Kosa la kuingilia msafara au kupita sehemu iliyozuiwa kupisha uwepo wa mtu mkubwa serikalini

Kosa la kuingilia msafara au kupita sehemu iliyozuiwa kupisha uwepo wa mtu mkubwa serikalini

Kwa akili ndogo tu ni kuwa umetapeliwa tena kizembe sana pole sana mkuu
 
July 2010 Tarime.

Kuna ambao wanadai aliuawa kwa siri ili kulinda vibarua vya watu, na inasemekana hakufanya vile kwa lengo la kupoteza bali maelekezo kutoka juu.

Jiulize tangu lini mtu awekwe rumande akiwa na bastola
Wakuu mwenye details za hii stori ,nimeshangaa imekuaje akampoteza nambari 1 kwamba hakuwa anafahamu route?
Na maelekezo hayo ni juu ya nambari 1 au chini ?
 
Pole ila ulichofanya ni sahihi kabisa, ungepata tabu tu. Maana bwana mkubwa kwenye simu angewa komalia hao wa chini.

Mimi nishapata mkasa Mdogo wakuta kuingia msafara bila kujua, Askali alitoka onyo Kali tu. Na mara nyingi atakwambia hivyo unataka kututia matatani.

Wakati Lowasa Waziri Mkuu, nilikuwa na Honda Baja XRL 250. Mhe. Baada tu ya kupita pale mbuyuni kama sekunde 40, askali akalegeza mkono nikachomoka mwendo mdundo muffler la exhaust inamwa mwimbo, Hamad! Nashtuka nimewavuta kama mita 30, ghafra naona mlango wa nyuma wa Mercedes Benz unafunguliwa mtu ananinyooshea miguu wa kukuu Kwa kunipa onyo, bomba la silencer likinesa juu chini juu chini. Nikafinya break quaaaaah kiroho juu.

Toka Siku hiyo nimekuwa na adabu, zaidi ya kufata Ambulance tu.
 
Wakuu mwenye details za hii stori ,nimeshangaa imekuaje akampoteza nambari 1 kwamba hakuwa anafahamu route?
Na maelekezo hayo ni juu ya nambari 1 au chini ?
Kitengo cha itifaki
 
Wewe ni mpumbavu au mjinga sijajua tofauti ya hayo maneno ila lengo langu ni lile neno ambalo sio tusi kwako
 
Mimi niliwahi kukutwa na issue kama yako. Nilipigwa mkono na kuwekwa pembeni.

Huyo mkubwa alipoondoka tu, askari alinifuata fasta na nikampa leseni yangu huku kwa chini kukiwa na elfu 5 tatu (huenda alijua ni misimbazi ya kutosha). Nilimwambia Askari nilikuwa nawahi job na kumuonyesha ID yangu

Kesi iliishia pale. Sasa wewe hizo story zooote unaambiwa kwa simu tena umewekewa loud speaker? Real policemen hawana story nyingi hivyo
 
Back
Top Bottom