Kosa la kuingilia msafara au kupita sehemu iliyozuiwa kupisha uwepo wa mtu mkubwa serikalini

Kosa la kuingilia msafara au kupita sehemu iliyozuiwa kupisha uwepo wa mtu mkubwa serikalini

Ok. Pole sana. Uliibiwa. Barabara ikifungwa kwa ajili ya kiongozi askari husimama barabarani kabisa, ungeomuona. Hakukuwa na msafara wowote. Ile maaskri kuongea nawe mda mrefu kisha kupigiwa simu na eti mkubwa wao nao wakaweka laudi spika kisha mkubwa atoa vitisho kwa namna ile, walijuwa utapoteza netweki na uchomoe hela.
Ni kweli,askari huwa wengi barabaran yaan utawaona tu

Tena askar huanza kusimamisha magar wakat rais yupo bafuni anaoga
 
Ndugu wanajamvi,

Kabla ya yote ningependa kutanguliza pongezi na hongera nyingi za kuweza kufika December tukiwa na pumzi. Pasipo kupoteza muda, ningependa kwenda moja kwa moja kwenye mkasa ulionikumba weekend hii maeneo fulani hapa jijini Dar es Salaam. Kwa ufupi nilikuwa napita tu kwenye njia moja mara nikaona kwa mbele yangu kuna pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na askari mwenye uniform pamoja na abiria aliyejitambulisha kuwa ni askari pia lakini hakuwa kwenye uniform.

Baada ya kusimama nikashangaa naulizwa "kwanini tunakusimamisha na hausimami tangu kule nyuma? Huoni wenzio wote wamesimama? Kwanini unakuwa na kiburi? Unataka kutusababishia shida wewe, yani mkubwa yupo maeneo haya na haturuhusu magari kupita ila wewe umepita! Yakaongelewa maneno mengine mengi ya kufanana na hayo. Mimi nikawajibu tu kwa upole kuwa kusema kweli sikuona mtu yeyote akinisimamisha na sikutambua kabisa kuwa magari yanasimama. Na isitoshe ni njia ambayo huwa haina magari mengi hivyo sikuwa na idea kabisa kuwa kuna kuzuiwa magari kupisha uwepo wa huyo mkubwa.

Mara yule askari ambaye alikuwa na nguo za kiraia akapokea simu na kuitikia kwa heshima kuashiria ni mkubwa wake alikuwa anampigia simu. Akaweka loud speaker na kwa masikio yangu alisikika akisema "umempata huyo mtu? mfunge pingu natuma gari lije kumchukua haraka sana. Ataenda kutoa maelezo kituoni" Yani niliishiwa nguvu ghafla na kula nikijaribu kuongea nao walikuwa wakipigiwa simu mara kwa mara na huyo mkubwa wao na kuwaamuru kuwa nipelekwe mahabusu nitafunguliwa kesi ambapo nitalipishwa faini ya shilingi milioni nane, kupekuliwa nyumbani kwangu, kutaifishwa kwa gari langu, na kwenda jela kwa kipindi kisichopungua 06 months.

Naomba tu nifupishe kwa kusema kuna kiasi kikubwa tu cha pesa kilinitoka kunusuru huo msukosuko kwasababu nilijiuliza mambo mengi:-
1. Kitendo cha mimi kuingizwa mahabusu kuna hati hati ya kupoteza ajira.
2. Kutaifishwa kwa gari ambalo ni la kampuni ni swala jingine kabisa.
3. Kupekuliwa nyumba naweza hata kubambukizwa madawa, silaha au nyara nikaishia jela.
4. Watoto wangu wadogo watalelewa na nani?
5. Reputation yangu itaharibika kwasababu nitakuwa na fingerprints interpol.
6. Hata nikienda mahakamani, kushindana na system ni ndoto ya mchana.

So, kutokana na hayo yote ilibidi tu niingie mfukoni na hata kukopa kidogo ili niweze kumalizana na hao watu nje ya sheria. Ni jambo ambalo linaniumiza sana kwasababu si kwa pesa iliyonitoka ila kwa kukiuka maadali yangu binafsi ya kutoa chochote.

Tanzania ni nchi yangu na ninaipenda lakini kwa haya niliyopitia, Mungu ndiye anajua hisia zangu na hii nchi zipoje kwa sasa.

Kama kuna mdau aliwahi kupitia mkasa kama wangu naomba tupeane uzoefu na kama kuna mwenye mchango wowote ningependa tujadiliane.

Asanteni sana.
Pole Sana mkuu
 
Niliwahi kupatwa na kadhia hiyo ya kuingilia msafara, tena bora wewe mimi nilikatiza kabisa wakati msafara unakuja, sikunyanyaswa kiasi hicho ila nilienda mahakamani nikalipa faini ya makosa ya barabarani.
Kiuhalisia hilo ni kosa kubwa na ukweli wanaweza kuhisi ulikuwa unahatarisha usalama wa huyo mkubwa.
Mimi nilifikishwa kituoni kabisa na nilikuwa na ujasiri wa kujibu kwa utulivu mkubwa na baadae siku hiyo hiyo nilitoka na gari yangu nilipewa nikafunguliwa traffic case tu na nikaenda mahakamani nikakubali kosa nikapigwa faini ya 150k nafikir nilisomewa makosa 3.
Ukiniuliza sijui hata nilitumia nguvu gani kuwafanya wawe wapole wenyewe japo nilipokamatwa ilikuwa hatar ila nilitulia bila kujibishana nao zaid ya kukubali lile ni kosa.
Kosa kubwa Sawa ila mpaka amefikisha 8M hawa watakuwa matapeli
 
Miaka hiyo Niko na ka baby walker na washikaji tunaaelekea Kigali Rwanda nimefika eneo linaitwa kirehe nafikiri, na kilikuwa kipindi cha uchaguzi mkuu ndani ya rwanda kumbe kagame anaenda kupiga kampeni eneo hilo sasa barabarani sioni gari wala askari na sikujua kama gari zimezuiliwa huko mbele ninakoelekea Mara ghafra ilikuja gari Moja nyeusi king'ora juu ikaniashiria nisimame haraka wakashuka jamaa wanne warefu miwani black wakaniuliza unakwenda wapi nikajibu Kigali kuangalia mechi maana siku hiyo ilikuwa game ya taifa stars na amavubi
Kwenye majibizano hayo ndio Msafara ukapita kwa mwendo wa ngiri mkia juu, wale jamaa na gari lao nao wakaunga palepale Msafara ule wakaacha wameniambia nisitoke hapo watarudi fasta, hapo nishatetemeka balaa, nikawasubiri kama robo saa sioni wakinirudia aaah, nikawasha gari nikaendelea na safari
 
Angekuwa wa mkorani mtu kuja jijini mgesema mshamba ila Kwa sababu umetapeliwa na wahuni wenzio sawa tu ongeza juhudi Ili utapeliwe zaidi.

Hakuna kitu kama hicho Mimi sikupi pole Bali hongera Kwa kulisha familia ya matapeli. Ubaya ubwela hakuna mwaisa mshamba
 
umetapeliwa,,,,hakuna kitu kama hicho,,,kitendo cha kupokea simu kwa loud speaker ulitakiwa ustuke
 
Kwa situatio kma yako mimi nisingewapa shilingi na wasingenifunga ata kidogo

Kila mtu aringie na alichonacho bhana
 
Nakumbuka Kuna Askari wa usalqma barabarani alipoteza msafara wa Rais alijiua, sijajua Sheria yake ni Kali kiasi Gani Kwa Kosa kama hilo, ngoja tusubiri wanaojua watatuambia,ila Mimi niliogopa sana yule alivyojiua
July 2010 Tarime.

Kuna ambao wanadai aliuawa kwa siri ili kulinda vibarua vya watu, na inasemekana hakufanya vile kwa lengo la kupoteza bali maelekezo kutoka juu.

Jiulize tangu lini mtu awekwe rumande akiwa na bastola
 
Ndugu wanajamvi,

Kabla ya yote ningependa kutanguliza pongezi na hongera nyingi za kuweza kufika December tukiwa na pumzi. Pasipo kupoteza muda, ningependa kwenda moja kwa moja kwenye mkasa ulionikumba weekend hii maeneo fulani hapa jijini Dar es Salaam. Kwa ufupi nilikuwa napita tu kwenye njia moja mara nikaona kwa mbele yangu kuna pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na askari mwenye uniform pamoja na abiria aliyejitambulisha kuwa ni askari pia lakini hakuwa kwenye uniform.

Baada ya kusimama nikashangaa naulizwa "kwanini tunakusimamisha na hausimami tangu kule nyuma? Huoni wenzio wote wamesimama? Kwanini unakuwa na kiburi? Unataka kutusababishia shida wewe, yani mkubwa yupo maeneo haya na haturuhusu magari kupita ila wewe umepita! Yakaongelewa maneno mengine mengi ya kufanana na hayo. Mimi nikawajibu tu kwa upole kuwa kusema kweli sikuona mtu yeyote akinisimamisha na sikutambua kabisa kuwa magari yanasimama. Na isitoshe ni njia ambayo huwa haina magari mengi hivyo sikuwa na idea kabisa kuwa kuna kuzuiwa magari kupisha uwepo wa huyo mkubwa.

Mara yule askari ambaye alikuwa na nguo za kiraia akapokea simu na kuitikia kwa heshima kuashiria ni mkubwa wake alikuwa anampigia simu. Akaweka loud speaker na kwa masikio yangu alisikika akisema "umempata huyo mtu? mfunge pingu natuma gari lije kumchukua haraka sana. Ataenda kutoa maelezo kituoni" Yani niliishiwa nguvu ghafla na kula nikijaribu kuongea nao walikuwa wakipigiwa simu mara kwa mara na huyo mkubwa wao na kuwaamuru kuwa nipelekwe mahabusu nitafunguliwa kesi ambapo nitalipishwa faini ya shilingi milioni nane, kupekuliwa nyumbani kwangu, kutaifishwa kwa gari langu, na kwenda jela kwa kipindi kisichopungua 06 months.

Naomba tu nifupishe kwa kusema kuna kiasi kikubwa tu cha pesa kilinitoka kunusuru huo msukosuko kwasababu nilijiuliza mambo mengi:-
1. Kitendo cha mimi kuingizwa mahabusu kuna hati hati ya kupoteza ajira.
2. Kutaifishwa kwa gari ambalo ni la kampuni ni swala jingine kabisa.
3. Kupekuliwa nyumba naweza hata kubambukizwa madawa, silaha au nyara nikaishia jela.
4. Watoto wangu wadogo watalelewa na nani?
5. Reputation yangu itaharibika kwasababu nitakuwa na fingerprints interpol.
6. Hata nikienda mahakamani, kushindana na system ni ndoto ya mchana.

So, kutokana na hayo yote ilibidi tu niingie mfukoni na hata kukopa kidogo ili niweze kumalizana na hao watu nje ya sheria. Ni jambo ambalo linaniumiza sana kwasababu si kwa pesa iliyonitoka ila kwa kukiuka maadali yangu binafsi ya kutoa chochote.

Tanzania ni nchi yangu na ninaipenda lakini kwa haya niliyopitia, Mungu ndiye anajua hisia zangu na hii nchi zipoje kwa sasa.

Kama kuna mdau aliwahi kupitia mkasa kama wangu naomba tupeane uzoefu na kama kuna mwenye mchango wowote ningependa tujadiliane.

Asanteni sana.

Pole sana.

Kwa kufupi ulitapeliwa.

Ulitakuwa kuwaambia wakwambie kituo kipi cha Polisi uende. Hakuna faini kubwa hivyo za traffic cases. Kwa sasa limezuka wimbi la wezi wanaotumia mtindo huu unaohusisha watu wenye uniforms za kiaskari. Matukio kama hayo ni matatu niliyoyasikia na yametokea Magengeni ukiwa unaelekea Bunju, barabara ya Mbezi Beach (Bagamoyo Road baada ya Mwenge) na maeneo ya Mlimani City kuelekea Ubungo/Mwenge. Na yanatokea wakati kuna msafara wa ukweli ila kabla askari hawajaanza kuzuia magari rasmi kwenye sehemu wanayokusimamisha.

Cha kuzingatia hakikisha usalama wako ila

1. Husiruhusu mtu aingie kwenye gari lako na chunga ufunguo wako wa gari husijechukuliwa ili kukuingiza kwenye vitisho zaidi

2. Waambie muongozane mwende kituo cha polisi kilicho karibu. Ukipata bahati ya kuwaona karibu traffic police wenye uniforms elekea kwa hao kwa ajili ya kupata ufafanuzi zaidi.

Matukio ya hivi yapo yapo na polisi wanayajua na wanapambana nayo kwa nguvu nyingi wakipata taarifa. Kuna wahusika kadhaa wamekamatwa kinachotakiwa tuchukue tahadhari.

kitu muhimu tutambue polisi ni mahala salama kwa mtu yeyote hata kama una makosa, utaelimishwa ikilazimu kutozwa faini hata kupelekwa mahakamani ila uhakika wa usalama wako ndo jambo kubwa la kuzingatia.
 
Mimi wangeniua nilivyozaliwa mbishi Kama nywele zangu za kipilipili...labda niwe nilifanya makusudi
 
Ilishanitokea 2016.. nikaliwa 300k.. bahati magufuli alikula vichwa polisi wote (3) waliohusika.. ilikuwa coincidence tu..
 
Kwanza inaonekana ulikua na ndinga la maana sana linaloashiria unaogelea kwenye ukwasi ,wavuta bange wakajua wakikuchekecha hawakosi fungu nene kwako , ungekua na kigari cha kipuuzi ungeishia kutukanwa au kula mambata ,ila kujipachika kwenye katikati ya msafara wa namba moja au wadogo zake wawili apo utachezea hata submachine gun
We ni muoga...ulipotishwa kuhusu kazi yako ukajinyea...msafara uliuona?Bora ungeenda.kituoni akala mkubwa wao Kama NI kweli hakina jinai hapo
 
We ni muoga...ulipotishwa kuhusu kazi yako ukajinyea...msafara uliuona?Bora ungeenda.kituoni akala mkubwa wao Kama NI kweli hakina jinai hapo
kumbuka mimi sio mtoa mada mkuu hata hio gar yakuingilia msafara sina pia
 
Back
Top Bottom