Habarini wana MMU...
Nimekuwa nikipata tabu kufahamu juu ya hili swala la kuanguka bafuni/chooni na maswala ya kishirikina hii ni kutokana na matukio niliyo wahi kuyaona au kusikia..kwanza kabisa
2011 Nilipo kuwa shule fulani hivi ya wavulana usiku kuna kijana alitoka kwenda kujisaidia usiku wa manane then aliteleza na kuanguka baada ya hapo akadai kwamba ameona vitu vya ajabu, hakurudi alienda kwao akakaa kwa muda mrefu alipo rudi akadai ameenda kufanya mambo ya kimila la sivyo angefarik
2014 nakumbuka wakati fulan pale hall 5 chuo rummate alitoka usiku kwenda kujisaidia wakati anatoka chooni aliteleza na kuanguka aliishiwa nguvu kutoka bafuni alirud anajiburuza paka rum alikuwa na stress saana, alirudi kwao alipo waeleza wazazi wake alisema kwamba ni kama neema za mungu tu yeye kupona ila asingepona kabisa..
2015 Kuna kijana alikuwa anasumbuliwa na vidonda vya tumbo but kuna siku alienda choon mabibo hostel aliteleza na kuanguka choon alipo kimbizwa hospitali alifarik..watu wakawa wanahusianisha na maswala ya kishirikina..
Leo pia jirani yangu ameanguka chooni amelalamika saana na kuogopa sana, amehusisha na mambo ya kishirikina..
Wana MMU naomba ushauri wenu na uzoefu wenu juu ya hili..binafsi ni mkrist safi sipend kuyapa nguvu saana mambo ya kishirikina..
Cc.
mshana jr njoo hapa mzee tusaidiane na kueleweshana