Kuanguka chooni/bafuni na kufa, kuna uhusiano gani?

Good.
 
Nashukuru nami ningejibu hivyo hivyo. na kama hakuna majimaji hakuna utelezi na huezi anguka. Ukianguka kinyume usipogonga kichwa ukutani au chini huuezi kufa. Hata mimi nimeanguka sikugonga kichwa, wife naye kaanguka hajagonga kwa kuwa bafu ni kubwa lina nafasi ya kutosha kujitetea. Ila pia naye Mungu anasaidia kutulinda katika yote. Amen
 
Mimi nimeanguka leo pale kariakoo kuna Hotel inaitwa pop inn.. ndani ilikuwa imechakaa na bafu ni chafu chafu na uterezi pia na kama imetoka kupigwa rangi siku chache hivyo kuna harufu kali sana ndani. nilikuwa nasex na demu sasa mkojo ukaja asubuhi hii nikaenda chooni kukojoa kwa kukiface choo cha kukaa nikasafisha uume kwanza kisha nikawa nakojoa huku nainuka hapo hapo ukaja kama usingizi wa ajabu nikaslide nikasikia kishindo kisogoni then nikapoteza fahamu demu akapatwa na khofu kusikia kishindo akachungulia chooni akaona mguu mmoja umenyooka na mwingine umenyenyuka akaanza kuniita nikawa napata fahamu kidogo ila sikutambua nipo wapi nikamuuliza nipo wapi hapa huku nikawa najihisi nipo Kitandani and then nikastuka nimeanguka na kisogo kinauma nikakumbuka nimeanguka but usingizi ni duh nikakumbuka mambo ya kiswahili ila utotoni nimeanguka sana na ukubwani mara moja ila sikuwahi poteza fahamu na kabla ya kulala nilikula ndizi... hii imekaaje wadau!?

My girl ananishauri anipeleke kwa maustaadhi mimi baada ya kusoma comment humu nikaona imekaa kihospital zaidi Dr kaniambia ninywe maji kama glasi moja nikoge nile and then nione kama kizunguzungu kitaisha na ni hatari kama nikitapika ndio nataka nile nione
 
Upo vizuri.
 
Asilimia kubwa watu wakianguka chooni hufariki dunia au kupooza mwili. Kuna uhusiano gani kati ya kifo na chooni?
Hii inaana kuwa aliyeanguka chooni kwa aina hiyo alikuwa ana shida ya kuwa na shinikizo kubwa la damu, BP, hivyo harakati za kuchuchumaa hasa kwenye vyoo vya mashimo, kujikamua na kunyanyuka haraka baada ya kumaliza shughuli kumesababisha BP ipande zaidi na zaidi, hivyo kusababisha kuanguka na kutokea hivyo unachokisema. Wanakufa kwakuwa baada ya kuanguka anaplekwa kwa waganga badala ya kukimbizwa hospital haraka kupata matibabu ya haraka. Watu wanadhani amekumbwa na jini chooni. Jambo kama hilo ni nadra kutokea kwa wanaotumia vyoo vya kukaa.
 
Issue ni Jina la Yesu linauwezo wa kuvunja yote haya
 
Ukiwa chooni kujisaidia kuna kujikamua kama ni haja kubwa endapo pressure ikapanda ghafla ndio inapata mahali pake unaondoka. Bafuni kuoga endapo mishipa ya damu imepanuka na una pressure ukijimwagia maji ghafla hasa kichwani mishipa inajaribu kubana matokeo yake mishipa dhaifu inapasuka ndio mtu anadondoka.Haishauriwi kukimbia ukawa unahema sana kisha unywe maji au ujiwagie maji mara moja bila kupumzika kwanza.Tatizo wenye mawazo mfupi kila kitu wanawaza ushirikina
 
Kwa nini watu wengi wanaanguka bafuni na kupata Ugonjwa wa stroke mara nyingi?



Imetokea mara nyingi kusikia kuwa jamaa kaanguka bafuni na kufariki au kupata stroke au hajitambui na wala haongei!

Kuna sababu kuu mbili:

Ya kwanza ni ya kisayansi: Ukiwa unapresha na ukaingia bafuni kuoga, unapoanza kichwani kujimwagia maji ni hatari kwani mwili wote na viungo upata mawasiliano kwa kuongozwa na sehemu maalum kichwani iitwayo control centre, hii ina idara nyingi kwa kazi husika kiasi kwamba mwili na viungo vyake uendeshwa kwa ustadi mkubwa kama Mungu mmoja wa pekee alivyoumba na kukadiria. Maji yakimwagiwa kichwani yanastua sehemu muhimu zikiwemo za mfumo wa moyo na fahamu ghafla kiasi kwamba uwiano ukikosa kati ya moyo na fahamu inatokea mtu kuzirai na hatimaye stroke inatokea. Ushauri anza kujimwagia kiunoni na kushuka chini kwenye miguu na kisha kifunoni hadi kifuani na kumalizia kichwani na hii inaweka uwiano sawa kati ya mwili na ubongo kupokea maji mwilini.

Ya pili ya kiimani: Katika vitabu vyote vya dini kama Injili, Taurati, Zaburi na Qur’an yametajwa mapepo na shetani, haya mapepo/majini yana makundi na kuna yale yanayoishi sehemu chafu kama bafu,choo,dampo, nk. sasa ukiingia bafuni inabidi uombe ili Mungu akuepushe lakini wengi hawaombi na hawajui namna ya kuomba na wengine hawaamini hayo, lakini mashetani wa chooni na bafuni yanaweza kukudhuru na ukaumizwa kama kuanguka na kupata stroke na hadi kifo bila kujua, kuna baadhi yanatumwa na wachawi yakusubiri chooni au bafuni ukiwa umevua na yakuingie na kukuzuru hadi madhara kama hayo makubwa! Jitahidi kuomba kabla ya kuingia bafuni au chooni, oga kwa utaratibu wa kujimwagia maji kuanzia kiunoni kwenda miguuni na kisha kiunoni kwenda kichwani ili uweke uwiano sawa kati ya mwili na ubongo katika kupokea maji.

Wakati mwingine pulizia bafuni mafuta rasmi kwa ajili ya kufukuza majini/mapepo chooni na bafuni kwani viumbe hivi vipo na vingine ni maadui kwetu ingawa hatuvioni na madhara yake yapo na makubwa kuliko kiwango ila shida hatuoni na kutambua madhara yake wazi wazi kama tunavyoona mbu wanapaa vyumbani kwetu na kuchukua hatua ya haraka ya kunyunyizia dawa za mbu ili wafe tusiumwe na kupata malaria, heri ya malaria ina vipimo na dawa ziko wazi kuliko mapepo/majini na wachawi wasioonekana kwa macho.

Dawa ya kunyunyizia kwenye nyumba ni mafuta yenye madawa yatokanayo na mimea maalum iliyotajwa ndani ya taurati, Injili, Zaburi na Qur’an kiasi kwamba majini/mapepo na wachawi hawatapenya ukisha puliza nyumbani kwako, bafuni na ukajipaka wewe na watu wako, Mungu mmoja wa pekee atawalinda kwa uwezo wake! Pia kuna sabuni ina madawa hayo hayo ya kuondoa nguvu za giza na athari zake kama mikosi na nuksi, unaoga na kisha kujipaka mafuta hayo.

Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu Au boonyeza hapa.Mzizi Mkavu
 
Sio Bismillah
Kuna dua maalum
 
Nakubaliana wa waliotoa majibu kuwa;
1.Chooni/Bafuni pana utelezi wa sabuni na maji maji machafu ambayo hurahisisha tukio la kuteleza.
2.Nakubaliana pia kuwa vyumba vya vyoo huwa vidogo tena vyenye madirisha madogo yakiwa yanefungwa hivyo, mzunguko wa hewa safi ni mdogo.
3.Kuna suala la maji kuwa baridi na itategemea hayo maji yametangulia kugusa sehemu gani ikiwa kichwani hali inakuwa hatari zaidi kwani hata usipoanguka unapigwa ganzi kwa muda.
4.Vile vile kuna suala la kukosa msaada wa haraka inapotokea umeanguka chooni/bafuni kwa kuwa unakuwa peke yako.
5.Suala la miundombinu ya chooni/Bafuni nalo lipo yaani masinki na mabomba uangupo juu yao.
6.Suala la umri nalo lina mantiki kwa kuwa watu wa umri mkubwa na ambao hawafanyi mazoezi mishipa yao hazijafunguka sana na hivyo msunguko wao wa damu si mzuri sana.
7.Suala la imani hilo nawaachia wenyewe
 
Somo tajwa hapo juu lahusika.

Ukiona mtu amedondoka chooni au bafuni ujue lazima tu amerogwa au kapigwa chuma ulete. Na mara nyingi hutokea kwenye vyoo au bafu zilizofunika ( vya ndani), maana ndo sehemu pendwa ya majini.Majini hayapendi vyoo na bafu za wazi juu. Na yanapenda sana mahala pasafi.

Ukidondoka lazima tu utakuwa umetupiwa jini fulani na mtaalam ! Ukizimia ukaamka ujue limekukosa kosa tu lakini haliondoki hiyo sehemu mpaka likamilishe lengo lake.

Jipange ndugu.
 
kwa kawaida watu wenye magonjwa ya moyo na wanatumia dawa fulani hushauriwa. kutosimama kwa muda mrefu na wanaume wanatakiwa kukojoa wakiwa wamekaa. Mbali na hivyo huwa katika hatari ya kuanguka kwa kizunguzungu. Ndiyo maana wengi wanaoanguka chooni huwa wanaume.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…