Korogwe: Bodaboda wadaiwa kuchoma basi la Saibaba baada ya mwenzao kugongwa

Korogwe: Bodaboda wadaiwa kuchoma basi la Saibaba baada ya mwenzao kugongwa

Habari zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa kundi la waendesha bodaboda, leo Februari 27, 2024 wamelichoma moto na kuliteketeza basi linalodaiwa kuwa ni mali ya Kampuni ya Saibaba, lililokuwa linatoka jijini Dar es Salaam kuelekea Arusha, baada ya kudaiwa kumgonga bodaboda mmoja na kusababisha kifo chake.

Habari zilizotufikia hivi punde, zimeeleza kuwa tukio hilo limetokea katika eneo la Kona ya Semkiwa, Korogwe mkoani Tanga na kusababisha kukatika kwa mawasiliano kati ya pande mbili za barabara hiyo, jambo lililosababisha foleni iliyodumu kwa takribani saa mbili.

Kwa mujibu wa mashuhuda, baada ya ajali iliyosababisha kifo cha mwendesha bodaboda, wenzake walijikusanya na kulizingira basi hilo, wakawaamuru abiria wote kushuka na kushusha mizigo yao kabla ya kuliteketeza kwa moto.

sasa mbona boda boda ndio kaigonga gari , gari ipo kwenye njia yake
 
Duu kampuni yenyewe ishajichokea inatembea jina tuu,
Hilo basi lililochomwa ndio First Class yake.

Polisi nao walikua wapi? Si wapo karibu tuu hapo.
 
Boda boda ni washenzi sana, Kuna jamaa mzungu alikua na demu wake mswazi wanatoka kulewa usiku mida Kama saa 7 sijui alipatana na msala gani na Hawa maofisa mishikaki Huko atokako walikuja mkamata maeneo ya mikocheni demu ndo akiwa dereva. Hallo waliijaa kwa gari mmoja ndo anazozana na mdada dereva wengine wanazunguka zunguka kuiba vilivyoma ndani ya gari lilikua timbwili mpaka nkajua kumbe Kuna PC za mjini Zina nguvu kidemu chembamba boda alikua kimelewa akajalibu kukipiga mtama kikamgomea yeye ndo kikamuweka Punch akayumba nusra ailambe lami. Kilichosaidia kulikua na mobile ya gardaworld security jamaa wakawa wamesogea pale kuwashauri jamaa.

Soln ya Hawa viumbe ukimuhenyeka na gari
1.kama ni usiku au ni mchana na uko sehemu n, uri yenye kuweza kukimbia we sepa kabsa Wana ushirikiano Kama siafu hata Kama hawamjui lazma wampe ushikiano
2.kama huna nafasi ya kukimbia shukaz chini lock gari lako kabsa. Wengi ni wezi wakubwa wakati mnabishana ama mnasubiri trafki wengine hutumia mwanya huo kuiba na pia kua makni na gari lako wanaweza shusha hata engine au battery
3 usipaniki Wala kuonyeaha woga
 
Hao ni waalifu kama waalifu wengine wakamatwe na washtakiwe tabia nyingine sio za kuzivumilia kuna siku watakamata gari la kiongozi na kulichoma.
hao waendesha bodaboda ni wajeuri barabarani hawajali wanaingia barabarani vile wanataka wakipata ajali wanadai wanaonewa na magari inatakiwa wachapwe hasa maana ajali nyingi wao ndio sababu
 
Basi la Kampuni ya Sai Baba linalofanya Safari kutoka Dar es Salaam kuelekea Mkoani Arusha limeteketezwa kwa Moto mara baada ya kusababisha Ajali kwa kumgonga Dereva wa Bodaboda na kudaiwa kusababisha kifo kwa dereva huyo wa Bodaboda katika eneo la Msambiazi wilayani Korogwe mkoani Tanga leo Februari 27, 2024.

Waendesha Pikipiki (Bodaboda) katika eneo hilo wamejichukulia sheria mkononi mara baada ya kushuhudia ajali hiyo ikitokea kwa kulichoma basi hilo moto kwa kutumia mafuta ya Petroli.





View attachment 2918376View attachment 2918378View attachment 2918377


Saibaba na magari yake mabovu kadunduliza kapata namba E wamechoma? Hawa sio watu
 
Ikithibika kwamba bodaboda ndio waliochoma hilo basi nashauri vijiwe vya boda vilivyopo karibu na eneo la tukio wajipe likizo au watafute pahala pengine pa kufanyia shughuli zao kwa muda.

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
Yani hao wahuni sjui watajificha wapi.
Usiku tu wa leo zaidi ya 50 watatiwa mbaroni.
Na baada ya hapo mji wa korogwe na vitongoji vyake hakuna boda atakayeonekana kitaa.
Wamechukua sheria mikononi ila itawagharimu kwa mda mrefu
 
Hao wapuuzi sana. Juzi kuna mmoja kaja kunigonga mi nikiwa na gari. Jamaa nimemuona toka mbali akikimbiza pikipiki pamoja na kumpungia mkono kuashiria apunguze mwendo bado kaja nivaa.

Siku wakinigonga na kujifanya kutaka choma gari au nipiga mawe, mtasikia jamaa kaua Bodaboda 20 kwa kuwagonga na gari. Mapuuzi sana, hayajui sheria yenyewe ni kukimbia na kujichomeka kila sehemu.
Mkuu usiombee hivyo hayo majamaa mapuuzi sana sijui yanavutaga bangi? Yanaweza kukudhibiti yakakuchoma pamoja na gari! Kuna jirani yetu mtaa wa tatu yalimpiga mawe mpaka kupelekea kifo chake! Kosa alilolifanya ni kutoa bastola na kupiga hewani baada ya dereva kuchoropoka!
 
Zamani dereva alikuwa anaambiwa heshimu mtu yoyote anaetembea barabarani.Siku hizi madereva hawaheshimu matokeo yake ndo haya.Ajali nyingi za bodaboda huwa zinatokea iweje leo inawezekana kuna kitu.Madereva wa mabasi makubwa pamoja na haraka zenu muwapo barabarani jitahidi kujali watembea kwa miguu na hata pikpik maana huwa nao ni binadamu wengine wanategemewa pia.
 
Back
Top Bottom