbiza pikipiki pamoja na kumpungia mkono kuashiria apunguze mwendo bado kaja nivaa.

Siku wakinigonga na kujifanya kutaka choma gari au nipiga mawe, mtasikia jamaa kaua Bodaboda 20 kwa kuwagonga na gari. Mapuuzi sana, hayajui sheria yenyewe ni kukimbia na kujichomeka kila sehemu.
Gari ulitoe wapi wewe acha kujinasibu we ni muuza uji tu stendi kuku wewe
 
Basi likigonga mtu faini yake 30,000 tu kesi imeisha wanabadilisha dereva gari linaondoka
 
Hao ni waalifu kama waalifu wengine wakamatwe na washtakiwe tabia nyingine sio za kuzivumilia kuna siku watakamata gari la kiongozi na kulichoma.
Sasa kama kiongozi wenyewe ndio hawa wanaotajwa kila siku kwenye report za CAG kuna hasara gani wakichomwa??
 
Huo ni unyasaji wa kijinsia hata km umegongwa Sawa lakini haikufaa kufanya Jambo km hilo wanakuaje km vichaa namna hio unachomaje Gari unajua gharama yake wewe?

Hio clip ionyeshe pia waliofanya tukio hilo alafu Jeshi la Polisi lidili nao hao vichaa waliojificha kwenye kichaka cha ubodaboda
aliekufa angekua nduguyo ungeandika haya?
 
Back
Top Bottom