Kosa la kuingilia msafara au kupita sehemu iliyozuiwa kupisha uwepo wa mtu mkubwa serikalini

Kosa la kuingilia msafara au kupita sehemu iliyozuiwa kupisha uwepo wa mtu mkubwa serikalini

nasssen

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2012
Posts
489
Reaction score
535
Ndugu wanajamvi,

Kabla ya yote ningependa kutanguliza pongezi na hongera nyingi za kuweza kufika December tukiwa na pumzi. Pasipo kupoteza muda, ningependa kwenda moja kwa moja kwenye mkasa ulionikumba weekend hii maeneo fulani hapa jijini Dar es Salaam. Kwa ufupi nilikuwa napita tu kwenye njia moja mara nikaona kwa mbele yangu kuna pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na askari mwenye uniform pamoja na abiria aliyejitambulisha kuwa ni askari pia lakini hakuwa kwenye uniform.

Baada ya kusimama nikashangaa naulizwa "kwanini tunakusimamisha na hausimami tangu kule nyuma? Huoni wenzio wote wamesimama? Kwanini unakuwa na kiburi? Unataka kutusababishia shida wewe, yani mkubwa yupo maeneo haya na haturuhusu magari kupita ila wewe umepita! Yakaongelewa maneno mengine mengi ya kufanana na hayo. Mimi nikawajibu tu kwa upole kuwa kusema kweli sikuona mtu yeyote akinisimamisha na sikutambua kabisa kuwa magari yanasimama. Na isitoshe ni njia ambayo huwa haina magari mengi hivyo sikuwa na idea kabisa kuwa kuna kuzuiwa magari kupisha uwepo wa huyo mkubwa.

Mara yule askari ambaye alikuwa na nguo za kiraia akapokea simu na kuitikia kwa heshima kuashiria ni mkubwa wake alikuwa anampigia simu. Akaweka loud speaker na kwa masikio yangu alisikika akisema "umempata huyo mtu? mfunge pingu natuma gari lije kumchukua haraka sana. Ataenda kutoa maelezo kituoni" Yani niliishiwa nguvu ghafla na kula nikijaribu kuongea nao walikuwa wakipigiwa simu mara kwa mara na huyo mkubwa wao na kuwaamuru kuwa nipelekwe mahabusu nitafunguliwa kesi ambapo nitalipishwa faini ya shilingi milioni nane, kupekuliwa nyumbani kwangu, kutaifishwa kwa gari langu, na kwenda jela kwa kipindi kisichopungua 06 months.

Naomba tu nifupishe kwa kusema kuna kiasi kikubwa tu cha pesa kilinitoka kunusuru huo msukosuko kwasababu nilijiuliza mambo mengi:-
1. Kitendo cha mimi kuingizwa mahabusu kuna hati hati ya kupoteza ajira.
2. Kutaifishwa kwa gari ambalo ni la kampuni ni swala jingine kabisa.
3. Kupekuliwa nyumba naweza hata kubambukizwa madawa, silaha au nyara nikaishia jela.
4. Watoto wangu wadogo watalelewa na nani?
5. Reputation yangu itaharibika kwasababu nitakuwa na fingerprints interpol.
6. Hata nikienda mahakamani, kushindana na system ni ndoto ya mchana.

So, kutokana na hayo yote ilibidi tu niingie mfukoni na hata kukopa kidogo ili niweze kumalizana na hao watu nje ya sheria. Ni jambo ambalo linaniumiza sana kwasababu si kwa pesa iliyonitoka ila kwa kukiuka maadali yangu binafsi ya kutoa chochote.

Tanzania ni nchi yangu na ninaipenda lakini kwa haya niliyopitia, Mungu ndiye anajua hisia zangu na hii nchi zipoje kwa sasa.

Kama kuna mdau aliwahi kupitia mkasa kama wangu naomba tupeane uzoefu na kama kuna mwenye mchango wowote ningependa tujadiliane.

Asanteni sana.
 
Mkubwa ambaye anapaswa kuwatumikia wananchi, anajitenga na wananchi kwa gharama za wananchi!

Ukubwa wake unatokana na nini? Siasa au Ajira?

Ingawa kuna wakati na nyie madereva huwa mnajiona mna akili sana kuliko wengine wanaokaa kwenye foleni, mnaleta ujuaji na haraka kuzidi haraka yenyewe.

Enewei, pole kwa mkasa mkuu! We amini limetokea jambo hilo ili wengine walaanike!
- Miaka hiyo ndo wakuja mjini hapa, si nikaelekea geti la BOT la kutolea minoti, naona jamaa wanajipanga na mibunduki yao, mi nikaona labda wanataka kunifungulia geti sasa niingie....mpaka leo sijawa mwenyeji bado.

- Wao wakigonga watu, wanakimbia! Wewe kukosea kidogo, mtu anataka ku-practice unduli kamili.
 
Polisi si waelewa,ni watu wa dhulma,kuminya haki na rushwa........umemkamata muhalifu umemuona hana kosa,baada ya kumuachia unaanza kumtweza utu wake na kumdhulumu kidogo alichonacho.
Hio pesa polisi anaenda kumlipia ada mwanae,....mwanae akifeli shule anamlaumu nani..
Binafsi Huwa siwasaidii polisi,hata akitaka aje kupanga nyumba,namwambia hamna chumba,........yaani ni watu ambao sitaki nao mazoea ya namna yeyote ile
 
Rushwa na ufisadi Tanzania unaofanywa na watu wa serikali kwa 100% vinachochewa na wananchi wenyewe cha ajabu ndio watu wanaoongoza kulalamika kuwa nchi imejaa rushwa.
Kama kukiwa na utaratibu wa wananchi kugomea kutoa rushwa nchi nzima ni askari gani atambambikia kesi mwananchi?
Kama mwananchi anaweza kuachiwa baada ya kufanya kosa na kutoa pesa itambulike kuwa pia anaweza kuachiwa katika hali hiyo hiyo bila kutoa pesa
 
Mkubwa ambaye anapaswa kuwatumikia wananchi, anajitenga na wananchi kwa gharama za wananchi!

Ukubwa wake unatokana na nini? Siasa au Ajira?

Ingawa kuna wakati na nyie madereva huwa mnajiona mna akili sana kuliko wengine wanaokaa kwenye foleni, mnaleta ujuaji na haraka kuzidi haraka yenyewe.

Enewei, pole kwa mkasa mkuu! We amini limetokea jambo hilo ili wengine walaanike!
- Miaka hiyo ndo wakuja mjini hapa, si nikaelekea geti la BOT la kutolea minoti, naona jamaa wanajipanga na mibunduki yao, mi nikaona labda wanataka kunifungulia geti sasa niingie....mpaka leo sijawa mwenyeji bado.

- Wao wakigonga watu, wanakimbia! Wewe kukosea kidogo, mtu anataka ku-practice unduli kamili.
Asante sana mkuu na pole pia kwa yaliyokupata na wewe.

Si kwamba najiteta au najisafisha ila ni kwamba hiyo njia huwa ina magari machache sana na ni vigumu kukuta foleni weekenda, especially mchana. So, hata sikuwaona wakinisimamisha wala kuona magari yamesimama. Ila sikutaka kabisa kubishana na hao watu.
 
Ndugu wanajamvi,

Kabla ya yote ningependa kutanguliza pongezi na hongera nyingi za kuweza kufika December tukiwa na pumzi. Pasipo kupoteza muda, ningependa kwenda moja kwa moja kwenye mkasa ulionikumba weekend hii maeneo fulani hapa jijini Dar es Salaam. Kwa ufupi nilikuwa napita tu kwenye njia moja mara nikaona kwa mbele yangu kuna pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na askari mwenye uniform pamoja na abiria aliyejitambulisha kuwa ni askari pia lakini hakuwa kwenye uniform.

Baada ya kusimama nikashangaa naulizwa "kwanini tunakusimamisha na hausimami tangu kule nyuma? Huoni wenzio wote wamesimama? Kwanini unakuwa na kiburi? Unataka kutusababishia shida wewe, yani mkubwa yupo maeneo haya na haturuhusu magari kupita ila wewe umepita! Yakaongelewa maneno mengine mengi ya kufanana na hayo. Mimi nikawajibu tu kwa upole kuwa kusema kweli sikuona mtu yeyote akinisimamisha na sikutambua kabisa kuwa magari yanasimama. Na isitoshe ni njia ambayo huwa haina magari mengi hivyo sikuwa na idea kabisa kuwa kuna kuzuiwa magari kupisha uwepo wa huyo mkubwa.

Mara yule askari ambaye alikuwa na nguo za kiraia akapokea simu na kuitikia kwa heshima kuashiria ni mkubwa wake alikuwa anampigia simu. Akaweka loud speaker na kwa masikio yangu alisikika akisema "umempata huyo mtu? mfunge pingu natuma gari lije kumchukua haraka sana. Ataenda kutoa maelezo kituoni" Yani niliishiwa nguvu ghafla na kula nikijaribu kuongea nao walikuwa wakipigiwa simu mara kwa mara na huyo mkubwa wao na kuwaamuru kuwa nipelekwe mahabusu nitafunguliwa kesi ambapo nitalipishwa faini ya shilingi milioni nane, kupekuliwa nyumbani kwangu, kutaifishwa kwa gari langu, na kwenda jela kwa kipindi kisichopungua 06 months.

Naomba tu nifupishe kwa kusema kuna kiasi kikubwa tu cha pesa kilinitoka kunusuru huo msukosuko kwasababu nilijiuliza mambo mengi:-
1. Kitendo cha mimi kuingizwa mahabusu kuna hati hati ya kupoteza ajira.
2. Kutaifishwa kwa gari ambalo ni la kampuni ni swala jingine kabisa.
3. Kupekuliwa nyumba naweza hata kubambukizwa madawa, silaha au nyara nikaishia jela.
4. Watoto wangu wadogo watalelewa na nani?
5. Reputation yangu itaharibika kwasababu nitakuwa na fingerprints interpol.
6. Hata nikienda mahakamani, kushindana na system ni ndoto ya mchana.

So, kutokana na hayo yote ilibidi tu niingie mfukoni na hata kukopa kidogo ili niweze kumalizana na hao watu nje ya sheria. Ni jambo ambalo linaniumiza sana kwasababu si kwa pesa iliyonitoka ila kwa kukiuka maadali yangu binafsi ya kutoa chochote.

Tanzania ni nchi yangu na ninaipenda lakini kwa haya niliyopitia, Mungu ndiye anajua hisia zangu na hii nchi zipoje kwa sasa.

Kama kuna mdau aliwahi kupitia mkasa kama wangu naomba tupeane uzoefu na kama kuna mwenye mchango wowote ningependa tujadiliane.

Asanteni sana.
Nakumbuka Kuna Askari wa usalqma barabarani alipoteza msafara wa Rais alijiua, sijajua Sheria yake ni Kali kiasi Gani Kwa Kosa kama hilo, ngoja tusubiri wanaojua watatuambia,ila Mimi niliogopa sana yule alivyojiua
 
Ndugu wanajamvi,

Kabla ya yote ningependa kutanguliza pongezi na hongera nyingi za kuweza kufika December tukiwa na pumzi. Pasipo kupoteza muda, ningependa kwenda moja kwa moja kwenye mkasa ulionikumba weekend hii maeneo fulani hapa jijini Dar es Salaam. Kwa ufupi nilikuwa napita tu kwenye njia moja mara nikaona kwa mbele yangu kuna pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na askari mwenye uniform pamoja na abiria aliyejitambulisha kuwa ni askari pia lakini hakuwa kwenye uniform.

Baada ya kusimama nikashangaa naulizwa "kwanini tunakusimamisha na hausimami tangu kule nyuma? Huoni wenzio wote wamesimama? Kwanini unakuwa na kiburi? Unataka kutusababishia shida wewe, yani mkubwa yupo maeneo haya na haturuhusu magari kupita ila wewe umepita! Yakaongelewa maneno mengine mengi ya kufanana na hayo. Mimi nikawajibu tu kwa upole kuwa kusema kweli sikuona mtu yeyote akinisimamisha na sikutambua kabisa kuwa magari yanasimama. Na isitoshe ni njia ambayo huwa haina magari mengi hivyo sikuwa na idea kabisa kuwa kuna kuzuiwa magari kupisha uwepo wa huyo mkubwa.

Mara yule askari ambaye alikuwa na nguo za kiraia akapokea simu na kuitikia kwa heshima kuashiria ni mkubwa wake alikuwa anampigia simu. Akaweka loud speaker na kwa masikio yangu alisikika akisema "umempata huyo mtu? mfunge pingu natuma gari lije kumchukua haraka sana. Ataenda kutoa maelezo kituoni" Yani niliishiwa nguvu ghafla na kula nikijaribu kuongea nao walikuwa wakipigiwa simu mara kwa mara na huyo mkubwa wao na kuwaamuru kuwa nipelekwe mahabusu nitafunguliwa kesi ambapo nitalipishwa faini ya shilingi milioni nane, kupekuliwa nyumbani kwangu, kutaifishwa kwa gari langu, na kwenda jela kwa kipindi kisichopungua 06 months.

Naomba tu nifupishe kwa kusema kuna kiasi kikubwa tu cha pesa kilinitoka kunusuru huo msukosuko kwasababu nilijiuliza mambo mengi:-
1. Kitendo cha mimi kuingizwa mahabusu kuna hati hati ya kupoteza ajira.
2. Kutaifishwa kwa gari ambalo ni la kampuni ni swala jingine kabisa.
3. Kupekuliwa nyumba naweza hata kubambukizwa madawa, silaha au nyara nikaishia jela.
4. Watoto wangu wadogo watalelewa na nani?
5. Reputation yangu itaharibika kwasababu nitakuwa na fingerprints interpol.
6. Hata nikienda mahakamani, kushindana na system ni ndoto ya mchana.

So, kutokana na hayo yote ilibidi tu niingie mfukoni na hata kukopa kidogo ili niweze kumalizana na hao watu nje ya sheria. Ni jambo ambalo linaniumiza sana kwasababu si kwa pesa iliyonitoka ila kwa kukiuka maadali yangu binafsi ya kutoa chochote.

Tanzania ni nchi yangu na ninaipenda lakini kwa haya niliyopitia, Mungu ndiye anajua hisia zangu na hii nchi zipoje kwa sasa.

Kama kuna mdau aliwahi kupitia mkasa kama wangu naomba tupeane uzoefu na kama kuna mwenye mchango wowote ningependa tujadiliane.

Asanteni sana.
Kwa ufupi umetapeliwa! Hao ni matapeli! Ungesema nipeleke kituoni hapa hata mia mbovu sina na hili gari nimeliazima kwa rafiki yangu! Hakuna faini kali kama hiyo! Ulipigwa!
 
Back
Top Bottom